Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 5

WIMBO 27 Kufunuliwa kwa Wana wa Mungu

“Sitakutupa Hata Kidogo”!

“Sitakutupa Hata Kidogo”!

“[Mungu] amesema: ‘Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.’”EBR. 13:5b.

WAZO KUBWA

Kuhakikishia watu wa Mungu wenye kuwa ku dunia kama Yehova hatawatupa wakati Wakristo wote watiwa-mafuta wataenda mbinguni.

1. Ni wakati gani watiwa-mafuta wote watakuwa mbinguni?

 MIAKA yenye imepita, watu wa Yehova walijiuliza, ‘Ni wakati gani njo mutiwa-mafuta wa mwisho ataenda mbinguni?’ Ku mwanzo tulifikiri kama watiwa-mafuta fulani wanaweza kubakia mu dunia Paradiso kwa wakati fulani kisha vita ya Armagedoni. Lakini mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 7, 2013, tulijifunza kama watiwa-mafuta wote wenye wangali ku dunia wataenda mbinguni mbele vita ya Armagedoni ianze.—Mt. 24:31.

2. Tunaweza kujiuliza maulizo gani, na tutajifunza nini mu hii habari?

2 Sasa, tunaweza kujiuliza hivi: Mambo itakuwa namna gani juu ya “kondoo wengine,” ni kusema Wakristo wenye watakuwa namutumikia Yehova kwa uaminifu ku dunia mu kipindi ya “taabu kubwa”? (Yoh. 10:16; Mt. 24:21) Wakristo fulani wanaweza kuwa na wasiwasi kama watajisikia kuwa wameachwa wakati ndugu na dada zao wapendwa watiwa-mafuta wataenda mbinguni. Acha tuzungumuzie habari mbili zenye kuwa mu Biblia zenye zinaweza kufanya wawaze vile, kisha tutazungumuzia juu ya nini hawapaswe kuwa na wasiwasi.

JAMBO YENYE HAITATOKEA

3-4. Wakristo fulani wanaweza kujiuliza nini, na juu ya nini?

3 Wakristo fulani wanaweza kujiuliza ikiwa kondoo wengine hawataacha kweli wakati Wakristo watiwa-mafuta wa mu Baraza Yenye Kuongoza hawatakuwa tena ili kuwatolea muongozo. Pengine habari fulani zenye kuwa mu Biblia zinaweza kuwafanya wawaze vile na waogope. Tuzungumuzie mifano mbili. Ya kwanza inahusu Kuhani Mukubwa Yehoyada. Alikuwa mutumishi muaminifu wa Mungu. Yeye na bibi yake, Yehoshabeati, walilinda kijana Yehoashi na walimusaidia akuwe mufalme muzuri na muaminifu. Wakati wote wenye Yehoyada alikuwa muzima, Yehoashi alifanya mambo ya muzuri. Lakini kisha tu Yehoyada kufa, Yehoashi alianza kufanya mambo ya mubaya. Alisikiliza wakubwa wabaya na alimuacha Yehova.—2 Ny. 24:2, 15-19.

4 Mufano ingine ni ya Wakristo wa mu karne ya pili. Kisha mitume wote kufa, mutume Yohana njo alibakia na alikuwa mufano kwa Wakristo wengi. Aliwasaidia waendelee kuwa waaminifu kwa Yehova. (3 Yo. 4) Kwa wakati fulani, Yohana na mitume wengine waaminifu walikuwa najikaza sana ili kuzuia uasi-imani usienee mu kutaniko ya Kikristo. (1 Yo. 2:18; 2 Te. 2:7) Lakini kisha Yohana kufa, uasi-imani ulienea sawa moto wa pori. Kisha makumi fulani ya miaka, kutaniko ya Kikristo ilijaa uasi-imani.

5. Zile habari mbili hazipaswe kutufanya tuwaze nini?

5 Je, zile habari mbili zenye kuwa mu Maandiko zinaonyesha kama jambo ya vile itafikia kondoo wengine wakati Wakristo watiwa-mafuta wataenda mbinguni? Ile wakati, Wakristo waaminifu wenye kuwa ku dunia wataacha mazoezi yenye walipewa sawa vile Yehoashi alifanya, ao wataangukia mu uasi-imani sawa vile Wakristo wengi walifanya mu karne ya pili K.K.Y.? Hapana, haitakuwa vile! Tunaweza kuwa hakika kama wakati watiwa-mafuta wataenda mbinguni, kondoo wengine wataendelea kuhangaikiwa na kumuabudu Yehova kwa uaminifu. Juu ya nini tuko hakika na ile jambo?

IBADA SAFI HAITACHAFULIWA

6. Tutazungumuzia vipindi gani tatu?

6 Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama ibada safi haitachafuliwa hata mu wakati wa nguvu wenye kuwa mbele yetu? Juu ya mambo yenye tunasoma mu Biblia kuhusu kipindi yenye tuko ndani. Hii kipindi ya wakati, iko tofauti kabisa na wakati wa Waisraeli wa zamani na wakati wa Wakristo wa karne ya pili. Tuchunguze basi kwa undani hivi vipindi tatu vya wakati: (1) Wakati wa Waisraeli wa zamani, (2) wakati wa kisha kifo cha mitume, na (3) wakati wetu, “wakati wa kurudishwa kwa mambo yote.”—Mdo. 3:21.

7. Mu Israeli ya zamani juu ya nini watu waaminifu hawakuvunjika moyo wakati taifa na wafalme walichagua kufanya mambo ya mubaya?

7 Wakati wa Waisraeli wa zamani. Muda mufupi mbele akufe, Musa aliambia hivi Waisraeli: “Ninajua muzuri kwamba kisha kifo changu hakika mutatenda uovu na kuacha njia yenye nimewaamuru.” (Kum. 31:29) Musa alionya pia kama ikiwa Waisraeli wanaasi, taifa yote ingepelekwa mu uhamisho. (Kum. 28:35, 36) Ile maneno ilitimia? Ndiyo. Kwa miaka mingi, wafalme wengi walichagua kufanya mambo ya mubaya na walifanya watu wa Mungu wapotee. Ile ilifanya Yehova apatie watu wake malipizi na akatize utawala wa wafalme Waisraeli. (Eze. 21:25-27) Lakini wakati Waisraeli waaminifu waliona kama maneno ya Mungu inatimia, ile iliwapatia uhodari wa kuendelea kumutumikia kwa uaminifu.—Isa. 55:10, 11.

8. Tunapaswa kushangaa kuona kama uasi uliingia mu kutaniko ya Kikristo mu karne ya pili? Fasiria.

8 Wakati wa kisha kifo ya mitume. Je, tunaweza kushangaa kuona kama uasi uliingia mu kutaniko ya Kikristo mu karne ya pili? Hapana. Yesu alitabiri kama kungetokea uasi-imani mukubwa sana. (Mt. 7:21-23; 13:24-30, 36-43) Mutume Paulo, Petro, na Yohana walionyesha kama unabii wa Yesu ulikuwa umeanza kutimia mu karne ya kwanza K.K.Y. (2 Te. 2:3, 7; 2 Pe. 2:1; 1 Yo. 2:18) Mu karne ya pili K.K.Y., kutaniko ya Kikristo ilichafuliwa. Ukristo wa waasi-imani ulianza na ukakuwa sehemu ya maana ya Babiloni Mukubwa, ni kusema dini zote za uongo. Mu ile kipindi pia, mambo yenye Maandiko ilitabiri ilitimia.

9. Namna gani wakati wetu uko tofauti na wakati wa Waisraeli na kipindi ya mu karne ya pili?

9 “Wakati wa kurudishwa kwa mambo yote.” Wakati wetu uko tofauti na wakati wa Waisraeli na wakati wenye uasi-imani uliingia mu kutaniko mu karne ya pili K.K.Y. Kipindi yenye tunaishi inaitwa namna gani? Tunazoea kuiita “siku za mwisho” za mupangilio huu mubaya wa mambo. (2 Ti. 3:1) Lakini Biblia inaonyesha kama kuko kipindi ingine kubwa na ya murefu zaidi yenye ilianza wakati siku za mwisho zilianza. Ile kipindi itaendelea mupaka wakati Ufalme wa Kimasiya utarudishia wanadamu ukamilifu na kufanya dunia kuwa paradiso. Ile kipindi inaitwa “wakati wa kurudishwa kwa mambo yote.” (Mdo. 3:21) Ilianza mu mwaka wa 1914. Ni nini njo ilirudishwa ile wakati? Yesu aliwekwa kuwa Mufalme mbinguni. Kwa hiyo, Yehova alikuwa tena na mutawala wa kumuwakilisha mwenye alikuwa muzao wa mufalme muaminifu Daudi. Lakini, haiko ule Ufalme tu njo Yehova alirudisha. Muda mufupi kisha pale, ibada safi ilianza kurudishwa! (Isa. 2:2-4; Eze. 11:17-20) Itachafuliwa tena?

10. (a) Biblia ilitabiri nini juu ya ibada safi mu wakati wetu? (Isaya 54:17) (b) Juu ya nini ule unabii ni wenye kutia moyo?

10 Soma Isaya 54:17. Fikiria maneno yenye kuwa mu hii unabii: “Hakuna silaha yenye itafanywa juu yako yenye itafanikiwa”! Ile maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu iko natimia leo. Maneno yenye kufuata yenye kutia moyo inahusu wakati wetu: “Wana wako wote watafundishwa na Yehova, na amani ya wana wako itakuwa nyingi. Utafanywa imara kabisa katika haki. . . . Hautaogopa kitu chochote na hautakuwa na hofu, kwa maana hakitakukaribia.” (Isa. 54:13, 14) Hata “mungu wa mupangilio huu wa mambo,” Shetani, hana uwezo wa kuzuia kazi ya kufundisha yenye watu wa Yehova wako nafanya. (2 Ko. 4:4) Ibada safi imerudishwa, na haitachafuliwa tena hata kidogo. Itabakia milele na milele. Hakuna silaha yoyote yenye itafanywa juu yetu yenye itakuwa na matokeo!

JAMBO YENYE ITATOKEA

11. Ni nini inatuhakikishia kama Wakristo wa mu kundi kubwa hawataachwa wakati watiwa-mafuta wataenda mbinguni?

11 Nini njo itatokea wakati watiwa-mafuta wataenda mbinguni? Kumbuka kama, Yesu ni Muchungaji wetu. Yeye njo kichwa cha kutaniko ya Kikristo. Yesu alisema hivi waziwazi: “Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo.” (Mt. 23:10) Mufalme wetu mwenye iko natawala mbinguni, hatashindwa hata kidogo kufanya kazi yake. Juu Kristo njo atasimamia mambo, wafuasi wake hapa ku dunia hawatakuwa na sababu yoyote ya kuogopa. Ni kweli kwamba hatujue mambo yote juu ya namna Kristo ataongoza watu wake ile wakati. Hata vile, tuone mifano fulani yenye kuzungumuziwa mu Biblia yenye inaweza kutuhakikishia kama mambo itakuwa tu muzuri.

12. Yehova alihangaikia namna gani watu wake (a) kisha kifo ya Musa? (b) kisha Eliya kupata mugao ingine? (Ona pia picha.)

12 Mbele Waisraeli waingie mu Inchi ya Ahadi, Musa alikufa. Ni nini ilifikia watu wa Mungu? Juu ule mwanaume muaminifu hakukuwa tena, walibakia bila musaada wowote? Hapana. Muda wote wenye waliendelea kuwa waaminifu, Yehova aliwapatia mambo yenye walikuwa nayo lazima. Mbele Musa akufe, Yehova alimuamuru apatie Yoshua mugao wa kuongoza watu wake. Musa alikuwa amezoeza Yoshua kwa miaka mingi. (Kut. 33:11; Kum. 34:9) Zaidi ya Yoshua, kulikuwa wanaume wengi wenye kustahili wenye walikuwa naongoza; wakubwa wa maelfu, wakubwa wa mamia, wakubwa wa makumi tano, na wakubwa wa makumi. (Kum. 1:15) Watu wa Mungu walihangaikiwa muzuri. Mufano ingine ni ya Eliya. Alikuwa ametumika kwa miaka mingi ili kusaidia Waisraeli wamutumikie Yehova. Lakini wakati wa Yehova wa kumupatia mugao mwingine ulifika, alimuhamisha kusini mwa Yuda. (2 Fa. 2:1; 2 Ny. 21:12) Watu waaminifu wa mu makabila kumi ya Israeli, walibakia bila muchungaji? Hapana. Eliya alikuwa amemuzoeza Elisha kwa miaka mingi. Kulikuwa pia “wana wa manabii,” wenye inawezekana walikuwa wamepangwa muzuri na walikuwa wamezoezwa. (2 Fa. 2:7) Kwa hiyo, kulikuwa wanaume wengi waaminifu wa kuongoza watu wa Mungu. Na kusudi ya Yehova iliendelea mbele na alihangaikia waabudu wake waaminifu.

Musa (picha ya kushoto) na Eliya (picha ya kuume), kila mumoja wao alizoeza muzuri sana mwanaume mwenye alikamata nafasi yake (Ona fungu ya 12)


13. Mu Waebrania 13:5b muko maneno gani yenye kutia moyo? (Ona pia picha.)

13 Wakati unafikiria ile mifano, unawaza ni mambo gani njo itatokea wakati mutiwa-mafuta wa mwisho ataenda mbinguni? Hatuna hata lazima ya kujiuliza-uliza. Biblia inatufunulia kweli fulani ya mwepesi na yenye kutia moyo: Yehova hatatupa hata kidogo watu wake ku dunia. (Soma Waebrania 13:5b.) Kama Musa na Eliya, kikundi kidogo ya Wakristo watiwa-mafuta wenye kuongoza leo, wanajua kama ni jambo ya maana sana kuzoeza wengine. Kwa miaka mingi ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wako nazoeza wanaume fulani kati ya kondoo wengine ili waweze kuongoza. Kwa mufano, wametayarisha masomo mbalimbali ili kuzoeza wazee, waangalizi wenye kusafiri, ndugu wa mu Halmashauri ya Tawi, waangalizi ku Beteli, na wengine. Baraza Yenye Kuongoza iko nazoeza moja kwa moja wasaidizi wa mu halmashauri mbalimbali za Baraza Yenye Kuongoza. Leo wale wasaidizi wako nashugulikia madaraka makubwa mu tengenezo. Wametayarishwa muzuri ili waendeleze kazi ya kuhangaikia kondoo wa Kristo.

Baraza Yenye Kuongoza imetumika sana ili kuzoeza wasaidizi na kutayarisha masomo mbalimbali ili kuzoeza wazee, waangalizi wenye kusafiri, ndugu wa Halmashauri za Tawi, waangalizi ku Beteli, na wamisionere mu dunia yote (Ona fungu ya 13)


14. Wazo kubwa ya mazungumuzo yetu ni nini?

14 Wazo kubwa ya mazungumuzo yetu ni hii: Wakati mutiwa-mafuta wa mwisho ataenda mbinguni karibu na mwisho wa taabu kubwa, ibada safi itaendelea ku dunia. Chini ya uongozi wa Yesu Kristo, waabudu wa Yehova wataendelea kumutumikia. Ni kweli kwamba, ile wakati, tutashambuliwa na Gogu wa Magogu, muungano wa mataifa wenye kutuchukia. (Eze. 38:18-20) Lakini ile shambulio ya muda mufupi haitakuwa na matokeo; haitazuia watu wa Mungu kumuabudu Yehova. Bila shaka atawakomboa! Mu maono, mutume Yohana aliona “kundi kubwa” ya kondoo wengine wa Kristo. Yohana aliambiwa kama wale wenye kuwa mu ile “kundi kubwa” wanatoka “katika ile taabu kubwa.” (Ufu. 7:9, 14) Kwa kweli, tunajua kama Yehova atawaokoa!

15-16. Kulingana na Ufunuo 17:14, watiwa-mafuta wa Kristo watafanya nini wakati wa vita ya Armagedoni, na juu ya nini ile inatia moyo?

15 Lakini, Wakristo fulani wanaweza kujiuliza: ‘Mambo itakuwa namna gani juu ya watiwa-mafuta? Watafanya nini kisha kuenda mbinguni?’ Biblia inajibia moja kwa moja ile maulizo. Inaonyesha kama serikali za huu ulimwengu ‘zitapigana na Mwana-Kondoo.’ Bila shaka, hazitapata ushindi. Biblia inasema hivi: “Mwana-Kondoo atawashinda.” Na ni nani watamusaidia? Ile andiko inatoa jibu. Wale wenye “waliitwa,” ‘walichaguliwa,’ na “wenye kuwa waaminifu.” (Soma Ufunuo 17:14.) Ni nani? Ni Wakristo watiwa-mafuta wenye kufufuliwa! Kwa hiyo, wakati mutiwa-mafuta wa mwisho ku dunia ataenda mbinguni, karibu na mwisho wa taabu kubwa, mugao wa kwanza kati ya migao yenye watiwa-mafuta watapewa, itakuwa kupigana. Ule ni mugao wa ajabu sana! Wamoja kati ya Wakristo watiwa-mafuta walikuwa napigana mbele wakuwe Mashahidi wa Yehova. Na hata wengine walitumika mu jeshi ya huu ulimwengu. Lakini wakakuwa Wakristo wa kweli na wakajifunza njia ya amani. (Gal. 5:22; 2 Te. 3:16) Waliacha kabisa kuunga mukono mambo ya vita. Lakini, kisha kufufuliwa watatumika pamoja na Kristo na malaika watakatifu ili kupiganisha maadui wa Mungu ku vita ya mwisho.

16 Waza kidogo: Ku dunia, Wakristo fulani watiwa-mafuta walishazeeka na hata ni wazaifu. Lakini wakati watafufuliwa ili kuishi mbinguni, watakuwa viumbe wa roho wenye nguvu na wenye hawawezi kufa. Watapewa mugao wa kupigana vita wakiwa pamoja na Mufalme Mupiganaji-Vita, Yesu Kristo. Kisha kupigana vita ya Armagedoni, watatumika pamoja na Yesu ili kusaidia wanadamu wakuwe wakamilifu. Kwa kweli, wakati watakuwa mbinguni, watafanyia ndugu na dada zao wapendwa mambo mingi ya muzuri yenye hawangeweza kuwafanyia wakati walikuwa wanadamu wenye hawakamilike!

17. Ni nini inaonyesha kama watumishi wote wa Mungu watakuwa salama wakati wa vita ya Armagedoni?

17 Uko kati ya kondoo wengine? Kama ni vile, utafanya nini wakati vita ya Armagedoni itaanza? Jambo ya kufanya ni ya mwepesi: Umutumainie Yehova na ufuate muongozo wake. Ile inaweza kumaanisha nini? Biblia inasema hivi: “Muingie katika vyumba vyenu vya ndani, na mufunge milango nyuma yenu. Mujifiche kwa wakati mufupi mupaka kasirani kali ipite.” (Isa. 26:20) Watumishi wote waaminifu wa Mungu, mbinguni na ku dunia, watakuwa salama mu ile wakati. Kama mutume Paulo, tuko hakika kama hata “serikali ao mambo yenye kuwa sasa ao mambo yenye yatakuja . . . havitaweza kututenganisha na upendo wa Mungu.” (Ro. 8:38, 39) Sikuzote ukumbuke kama Yehova anakupenda, na hatakutupa hata kidogo!

WAKATI MUTIWA-MAFUTA WA MWISHO ATAENDA MBINGUNI,

  • ni mambo gani njo itatokea?

  • juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama ibada safi haitachafuliwa?

  • juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova atahangaikia watu wake?

WIMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Yangu