Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 6

WIMBO 10 Tumusifu Yehova Mungu Wetu!

“Musifu Jina la Yehova”

“Musifu Jina la Yehova”

“Mumusifu, ninyi watumishi wa Yehova, musifu jina la Yehova.”ZB. 113:1.

WAZO KUBWA

Kuonyesha mambo yenye inatuchochea kusifu jina takatifu ya Yehova kila wakati.

1-2. Ni nini inaweza kutusaidia kuelewa namna Yehova anajisikia wakati mambo ya uongo inasemwa juu ya jina yake?

 WAZIA hii mufano: Mutu fulani mwenye unapenda anasema jambo fulani ya mubaya sana juu yako. Unajua kama mambo yenye alisema ni ya uongo; lakini watu fulani wanaiamini. Na jambo ya kuhuzunisha zaidi ni kwamba, wanaanza hata kuielezea wengine, na watu wengine wengi wanaiamini pia. Utajisikia namna gani? Ikiwa unahangaikia watu na unahangaikia namna wengine wanakuona, ule uongo utafanya ujisikie mubaya sana, haiko vile?—Mez. 22:1.

2 Ile mufano inatusaidia kuelewa namna Yehova alijisikia wakati jina yake ilichafuliwa. Mumoja kati ya malaika wake aliambia mwanamuke wa kwanza, Eva, mambo ya uongo kumuhusu. Eva aliamini ule uongo. Ule uongo ulifanya wazazi wetu wa kwanza wamuasi Yehova. Na ile ikafanya zambi na kifo viingie mu familia ya wanadamu. (Mwa. 3:1-6; Ro. 5:12) Magumu yote yenye tunaona mu dunia leo, ni kusema kifo, vita, maisha ya mateso, yote ilianza kwa sababu ya ule uongo wenye Shetani alianzisha mu bustani ya Edeni. Ule uongo na matokeo ya ule uongo vinamuumiza Yehova? Bila shaka. Lakini Yehova hakaziake akili mambo ya mubaya, ao kuweka kinyongo. Biblia inasema kama anaendelea kuwa “Mungu mwenye furaha.”—1 Ti. 1:11.

3. Tuko na pendeleo gani?

3 Tuko na pendeleo ya kuchangia kutakasa jina ya Yehova kwa kutii hii amri: “Musifu jina la Yehova.” (Zb. 113:1) Tunafanya vile kwa kusema mambo ya muzuri juu ya mwenye ile jina. Na weye utafanya vile? Tuchunguze basi mambo tatu yenye itatuchochea kabisa kusifu jina ya Mungu wetu kwa moyo wote.

TUNAMUFURAHISHA YEHOVA WAKATI TUNASIFU JINA YAKE

4. Juu ya nini Yehova anafurahi wakati tunamusifu? Toa mufano. (Ona pia picha.)

4 Tunamufurahisha Baba yetu wa mbinguni wakati tunasifu jina yake. (Zb. 119:108) Ni kusema kama Mungu Mweza-Yote, iko sawa vile wanadamu wenye hawakamilike, wenye wanapenda kusifiwa ili watiwe moyo ao ili waweze kujitumainia? Hapana. Fikiria hii mufano: Mutoto mudogo mwanamuke anakumbatia baba yake kwa upendo na kumuambia hivi: “Weye njo papa wa muzuri sana mu dunia yote!” Ile tendo yenye mutoto wake alifanya kwa kujipendea inafurahisha sana baba yake na inamugusa moyo. Juu ya nini? Tunaweza kusema kama ni juu ule baba ni mutu mwenye hajitumainie na anapenda sana kusifiwa ao hata iko na lazima ya sifa kutoka kwa mutoto wake juu ajisikie muzuri? Hapana. Lakini, tuko hakika kama ni baba mwenye nguvu, mwenye anafurahi kuona mutoto wake mwanamuke anamuonyesha upendo na shukrani. Anajua kama kuonyesha upendo na shukrani kutasaidia mutoto wake akuwe na furaha wakati ataendelea kukomaa. Sawa ule baba, zile njo sababu zenye zinafanya Yehova, Baba mukubwa zaidi, afurahi wakati tunamusifu.

Sawa vile baba anafurahi wakati mutoto wake anamuonyesha kama anamupenda na anamuonyesha shukrani, Yehova anafurahi wakati tunasifu jina yake (Ona fungu ya 4)


5. Wakati tunasifu jina ya Yehova tunasaidia kujibia mashitaka gani ya uongo?

5 Wakati tunasifu Baba yetu wa mbinguni tunasaidia kuonyesha kama jambo yenye Shetani anasema juu ya kila mumoja wetu ni ya uongo. Shetani anasema kama hakuna mwanadamu mwenye atatetea kwa ushikamanifu jina ya Mungu. Anasema pia kama hakuna hata mumoja wetu mwenye kuwa mushikamanifu. Tena anasema kama siye wote tutamukatala Mungu ikiwa tunaona kuwa kufanya vile kutatuletea faida. (Yob. 1:9-11; 2:4) Lakini Yobu mutumishi muaminifu wa Yehova alionyesha kama Shetani ni muongo. Halafu weye? Kila mumoja wetu iko na pendeleo ya kutetea jina ya Baba yetu kwa ushikamanifu na kumufurahisha kwa kumutumikia kwa ushikamanifu. (Mez. 27:11) Ile ni pendeleo kubwa sana.

6. Namna gani tunaweza kuiga Mufalme Daudi na Walawi? (Nehemia 9:5)

6 Watu waaminifu wanamupenda Mungu, na ile inawachochea wasifu jina yake kwa moyo wote. Mufalme Daudi aliandika hivi: “Acha nimusifu Yehova; acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.” (Zb. 103:1) Daudi alielewa kama kusifu jina ya Mungu ni kumusifu Mungu mwenyewe. Jina ya Mungu, Yehova, inamaanisha mambo mingi, inatukumbusha sifa zake za muzuri, na matendo yake ya ajabu. Daudi aliona jina ya Baba yake kuwa takatifu na aliisifu. Alipenda kufanya vile kwa “kila kitu chenye kuwa ndani” yake, ni kusema, kwa moyo wote. Kuhusu kumusifu Yehova, Walawi njo walikuwa ku mustari wa mbele. Kwa unyenyekevu, walikubali kama maneno yao haingeweza kusifu jina ya Yehova kwa ukamili vile inastahili. (Soma Nehemia 9:5.) Bila shaka, ile sifa yenye kutoka ku moyo na yenye kufanywa kwa unyenyekevu, ilifurahisha moyo wa Yehova.

7. Namna gani tunaweza kumusifu Yehova mu mahubiri na mu maisha yetu ya kila siku?

7 Leo, tunaweza kumusifu Yehova kwa kuzungumuza kwa upendo, kwa shukrani, na kwa uchangamufu kumuhusu. Wakati tuko mu mahubiri, tunakumbuka kama kusudi yetu kubwa ni kusaidia watu wamukaribie Yehova, na kuwasaidia waone Baba yetu mwenye upendo vile siye tunamuona. (Yak. 4:8) Tunafurahia kuonyesha watu mambo yenye Biblia inasema juu ya Yehova, namna inafunua upendo wake, haki, hekima, nguvu, na sifa zake zingine za muzuri. Pia tunamusifu Yehova na kumufurahisha wakati tunajikaza kumuiga. (Efe. 5:1) Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko tofauti na watu wa mu huu ulimwengu. Watu wanaweza kuona namna tuko tofauti na wanaweza kutuuliza ni juu ya nini tuko vile. (Mt. 5:14-16) Na wakati tuko nao mu maisha yetu ya kila siku, tunaweza kuwafasiria juu ya nini tunatendaka vile. Matokeo ni kwamba, watu wenye moyo muzuri wanachochewa kumukaribia Yehova. Wakati tunasifu Yehova mu zile njia, tunafurahisha sana moyo wake.—1 Ti. 2:3, 4.

TUNAMUFURAHISHA YESU WAKATI TUNASIFU JINA YA MUNGU

8. Namna gani Yesu alionyesha mufano muzuri zaidi wakusifu jina ya Yehova?

8 Kati ya viumbe wote wenye akili wenye kuwa mbinguni na ku dunia, hakuna mwenye anamujua Baba muzuri zaidi kupita Mwana. (Mt. 11:27) Yesu anapenda Baba yake, na amefanya yake yote ili kusifu jina ya Yehova. (Yoh. 14:31) Mu sala yenye alitoa kwa Baba yake usiku wenye ulitangulia kifo yake, alionyesha jambo ya maana zaidi yenye alifanya. Alisema hivi: “Nimewajulisha jina lako.” (Yoh. 17:26) Ile maneno iko na maana gani?

9. Yesu alitumia mufano gani ili kufasiria waziwazi namna Baba yake iko?

9 Yesu hakuambia tu watu kama jina ya Mungu ni Yehova. Wayahudi wenye Yesu alifundisha, tayari walikuwa najua jina ya Mungu. Lakini Yesu alikuwa ule ‘mwenye . . . alieleza juu Yake.’ (Yoh. 1:17, 18) Kwa mufano, Maandiko ya Kiebrania inaonyesha kama Yehova iko na rehema na huruma. (Kut. 34:5-7) Yesu alisaidia watu waelewe zaidi ile kweli wakati alieleza mufano wa mwana mupotevu na baba yake. Wakati tunasoma namna ule baba aliona mutoto wake “wakati alikuwa angali mbali,” namna alikimbia ili kukutana naye, namna alimukumbatia, na kumusamehe kwa moyo wote, tunaelewa muzuri zaidi rehema na huruma ya Yehova. (Lu. 15:11-32) Yesu alionyesha waziwazi Baba yake ni mutu wa namna gani.

10. (a) Tunajua namna gani kama Yesu alitumia jina ya kipekee ya Baba yake na alipenda wengine pia wafanye vile? (Marko 5:19) (Ona pia picha.) (b) Yesu anapenda tufanye nini leo?

10 Yesu alipenda watu wengine pia watumie jina ya kipekee ya Baba yake? Ndiyo kabisa. Wakubwa fulani wa dini wa ile wakati walisema kama juu jina ya Mungu ilikuwa takatifu sana, haikupaswa kutajwa. Lakini Yesu hakuruhusu ile mafundisho yenye haikupatana na Maandiko imuzuie kutukuza jina ya Baba yake. Fikiria wakati aliponyesha mwanaume mwenye alikuwa na pepo wachafu mu eneo ya Wagerasene. Watu waliogopa sana na wakamuomba Yesu atoke mu eneo yao. Kwa hiyo hakubakia mu ile eneo. (Mk. 5:16, 17) Lakini, Yesu alipenda watu wa mu ile eneo wajue jina ya Mungu. Kwa hiyo aliambia ule mwanaume mwenye aliponyesha aambie watu mambo yenye Yehova alikuwa amefanya, hapana mambo yenye yeye alikuwa amefanya. (Soma Marko 5:19.) a Leo pia Yesu anapenda jina ya Baba yake ijulikane mu dunia yote! (Mt. 24:14; 28:19, 20) Wakati tunasaidia wengine wajue jina ya Yehova, tunafurahisha Yesu, Mufalme wetu.

Yesu aliamuru ule mwanaume mwenye alikuwa na pepo wachafu, aambie watu namna Yehova alimusaidia (Ona fungu ya 10)


11. Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali kuhusu nini, na juu ya nini ile ni ya maana? (Ezekieli 36:23)

11 Yesu alijua kama kusudi ya Yehova ni kutakasa jina yake, ni kusema kuonyesha kama mambo mingi yenye imesemwa juu yake ni ya uongo. Njo maana Bwana wetu alifundisha wanafunzi wake kusali hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.” (Mt. 6:9) Yesu alielewa kama ile njo jambo ya maana zaidi mu ulimwengu wote. (Soma Ezekieli 36:23.) Kati ya viumbe wote wenye akili, Yesu njo amefanya mambo mingi sana ili kutakasa jina ya Yehova. Hata kama alifanya ile mambo yote, wakati alikamatwa, maadui wake walimushitaki nini? Walisema kama alimutukana Mungu! Kwa kweli, Yesu aliona kama kutukana ao kusema mubaya juu ya jina takatifu ya Baba yake njo zambi ya mubaya sana. Kuona kama alishitakiwa na kuhukumiwa kuwa alimutukana Mungu, kulimuumiza sana. Inawezekana ile njo sababu kubwa yenye ilifanya Yesu akuwe “katika maumivu makali” saa fulani mbele akamatwe.—Lu. 22:41-44.

12. Namna gani Yesu alitakasa jina ya Baba yake mu njia kubwa zaidi?

12 Juu ya kutakasa jina ya Baba yake, Yesu alivumilia wakati aliteswa, wakati alitukanwa, na kushitakiwa mambo ya uongo. Alijua kama alikuwa amemutii Baba yake mu mambo yote; hakukuwa na sababu ya kusikia haya. (Ebr. 12:2) Alijua kama Shetani alikuwa namujaribu moja kwa moja mu ile wakati ya nguvu sana. (Lu. 22:2-4; 23:33, 34) Shetani alitumainia kama Yesu atavunja ushikamanifu wake, lakini mambo haikukuwa vile hata kidogo! Yesu alionyesha waziwazi kama Shetani ni muongo kabisa na kama Yehova iko na watumishi washikamanifu wenye wanaendelea kuwa washikamanifu hata wakati wanapatwa na majaribu ya nguvu sana!

13. Unaweza kufanya nini ili kufurahisha Mufalme wako mwenye iko natawala?

13 Na weye unapenda kumufurahisha Mufalme wetu mwenye iko natawala? Endelea kusifu jina ya Yehova kwa kusaidia wengine wajue Mungu wetu iko namna gani. Wakati unafanya vile, unafuata hatua za Yesu. (1 Pe. 2:21) Kama Yesu, uko namufurahisha Yehova na kuonyesha kama adui yake Shetani ni muongo kabisa!

TUNASAIDIA WATU WAOKOKE WAKATI TUNASIFU JINA YA YEHOVA

14-15. Wakati tunafundisha watu kuhusu Yehova, tunaweza kupata matokeo gani ya muzuri?

14 Wakati tunasifu jina ya Yehova, tunasaidia watu waokoke. Namna gani? Shetani “amepofusha akili za wenye hawaamini.” (2 Ko. 4:4) Matokeo ni kwamba, watu wengi wanafikia kuamini mambo ya uongo yenye Shetani anasema. Mambo sawa vile Mungu hakuwake, Mungu iko mbali sana na haangaikie wanadamu, Mungu hana huruma na anatesa watenda-zambi milele. Ile mambo yote ya uongo iko na kusudi ya kuchafua jina ya Yehova na kufanya watu wasipende kumukaribia. Lakini wakati tunahubiri, tunafanya Shetani asifikie kusudi yake. Tunafundisha watu kweli kuhusu Baba yetu, na kusifu jina takatifu ya Mungu wetu. Matokeo inakuwa nini?

15 Mafundisho ya kweli yenye kuwa mu Neno ya Mungu iko na nguvu mingi. Wakati tunafundisha watu kuhusu Yehova na namna anakuwaka kabisa, tunawasaidia wapate jambo fulani ya ajabu sana. Kitambaa ya mafundisho ya uongo yenye Shetani anawafunika, inaanza kutoka polepole na wale watu wanaanza kuona baba yetu mwenye upendo sawa vile tunamuonaka. Wanabakia kinywa wazi wakati wanafikiria nguvu yake yenye haina mipaka. (Isa. 40:26) Wanajifunza kumutumainia Yehova kwa sababu ya haki yake kamilifu. (Kum. 32:4) Wanajifunza mambo mingi sana kupitia hekima yake yenye haina mipaka. (Isa. 55:9; Ro. 11:33) Na wanatiwa moyo kujua kama yeye ni upendo. (1 Yo. 4:8) Kadiri wanaendelea kumukaribia Yehova, ni vile tumaini yao ya kuishi milele kama watoto wake inakuwa hakika kabisa. Tuko na pendeleo kubwa sana ya kusaidia watu wamukaribie Baba yao! Wakati tunafanya vile, Yehova anatuona kuwa “wafanyakazi pamoja” naye.—1 Ko. 3:5, 9.

16. Wakati watu fulani wanajifunza kuhusu jina ya Mungu wanajisikia namna gani? Toa mufano.

16 Ku mwanzo, tunaweza tu kufundisha watu kama jina ya Mungu ni Yehova. Ile tu inaweza kugusa mutu mwenye moyo muzuri. Kwa mufano, kijana mwanamuke mwenye kuitwa Aaliyah b alikomalia mu familia yenye haiko ya Wakristo. Mu dini yenye alikuwa ndani, alijisikia kuwa anakosa jambo fulani na hakujisikia kuwa karibu na Mungu. Lakini mambo ilibadilika wakati alianza kujifunza pamoya na mashahidi wa Yehova. Alianza kumuona Mungu kuwa rafiki yake. Alishangaa kujua kama jina ya Mungu ilikuwa imeondolewa mu Biblia za mingi na majina ya cheo sawa vile Bwana ikawekwa pa nafasi ya jina ya Mungu. Kujua jina ya Mungu kulibadilisha maisha yake. Alisema hivi: “Rafiki yangu mukubwa zaidi iko na jina!” Matokeo ilikuwa nini? Anasema hivi: “Sasa niko na amani mingi ya moyo. Naona kama niko na pendeleo kubwa sana.” Mwanaume mwenye kuitwa Steve alikuwa mwanamuziki mwenye alikomalia mu familia ya Wayahudi wenye kushikilia sana desturi zao. Hakupenda kuwa mu dini yoyote yenye kujulikana juu aliona kama mulikuwa unafiki mwingi. Mu kipindi fulani wakati alikuwa na huzuni, alikubali kukaa na kusikiliza wakati Shahidi fulani wa Yehova alikuwa naongoza funzo ya Biblia. Aliguswa sana kujua kama Mungu iko na jina. Anasema hivi: “Sikukuwa nilishafundishwa jina ya Mungu. Kwa mara ya kwanza, nilielewa kama Mungu ni mutu wa kweli kabisa. Ile wakati nilielewa kama nimepata Rafiki.”

17. Juu ya nini unaazimia kuendelea kusifu jina ya Yehova? (Ona pia picha.)

17 Wakati uko nahubiri na wakati uko nafundisha, unaambiaka wengine jina takatifu ya Mungu, ni kusema Yehova? Unawasaidiaka waelewe Mungu wetu ni mutu wa namna gani kabisa. Wakati unafanya vile, unasifu jina ya Mungu. Uendelee basi kusifu jina takatifu ya Yehova, kwa kusaidia watu wajue yeye ni nani kabisa. Kama unafanya vile, utasaidia wengine waokoke. Utafuata mufano wa Mufalme wako Kristo Yesu. Zaidi ya yote, utamufurahisha Baba yako mwenye upendo, Yehova. Basi, “usifu jina lake milele na milele.”—Zb. 145:2.

Tunasifu jina ya Yehova wakati tunafundisha watu ile jina na kuwaonyesha Yehova ni mutu wa namna gani (Ona fungu ya 17)

NAMNA GANI KUSIFU JINA YA MUNGU . . .

  • kunamufurahisha Yehova?

  • kunamufurahisha Kristo Yesu?

  • kunasaidia kuokoa wengine?

WIMBO 2 Jina Yako Ni Yehova

a Kuko ushuhuda wenye kuonyesha kabisa kama wakati Marko aliandika Injili yake, alitumia jina ya Mungu mu hii maneno yenye Yesu alisema. Njo maana imerudishwa mu Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

b Majina fulani imebadilishwa.