Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 7

WIMBO 51 Ninajitoa kwa Mungu!

Mufano wa Wanaziri Unaweza Kutufundisha Nini?

Mufano wa Wanaziri Unaweza Kutufundisha Nini?

“Yeye ni mutakatifu kwa ajili ya Yehova siku zote za Unaziri wake.”HES. 6:8.

WAZO KUBWA

Namna mufano wa Wanaziri unaweza kutusaidia tumutumikie Yehova kwa uhodari na roho ya kujitoa.

1. Ni muelekeo gani wa muzuri wenye waabudu wa Yehova wameonyesha tangu zamani?

 UNAFURAHIA sana uhusiano wenye uko nao pamoya na Yehova? Bila shaka unaufurahia! Na haiko weye peke. Tangu zamani, watu wengi wamefurahia uhusiano wao pamoya na Yehova. (Zb. 104:33, 34) Wengi wamejitoa sana ili kumuabudu. Ni vile Wanaziri wa mu Israeli ya zamani walifanya. Wanaziri walikuwa nani, na mufano wao unaweza kutufundisha nini?

2. (a) Wanaziri walikuwa nani? (Hesabu 6:1, 2) (b) Juu ya nini Waisraeli fulani walitoa naziri ya kuwa Wanaziri?

2 Neno “Munaziri” inatokana na neno ya Kiebrania yenye inamaanisha “Mwenye Alitengwa,” ao“Mwenye Aliwekwa Pembeni,” ao “Mwenye Alitolewa kwa Mungu.” Ile neno ilitumiwa ili kuzungumuzia Waisraeli wenye bidii wenye walijitoa wenyewe ili kumutumikia Yehova mu njia ya pekee. Sheria ya Musa iliruhusu mwanaume ao mwanamuke afanye naziri ya pekee kwa Yehova kwa kuchagua kuwa Munaziri kwa kipindi fulani ya wakati. a (Soma Hesabu 6:1, 2.) Wakati Mwisraeli alifanya ile naziri ao ahadi, alipaswa kufuata maagizo yenye Waisraeli wengine hawakulazimika kufuata. Juu ya nini sasa Mwisraeli alichagua kuwa Munaziri? Inawezekana kabisa kama Mwisraeli mwenye alifanya vile alichochewa na upendo wake kwa Yehova, na alipenda kumuonyesha shukrani kwa sababu ya baraka zake za mingi.—Kum. 6:5; 16:17.

3. Namna gani watu wa Mungu leo wako sawa vile Wanaziri?

3 Mupango wa Unaziri ulifikia mwisho wakati “sheria ya Kristo” ilikamata nafasi ya Sheria ya Musa. (Gal. 6:2; Ro. 10:4) Lakini, sawa Wanaziri, watu wa Yehova leo wanaendelea kuonyesha kama wanapenda kabisa kumutumikia Yehova kwa moyo wote, nafsi yote, akili yote, na nguvu yote. (Mk. 12:30) Kwa kujipendea tunafanya naziri ya kumutumikia Yehova wakati tunajitoa kwake. Ili kuheshimia ile naziri, tunapaswa kuishi kulingana na mapenzi ya Yehova na kujitoa kumutumikia. Wakati tutakuwa nachunguza namna Wanaziri waliheshimia naziri yao, tutajifunza mambo fulani ya maana yenye itatusaidia siye pia tuheshmie naziri yetu. b (Mt. 16:24) Tuone basi mifano fulani.

UKUWE TAYARI KUJITOA

4. Kulingana na Hesabu 6:3, 4, munaziri alijiima mambo gani?

4 Soma Hesabu 6:3, 4. Wanaziri walipaswa kuepuka divai na vinywaji vyenye kutengenezwa na zabibu ao tini. Watu wenye waliwazunguka walizoea kunywa vile vinywaji, na kufanya vile haikukuwa makosa. Biblia inasema kama “divai yenye inafanya moyo wa mwanadamu ufurahi” ni zawadi kutoka kwa Mungu. (Zb. 104:14, 15) Hata vile, kwa kujipendea Wanaziri walijiima haki yao ya kutumia vile vitu. c

Uko tayari kujiima sawa Wanaziri? (Ona fungu ya 4-6)


5. Madián na Marcela waliamua kujiima mambo gani, na juu ya nini?

5 Sawa Wanaziri, siye pia tunajitoa ili kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Fikiria mufano wa Madián na Marcela. d Wale bibi na bwana Wakristo hawakukuwa nakosa kitu. Madián alikuwa na kazi ya muzuri yenye iliwasaidia waishi mu nyumba ya muzuri. Lakini, walipenda kumutumikia Yehova zaidi. Ili kufikia muradi wao, waliamua kufanya mabadiliko fulani. Wanasema hivi: “Tulianza kupunguza garama zetu, tulihamia mu nyumba ya kidogo na tukauzisha gari yetu.” Madián na Marcela hawakulazimika kujiima vile. Walichagua kufanya vile juu waweze kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Wanatosheka na wako wenye furaha kwa sababu ya maamuzi yenye walikamata.

6. Juu ya nini Wakristo leo wanajiima mambo mbalimbali? (Ona pia picha.)

6 Wakristo leo wanafurahia kujiima mambo mbalimbali ili wapate wakati mingi ya kufanya kazi mbalimbali za kiteokrasi. (1 Ko. 9:3-6) Yehova hatuombe tujiime ile mambo; na mambo yenye tunajiima haiko ya mubaya. Kwa mufano, Wakristo fulani wanaacha kazi ya muzuri, nyumba, na wanyama wao wenye wanapenda sana. Wengi wamechagua kubakia bila kuoa ao kuolewa kwa wakati fulani ao kubakia bila kuzaa watoto. Wengine wameamua kutumikia fasi kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, hata kama ile inawaomba waende mbali na wapendwa wao. Wengi wetu wanajiima vile kwa sababu wanapenda kumutumikia Yehova kwa nguvu yao yote. Ukuwe hakika kama Yehova anafurahi sana kuona vile unajitoa sana ili kumutumikia, ikuwe mambo yenye unajiima ni ya kidogo ao ni ya mingi.—Ebr. 6:10.

UKUWE TAYARI KUWA TOFAUTI

7. Ni nini ingefanya ikuwe nguvu kwa Munaziri kuheshimia naziri yake? (Hesabu 6:5) (Ona pia picha.)

7 Soma Hesabu 6:5. Wanaziri hawakupaswa kukata nywele zao. Ile ilikuwa njia ya kuonyesha kama wanajitiisha kabisa kwa Yehova. Kama Mwisraeli angekuwa Munaziri kwa muda murefu, nywele zake zingekuwa za murefu na wengine wangeona ile. Na kama wenye walimuzunguka waliunga mukono Unaziri wake, ile haingekuwa shida. Lakini, jambo ya kuhuzunisha ni kwamba mu historia ya Israeli, wakati fulani watu hawakuheshimia Wanaziri na hawakuwaunga mukono. Wakati wa nabii Amosi, Waisraeli waasi ‘waliendelea kupatia Wanaziri divai ili wakunywe.’ Inawezekana walifanya vile ili kujaribu kuwachochea wavunje naziri yao ya kuepuka divai. (Amo. 2:12) Wakati fulani, iliomba Wanaziri wakuwe na uhodari ili waheshimie naziri yao na wakuwe tofauti.

Munaziri mwenye aliheshimia unaziri wake alikuwa tayari kuwa tofauti (Ona fungu ya 7)


8. Mufano wa kijana Benjamin unakutia moyo namna gani?

8 Kwa musaada wa Yehova, siye pia tunaweza kuwa hodari na kuwa tofauti, hata kama tunakuwaka watu wa haya-haya. Fikiria mufano wa Benjamin, Shahidi wa Yehova wa miaka kumi wa mu inchi ya Norvège. Ku masomo yao kulikuwa tukio ya kuunga mukono watu wa Ukraine kwa sababu ya vita. Watoto waliombwa waimbe nyimbo na walivaa nguo za rangi ya bendera ya Ukraine. Benjamin aliamua kama ili kuepuka ile tukio ya kitaifa atasimama mbali na fasi kwenye ile tukio ingefanywa. Lakini, mwalimu wake alimuona na kumuambia hivi kwa sauti kubwa: “Unapaswa kuya na kujiunga na siye. Siye wote tuko nakungoya!” Kwa uhodari Benjamin alikaribia mwalimu wake na kumuambia hivi: “Siunge mukono upande wowote, na sijiingize mu mambo ya politike. Njo maana Mashahidi wa Yehova wengi wako mu gereza kwa sababu wanakatala kuunga mukono vita.” Mwalimu wake alielewa ile mafasirio na akamuruhusu asiingie mu ile tukio. Lakini, wanafunzi wenzake walianza kumuuliza juu ya nini hajiunge nao. Benjamin alijisikia mubaya mupaka akatafuta kulia; lakini, kwa uhodari aliambia wanafunzi wote mambo yenye alikuwa amemuambia mwalimu. Kisha, Benjamin aliambia wazazi wake kama aliona kuwa ni Yehova njo alimusaidia atetee imani yake.

9. Tunaweza kufanya nini ili kufurahisha moyo wa Yehova?

9 Juu tunachagua kufanya mapenzi ya Yehova, tunakuwa tofauti na watu wenye wanatuzunguka. Inaomba uhodari ili kuambia wengine ku masomo ao ku kazi kama siye ni Mashahidi wa Yehova. Na juu watu wa mu hii dunia wanaendelea kuwa na muelekeo na mwenendo mubaya zaidi, inaweza kuwa nguvu zaidi kuishi kulingana na kanuni za Biblia na kuhubiria wengine habari njema. (2 Ti. 1:8; 3:13) Lakini, kila siku ukumbuke kama ‘tunafurahisha moyo [wa Yehova]’ wakati kwa uhodari, tunakuwa tofauti na wale wenye hawamutumikie.—Mez. 27:11; Mal. 3:18.

UTIE YEHOVA PA NAFASI YA KWANZA MU MAISHA YAKO

10. Juu ya nini ingekuwa nguvu sana kwa Munaziri kufuata muongozo wenye kuwa mu Hesabu 6:6, 7?

10 Soma Hesabu 6:6, 7. Wanaziri hawangepaswa kukaribia maiti. Ku mwanzo, tunaweza kuona kama kufanya vile haikukuwa kujitoa sana. Lakini ingekuwa nguvu sana kwa Munaziri kutii ile amri wakati mutu wa familia yake anakufa. Ile wakati, desturi za mazishi ziliomba mutu akuwe karibu na mutu mwenye kufa. (Yoh. 19:39, 40; Mdo. 9:36-40) Kwa sababu ya naziri yake, Munaziri hangefuata zile desturi. Hata wakati alipambana na hali ya huzuni sana mu familia, Munaziri alionyesha kama alikuwa na imani ya nguvu kwa kuheshimia naziri yake. Bila shaka Yehova alitia nguvu wale watumishi wake washikamanifu ili waweze kupambana na magumu mbalimbali.

11. Mukristo anapaswa kuwa tayari kufanya nini wakati iko nashugulikia mambo ya familia? (Ona pia picha.)

11 Juu tuko Wakristo, tunakamata kwa uzito naziri yetu ya kujitoa kwa Yehova. Ile inaonekana mu maamuzi yetu na mu namna tunashugulikia mambo mu familia. Tunajikaza kutimiza madaraka yetu mu familia, lakini hatuweke pa nafasi ya kwanza mambo yenye watu wa familia yetu wanapenda kuliko kufuata mambo yenye Yehova anatuomba. (Mt. 10:35-37; 1 Ti. 5:8) Wakati fulani, inaomba kukamata uamuzi wenye unamufurahisha Yehova hata kama watu wa familia yetu hawaufurahie.

Uko tayari kutia mapenzi ya Yehova pa nafasi ya kwanza hata mu hali za nguvu? (Ona fungu ya 11) e


12. Wakati Alexandru alishugulikia hali fulani mu familia, alifanya nini na aliepuka nini?

12 Fikiria mufano wa Alexandru na bibi yake Dorina. Kisha kujifunza Biblia kwa mwaka moya, Dorina aliamua kuacha kujifunza, na alipenda Alexandru naye aache kujifunza. Lakini, kwa upole na kwa busara Alexandru alimuambia kama ataendelea kujifunza. Dorina hakufurahia ile na alijaribu kumukaza aache kujifunza. Alexandru anasema kama alijaribu kumuelewa, lakini haikukuwa mwepesi. Wakati Dorina alikuwa namusema mubaya na kumujibu kwa ukali, wakati fulani alijisikia tu aache kujifunza Biblia. Lakini, Alexandru aliendelea kumutia Yehova pa nafasi ya kwanza, na mu ile wakati yote aliendelea kuonyesha bibi yake upendo na heshima. Ku mwisho, mufano wake muzuri ulichochea bibi yake aanze tena kujifunza Biblia, na akafikia kukubali kweli.—Ona ku jw.org video Alexandru na Dorina Vacar: “Upendo Ni Wenye Uvumilivu na Wenye Fazili” mu sehemu “Kweli Inabadilisha Maisha.”

13. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda Yehova na familia yetu?

13 Yehova njo alianzisha mupango wa familia, na anapenda tukuwe na familia yenye furaha. (Efe. 3:14, 15) Kama tunapenda kuwa na furaha ya kweli, tunapaswa kufanya mambo yenye Yehova anapenda. Siku zote ukuwe hakika kama Yehova anafurahi sana kuona namna uko najiima ili kumuabudu na wakati uleule unahangaikia watu wa familia yako na kuwatendea kwa upendo na heshima.—Ro. 12:10.

TUCHOCHEANE KUONYESHA ROHO YA UNAZIRI

14. Ni nani njo tupaswa kujikaza sana kutia moyo kupitia maneno yetu?

14 Wale wote wenye wanachagua kumutumikia Yehova leo wanapaswa kuwa tayari kujitoa kwa kupenda. Wakati fulani, kufanya vile haikuwake mwepesi. Namna gani tunaweza kuchocheana kuonyesha roho ya kujitoa? Kwa kutiana moyo kupitia maneno. (Yob. 16:5) Kuko mutu fulani mu kutaniko yenu mwenye iko najaribu kufanya maisha yake kuwa mwepesi ili ajitoe zaidi mu kazi mbalimbali za kiteokrasi? Unajua vijana fulani wenye kwa uhodari wanajikaza kuwa tofauti na wengine ku masomo, hata kama ni nguvu kufanya vile? Halafu wanafunzi wa Biblia na Wakristo wenzetu wenye wako najikaza sana ili kubakia waaminifu hata kama watu wa familia yao wako nawapinga? Tutumie kila nafasi ili kuambia wale waabudu wenzetu maneno yenye kutia moyo, na tuwaambie kama tunawapenda sana kwa sababu ya uhodari wao na roho yao ya kujitoa.—Flm. 4, 5, 7.

15. Wakristo fulani wamefanya nini ili kutegemeza wale wenye kuwa mu utumishi wa wakati wote?

15 Wakati fulani, tunaweza kutolea Wakristo wenye kuwa mu utumishi wa wakati wote musaada fulani. (Mez. 19:17; Ebr. 13:16) Ni vile dada fulani wa Sri Lanka alipenda kufanya. Kwa sababu amezeeka na hawezi tena kutumika, alikuwa napokea kiasi fulani ya makuta, kisha hesabu ya ile makuta ikaongezwa. Alipenda kusaidia dada wawili vijana wenye walikuwa mapainia ili waendelee na utumishi wao hata kama kulikuwa matatizo ya kupata makuta. Kwa hiyo aliamua kama atakuwa natoa kiasi fulani ya makuta kila mwezi ili kulipia garama zao za telefone. Ule dada alionyesha roho ya kujitoa kabisa!

16. Mupango wa zamani wa Unaziri unaweza kutufundisha nini?

16 Kwa kweli, mufano wa Wanaziri wa zamani unaweza kutufundisha mambo mingi! Lakini, mupango wa Unaziri unatufundisha pia jambo fulani juu ya Baba yetu wa mbinguni, Yehova. Iko hakika kama tunapenda kumufurahisha na kama tuko tayari kujiima ili tuheshimie naziri yetu. Anatuheshimisha kwa kutupatia nafasi ya kuonyesha kama tunamupenda mu njia mbalimbali. (Mez. 23:15, 16; Mk. 10:28-30; 1 Yo. 4:19) Mupango wa unaziri unaonyesha kama Yehova anaona na anafurahi wakati tunajitoa sana ili kumutumikia. Basi, tuazimie kuendelea kumutumikia Yehova, kwa kumutolea nguvu yetu yote kwa kupenda.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Namna gani Wanaziri walijiima mambo mbalimbali na kuonyesha uhodari?

  • Tunaweza kuchocheana namna gani kuonyesha roho ya Unaziri leo?

  • Mupango wa Unaziri unatufundisha nini juu ya Yehova?

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

a Hata kama Wanaziri fulani waliwekwa na Mungu, inawezekana wengi walikuwa Waisraeli wenye walijitolea ili kuwa Wanaziri.—Ona kisanduku “ Wanaziri Wenye Waliwekwa na Yehova.”

b Wakati fulani, vichapo vyetu vinafananisha Wanaziri na wale wenye kuwa mu utumishi wa wakati wote. Lakini mu hii habari, tutaona namna watumishi wa Yehova wote wenye kujitoa kwake wanaweza kuonyesha roho ya Unaziri.

c Kwa ujumla, inaonekana kama hakuna maagizo ingine yenye Wanaziri walipaswa kufuata, sawa vile maagizo kuhusu kazi, ili kutimiza naziri yao.

d Ona ku jw.org habari “Tuliamua Kufanya Maisha Yetu Ikuwe Mwepesi” mu sehemu “Ushuhuda wa Mashahidi wa Yehova.”

e MAFASIRIO YA PICHA : Munaziri iko ku sehemu ya juu ya nyumba, iko naangalia wenye wanaenda kuzika mutu wa familia yake mwenye alikuwa napenda. Iko naangalilia kwa mbali juu ya kuheshimia naziri yake kwa Yehova.