Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uendelee Kuwa na Furaha Wakati Uko Namungojea Yehova kwa Uvumilivu

Uendelee Kuwa na Furaha Wakati Uko Namungojea Yehova kwa Uvumilivu

UKO nangojea kwa hamu siku yenye Yehova atatosha mambo yote ya mubaya na kufanya mambo yote kuwa mupya? (Ufu. 21:1-5) Bila shaka. Lakini haikuwake mwepesi sikuzote kuendelea kumungojea Yehova kwa uvumilivu, zaidi sana ikiwa tuko napambana na magumu. Wakati jambo yenye tunatumainia inakawia, ile inaweza kufanya moyo ugonjwe.—Mez. 13:12, maelezo ya chini.

Lakini, Yehova anapenda tumungojee kwa uvumilivu ili atende kwa wakati wenye ameweka. Juu ya nini anapenda vile? Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe na furaha wakati tuko nangojea?

JUU YA NINI YEHOVA ANAPENDA TUNGOJEE?

Biblia inasema hivi: “Yehova anawangojea kwa uvumilivu ili awaonyeshe wema, na atasimama ili kuwaonyesha rehema. Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki. Wenye furaha ni wale wote wenye wanaendelea kumungojea.” (Isa. 30:18) Ku mwanzo, Isaya aliandika ile maneno kwa ajili ya Wayahudi wenye walikuwa na kichwa nguvu. (Isa. 30:1) Lakini Wahayudi fulani walikuwa waaminifu na ile maneno iliwatolea tumaini. Ile maneno inatolea pia tumaini watumishi waaminifu wa Yehova leo.

Kwa hiyo tunapaswa kungojea kwa uvumilivu kwa sababu Yehova anangojea kwa uvumilivu. Ameweka wakati wenye ataharibu huu ulimwengu na iko nangoya ile siku na ile saa ifike. (Mt. 24:36) Ile wakati, itakuwa imeonekana wazi kama mashitaka yenye Shetani alimushitaki Yehova na watumishi wake ni ya uongo. Kisha Yehova atamutosha Shetani na wote wenye watajiunga naye. Lakini ‘atatuonyesha rehema.’

Mbele ile wakati ifike, inawezekana Yehova hatatosha magumu yetu, lakini anatuhakikishia kama tunaweza kuwa na furaha wakati tuko nangojea. Sawa vile Isaya alisema tunaweza kuwa na furaha wakati tuko nachunga ao tuko natumainia jambo fulani ya muzuri itokee. (Isa. 30:18) a Tunaweza kufanya nini juu tukuwe na furaha? Kuko mambo ine yenye inaweza kutusaidia.

NAMNA YA KUWA NA FURAHA WAKATI TUKO NANGOJEA

Kazia akili mambo ya muzuri. Mufalme Daudi aliona mambo mingi ya mubaya mu maisha yake. (Zb. 37:35) Lakini aliandika hivi: “Nyamaza mbele ya Yehova na umungojee kwa matumaini. Usikasirishwe na mutu mwenye anafanikiwa katika kutimiza mipango yake ya mubaya.” (Zb. 37:7) Daudi yeye mwenyewe alitumikisha ile mashauri kwa kukazia akili tumaini yake ya kuokolewa. Alikuwa pia mwenye shukrani juu ya baraka zote zenye Yehova alimupatia. (Zb. 40:5) Kama siye pia tunakazia akili mambo ya muzuri, hata tukuwe mu hali gani, na kuepuka kuhangaika sana kwa sababu ya mambo ya mubaya yenye iko natokea, itakuwa mwepesi zaidi kwetu kumungojea Yehova.

Tumia kila nafasi ili kumusifu Yehova. Muandikaji wa Zaburi ya 71, mwenye inaonekana ni Daudi, alimuambia hivi Yehova: “Nitaendelea kungojea; nitakusifu hata zaidi.” (Zb. 71:14) Angemusifu Yehova namna gani? Angeambia wengine kuhusu Yehova, na kumuimbia sifa. (Zb. 71:16, 23) Kama Daudi tunaweza kuwa na furaha wakati tuko namungojea Yehova. Tunamusifu wakati tunahubiri, mu maongezi yetu ya kila siku, na kupitia nyimbo zetu za ibada. Wakati utaimba tena wimbo fulani wa Ufalme, fikiria kwa uangalifu maneno ya ule wimbo, na namna inakuletea furaha.

Acha ndugu na dada zako wakutie moyo. Wakati Daudi alipambana na magumu, alimuambia hivi Yehova: “Mbele ya washikamanifu wako, nitatumainia jina lako.” (Zb. 52:9) Siye pia tunaweza kutiwa moyo na waabudu wenzetu washikamanifu, hapana tu ku mikutano ao mu mahubiri lakini pia wakati tunakutana pamoja ili kujifurahisha.—Ro. 1:11, 12.

Tia nguvu tumaini yako. Zaburi 62:5 inasema: “Ninamungojea Mungu kimya-kimya kwa sababu tumaini langu linatoka kwake.” Inaomba kuwa na tumaini yenye nguvu, zaidi sana ikiwa mwisho haukuye mbio sawa vile tulitazamia. Tunapaswa kuwa hakika kama ahadi za Yehova zitatimia, hata kama inaomba tuzingojee kwa muda gani. Tunaweza kutia nguvu tumaini yetu kwa kujifunza Neno ya Mungu. Kwa mufano, tunaweza kujifunza maunabii, namna Biblia inapatana, na mambo mbalimbali yenye Yehova anafunua juu yake. (Zb. 1:2, 3) Pia tunapaswa kuendelea ‘kusali tukiwa na roho takatifu’ ili tuendelee kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na Yehova wakati tuko nangojea ahadi yake ya kutupatia uzima wa milele itimie.—Yud. 20, 21.

Kama Daudi, ukuwe hakika kama Yehova anaona wale wenye wanaendelea kumungojea na anawaonyesha upendo mushikamanifu. (Zb. 33:18, 22) Endelea kumungojea Yehova kwa uvumilivu kwa kukazia akili mambo ya muzuri mu maisha yako, kwa kumusifu, kwa kuacha Mashahidi wenzako wakutie moyo, na kwa kuendelea kutia nguvu tumaini yako.

a Mu luga ya kwanza-kwanza, neno yenye kutafsiriwa “wanaendelea kumungojea” inaweza pia kumaanisha “kupenda sana ao kutumainia jambo fulani itokee.” Ile inaonyesha kama ni jambo ya kawaida tupende sana kuokolewa.