Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ndugu Wawili Wapya wa Baraza Yenye Kuongoza

Ndugu Wawili Wapya wa Baraza Yenye Kuongoza

SIKU YA TATU, tarehe 18, Mwezi wa 1, 2023, tangazo fulani ya pekee ilionekana ku Jw.org. Ilisema kama Ndugu Gage Fleegle na Jeffrey Winder waliwekwa ili kutumikia mu Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova. Wote wawili, wamemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi.

Gage Fleegle na bibi yake Nadia

Ndugu Fleegle alikomalishwa na wazazi Wakristo mangaribi mwa Pennsylvania, katika Amerika. Wakati alikuwa kijana, familia yake ilihamia mu kijiji ya kidogo kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kisha wakati kidogo alibatizwa tarehe 20, Mwezi wa 11, 1988.

Wazazi wa Ndugu Fleegle walizoea kumutia moyo aingie mu utumishi wa wakati wote. Familia yao ilizoea kukaribisha waangalizi na wanabeteli. Na Ndugu Fleegle aliona namna wale ndugu na dada walilkuwa na furaha. Wakati kidogo kisha Ndugu Fleegle kubatizwa akakuwa painia wa kawaida; alianza upainia tarehe 1, Mwezi wa 9, 1989. Kisha miaka mbili alitimiza muradi wenye alijiwekeaka wakati alikuwa na miaka 12, muradi wa kutumikia ku Beteli. Alianza utumishi wake ku Beteli ya Brooklyn Mwezi wa 10, 1991.

Ku Beteli Ndugu Fleegle alitumikia kwa miaka munane fasi ya kuunganishia vichapo. Kisha alipewa mugao wa kutumikia mu Idara ya Utumishi. Mu ile wakati alitumikia mu kutaniko ya luga ya Kirusi kwa miaka fulani. Mu 2006, alioa bibi yake Nadia, mwenye alijiunga naye mu utumishi wa Beteli. Kwa zaidi ya miaka kumi, wametumikia pamoya mu makutaniko ya Portuguée na ya Kihispania. Kisha kutumika miaka mingi mu Idara ya Utumishi, Ndugu Fleegle alipewa mugao wa kutumikia mu Biro ya Halmashauri ya Ufundishaji. Na kisha alitumikia mu Biro ya Halmashauri ya Utumishi. Mwezi wa 3, 2022 aliwekwa kuwa musaidizi mu halmashauri ya Utumishi ya Baraza Yenye Kuongoza.

Jeffrey Winder na bibi yake Angela

Ndugu Winder alikomalia Murrieta, California, katika Amerika. Wazazi wake njo walimufundisha kweli, na alibatizwa tarehe 29, Mwezi wa 3, 1986. Mwezi wenye ulifuata, aliamua kuwa painia musaidizi. Ilimufurahisha sana. Na alipenda kuendelea. Kisha kuwa painia musaidizi kwa miezi mingi, akakuwa painia wa kawaida tarehe 1, Mwezi wa 10, 1986.

Wakati alikuwa kijana Ndugu Winder alitembelea kaka zake wawili wenye walikuwa ku Beteli ile wakati. Ile ilifanya akuwe na hamu sana ya kujaza fomu ya kuingia ku Beteli wakati angekomaa. Na mu Mwezi wa 5, 1990, alialikwa kutumikia ku Beteli ya Wallkill.

Ku Beteli, Ndugu Winder alitumikia mu idara mbalimbali; Idara ya Usafi, idara yenye ilishugulikia mashamba ya Beteli, na ku Biro ya Beteli. Mu 1997, alioa bibi yake Angela, na tangu pale wanaendelea kutumika pamoja ku Beteli. Mu 2014 walitumwa Warwick, kwenye Ndugu Winder alisaidia mu kazi ya kujenga makao makubwa. Mu 2016 walihamia ku Kituo ya Elimu ya Watchtower mu Patterson, kwenye Ndugu Winder alitumika mu Audio/Video. Kisha miaka ine walirudia Warwick, kwenye Ndugu Winder alipewa mugao wa kutumikia mu Biro ya Halmashauri ya Wafanyakazi. Mu Mwezi wa 3, 2022 aliwekwa kuwa musaidizi mu Halmashauri ya Wafanyakazi ya Baraza Yenye Kuongoza.

Tunasali sana ili Yehova abariki hawa “zawadi katika wanadamu.” wakati wanaendelea kutumika kwa bidii sana kwa ajili ya faida za Ufalme.—Efe. 4:8.