Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Biblia inasema nini kuhusu uwezo wa Yehova wa kutabiri wakati wenye kuya?

Biblia inaonyesha wazi kama Yehova iko na uwezo wa kutabiri mambo ya wakati wenye kuya. (Isa. 45:21) Lakini haiseme waziwazi kuhusu namna anafanya vile ao ni wakati gani anafanya vile, ao tena ni mambo gani anachagua kujua. Kwa hiyo, hatujue mambo yote kuhusu uwezo wa Yehova wa kutabiri mambo ya wakati wenye kuya. Lakini, fikiria mambo yenye kufuata.

Yehova hana mipaka, lakini wakati fulani anaamua kutofanya mambo fulani. Juu iko na hekima yenye haina mipaka, anaweza kutabiri mambo yote yenye anapenda. (Ro. 11:33) Lakini juu iko na uwezo wa kujizuia wenye kuwa kamilifu, anaweza pia kuchagua kutojua mambo yenye itatokea.—Linganisha na Isaya 42:14.

Yehova anafanya mapenzi yake itendeke. Namna gani ile inapatana na uwezo wake wa kutabiri mambo ya wakati wenye kuya? Isaya 46:10 inasema hivi: “Ninatabiri matokeo tangu mwanzo na tangu zamani sana mambo yenye bado hayajafanywa. Ninasema, ‘Uamuzi wangu utasimama, na nitafanya jambo lolote lenye ninapenda.’”

Sababu moya yenye inafanya Yehova aweze kutabiri mambo ya wakati wenye kuya, ni kwamba iko na uwezo wa kufanya mambo itokee. Hana lazima ya kuangalia mbali mu wakati wenye kuya ili kutafuta kujua mbele ya wakati mambo yenye itatokea. Lakini, Yehova anaweza kuamua jambo fulani itokee na wakati wenye ile jambo itatokea. Kisha anafanya ile jambo itokee kama ile wakati inafika.—Kut. 9:5, 6; Mt. 24:36; Mdo. 17:31.

Njo maana Biblia inatumia maneno sawa vile ‘kutayarisha,’ ‘kutengeneza,’ na ‘kukusudia’ ili kuzungumuzia mambo yenye Yehova anafanya kuhusu matukio fulani ya wakati wenye kuya. (2 Fa. 19:25; maelezo ya chini; Isa. 46:11) Ile maneno inatoka mu neno fulani ya mu luga ya kwanza-kwanza yenye inaweza kumaanisaha “mufinyanzi.” (Yer. 18:4) Sawa vile mufinyanzi mwenye uzoefu anaweza kuchanga udongo na maji na kuutumia ili kufanya chombo yenye kupendeza, Yehova anaweza kufanya ao anaweza kuongoza mambo ili itimize mapenzi yake.—Efe. 1:11.

Yehova anaheshimia uhuru wetu wa kuchagua. Yehova haamue mbele ya wakati namna maisha ya kila mutu itakuwa na hafanye watu wazuri watende mu njia yenye itawaongoza ku uharibifu. Anaacha watu wote waamue njia yenye watafuata, na anawashauria wachague njia ya muzuri.

Fikiria hii mifano mbili. Ya kwanza inahusu wakaaji wa Ninawi. Yehova alitabiri kama ule muji ungeharibiwa juu mu ule muji mulikuwa mumejaa mambo ya mubaya. Lakini wakati wakaaji wa Ninawi walitubu, Yehova “akabadilisha nia yake kuhusu musiba wenye alisema ataleta juu yao, na hakuuleta.” (Yon. 3:1-10) Yehova alibadilisha mawazo yake juu ya mambo yenye alikuwa ametabiri kuhusu Waninawi juu walitumia uhuru wao kwa kuamua kutubu wakati walisikia ujumbe wa kuwaonya kutoka kwa Yehova.

Mufano wa pili ni unabii wenye ulihusu mwanaume mwenye kuitwa Koreshi, mwenye angekomboa Wayahudi kutoka mu uhamisho na mwenye angetoa amri ya kujenga tena upya hekalu ya Yehova. (Isa. 44:26–45:4) Mufalme Koreshi wa Uajemi alitimiza ule unabii. (Ezr. 1:1-4) Lakini, Koreshi hakumuabudu Mungu wa kweli. Yehova alitumia Koreshi ili kutimiza ule unabii lakini, alimuacha atumie uhuru wake wa kuchagua ili kuamua ni nani mwenye angeabudu.—Mez. 21:1.

Kwa kweli, hii ni mambo kidogo tu yenye Yehova anafikiria wakati anaamua kutumia uwezo wa wake wa kujua mambo ya wakati wenye kuya. Kusema kweli, hakuna mwenye anaweza kuelewa kabisa-kabisa njia za Yehova. (Isa. 55:8, 9) Lakini mambo yenye Yehova ametufunulia inatia imani yetu nguvu na tunakuwa hakika kama sikuzote, anafanyaka tu mambo yenye kuwa sawa, hata wakati anatabiri mambo ya wakati wenye kuya.