Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Juu ya nini maneno fulani yenye kuwa mu Biblia inarudiliwa-rudiliwa?

WAKATI fulani waandikaji wa Biblia walirudilia misemwa ileile neno kwa neno. Ona sababu tatu zenye pengine ziliwachochea wafanye vile:

Kipindi yenye Biblia iliandikwa. Mu Israeli ya zamani, watu wengi hawakukuwa na kopi za Sheria. Kwa kawaida ni wakati Waisraeli walikutana pamoya ku tabenakulo njo walisikiliza wakati Sheria ilikuwa nasomwa. (Kum. 31:10-12) Inawezekana kabisa kama kulikuwa mambo yenye ingeweza kuwakengeusha wakati walikuwa nasikiliza wakiwa wamesimama kwa saa mingi mu kikundi ya watu wengi. (Ne. 8:2, 3, 7) Mu hali za vile, kurudilia misemwa ya maana kungefanya ikuwe mwepesi zaidi kwa watu kukumbuka maandiko na kuitumikisha. Kurudilia maneno fulani kungewasaidia zaidi kukumbuka mambo mbalimbali ya lazima, sawa vile masharti ya Mungu na maamuzi yake ya hukumu.—Law. 18:4-22; Kum. 5:1.

Aina ya maandishi. Karibu 10% ya Biblia ni nyimbo. Kwa mufano, kitabu ya Zaburi, Wimbo wa Sulemani, na Maombolezo. Wakati fulani nyimbo zilikuwa na maneno yenye ilirudiliwa-rudiliwa. Ile ilikazia wazo kubwa ya wimbo na ilisaidia wasikilizaji waweke maneno ya wimbo mu akili. Kwa mufano, ona maneno yenye kupatikana mu Zaburi 115:9-11: “Ee Israeli, mumutegemee Yehova —Yeye ndiye musaada wao na ngao yao. Ee nyumba ya Haruni, mumutegemee Yehova; —Yeye ndiye musaada wao na ngao yao. Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumutegemee Yehova —Yeye ndiye musaada wao na ngao yao.” Unaona namna kurudilia-rudilia ile maneno kungesaidia waimbaji waweke zile kweli za maana mu moyo na mu akili yao?

Kukazia mambo makubwa. Wakati fulani waandikaji wa Biblia walirudilia mambo ya maana. Kwa mufano, wakati Yehova aliamuru Waisraeli wasikule damu, Musa alipaswa kurudilia tena na tena juu ya nini hawakupaswa kufanya vile. Mungu alipenda kukazia kama uzima wa mwili uko katika damu, ni kusema damu inafananisha uzima. (Law. 17:11, 14) Kisha, wakati mitume na wazee katika Yerusalemu walitaya mambo mbalimbali yenye mutu anapaswa kuepuka ili amufurahishe Mungu, walikazia tena kama ni jambo ya maana kuepuka damu.—Mdo. 15:20, 29.

Hata kama misemwa fulani inarudiliwa-rudiliwa mu Biblia, Yehova hakukusudia tukuwe na desturi ya kurudilia-rudilia ile misemwa. Kwa mufano, Yesu alisema hivi: “Wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.” (Mt. 6:7) Kisha alionyesha mambo ya maana yenye tunaweza kutia mu sala zetu yenye inapatana na mapenzi ya Mungu. (Mt. 6:9-13) Kwa hiyo, hata kama tunapaswa kuepuka kurudilia-rudilia maneno ileile tena na tena mu sala zetu, tuko huru kuzungumuzia wazo ileile tena na tena.—Mt. 7:7-11.

Kuko sababu za muzuri zenye zinafanya maneno na misemwa fulani irudiliwe-rudiliwe tena na tena mu Neno ya Mungu. Ni moja kati ya njia zenye Mufundishaji wetu mukubwa anatumia ili kutufundisha kwa faida yetu.—Isa. 48:17, 18.