Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

DOKEZO LA KUJIFUNZA

Tafuta Hazina za Kiroho Ambazo Unaweza Kutumia

Tafuta Hazina za Kiroho Ambazo Unaweza Kutumia

Tunaposoma Biblia, tunaweza kutafuta hazina za kiroho kwa kufanya utafiti. Lakini tunaweza kunufaikaje kikamili zaidi?

Chimba zaidi kuhusu habari zote zinazohusu masimulizi ya Biblia. Kwa mfano, chunguza ni nani aliyeandika simulizi hilo, alimwandikia nani, na aliliandika lini. Ni hali zipi zilizotukia kabla ya simulizi hilo na ni nini kilichotukia baadaye?

Tambua mambo ya kujifunza kwa kufanyia utafiti maswali kama vile: ‘Watu waliohusika katika simulizi hilo walihisije? Walionyesha sifa gani? Kwa nini ninapaswa kuiga sifa hizo au kuziepuka?’

Tumia mambo uliyojifunza, labda katika huduma yako au unaposhughulika na watu wengine. Kwa kufanya hivyo, utaonyesha hekima inayotoka kwa Mungu, na kama Biblia inavyosema: “Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo.”—Zab. 107:43.

  • Dokezo: Ona jinsi habari itakayozungumziwa kwenye mkutano wa katikati ya juma katika sehemu ya Hazina za Neno la Mungu inavyotusaidia kukazia fikira jinsi tunavyoweza kutumia yale tunayojifunza. Mara nyingi sehemu hiyo inatia ndani maswali ambayo tunaweza kujiuliza, mambo ambayo tunaweza kutafakari, na mifano tunayoweza kuchunguza.