Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA YA KUJIFUNZA

Tafuta Mali ya Kiroho Yenye Unaweza Kutumikisha

Tafuta Mali ya Kiroho Yenye Unaweza Kutumikisha

Wakati tuko nasoma Biblia, tunaweza kutafuta mali ya kiroho kwa kutafuta habari. Tunaweza kufanya nini juu usomaji wetu utuletee faida zaidi?

Chimba ili ujue mambo mingi zaidi kuhusu habari za Biblia. Kwa mufano, tafuta kujua ni nani njo aliandika ile mambo, aliiandikia nani, na wakati gani. Hali ilikuwa namna gani, ni mambo gani ilitokea mbele ya pale, na ni mambo gani ilitokea kisha pale?

Tafuta somo kwa kujiuliza maulizo sawa vile: ‘Watu wenye kuzungumuziwa mu hii habari walijisikia namna gani? Walionyesha sifa gani? Juu ya nini ninapaswa kuiga ao kuepuka zile sifa?’

Tumikisha mambo yenye unajifunza, pengine mu mahubiri ao mu namna yako ya kutendea wengine. Kwa kufanya vile, unaonyesha hekima yenye kutoka kwa Mungu. Sawa vile Biblia inasema: “Mutu yeyote mwenye kuwa na hekima atachunguza mambo hayo.”—Zb. 107:43.

  • Pendekezo: Ona namna sehemu Utajiri wa Neno ya Mungu yenye kuwa mu mukutano wa katikati ya juma inatusaidia kujua namna ya kutumia mambo yenye tunajifunza. Mara mingi mu ile sehemu munakuwaka maulizo yenye tunaweza kujiuliza, mambo ya kutafakari, na picha zenye tunaweza kuchunguza.