Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 15

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

Tumainia Zaidi Tengenezo ya Yehova

Tumainia Zaidi Tengenezo ya Yehova

“Mukumbuke wale wenye wanaongoza kati yenu, wenye wamewafundisha neno la Mungu.”EBR. 13:7.

WAZO KUBWA

Namna ya kuendelea kutumainia zaidi tengenezo ya Yehova.

1. Watu wa Mungu walipangwa namna gani mu karne ya kwanza?

 WAKATI Yehova anapatia watu wake mugao, anatazamia waitimize mu namna yenye kupangwa muzuri. (1 Ko. 14:33) Kwa mufano, Yehova anapenda habari njema ihubiriwe mu dunia yote yenye kuikaliwa na watu. (Mt. 24:14) ameweka Yesu asimamie ile kazi. Yesu amehakikisha kwamba ile kazi inafanywa mu njia yenye kupangwa muzuri. Mu karne ya kwanza, wakati makutaniko ilikuwa naanzishwa mu maeneo mbalimbali, wazee waliwekwa ili watolee ndugu muongozo na ili wasimamie kazi. (Mdo. 14:23) Mu Yerusalemu, baraza yenye kuongoza yenye ilifanyizwa na mitume na wanaume wazee, ilikamata maamuzi fulani yenye makutaniko yote ilipaswa kufuata. (Mdo. 15:2; 16:4) Juu makutaniko ilitii maagizo yenye ilipewa, ‘iliendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka.’—Mdo. 16:5.

2. Tangu mwaka wa 1919, namna gani Yehova ametolea watu wake muongozo na chakula ya kiroho?

2 Hata leo, Yehova anaendelea kupanga muzuri watu wake. Tangu 1919, Yesu anatumia kikundi kidogo cha wanaume watiwa-mafuta ili kupanga kazi ya kuhubiri na kutolea wanafunzi wake chakula ya kiroho. a (Lu. 12:42) Bila shaka, Yehova iko nabariki kazi yao.—Isa. 60:22; 65:13, 14.

3-4. (a) Toa mufano wenye unaonyesha faida yenye tunapata juu tunapangwa muzuri. (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Kama hatukukuwa napangwa muzuri, hatungeweza kufanya kazi yenye Yesu alitupatia. (Mt. 28:19, 20) Kwa mufano, wazia mambo ingekuwa namna gani kama hatungepewa maeneo ya kuhubiri; kila mutu angehubiri kwenye anapenda. Maeneo fulani ingehubiriwa tena na tena na wahubiri tofauti-tofauti, na maeneo ingine ingebakia bila kuhubiriwa. Na weye unaona faida zingine zenye tunapata juu tunapangwa muzuri?

4 Yesu alipanga muzuri wafuasi wake wakati alikuwa ku dunia na anaendelea kufanya vile leo. Mu hii habari, tutaona mufano wenye Yesu alituachia na namna tengenezo inafuata mufano wake. Tutaona pia namna tunaweza kuonyesha kama tunatumainia tengenezo ya Yehova.

TENGENEZO YETU INAFUATA MUFANO WA YESU

5. Tunafuata mufano wa Yesu mu njia gani moja? (Yohana 8:28)

5 Yesu alijifunza kutoka kwa Baba yake wa mbinguni mambo ya kufanya na mambo ya kusema. Kwa kufuata mufano wa Yesu, tengenezo ya Yehova inatosha mu Neno ya Mungu mafundisho kuhusu mwenendo na muongozo wenye inatutolea. (Soma Yohana 8:28; 2 Ti. 3:16, 17) Mara kwa mara tunakumbushwa kama tunapaswa kusoma Biblia na kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Kufuata ile shauri kunatuletea faida gani?

6. Zungumuzia faida moya yenye tunapata wakati tunajifunza Biblia.

6 Tunapata faida kubwa wakati tunajifunza Biblia kwa kutumia vichapo vyenye vinategemea Biblia. Kwa mufano ile inatusaidia tuweze kulinganisha mafundisho ya Biblia na muongozo wenye tengenezo inatutolea. Wakati tunaona kama ule muongozo unategemea Biblia, tunatumainia zaidi tengenezo ya Yehova.—Ro. 12:2.

7. Yesu alihubiri ujumbe gani, na namna gani tengenezo ya Yehova inafuata mufano wake?

7 Yesu alihubiri “habari njema ya Ufalme wa Mungu.” (Lu. 4:43, 44) Pia, Yesu aliamuru wanafunzi wake wahubiri kuhusu Ufalme. (Lu. 9:1, 2; 10:8, 9) Leo, wote wenye kuwa mu tengenezo ya Yehova wanahubiri ujumbe wa Ufalme hata wakuwe wanaishi wapi ao wakuwe na madaraka gani.

8. Tumepewa pendeleo gani?

8 Tunaona kuwa ni pendeleo kuambia wengine kweli kuhusu Ufalme wa Mungu! Haiko kila mutu njo iko na ile pendeleo. Kwa mufano, wakati Yesu alikuwa ku dunia, hakuruhusu roho wachafu watoe ushahidi juu yake. (Lu. 4:41) Leo, juu mutu akubaliwe kuhubiri na watu wa Mungu, anapaswa kutimiza mambo yenye inaombwa. Tunaonyesha kama tunaona pendeleo yetu kuwa ya maana wakati tunatoa ushahidi fasi yoyote na wakati wowote kadiri inawezekana. Kama Yesu, muradi wetu ni kupanda na kutilia maji mbegu za kweli ya Ufalme mu mioyo ya watu.—Mt. 13:3, 23; 1 Ko. 3:6.

9. Namna gani tengenezo ya Yehova inajulisha jina ya Mungu?

9 Yesu alijulisha wengine jina ya Mungu. Mu sala yenye alitolea Baba yake wa mbinguni, Yesu alisema: “Nimewajulisha jina lako.” (Yoh. 17:26) Kwa kufuata mufano wa Yesu, tengenezo ya Yehova inajikaza sana ili kusaidia watu wengine wajue jina ya Mungu. Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya imesaidia watu kujua jina ya Mungu, juu mu ile tafsiri jina ya Mungu imerudishwa kila fasi kwenye inastahili kuwa. Kwa sasa ile tafsiri ya Biblia inapatikana ya muzima ao kwa sehemu mu luga zaidi ya 270. Mu Nyongeza A4 na A5 yenye kuwa mu ile tafsiri, utajifunza mambo mingi kuhusu kurudisha jina ya Mungu mu Biblia. Mu Biblia ya funzo, Nyongeza C inazungumuzia mambo yenye kuhakikisha kama jina ya Mungu inapaswa kupatikana mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo mara 237.

10. Maneno ya mwanamuke fulani wa Myanmar inakufundisha nini?

10 Kama Yesu, tunapenda kusaidia watu wengi kadiri inawezekana ili wajue jina ya Mungu. Wakati mwanamuke fulani wa Myanmar wa miaka 67 alijua kama Mungu iko na jina, machozi ilimutoka na akasema hivi: “Hii njo mara yangu ya kwanza kusikia kama jina ya Mungu ni Yehova. . . . Mu maisha yangu yote, njo mara ya kwanza ninajifunza jambo ya maana sana hivi.” Sawa vile mufano wa ule mwanamuke unaonyesha, kujifunza jina ya Mungu kunagusa sana watu wenye mioyo mizuri.

ENDELEA KUTUMAINIA TENGENEZO YETU

11. Namna gani wazee wanaweza kuonyesha kama wanatumainia tengenezo ya Yehova? (Ona pia picha.)

11 Wazee wanaweza kuonyesha mu njia gani moja kwamba wanatumainia tengenezo ya Mungu? Wakati wanapewa muongozo, wanapaswa kuusoma kwa uangalifu na kisha kujikaza sana kuutumikisha. Kwa mufano, wanapewa muongozo kuhusu namna ya kuongoza mikutano na namna ya kusali kwa ajili ya kutaniko, lakini pia namna ya kuhangaikia kondoo wa Kristo. Wakati wazee wanafuata muongozo wa tengenezo, ile inafanya ndugu na dada wenye kuwa chini ya uongozi wao wajisikie kuwa salama na wajisikie kuwa wanapendwa.

Wazee wanatusaidia kutumainia muongozo wenye tengenezo ya Yehova inatutolea (Ona fungu ya 11) b


12. (a) Juu ya nini tunapaswa kutii wale wenye kuongoza? (Waebrania 13:7, 17) (b) Juu ya nini tunapaswa kukazia akili sifa za muzuri za wale wenye kuongoza?

12 Wakati wazee wanatutolea muongozo, tunapaswa kuwa tayari kuufuata. Kama tunafanya vile, tutasaidia wale wenye kuongoza wafanye kazi yao muzuri zaidi. Biblia inatutia moyo tutii na tujitiishe kwa wale wenye kuongoza. (Soma Waebrania 13:7, 17.) Wakati fulani haikuwake mwepesi kufanya vile. Juu ya nini? Juu wale wanaume hawakamilike. Kama tunakazia akili makosa yao kuliko kukazia akili sifa zao, itakuwa sawa vile tuko nasaidia maadui wetu. Namna gani? Tutakuwa tuko nafanya wengine wasitumainie tengenezo ya Mungu, jambo yenye maadui wetu wanajikaza kufanya. Tunaweza kufanya nini ili tuweze kutambua na kukataa mambo ya uongo yenye maadui wetu wanaeneza?

WENGINE WASIFANYE UACHE KUTUMAINIA TENGENEZO

13. Namna gani maadui wa Mungu wanajaribu kufanya watu wakuwe na mawazo ya mubaya juu ya tengenezo?

13 Maadui wa Mungu wanajaribu kufanya mambo ya muzuri ya tengenezo yake ionekane kuwa ya mubaya. Kwa mufano, Maandiko inaonyesha kama Yehova anapenda watu wake wakuwe safi kimwili, wakuwe na mwenendo muzuri, na wakuwe na hali ya muzuri ya kiroho. Yehova anaamuru kama wale wenye wanaendelea kuwa na mwenendo mubaya na hawapendi kutubu, waondolewe katika kutaniko. (1 Ko. 5:11-13; 6:9, 10) Tunatii ile amri ya Biblia. Lakini maadui wetu wanajaribu kutumia ile jambo ili kutushitaki kama hatuvumilie wengine, tunahukumu-hukumu watu, na hatuna upendo.

14. Habari za uongo kuhusu tengenezo yetu zinatoka kwa nani?

14 Tambua ule mwenye kutushambulia. Zile habari za uongo zinatoka kwa Shetani Ibilisi. Yeye ni “baba ya uongo.” (Yoh. 8:44; Mwa. 3:1-5) Kwa hiyo tunatazamia kama Shetani atatumia wale wenye kumuunga mukono ili kueneza habari za uongo kuhusu tengenezo ya Yehova. Ile ilionekana wazi mu karne ya kwanza.

15. Viongozi wa dini walitendea namna gani Yesu na wafuasi wake?

15 Hata kama Yesu, Mwana wa Mungu alikuwa mukamilifu na alifanya miujiza ya ajabu, Shetani alitumia watu fulani ili kueneza habari mingi za uongo kumuhusu. Kwa mufano, viongozi wa dini waliambia watu kama mamlaka ya Yesu ya kufukuza pepo wachafu ilitoka kwa “mutawala wa pepo wachafu.” (Mk. 3:22) Wakati Yesu alikuwa nasambishwa, viongozi wa dini walimushitaki kama alimutukana Mungu na walichochea watu waombe auawe. (Mt. 27:20) Kisha, wakati wanafunzi wa Yesu walikuwa nahubiri habari njema, wapinzani wao ‘walichochea mubaya watu’ ili wawatese. (Mdo. 14:2, 19) Kuhusu andiko ya Matendo 14:2, Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 12, 1998, ulisema hivi: “Zaidi ya kukataa ule ujumbe, Wayahudi wapinzani walianzisha kampanye ya kuchochea Watu wa Mataifa ili wao pia wasiwasikilize Wakristo.”

16. Tunapaswa kukumbuka nini kama tunasikia habari za uongo?

16 Shetani angali nasema uongo mupaka leo. Anaendelea ‘kupotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu.’ (Ufu. 12:9) Kama unasikia habari za mubaya kuhusu tengenezo ao kuhusu ndugu wenye kuongoza, kumbuka namna maadui wa Mungu walimutendea Yesu na wanafunzi wake mu karne ya kwanza. Leo, watu wa Yehova wanateswa na kusemewa mambo ya uongo sawa vile tu Biblia ilitabiri. (Mt. 5:11, 12) Hatutaamini habari za uongo kama tunatambua kwenye zile habari zinatoka, na kama tunakamata hatua palepale. Tunapaswa kukamata hatua gani?

17. Tunaweza kufanya nini ili habari za uongo zisikuwe na matokeo juu yetu? (2 Timoteo 1:13) (Ona pia kisanduku “ Namna ya Kutenda Ukisikia Habari za Uongo.”)

17 Kataa habari za uongo. Mutume Paulo alitoa maagizo yenye kuwa wazi juu ya namna ya kufanya ikiwa tunasikia habari za uongo. Aliambia Timoteo: “Uamuru watu fulani . . . wasisikilize hadisi za uongo” na ‘wakatae hadisi za uongo.’ (1 Ti. 1:3, 4; 4:7) Mutoto mudogo anaweza kuokota kitu kichafu na kukitia mu kinywa, lakini mutu muzima hatafanya vile juu anajua hatari. Tunakataa habari za uongo juu tunajua kwenye zile habari zinatoka. Lakini tunasikiliza “maneno yenye faida” ya ile kweli.—Soma 2 Timoteo 1:13.

18. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatumainia tengenezo ya Yehova?

18 Tengenezo inafuata mufano ya Yesu mu njia za mingi. Tumezungumuzia tu njia tatu. Wakati uko unajifunza Biblia, tafuta kujua ni mu njia zingine gani tengenezo inafuata mufano wa Yesu. Saidia wengine mu kutaniko watumainie zaidi tengenezo. Na uendelee kuonyesha kama unatumainia tengenezo kwa kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu, na pia kwa kushikamana na tengenezo yenye anatumikisha ili kutimiza mapenzi yake. (Zb. 37:28) Tuendelee basi kukamata kwa mikono mbili pendeleo yenye tuko nayo ya kuwa kati ya watu wa Yehova, watu wenye upendo na ushikamanifu.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni mu njia gani mbalimbali watu wa Mungu wanafuata mufano wa Yesu?

  • Namna gani tunaweza kuendelea konyesha kama tunatumainia tengenezo ya Yehova?

  • Tunapaswa kufanya nini kama tunasikia habari za uongo?

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

a Ona kisanduku “Juu ya Nini 1919?” mu kitabu Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena! uku. 102-103.

b MAFASIRIO YA PICHA: Kisha wazee wa kutaniko kuzungumuzia maagizo kuhusu kuhubiri mahali pa watu wengi, musimamizi wa kikundi ya mahubiri, anaelezea wahubiri ile maagizo yenye kuonyesha kama wanapaswa kusimama mugongo wao ukiwa pembeni ya ukuta.