Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Juu ya nini mu jeshi ya Mufalme Daudi mulikuwa watu wa mataifa ingine?

KATI ya watu wa mataifa ingine wenye walikuwa mu jeshi ya Daudi kulikuwa Seleki Mwamoni, Uria Muhiti, na Itma Mumoabu. a (1 Ny. 11:39, 41, 46) Mu jeshi ya Daudi mulikuwa pia ‘Wakereti, Wapeleti, na Wagati.’ (2 Sa. 15:18) Inawaziwa kama Wakereti na Wapeleti walikuwa ndugu za Wafilisti. (Eze. 25:16) Wagati walitokana na Wafilisti wa muji wa Gati.—Yos. 13:2, 3; 1 Sa. 6:17, 18.

Juu ya nini Daudi alikubali watu wa mataifa ingine katika jeshi yake? Alikuwa hakika kama watakuwa washikamanifu kwake, na zaidi sana kwa Yehova. Kwa mufano, kuhusu Wakereti na Wapeleti, kitabu fulani (The New Interpreter’s Dictionary of the Bible) kinasema hivi: “Waliendelea kuwa washikamanifu kwa Daudi mu hali za nguvu sana za utawala wake.” Namna gani? Wakati “watu wote wa Israeli” walimuacha Mufalme Daudi na kufuata “mufanya-fujo fulani mwenye aliitwa Sheba,” Wakereti na Wapeleti walibakia waaminifu kwa Daudi na walimusaidia kupiganisha upinzani wa Sheba. (2 Sa. 20:1, 2, 7) Wakati ingine, Adoniya mutoto wa Mufalme Daudi, alijaribu kukamata ufalme kwa kinguvu. Lakini Wakereti na Wapeleti walibakia waaminifu kwa Daudi na wakamusaidia kuweka Sulemani, mwenye Yehova alikuwa amechagua, kuwa mufalme pa nafasi yake.—1 Fa. 1:24-27, 38, 39.

Mutu mwingine wa mataifa mwenye alibakia kabisa mushikamanifu kwa Daudi alikuwa Itai Mugati. Itai pamoja na wapiganaji wake 600 walimuunga mukono Mufalme Daudi wakati Absalomu, mwana wa Daudi, aliasi na kuiba mioyo ya wanaume wa Israeli. Ku mwanzo, Daudi aliambia Itai kwamba, juu hakukuwa Mwisraeli, hakulazimishwa kumupigania. Lakini Itai alisema: “Kama vile hakika Yehova anaishi na kama vile hakika bwana wangu mufalme anaishi, kila mahali kwenye bwana wangu mufalme atakuwa, ikuwe kwa ajili ya kifo ao kwa ajili ya uzima, ni pale mutumishi wako atakuwa!”—2 Sa. 15:6, 18-21.

Itai alikuwa mushikamanifu kwa Daudi, mufalme mutiwa-mafuta wa Yehova

Hata kama Wakereti, Wapeleti na Wagati hawakukuwa Waisraeli, walimuona Yehova kuwa Mungu wa kweli na Daudi kuwa mutiwa-mafuta wake. Bila shaka, Daudi alifurahi sana kuwa na wanaume washikamanifu kama hao!

a Sheria ya Mungu yenye kuwa mu Kumbukumbu la Torati 23:3-6 ilisema kama Waamoni na Wamoabu hawakuruhusiwa kuingia mu kutaniko ya Israeli. Lakini inaonekana kama ile sheria ilikuwa inazungumuzia njo kukubaliwa kisheria kuwa Mwisraeli, lakini haikukataza wale watu wa mataifa kujiunga ao kuishi na watu wa Mungu. Ona kitabu Etude Perspicace des Ecritures, Buku ya 1, uku. 100.