Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MRADI WA KUJIFUNZA

Watu wa Kiroho Hufanya Maamuzi Yenye Hekima

Watu wa Kiroho Hufanya Maamuzi Yenye Hekima

Soma Mwanzo 25:​29-34 ili ujifunze ikiwa Esau na Yakobo walifanya maamuzi yenye hekima.

Chimba zaidi kwenye muktadha. Ni jambo gani lilitukia mapema? (Mwa. 25:​20-28) Ni jambo gani lilitukia baadaye?—Mwa. 27:​1-46.

Chimba zaidi katika habari hususa. Katika siku hizo, mzaliwa wa kwanza alikuwa na haki na majukumu gani?—Mwa. 18:​18, 19; w10 5/1 13.

  • Je, sikuzote mtu alihitaji kuwa mzaliwa wa kwanza ili awe babu wa Masihi? (w17.12 14-15)

Tafakari mambo ambayo umejifunza na uyatumie. Kwa nini Yakobo alithamini zaidi haki ya mzaliwa wa kwanza kuliko Esau? (Ebr. 12:​16, 17; w03 10/15 28-29) Yehova alihisije kuhusu ndugu hao wawili, na kwa nini? (Mal. 1:​2, 3) Esau angeweza kufanya jambo gani tofauti ili afanye maamuzi mazuri zaidi?

  • Jiulize hivi, ‘Ninawezaje kuonyesha kwamba ninathamini mambo ya kiroho inapohusu ratiba yangu ya kila juma, kama vile ninapopanga muda wa ibada ya familia?’