Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA

Watu wa Kiroho Wanakamata Maamuzi yenye Hekima

Watu wa Kiroho Wanakamata Maamuzi yenye Hekima

Soma Mwanzo 25:29-34 ili kujua ikiwa Esau na Yakobo walikamata maamuzi yenye hekima.

Soma maandiko yenye kutangulia na yenye kufuata. Nini ilitokea mbele ya pale? (Mwa. 25:20-28) Nini ilitokea kisha?—Mwa. 27:1-46.

Tafuta habari zaidi. Mu ile wakati, mwana muzaliwa wa kwanza alikuwa na haki gani na alikuwa na madaraka gani?—Mwa. 18:18, 19; w10 1/5 uku. 13.

  • Iliomba tu mutu akuwe muzaliwa wa kwanza juu aweze kuwa mu kizazi cha Masiya? (w17.12 uku. 14-15)

Ujiulize hii habari inakufundisha nini, na utumikishe mambo yenye unajifunza. Juu ya nini Yakobo alikamata kwa uzito haki ya muzaliwa wa kwanza kuliko Esau? (Ebr. 12:16, 17; w03 15/10 uku. 28-29) Yehova aliona wale ndugu wawili namna gani, na juu ya nini? (Mal. 1:2, 3) Esau alipaswaka kufanya nini ili akamate maamuzi ya muzuri zaidi?

  • Ujiulize hivi: ‘Mu namna yangu ya kutumikisha wakati kila juma, namna gani ninaweza kuonyesha kama ninaona mambo ya kiroho kuwa ya maana zaidi, kwa mufano kwa kupanga wakati ili kufanya ibada ya familia?’