Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

WIMBO 1 Sifa za Yehova

Tumainia “Muamuzi wa Dunia Yote” Mwenye Rehema!

Tumainia “Muamuzi wa Dunia Yote” Mwenye Rehema!

“Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?”MWA. 18:25.

WAZO KUBWA

Kuelewa muzuri zaidi namna Yehova ataonyesha rehema na haki wakati atafufua wale wenye hawako wenye haki.

1. Yehova alisaidia Abrahamu kujifunza jambo gani yenye kufariji?

 MIAKA mingi yenye imepita, kupitia malaika, Mungu aliambia Abrahamu kama alikuwa napanga kuharibu miji ya Sodoma na Gomora. Abrahamu hangesahau ile mazungumuzo hata siku moya. Hata kama alikuwa mwanaume muaminifu, ile mazungumuzo ilimuhangaisha sana. Aliuliza hivi: “Je, kweli utaharibu mwenye haki pamoja na muovu? . . . Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?” Kwa uvumilivu Yehova alisaidia rafiki yake Abrahamu ajifunze hii somo ya maana sana na yenye kufariji: Yehova hawezi kuharibu watu wenye haki.—Mwa. 18:23-33.

2. Nini njo inatuhakikishia kama sikuzote Yehova anahukumu watu kwa haki na kwa rehema?

2 Nini njo inatuhakikishia kama sikuzote Yehova anahukumu watu kwa haki na kwa rehema? Ni juu tunajua kama “Yehova anaona ndani ya moyo.” (1 Sa. 16:7) Kwa kweli, Yehova anajua “moyo wa kila mwanadamu.” (1 Fa. 8:39; 1 Ny. 28:9) Ile ni jambo ya ajabu sana. Juu Yehova iko na hekima mingi sana kutupita, ni nguvu kwetu kuelewa kabisa-kabisa namna yake ya kuhukumu. Njo maana, kupitia nguvu ya roho takatifu, mutume Paulo alisema hivi juu ya Yehova Mungu: “Hukumu zake haziwezi kuchunguzika.”—Ro. 11:33.

3-4. Tunaweza kujiuliza maulizo gani, na tutazungumuzia nini mu hii habari? (Yohana 5:28, 29)

3 Hata vile, wakati fulani tunaweza kujiuliza maulizo sawa yenye Abrahamu aliulizaka. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Kuko tumaini fulani kwa watu wenye waliharibiwa mu Sodoma na Gomora? Inawezekana wamoja kati yao wafufuliwe kati ya watu “wenye hawako wenye haki”?’—Mdo. 24:15.

4 Tujikumbushe mambo yenye tunajua kuhusu ufufuo. Karibuni, tulipewa mafasirio ya mupya juu ya “ufufuo wa uzima” na “ufufuo wa hukumu.” a (Soma Yohana 5:28, 29.) Ile mafasirio ya mupya ilileta mabadiliko juu ya namna yetu ya kuelewa mafundisho fulani ya Biblia. Mu hii habari na mu habari yenye kufuata tutazungumuzia ile mabadiliko. Tutaona kwanza mambo yenye hatujue na kisha tutaona mambo yenye tunajua kuhusu namna ya Yehova ya kuhukumu kwa haki.

MAMBO YENYE HATUJUE

5. Zamani vichapo vyetu vilisema nini kuhusu wale wenye waliharibiwa mu miji ya Sodoma na Gomora?

5 Zamani, vichapo vyetu vilisema kama wale wenye Yehova alihukumu kuwa hawako wenye haki, hawana tumaini. Kwa mufano, tulisema kama watu wa Sodoma na Gomora, hawana tumaini yoyote ya ufufuo. Lakini kisha kusali na kujifunza sana juu ya ile jambo, tumejiuliza hivi: Tunaweza kabisa kusema vile kwa uhakika?

6. Biblia inazungumuzia mifano gani ya watu wenye hawako wenye haki wenye Yehova alihukumu, na hatujue nini?

6 Kuko habari mingi za Biblia zenye zinazungumuzia namna Yehova alihukumu watu wenye hawako wenye haki. Kwa mufano, watu wengi wenye walikufa wakati wa Garika, mataifa saba yenye Yehova aliamuru Waisraeli waharibu mu Inchi ya Ahadi, ao tena maaskari wa Ashuru 185000 wenye malaika wa Yehova aliharibu mu usiku moya. (Mwa. 7:23; Kum. 7:1-3; Isa. 37:36, 37) Mu ile mifano, je, Biblia inatupatia habari zote zenye tuko nazo lazima ili kusema kama Yehova aliharibu wale watu milele, bila tumaini ya ufufuo? Hapana. Juu ya nini tunasema vile?

7. Hatujue nini kuhusu watu wenye waliharibiwa wakati wa Garika, ao mataifa ya Wakanaani yenye watu wa Mungu waliharibu? (Ona ku jalada.)

7 Hatujue namna Yehova alihukumu kila mumoja wao; na hatujue ikiwa wale wenye waliuawa walipata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova na nafasi ya kutubu. Kuhusu wakati wa garika, Biblia inasema kama Noa alikuwa “muhubiri wa haki.” (2 Pe. 2:5) Lakini haiseme kama wakati Noa alikuwa najenga safina, alikuwa pia najikaza kuhubiria kila mutu ku dunia. Vilevile kuhusu mataifa ya Wakanaani, hatujue ikiwa wale watu wote wabaya walipata nafasi ya kujifunza kumuhusu Yehova ili waweze kubadilika.

Noa na familia yake wako najenga safina kubwa. Wakati Noa alikuwa najenga safina, hatujue kama alifanya kampanye ya kuhubiria watu wote wenye walikuwa naishi ku dunia mbele garika ifike. (Ona fungu ya 7)


8. Hatujue nini juu ya watu wa Sodoma na Gomora?

8 Tuseme nini juu ya watu wa Sodoma na Gomora? Loti, mwanaume mwenye haki, aliishi kati yao. Lakini, tunajua ikiwa aliwahubiria wote? Hapana. Ni kweli kwamba walikuwa watu wabaya, lakini walijua kabisa tofauti kati ya mema na mabaya? Kumbuka kama kikundi ya wanaume wa mu ule muji walitafuta kulala kinguvu wageni wa Loti. Biblia inasema kama mu ile kikundi mulikuwa “kuanzia kijana mwanaume mupaka muzee.” (Mwa. 19:4; 2 Pe. 2:7) Tunajua kabisa ikiwa Yehova, Mungu mwenye rehema, alihukumu kila mumoja wao bila tumaini ya ufufuo? Yehova alihakikishia Abrahamu kama mu ule muji hamukukuwa hata wanaume kumi wenye haki. (Mwa. 18:32) Juu hawakukuwa wenye haki, Yehova alikuwa na haki ya kuwaharibu kwa sababu ya matendo yao. Lakini tunaweza kusema kwa uhakika kabisa kama hakuna hata mumoja wao mwenye atafufuliwa kati ya “wenye hawako wenye haki”? Hapana, hatuwezi kusema vile kwa uhakika!

9. Hatujue nini kuhusu Sulemani?

9 Mu Biblia muko pia habari za watu wenye walikuwa wenye haki, kisha wakageuka na wakakuwa wenye hawako wenye haki. Mufano moya ni ya Mufalme Sulemani. Alifundishwa muzuri njia za Mungu na Yehova alimubariki sana. Lakini kisha wakati, alimuacha Yehova na akaanza kuabudu miungu ya uongo. Zambi zake zilimukasirisha Yehova na zilikuwa na matokeo ya mubaya sana kwa wakati murefu. Ni kweli kama Maandiko inasema kuwa Sulemani ‘alilalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake’ kutia ndani wanaume waaminifu sawa vile Mufalme Daudi. (1 Fa. 11:5-9, 43; 2 Fa. 23:13) Lakini, juu tu Biblia inatumia ile maneno kuhusu namna Mufalme Sulemani alizikwa, ile inahakikisha kama atafufuliwa? Biblia haiseme. Lakini watu fulani wanaweza kusema kama “ule mwenye amekufa ameondolewa zambi yake.” (Ro. 6:7) Ile ni kweli, lakini ile haimaanishe kama kila mutu mwenye amekufa atafufuliwa. Kwa kweli, haiko tu juu mutu alikufa njo anakuwa na haki ya kuishi tena. Ufufuo ni zawadi yenye Mungu mwenye upendo anatoa. Anaipatia wale wenye anapenda kupatia nafasi ya kumutumikia milele. (Yob. 14:13, 14; Yoh. 6:44) Sulemani atapata ile zawadi? Yehova mwenyewe njo iko na jibu; siye hatujue. Lakini tunajua kama Yehova atatenda kwa haki.

MAMBO YENYE TUNAJUA

10. Yehova iko na mawazo gani kuhusu kuharibu watu? (Ezekieli 33:11) (Ona pia picha.)

10 Soma Ezekieli 33:11. Yehova anatuambia mawazo yake kuhusu kuhukumu watu. Kupitia muongozo wa roho takatifu, mutume Petro alirudilia mambo yenye Ezekieli aliandika. Alisema kama “Yehova . . . hataki mutu yeyote aharibiwe.” (2 Pe. 3:9) Ile kweli ya Biblia inatusaidia kujua kama, Yehova haiko haraka kuharibu watu milele. Ni mwenye rehema nyingi sana, na wakati wote wenye inawezekana, anaonyesha ile sifa.

Wakati wa ufufuo wa wale wenye hawako wenye haki, watu mbalimbali watapata nafasi ya kujifunza kumuhusu Yehova (Ona fungu ya 10)


11. Ni nani njo hawatafufuliwa, na tunajua vile namna gani?

11 Tunajua nini kuhusu watu wenye hawatafufuliwa? Biblia inazungumuzia tu mifano kidogo ya watu wenye hawatafufuliwa. b Yesu alionyesha kama Yuda Iskariote hatafufuliwa. c (Mk. 14:21) Yuda Iskariote alijua kama jambo yenye alitaka kufanya ilimupinga Yehova Mungu na Mwana wake, lakini aliifanya tu. d (Mk. 3:29) Vilevile, Yesu alisema kama viongozi fulani wa dini wenye walimupinga hawangekuwa na tumaini ya ufufuo. (Mt. 23:33) Na mutume Paulo alionya kama waasi-imani wenye hawatubu hawangefufuliwa.—Ebr. 6:4-8; 10:29.

12. Tunajua nini kuhusu rehema ya Yehova? Toa mufano.

12 Lakini, tunajua nini kuhusu rehema ya Yehova? Ameonyesha namna gani kama “hataki mutu yeyote aharibiwe”? Tuone namna alionyesha rehema watu fulani wenye walifanya makosa makubwa. Mufalme Daudi alifanya zambi nzito, alifanya uzinifu na aliua. Lakini, Daudi alitubu. Kwa hiyo, Yehova alimuonyesha rehema na akamusamehe. (2 Sa. 12:1-13) Mufalme Manase alifanya mambo mingi ya mubaya sana mu sehemu kubwa ya maisha yake. Hata vile, Yehova alimuonyesha rehema na akamusamehe juu alitubu. (2 Ny. 33:9-16) Ile mifano inaonyesha kama Yehova anaonyeshaka rehema wakati wowote wenye anaona kama kuko sababu ya kufanya vile. Yehova atafufua wale watu juu walitambua kama walifanya makosa makubwa na wakatubu.

13. (a) Juu ya nini Yehova alionyesha Waninawi rehema? (b) Yesu alisema nini kuhusu Waninawi?

13 Tunajua pia namna Yehova alionyesha watu wa Ninawi rehema. Mungu aliambia Yona hivi: “Nimeona uovu wao.” Lakini wakati walitubu zambi zao, Yehova aliwasamehe. Yehova alikuwa na rehema nyingi sana kuliko Yona. Mungu alimukumbusha nabii wake mwenye alikasirika sana kama, watu wa Ninawi “hawajue hata kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.” (Yon. 1:1, 2; 3:10; 4:9-11) Miaka mingi kisha pale, Yesu alitumia mufano wa watu wa Ninawi ili kufundisha watu juu ya haki na rehema ya Yehova. Yesu alisema kama Waninawi wenye walitubu “watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki na watakihukumu.”—Mt. 12:41.

14. “Ufufuo wa hukumu” utakuwa na maana gani kwa Waninawi?

14 Watu wa Ninawi “watasimama” katika “hukumu” gani? Yesu alifundisha kama kutakuwa “ufufuo wa hukumu.” (Yoh. 5:29) Yesu alikuwa nazungumuzia miaka 1000 ya utawala wake, wakati “wenye haki na wenye hawako wenye haki” watafufuliwa. (Mdo. 24:15) Kwa wale wenye hawako wenye haki, ule ufufuo utakuwa “ufufuo wa hukumu,” ni kusema, Yehova na Yesu wataangalia na kuchunguza mwenendo wao ili kuona ikiwa wako natumikisha mambo yenye wako nafundishwa. Ikiwa Muninawi mwenye alifufuliwa anakataa kujiunga na ibada safi, hukumu yake itakuwa uharibifu. (Isa. 65:20) Lakini wote wenye watachagua kumuabudu Yehova kwa uaminifu, hukumu yao itakuwa ya muzuri, ni kusema watakuwa na tumaini ya kuishi milele!—Da. 12:2.

15. (a) Juu ya nini tunapaswa kuepuka kusema kama wale wenye waliharibiwa mu miji ya Sodoma na Gomora hawatafufuliwa? (b) Tunaelewa namna gani maneno yenye kuwa mu Yuda 7? (Ona kisanduku “ Yuda Alimaanisha Nini?”)

15 Wakati Yesu alikuwa nazungumuzia watu wa Sodoma na Gomora, alisema kama ingekuwa mwepesi zaidi kwao kuokoka “Siku ya Hukumu” yenye kuya kuliko watu wenye walimukataa na kukataa mafundisho yake. (Mt. 10:14, 15; 11:23, 24; Lu. 10:12) Alipenda kumaanisha nini? Tunaweza kuwaza kama Yesu alikuwa natumikisha maneno ya mufano. Lakini inaonekana kama haiko vile, sawa vile tu hakukuwa natumia maneno ya mufano wakati alizungumuzia watu wa Ninawi. Mambo yenye alisema kuhusu watu wa Sodoma na Gomora, haiko maneno ya mufano. “Siku ya Hukumu” yenye Yesu anazungumuzia mu habari ya Waninawi na watu wa Sodoma na Gomora ni ileile. Sawa watu wa Ninawi, watu wa Sodoma na Gomora walifanya mambo ya mubaya. Lakini watu wa Ninawi walikuwa na nafasi ya kutubu. Zaidi ya ile, kumbuka mambo yenye Yesu alisema kuhusu “ufufuo wa hukumu.” Alisema kama kati ya wenye watafufuliwa kutakuwa “wale wenye walizoea kutenda mambo maovu.” (Yoh. 5:29) Inaonekana kama kunaweza kuwa tumaini fulani kwa ajili ya watu wa Sodoma na Gomora. Inawezekana hata wamoja kati yao wafufuliwe. Kama ni vile, tutakuwa na nafasi ya kuwafundisha juu ya Yehova na Yesu Kristo.

 

16. Tunajua nini kuhusu namna Yehova ataamua ikiwa ni nani atafufuliwa? (Yeremia 17:10)

16 Soma Yeremia 17:10. Hii andiko inatusaidia kusema kwa kifupi mambo yenye tunajua: Sikuzote Yehova ‘anachunguza moyo, anachunguza mawazo ya ndani kabisa.’ Hata kuhusu ufufuo, ni vile atafanya; ‘atamupatia kila mumoja kulingana na njia zake.’ Yehova atapatia watu malipizi wakati ni lazima kufanya vile, lakini ataonyesha rehema wakati inawezekana kufanya vile. Kwa hiyo, hatupaswe kuwaza kama mutu fulani hana tumaini ya ufufuo ikiwa Biblia haiseme vile waziwazi!

“MUAMUZI WA DUNIA YOTE” ATATENDA “JAMBO LENYE KUWA SAWA”

17. Mambo itakuwa namna gani juu ya wanadamu wenye wamekufa?

17 Tangu Adamu na Eva wajiunge na Shetani na wamuasi Yehova Mungu, mamiliare ya wanadamu wamekufa. Kifo ni “adui” mubaya sana! (1 Ko. 15:26) Mambo itakuwa namna gani juu ya wale watu wote wenye wamekufa? Kati ya wanafunzi waaminifu wa Yesu, hesabu kidogo ya watu, ni kusema watu 144000 watafufuliwa ili kuenda mbinguni na watapewa uzima wenye hauwezi kufa. (Ufu. 14:1) Hesabu kubwa ya wanaume na wanamuke waaminifu wenye walimupenda Yehova watafufuliwa kati ya “wenye haki,” na wataishi milele ku dunia kama wanaendelea kuwa waaminifu wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo na wakati wa jaribu ya mwisho. (Da. 12:13; Ebr. 12:1) Pia mu kipindi ya Miaka Elfu, “wenye hawako wenye haki,” ni kusema wale wenye hawakumutumikia Yehova ao hata wale wenye “walizoea kutenda mambo maovu,” watapewa nafasi ya kubadilisha tabia yao na kuwa waaminifu. (Lu. 23:42, 43) Lakini wanadamu fulani walikuwa waovu sana, waliazimia kabisa kumupinga Yehova na kusudi yake, kwa hiyo Yehova ameamua kama hatawafufua.—Lu. 12:4, 5.

18-19. (a) Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama Yehova atahukumu muzuri kabisa wale wenye wamekufa? (Isaya 55:8, 9) (b) Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

18 Unawaza tuko na sababu ya muzuri ya kutumainia hukumu zote za Yehova, hata zikuwe za namna gani? Ndiyo! Sawa vile Abrahamu alielewa, Yehova “Muamuzi wa dunia yote” ni mukamilifu, ni mwenye hekima mingi sana, na ni mwenye rehema. Amezoeza Mwana wake na amemupatia daraka ya kuhukumu wengine. (Yoh. 5:22) Yehova na Mwana wake wanaweza kusoma mambo yenye kuwa mu moyo wa kila mwanadamu. (Mt. 9:4) Sikuzote, wanafanya “jambo lenye kuwa sawa”!

19 Tuazimie basi kumutumainia Yehova na kuwa hakika kama maamuzi yake inakuwaka ya muzuri sikuzote. Tunajua kama hakuna hata mumoja kati yetu mwenye anastahili kuhukumu wengine, lakini Yehova yeye anastahili! (Soma Isaya 55:8, 9.) Kwa hiyo tunaachia Yehova na Mwana wake kazi ya kuhukumu watu. Tuko hakika kama Yesu anaiga rehema na haki ya Baba yake kwa ukamilifu. (Isa. 11:3, 4) Sasa, tuseme nini juu ya namna Yehova atahukumu watu wakati wa taabu kubwa? Hatujue nini? Lakini tunajua nini? Habari yenye kufuata itajibia ile maulizo.

WIMBO 57 Tuhubirie Watu Wote

c Maneno “mwana wa uharibifu” yenye kuwa mu Yohana 17:12 inamaanisha kama wakati Yuda alikufa, aliharibiwa milele bila tumaini ya ufufuo.”