Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MRADI WA KUJIFUNZA

Kuvumilia Ukosefu wa Haki

Kuvumilia Ukosefu wa Haki

Soma Mwanzo 37:​23-28; 39:​17-23 ili kujifunza kutokana na simulizi la Yosefu linalohusu kuvumilia ukosefu wa haki.

Chunguza muktadha. Ni nini kilichosababisha Yosefu atendewe kwa njia isiyo ya haki? (Mwa. 37:​3-11; 39:​1, 6-10) Yosefu alihitaji kuvumilia ukosefu wa haki kwa muda gani? (Mwa. 37:2; 41:46) Katika kipindi hicho, Yehova alimfanyia nini Yosefu, lakini hakumfanyia nini?—Mwa. 39:​2, 21; w23.01 17 ¶13.

Chimba zaidi. Biblia haisemi kwamba Yosefu alijitetea aliposhtakiwa kwa uwongo na mke wa Potifa. Maandiko yafuatayo yanawezaje kutusaidia kujua sababu iliyomfanya Yosefu aamue kunyamaza, au kujua kwa nini hatuhitaji kutarajia kwamba habari zote kuhusu simulizi fulani zitafunuliwa? (Met. 20:2; Yoh. 21:25; Mdo. 21:37) Ni sifa gani ambazo huenda zilimsaidia Yosefu kuvumilia ukosefu wa haki?—Mika 7:7; Luka 14:11; Yak. 1:​2, 3.

Nimejifunza nini? Jiulize hivi: