Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 26

WIMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Yangu

Umufanye Yehova Kuwa Mwamba Wako

Umufanye Yehova Kuwa Mwamba Wako

“Hakuna mwamba kama Mungu wetu.”1 SA. 2:2.

WAZO KUBWA

Kujifunza sifa za Yehova zenye zinafanya aitwe mwamba na namna tunaweza kuiga zile sifa.

1. Kulingana na Zaburi 18:46 Daudi anamulinganisha Yehova na nini?

 MU HII dunia, magumu yenye haitazamiwe inaweza kuvuruga ao hata kubadilisha kabisa maisha yetu. Lakini tunafurahi juu tunajua kama Yehova iko pale juu ya kutusaidia! Mu habari yenye kutangulia, tuliona kama Yehova ni Mungu mwenye kuishi na kama siku zote iko tayari kutusaidia. Wakati anatutegemeza, ile inatusaidia tukuwe hakika kama “ni mwenye kuishi.” (Soma Zaburi 18:46.) Lakini, kisha tu kusema ile maneno, Daudi alimuita Mungu kuwa “Mwamba wangu.” Juu ya nini Daudi alimufananisha Yehova, Mungu mwenye kuishi, na mwamba, kitu yenye haina uzima?

2. Daudi alimuita Yehova Mwamba wangu,” tutajifunza nini juu ya ile maneno?

2 Mu hii habari, tutaona juu ya nini Yehova anaitwa kuwa mwamba, na mambo yenye ile maneno ya mufano inatufundisha juu yake. Tutaona pia namna tunaweza kumufanya Yehova kuwa mwamba wetu. Na ku mwisho, tutaona namna tunaweza kuiga sifa mbalimbali zenye zinafanya Yehova aitwe kuwa mwamba.

JUU YA NINI YEHOVA NI MWAMBA

3. Mara mingi Biblia inatumia namna gani neno “mwamba”? (Ona jalada.)

3 Biblia inatumia neno “mwamba” ili kutusaidia kuelewa sifa zenye Yehova iko nazo. Mara mingi ile neno inatumiwa mu maandiko yenye watumishi wa Yehova wanamusifu kwa sababu ya sifa za ajabu zenye iko nazo. Mu andiko ya Kumbukumbu la Torati 32:4 njo Yehova anaitwa kwa mara ya kwanza “Mwamba.” Mu sala yenye Hana alitoa, alisema kama “hakuna mwamba kama Mungu wetu.” (1 Sa. 2:2) Habakuki alimuita Yehova “Mwamba wangu.” (Hab. 1:12) Muandikaji wa Zaburi 73 alimuita Mungu “mwamba wa moyo wangu.” (Zb. 73: 26) Na hata Yehova mwenyewe alijiita kuwa mwamba. (Isa. 44:8) Tuzungumuzie sifa tatu zenye zinamufanya Yehova kuwa mwamba na namna tunaweza kumufanya kuwa “Mwamba wetu.”Kum. 32:31.

Watu wa Mungu wanamuona Yehova kuwa Mwamba kwenye wanaweza kupata usalama (Ona fungu ya 3)


4. Ni mu maana gani Yehova ni Kimbilio yetu? (Zaburi 94:22)

4 Yehova ni kimbilio yetu. Sawa vile mwamba kubwa unaweza kuwa fasi kwenye mutu anaweza kujificha wakati wa mvua kubwa yenye upepo, Yehova anatulinda wakati tunakutana na hali za nguvu mu maisha. (Soma Zaburi 94:22.) Anatulinda na anatuhakikishia kama magumu yenye tuko nayo haitaendelea kututesa milele. Na zaidi ya ile, anatupatia hii ahadi: Atatosha mambo yote yenye inatuletea mahangaiko na mateso.—Eze. 34:​25, 26.

5. Namna gani tunaweza kumufanya Yehova kuwa mwamba kwenye tunakimbilia?

5 Njia moya ya kumufanya Yehova kuwa Kimbilio yetu ni kusali kwake. Wakati tunasali, Yehova anatupatia “amani ya Mungu” yenye inalinda moyo na akili yetu. (Flp. 4:​6, 7) Ona mufano wa ndugu Artem, mwenye alifungwa juu ya imani yake. Mara kwa mara alikuwa naulizwa maulizo na mwanaume mukali mwenye alikuwa namutendea mubaya, kumuzarau, na kumushushia heshima. Ndugu Artem alisema hivi: “Kila mara yenye aliniita ili kuniuliza maulizo, nilikuwa na mahangaiko mingi. . . . Nilikuwa nasali kila mara kwa Yehova. Nilikuwa namuomba anipatie amani ya moyo na hekima. Hata kama nilikuwa nateswa, nilibakia mwenye kutulia. . . . Kwa musaada wa Yehova, nilikuwa sawa vile nimesimama pembeni ya ukuta wa majiwe.”

6. Juu ya nini tunapaswa kumutegemea Yehova kila wakati? (Isaya 26:​3, 4)

6 Yehova ni mwenye kutegemeka. Sawa vile mwamba unakuwaka fasi ileile na haubadilishake fasi, kila siku Yehova iko pale kwa ajili yetu. Tunaweza kumutegemea kwa sababu yeye ni “Mwamba wa milele.” (Soma Isaya 26:​3, 4) Sikuzote atakuwa pale ili kutimiza ahadi zake, kusikiliza sala zetu, na kututegemeza. Tunaweza pia kumutegemea Yehova kwa sababu ni mushikamanifu kwa wale wenye kumutumikia. (2 Sa. 22:26) Hatasahau hata siku moya mambo yenye tunafanya, na kila wakati atakuwa tayari kutubariki.—Ebr. 6:10; 11:6.

7. Tutajionea nini wakati tunamutegemea Yehova? (Ona pia picha.)

7 Tunamufanya Yehova kuwa mwamba wetu wakati tunamutegemea kwa moyo wote. Tuko hakika kama tutapata faida wakati tunamutii hata mu hali za nguvu. (Isa. 48:​17, 18) Wakati tunajionea namna anatusaidia, tunamutegemea zaidi. Ile itatusaidia tukuwe tayari kupambana na magumu ya nguvu yenye Yehova tu njo anaweza kutusaidia kupambana nayo. Mara mingi ni wakati tunajikuta mu hali zenye hakuna mutu mwingine wa kutusaidia, njo tunatambua kama Yehova ni mwenye kutegemeka sana. Ndugu Vladimir anasema hivi: “Wakati nilikuwa mufungwa, nilijisikia kuwa karibu sana na Yehova. Nilijifunza kumutegemea Yehova zaidi juu nilikuwa tu peke yangu, na Yehova tu njo angeweza kunisaidia kuvumilia.”

Tunamufanya Yehova kuwa Mwamba wetu wakati tunamutegemea kwa moyo wote (Ona fungu ya 7)


8. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama Yehova habadilikake ? (b) Tunapata faida gani wakati tunamufanya Yehova kuwa mwamba wetu? (Zaburi 62:​6, 7)

8 Yehova habadilikake. Sawa vile mwamba mukubwa, Yehova ni uleule. Utu wake na kusudi yake havibadilikake. (Mal. 3:6) Wakati wanadamu waliasi mu Edeni, Yehova hakubadilisha kusudi yake kwa ajili ya wanadamu. Kama vile mutume Paulo aliandika, Yehova “hawezi kujikana yeye mwenyewe.” (2 Ti. 2:13) Ile inamaanisha kama hata kutokee nini ao wengine wafanye nini, Yehova hawezi kubadilisha sifa zake, kusudi yake, ao kanuni zake. Juu Yehova hawezi kubadilika, tuko hakika kama anaweza kutuokoa na kutusaidia mu wakati wa magumu.—Soma Zaburi 62:​6, 7.

9. Mufano wa Tatyana unakukumbusha nini?

9 Wakati tunafikiri juu ya sifa za Yehova na kusudi yake juu ya wanadamu na dunia, ile inatusaidia tumutumainie na kumufanya kuwa mwamba wetu. Kufanya vile kutatusaidia tubakie wenye kutulia na waaminifu wakati tunapambana na majaribu. (Zb. 16:8) Tatyana mwenye alifungwa juu ya imani yake, alijionea vile. Anasema hivi: “Nilijikuta peke yangu. Ku mwanzo ilikuwa nguvu, na mara mingi nilivunjika moyo.” Lakini, wakati alianza kufikiri juu ya Yehova na kusudi yake kwa ajili ya wanadamu, alielewa juu ya nini alipaswa kuvumilia magumu. Ile ilimusaidia atulie na ilimupatia nguvu ya kuvumilia. Anasema tena hivi: “Kuelewa juu ya nini ile mambo ilikuwa nanifikia, kulinisaidia kukumbuka kama nilijikuta mu ile hali juu niko muaminifu kwa Yehova. Ile ilinisaidia niache kujifikiria miye mwenyewe.”

10. Namna gani Yehova anaweza kuwa Mwamba wetu leo?

10 Mu siku zenye ziko nakuya, tutakutana na magumu ya nguvu yenye itaomba tumutegemee Yehova tena zaidi. Hii njo wakati ya kutia imani yetu nguvu na kuwa hakika kabisa kama Yehova atatusaidia kuvumilia kwa uaminifu. Tunaweza kufanya vile namna gani? Soma habari kuhusu watumishi wa Yehova wenye kuzungumuziwa mu Biblia na kuhusu watumishi wa Yehova leo. Ona namna Yehova ametegemeza watumishi wake. Fikiria sana zile habari. Kufanya vile kutakusaidia ufanye Yehova kuwa Mwamba wako.

IGA SIFA ZENYE ZINAMUFANYA YEHOVA KUWA MWAMBA

11. Juu ya nini tunapenda kuiga sifa zenye zinamufanya Yehova kuwa mwamba? (Ona pia kisanduku “ Muradi Wenye Ndugu Vijana Wanaweza Kujiwekea.”)

11 Tumeona sifa zenye zinamufanya Yehova kuwa mwamba. Tuone sasa namna tunaweza kuiga zile sifa. Kadiri tunajikaza kuiga zile sifa za Yehova, ni vile tutakuwa tayari kutia nguvu ndugu na dada zetu. Kwa mufano, Yesu alipatia Simoni jina Kefa (yenye inatafsiriwa “Petro”), yenye inamaanisha “Kipande ya Mwamba.” (Yoh. 1:42) Ile ilionyesha kama Petro angetia nguvu na kutegemeza wengine mu kutaniko. Wazee wa kutaniko wanafananishwa na “kivuli cha mwamba mukubwa.” Ile inaonyesha namna wanalinda kutaniko. (Isa. 32:2) Lakini, kutaniko inapata faida wakati ndugu na dada wote wanajikaza kuiga sifa zenye zinamufanya Yehova kuwa mwamba.—Efe. 5:1.

12. Ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kuwa kimbilio kwa wengine?

12 Ukuwe kimbilio. Wakati fulani, tunaweza kutolea ndugu zetu fasi ya kukimbilia wakati wa misiba ya asili ao vita. Vile mambo inaendelea kuwa mubaya sana mu “siku za mwisho,” ni wazi kwamba tutakuwa na nafasi mingi za kusaidiana. (2 Ti. 3:1) Tunaweza pia kuonyesha ndugu zetu upendo na kuwategemeza. Njia moya ya kufanya vile ni kuchangia hali ya muzuri ya kutaniko; kufanya ndugu na dada wajisikie kuwa wanakaribishwa muzuri na wanapendwa wakati wanafika ku Jumba ya Ufalme. Tunaishi mu dunia yenye watu wanatendeana mubaya na yenye kuwa na mahangaiko mingi. Kwa hiyo, wakati ndugu na dada wanafika ku mikutano, tunajikaza kufanya yote yenye tunaweza ili wajisikie kuwa wanapendwa, wanatiwa moyo, na wako salama.

13. Namna gani wazee wanaweza kuwa kimbilio kwa ajili ya wengine? (Ona pia picha.)

13 Wazee wanaweza kuwa kimbilio kwa wale wenye wanapambana na magumu mbalimbali. Wakati wa misiba na wakati wa matatizo ya afya yenye inaomba kutenda kwa haraka, wazee wanakamata mipango ya kusaidia. Wanatoa pia musaada wa kiroho. Ndugu na dada watajisikia huru kukaribia muzee ikiwa ule muzee anajulikana kuwa mutu mupole, mwenye anajitia pa nafasi ya wengine, na mwenye iko tayari kusikiliza. Zile sifa zinafanya wengine wajisikie kuwa wanahangaikiwa. Kwa hiyo inakuwa mwepesi kwao kutumikisha muongozo wenye kutegemea Biblia wenye muzee anaweza kuwatolea.—1 Te. 2:​7, 8, 11.

Wakati magumu mbalimbali inapata ndugu na dada, wazee ni kimbilio (Ona fungu ya 13) a


14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye kutegemeka?

14 Ukuwe mwenye kutegemeka. Tunapenda wengine watutumainie, zaidi sana wakati wanapambana na magumu. (Mez. 17:17) Tunaweza kufanya nini juu tukuwe watu wenye wengine wanaweza kutegemea? Tujikaze kila siku kuonyesha sifa za Kikristo. Kwa mufano tujikaze kutimiza ahadi zetu na kufanya yetu yote ili kuheshimia wakati. (Mt. 5:37) Tunaweza pia kusaidia wengine wakati wako na lazima ya musaada. Zaidi ya ile, tuhakikishe kama tunatimiza mugao wetu kulingana na maagizo yenye tumepewa.

15. Kutaniko inapata faida gani wakati wazee ni wenye kutegemeka?

15 Wazee wenye kutegemeka ni baraka kwa kutaniko. Namna gani? Wakati wazee wanapatikana wakati wowote wenye wahubiri wako nao lazima, wahubiri wanajisikia kuwa wenye kutulia. Wanajisikia pia kuwa wanahangaikiwa muzuri wakati wanajua kama wazee wako tayari kuwasaidia. Wanatumainia wazee wakati wanaona kama mashauri yao inategemea Biblia na vichapo vya mutumwa muaminifu na mwenye busara kuliko kutegemea mawazo yao wenyewe. Ndugu na dada wanatumainia zaidi sana muzee mwenye anajua kuchunga siri na mwenye anatimiza mambo yenye anaahidi.

16. Wakati hatuko watu wa kubadilisha-badilisha musimamo ile inaleta faida gani kwetu na kwa wengine?

16 Usibadilishe-badilishe musimamo. Tunaweza kuwa mufano muzuri kwa wengine kama tunashikamana na mambo ya muzuri na kama tunakamata maamuzi yenye inategemea kabisa kanuni za Biblia. Kadiri tunaendelea kuwa na imani ya nguvu na kuendelea kuwa na ujuzi wa kweli, ni vile tunakuwa imara zaidi katika kweli. Hatuko watu wenye kusitasita, wenye kuyumbayumba, ao wenye kudanganywa haraka na mafundisho ya uongo na mawazo ya ulimwengu. (Efe. 4:14; Yak. 1:​6-8) Juu tuko na imani kwa Yehova na tunaamini ahadi zake, ile inafanya tukuwe wenye kutulia wakati tunapata habari za mubaya. (Zb. 112:​7, 8) Tuko pia tayari kusaidia wale wenye wanapambana na majaribu.—1 Te. 3:​2, 3.

17. Namna gani wazee wanasaidia wengine wasiyumbeyumbe?

17 Wazee wanapaswa kuwa na kiasi, na akili ya muzuri, wenye utaratibu, na wenye usawaziko. Wazee wanasaidia wengine wasiyumbeyumbe na wanatia kutaniko nguvu ili ‘ishikamana kabisa na neno la uaminifu.’ (Tit. 1:9; 1 Ti. 3:​1-3) Kupitia mufano wao na kazi yao ya uchungaji, wazee wanasaidia wahubiri wakuwe wanakusanyika na kuhubiri kwa ukawaida, na wakuwe wanafanya funzo yao ya kipekee. Wakati ndugu na dada wanapambana na mambo yenye inawaletea mahangaiko, wazee wanawatia moyo wamutegemee Yehova na wakazie akili ahadi zake.

18. Juu ya nini tunapenda kumusifu Yehova na kumukaribia zaidi? (Ona pia kisanduku “ Namna ya Kumukaribia Yehova.”)

18 Kisha kuona sifa za ajabu za Yehova, tunaweza pia kusema hivi kama Mufalme Daudi: “Yehova, Mwamba wangu, asifiwe.” (Zb. 144:1) Tunaweza kumutegemea Yehova kila siku. Hata wakati tutazeeka, tuko hakika kama Yehova ataendelea kutusaidia kuwa karibu naye na tuko na sababu ya kusema: “Yeye ni Mwamba wangu.”—Zb. 92:​14, 15.

WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe

a MAFASIRIO YA PICHA: Ku Jumba ya Ufalme, dada anajisikia huru kukaribia wazee.