Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 23

WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?

Yehova Anatualika Tukuwe Wageni Wake

Yehova Anatualika Tukuwe Wageni Wake

“Hema yangu itakuwa pamoja nao, na mimi nitakuwa Mungu wao.”EZE. 37:27.

WAZO KUBWA

Kutusaidia kuelewa maana ya kuwa wageni mu hema ya mufano ya Yehova, na namna Yehova anahangaikia wageni wake.

1-2. Yehova anapatia mwaliko gani waabudu wake washikamanifu?

 KAMA mutu anakuuliza Yehova ni nani mu maisha yako, utajibu namna gani? Unaweza kujibu, ‘ni Baba yangu, Mungu wangu, na Rafiki yangu.’ Na kuko majina ingine mingi ya cheo yenye unaweza kumuita. Lakini, unamuona pia Yehova kuwa mutu mwenye anakualika kwake?

2 Mufalme Daudi alionyesha kama uhusiano wenye Yehova iko nao pamoya na waabudu wake washikamanifu uko sawa uhusiano wenye kuwa kati ya mugeni na mutu mwenye alimualika. Daudi aliuliza hivi: “Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako? Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?” (Zb. 15:1) Ile maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu inaonyesha kama tunaweza kuwa wageni wa Yehova, ni kusema marafiki wake. Hauone kama ule ni mualiko wa muzuri sana?

YEHOVA ANAPENDA TUKUWE WAGENI WAKE

3. Ni nani alikuwa mugeni wa kwanza wa Yehova, na Yehova na mugeni wake walijisikia namna gani?

3 Mbele aanze kuumba, Yehova alikuwa peke yake. Lakini wakati fulani, aliumba Mwana wake muzaliwa wa kwanza. Alimualika mu hema yake ya mufano na ile ilimufurahisha sana. Biblia inasema kama Yehova “alipenda sana” Mwana wake. Mugeni wake wa kwanza, ni kusema Mwana wake, ‘alifurahi [pia] mbele yake wakati wote.’—Mez. 8:30.

4. Namna gani Yehova aliendelea kuongeza wageni hatua kwa hatua mu hema yake?

4 Kisha Yehova aliumba viumbe wengine wa roho, aliwaalika ili wao pia wakuwe wageni wake. Malaika wake wanaitwa kuwa ‘wana wa Mungu’ na Biblia inaonyesha kama wanafurahi kuwa pamoya naye. (Yob. 38:7; Da. 7:10) Kwa wakati fulani, marafiki wa Yehova walikuwa tu wale wenye walikuwa naishi pamoya naye mbinguni. Kisha aliumba wanadamu ku dunia. Nao pia wangekuwa wageni mu hema yake. Kisha wakati, kati ya wanadamu wenye walifikia kuwa wageni wa Yehova kulikuwa Enoko, Noa, Abrahamu, na Yobu. Biblia inasema kama wale waabudu wa kweli walikuwa marafiki wa Mungu, ao walitembea “pamoja na Mungu wa kweli.”—Mwa. 5:24; 6:9; Yob. 29:4; Isa. 41:8.

5. Unabii wenye kuwa mu Ezekieli 37:​26, 27 unatufundisha nini?

5 Kwa miaka mingi, Yehova aliendelea kualika marafiki wake ili wakuwe wageni wake. (Soma Ezekieli 37:​26, 27.) Kwa mufano, unabii wa Ezekieli unaonyesha kama Mungu anapenda kabisa waabudu wake washikamanifu wakuwe na urafiki wa karibu pamoya naye. Anaahidi kufanya “agano la amani pamoja nao.” Ule unabii unazungumuzia wakati wenye wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi mbinguni na wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi milele ku dunia, wataunganishwa na kuwa “kundi moja” mu hema yake ya mufano. (Yoh. 10:16) Ule unabii uko natimia mu wakati wetu!

MUNGU ANATUHANGAIKIA FASI YOYOTE KWENYE TUKO

6. Namna gani mutu anafikia kuwa mugeni mu hema ya Mungu, na hema yake inapatikana wapi?

6 Zamani, hema ya mutu ilikuwa fasi ya kupumuzikia, na fasi kwenye mutu angeweza kujilinda na mvua ao jua. Mugeni mu ile hema alitazamia kuwa atahangaikiwa muzuri. Wakati tunatoa maisha yetu kwa Yehova, tunakuwa wageni mu hema yake ya mufano. (Zb. 61:4) Tunapata chakula mingi ya kiroho na tunafurahia uhusiano wa muzuri pamoya na wageni wengine wa Yehova. Hema ya mufano ya Yehova haiko tu fasi moya. Inawezekana ulishaendaka mu inchi ingine, pengine juu ya kuhuzuria mukusanyiko wa pekee, na ulikutana na watu wengine wenye wako pia na pendeleo ya kuwa mu hema ya Mungu. Hema ya Mungu iko fasi yoyote kwenye waabudu wake watiifu wanapatikana.—Ufu. 21:3.

7. Juu ya nini tunaweza kusema kama waaminifu wenye walishakufa wangali wageni mu hema ya Yehova? (Ona pia picha.)

7 Tuseme nini juu ya watu waaminifu wenye wamekufa? Tunaweza kusema kama wangali wageni mu hema ya Yehova? Ndiyo! Juu ya nini tunasema vile? Juu Yehova anaendelea kuwakumbuka. Yesu alisema hivi: “Wafu watafufuliwa, hata Musa alionyesha jambo hilo katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, wakati anamuita Yehova ‘Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ Yeye haiko Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wenye kuwa wazima, kwa maana kwake wote ni wazima.”—Lu. 20:​37, 38.

Tunaweza kusema kama hata waaminifu wenye wamekufa wangali wageni mu hema ya Mungu (Ona fungu ya 7)


FAIDA NA PIA MADARAKA

8. Wageni wa Yehova wanapata faida gani juu wako mu hema yake?

8 Hema ni fasi ya kupumuzikia na pia inatulinda wakati wa mvua na jua. Wageni wenye wako mu hema ya Yehova wanalindwa na mambo yenye inaweza kuharibu hali yao ya kiroho, na wanapata tumaini juu ya wakati wenye kuya. Wakati tunabakia karibu na Yehova, Shetani hawezi kutufanyia jambo yoyote yenye inaweza kutuumiza milele. (Zb. 31:23; 1 Yo. 3:8) Mu dunia mupya, Yehova ataendelea kulinda kiroho marafiki wake waaminifu lakini pia atawalinda ili wasikufe tena.—Ufu. 21:4.

9. Yehova anatazamia wageni wake wafanye nini?

9 Ni pendeleo kubwa kuwa mugeni mu hema ya Yehova, ni kusema kuwa na uhusiano wa pekee na wa milele pamoya naye. Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa wageni mu hema yake? Kama mutu fulani anakualika kwake, utapenda kujua mambo yenye anatazamia ufanye. Kwa mufano, anaweza kutazamia utoshe viatu mbele ya kuingia mu nyumba, na utakuwa tayari kufanya vile. Vilevile, tunapenda kujua mambo yenye Yehova anaomba wageni wake wafanye. Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea tufanye yetu yote “ili kumupendeza kwa ukamili.” (Kol. 1:10) Ni kweli kwamba Yehova ni rafiki yetu, lakini pia ni Mungu wetu na Baba yetu, na kwa hiyo anastahili heshima kutoka kwetu. (Zb. 25:14) Hatupaswe kusahau ile hata siku moya, na tunapaswa kumuheshimia sikuzote. Kufanya vile kutatusaidia tuepuke tabia zenye zinaweza kumukasirisha. Sikuzote tunapenda ‘kutembea kwa kiasi’ pamoya na Mungu wetu.—Mik. 6:8.

MU JANGWA YEHOVA ALIONYESHA KAMA HANA UBAGUZI

10-11. Namna Yehova alitendea Waisraeli mu jangwa ya Sinai inatuonyesha namna gani kama hana ubaguzi?

10 Yehova anatendea wageni wake bila ubaguzi. (Ro. 2:11) Ile inaonekana mu namna alitendea Waisraeli mu jangwa ya Sinai.

11 Kisha kukomboa watu wake kutoka mu utumwa katika Misri, Yehova aliweka Makuhani ili watumikie ku tabenakulo. Walawi walikuwa na mugao wa kufanya kazi zingine mbalimbali ku tabenakulo. Je, wale wenye walikuwa natumika ku tabenakulo ao wenye waliishi karibu na tabenakulo njo wenye Yehova alihangaikia sana kupita wengine? Hapana! Yehova hana ubaguzi.

12. Namna Yehova alitendea wageni wake Waisraeli ilionyesha namna gani kama hana ubaguzi? (Kutoka 40:38) (Ona pia picha.)

12 Kila mutu mu kambi alikuwa na nafasi ileile ya kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova, hata ikuwe alikuwa na mugao gani ao ikuwe aliishi karibu ao mbali na tabenakulo. Kwa mufano, Yehova alihakikisha kama taifa yote ingeweza kuona nguzo ya wingu na nguzo ya moto yenye aliweka kwa njia ya muujiza juu ya tabenakulo. (Soma Kutoka 40:38.) Wakati wingu ilianza kuenda upande fulani, hata wale wenye walikuwa mbali sana na tabenakulo wangeweza kuiona, kukusanya vitu vyao, kubomoa hema za familia yao, na kuanza kufuata ile wingu pamoya na taifa yote. (Hes. 9:​15-23) Wote wangeweza kusikia mulio mukubwa wa tarumbeta mbili za feza wenye ulionyesha kama watu wote walipaswa kuenda. (Hes. 10:2) Ni wazi kwamba, haiko kuishi karibu na tabenakulo njo kungeonyesha kama mutu iko na urafiki wa karibu pamoya na Yehova. Lakini, kila mutu mu ile taifa angeweza kuwa mugeni mu hema ya Yehova na kuwa hakika kama Yehova atamutolea muongozo na kumulinda. Ni vile pia leo, hata kama tunaishi wapi ku dunia, Yehova anatupenda, anatuhangaikia, na kutulinda.

Mupango wa Mungu juu ya tabenakulo ulionyesha kama hana ubaguzi (Ona fungu ya 12)


NAMNA YEHOVA ANAONYESHA KAMA HANA UBAGUZI LEO

13. Leta mufano wa njia moya yenye Yehova anaonyesha kama hana ubaguzi leo.

13 Wamoja kati ya watu wa Mungu leo wanaishi karibu na makao makubwa ao karibu na biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova. Na hata wengine wanatumikia ku ile majengo. IIe inafanya wakuwe na nafasi ya kusaidia mu mambo mbalimbali yenye inafanyika mu ile majengo, na hata kuwa karibu na wale wenye kuongoza. Wengine ni waangalizi wa muzunguko ao wako mu aina ingine ya utumishi wa pekee wa wakati wote. Kama uko kati ya Wakristo wengi sana wenye kwa sasa hawako mu ile aina ya utumishi, ukuwe hakika kama Yehova anapenda wageni wake wote. Anakujua kipekee na anakuhangaikia. (1 Pe. 5:7) Watu wote wa Yehova wanapata chakula ya kiroho, muongozo, na ulinzi wenye wako nao lazima.

14. Ni nini ingine inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi?

14 Jambo ingine yenye inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi ni hii: Anahakikisha kama watu wote mu dunia wanaweza kupata Biblia. Maandiko Matakatifu iliandikwa mu luga tatu za kwanza-kwanza: Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Je, wale wenye wanajua kusoma zile luga wako na urafiki wa karibu pamoya na Yehova kuliko watu wengine? Hapana.—Mt. 11:25.

15. Nini njo inahakikisha kama Yehova hana ubaguzi? (Ona pia picha.)

15 Haiko masomo yenye tulisoma ao uwezo wetu wa kujua luga fulani njo unafanya Yehova atukubali. Haiko wale wenye walisoma sana njo tu Yehova anapatiaka hekima yake. Watu wote wenye kuwa ku dunia wanaweza kupata hekima yake, ikuwe walisoma sana ao hapana. Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake takatifu, imetafsiriwa mu maelfu ya luga. Kwa hiyo, watu mu dunia yote wanaweza kupata mafundisho yake na kujifunza mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake.—2 Ti. 3:​16, 17.

Juu Biblia imetafsiriwa mu luga za mingi leo, ile inaonyesha namna gani kama Yehova hana ubaguzi? (Ona fungu ya 15)


ENDELEA ‘KUKUBALIWA’ NA YEHOVA

16. Kulingana na Matendo 10:​34, 35, tunaweza kufanya nini juu Yehova aendelee kutukubali?

16 Ni pendeleo kubwa sana kuwa wageni wa Yehova mu hema yake ya mufano. Yehova ni mwema, ni mwenye upendo zaidi, na ni mukarimu sana kupita watu wote. Zaidi ya ile, hana ubaguzi, anakaribisha watu wote ikuwe wanaishi wapi, walikomala namna gani, walisoma ao hapana, ikuwe ni wa rangi gani ya ngozi, wa kabila gani, wa miaka ngapi, ao ikuwe ni wanaume ao wanamuke. Lakini, ni wale tu wenye wanaendelea kumutii, njo wenye anakubali kuwa wageni wake.—Soma Matendo 10:​34, 35.

17. Ni wapi njo tutapata habari zaidi juu ya mambo yenye tunapaswa kufanya ili tuendelee kuwa wageni mu hema ya Yehova?

17 Mu Zaburi 15:​1, Daudi aliuliza hivi: “Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako? Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?” Kisha Yehova alimuongoza Daudi ili alete jibu ya ile maulizo. Mu habari yenye kufuata tutazungumuzia mambo fulani yenye tunapaswa kutimiza ili tuendelee kukubaliwa na Yehova.

WIMBO 32 Ukuwe Upande wa Yehova!