Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 24

WIMBO 24 Tuende ku Mulima wa Yehova

Endelea Kuwa Mugeni wa Yehova Milele!

Endelea Kuwa Mugeni wa Yehova Milele!

“Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako?”ZB. 15:1.

WAZO KUBWA

Ona mambo yenye Yehova anatuomba tufanye ili tuendelee kuwa marafiki wake, na namna anapenda tutendee marafiki wake wengine.

1. Juu ya nini ni jambo ya maana tuchunguze Zaburi 15:​1-5?

 MU HABARI yenye kutangulia, tuliona kama wale wenye wamejitoa kwa Yehova na wanajikaza kuwa na urafiki wa karibu pamoya naye, wanaweza kuwa wageni mu hema yake ya mufano. Lakini tunaweza kufanya nini ili tukuwe wageni wa Yehova? Zaburi 15 inatuonyesha mambo ya kufanya. (Soma Zaburi 15:​1-5.) Ile Zaburi inatuambia mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe na urafiki wa karibu pamoya na Mungu.

2. Pengine Daudi alikuwa nafikiria nini wakati alizungumuzia hema ya Yehova?

2 Zaburi ya 15 inaanza na hii maneno: “Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako?” (Zb. 15:1) Wakati Daudi alizungumuzia “hema” ya Yehova, pengine alikuwa nafikiria tabenakulo yenye ilikuwa Gibea kwa wakati fulani. Pia wakati Daudi alizungumuzia “mulima mutakatifu” wa Yehova, pengine alikuwa nafikiria mulima Sayuni katika Yerusalemu. Ni kule Sayuni, yenye ilikuwa ku kilometre fulani kutoka Gibea, njo Daudi alifanya hema na walitia ndani sanduku ya agano mupaka wakati hekalu ilijengwa.—2 Sa. 6:17.

3. Juu ya nini tunapenda kuelewa Zaburi 15? (Ona pia picha.)

3 Waisraeli wengi hawakuruhusiwa kutumikia ku tabenakulo, na zaidi sana hawakuruhusiwa kuingia ndani ya hema kwenye kulikuwa sanduku ya agano. Lakini watumishi wote waaminifu wa Yehova wangeweza kuwa wageni mu hema yake ya mufano kwa kuwa marafiki wake na kujikaza kuendelea kuwa marafiki wake. Siye wote tunapenda kuwa wageni wa Yehova. Zaburi 15, inazungumuzia sifa fulani zenye tunapaswa kuonyesha ili tuendelee kuwa marafiki wa Yehova.

Waisraeli mu wakati wa Daudi wangeweza kuwazia katika akili yao maana ya kuwa mugeni mu hema ya Yehova (Ona fungu ya 3)


TEMBEA BILA KOSA NA UZOEE KUFANYA MAMBO YENYE KUWA SAWA

4. Nini njo inaonyesha kama ubatizo haiko tu njo jambo yenye Yehova anatuomba kufanya? (Isaya 48:1)

4 Zaburi 15:​2, inaonyesha kama rafiki ya Mungu ni “ule mwenye anatembea bila kosa, mwenye anazoea kufanya mambo yenye kuwa sawa.” Maneno “anatembea” na “anazoea kufanya” inaonyesha kama tunapaswa kuendelea kufanya jambo fulani. Lakini inawezekana kabisa ‘kutembea bila kosa’? Ndiyo. Ni kweli kwamba hakuna mwanadamu mukamilifu. Lakini Yehova anaweza kuona kuwa ‘tunatembea bila kosa’ ikiwa tunafanya yetu yote ili kumutii. Wakati tunajitoa kwa Mungu na kubatizwa, ni sawa vile tunaanza safari pamoya na Mungu. Kumbuka kama zamani, kuwa mu taifa ya Israeli hakukufanya mara moya mutu astahili kuwa mugeni wa Yehova. Waisraeli fulani walikuwa namuitia Yehova, lakini hapana “katika kweli na haki.” (Soma Isaya 48:1.) Waisraeli waaminifu walipaswa kujifunza kuhusu mambo yenye Yehova anaomba na kuifuata. Leo pia, juu Mungu atukubali, haitoshe tu kubatizwa na kupitisha wakati pamoya na Wakristo mu kutaniko. Tunapaswa ‘kuzoea kufanya mambo yenye kuwa sawa.’ Ile inamaanisha nini?

5. Kumutii Yehova mu mambo yote maana yake nini?

5 Kwa Yehova, ‘kutembea bila kosa’ na ‘kuzoea kufanya mambo yenye kuwa sawa’ ni zaidi ya kuenda ku mikutano ku Jumba ya Ufalme. (1 Sa. 15:22) Tunapaswa kujikaza kumutii Mungu mu sehemu zote za maisha yetu, hata wakati tuko peke yetu. (Mez. 3:6; Muh. 12:​13, 14) Ni jambo ya maana tujikaze kumutii Yehova hata mu mambo ya kidogo-kidogo. Kufanya vile kunaonyesha kama tunamupenda kabisa, na ile inafanya atupende sana.—Yoh. 14:23; 1 Yo. 5:3.

6. Kulingana na Waebrania 6:​10-12, ni jambo gani yenye kuwa ya maana zaidi kupita mambo ya muzuri yenye tulifanya zamani?

6 Yehova anafurahia sana mambo yenye tulimufanyia zamani. Lakini haiko ile mambo tu njo itafanya tuendelee kuwa wageni mu hema ya Yehova. Ile inaonekana wazi mu Waebrania 6:​10-12. (Soma.) Yehova hasahau mambo ya muzuri yenye tulifanya zamani. Lakini anapenda tuendelee kumuabudu kwa moyo wote “mupaka mwisho.” Ataendelea kuwa rafiki yetu milele “kama hatuchoke kabisa.”—Gal. 6:9.

SEMA KWELI KATIKA MOYO WAKO

7. Kusema kweli katika moyo wetu maana yake nini?

7 Mutu mwenye anapenda Yehova amukubali kuwa mugeni mu hema yake, anapaswa “kusema kweli katika moyo wake.” (Zb. 15:2) Kusema kweli katika moyo haiko tu kuepuka kudanganya. Yehova anapenda tukuwe wanyoofu mu mambo yote. (Ebr. 13:18) Ile ni jambo ya maana juu “Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.”—Mez. 3:32.

8. Tunapaswa kuepuka kufanya nini?

8 Wale wenye ‘kusema kweli katika moyo wao’ hawajifanye kuwa watiifu wakati wako pamoya na watu wengi na kuvunja sheria ya Mungu wakati wako peke yao. (Isa. 29:13) Wanaepuka kutenda kwa udanganyifu. Mutu mudanganyifu anaweza kuwaza kama sheria fulani za Yehova hazifae. (Yak. 1:​5-8) Anaweza kukosa kumutii Yehova mu mambo yenye anaona kuwa ya kidogo kidogo. Kisha kama anaona kuwa matendo yake hailete matokeo ya mubaya, anaweza kuvunja sheria zingine za Mungu, na ile inafanya ibada yake ikuwe ya kinafiki. (Muh. 8:11) Lakini, tunapenda kuwa wanyoofu mu mambo yote.

9. Mambo yenye Yesu alisema wakati alikutana na Natanaeli kwa mara ya kwanza, inatufundisha nini ? (Ona pia picha.)

9 Mambo yenye Yesu alisema wakati alikutana na Natanaeli kwa mara ya kwanza inaweza kutufundisha jambo ya maana kuhusu kuwa na moyo wenye hauna udanganyifu. Wakati Filipo alileta rafiki yake Natanaeli ili akutane na Yesu, jambo fulani ya pekee ilitokea. Hata kama ilikuwa mara ya kwanza Yesu aonane na Natanaeli, alisema hivi: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.” (Yoh. 1:47) Ni kweli kama Yesu aliona wanafunzi wake wote kuwa wanyoofu, lakini aliona unyoofu wa pekee katika Natanaeli. Kama siye wote, Natanaeli pia hakukuwa mukamilifu. Lakini hakukuwa na udanganyifu ndani yake. Yesu alifurahia ile jambo na alimupongeza. Inaweza kuwa pendeleo kubwa sana kama Yesu anasema vile juu yetu!

Filipo analeta mbele ya Yesu rafiki yake Natanaeli, mwanaume mwenye hakukuwa na udanganyifu. Na weye unajulikana kuwa mutu mwenye hana udanganyifu? (Ona fungu ya 9)


10. Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunasema? (Yakobo 1:26)

10 Mambo mingi yenye Yehova anatuomba tufanye mu Zaburi 15 inahusu namna tunatendea wengine. Zaburi 15:3 inasema kama mugeni mu hema ya Yehova “hasingizie kwa ulimi wake, hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya, naye hawaharibishie marafiki wake sifa.” Kutumia mubaya ulimi wetu mu ile njia kunaweza kuumiza sana wengine na kufanya tusistahili tena kuwa wageni mu hema ya Yehova—Soma Yakobo 1:26.

11. Kusingizia maana yake nini, na kutaniko inafanya nini juu ya watu wenye wanasingizia wengine na hawapendi kutubu?

11 Muandikaji wa Zaburi anazungumuzia kusingizia. Kusingizia maana yake nini? Ni maneno ya uongo yenye inaweza kuharibu sifa ya mutu. Wenye wanasingizia wengine na hawapendi kutubu, wanatengwa na kutaniko.—Yer. 17:10.

12-13. Ni mu hali gani tunaweza kuharibishia marafiki wetu sifa bila kukusudia? (Ona pia picha.)

12 Zaburi 15:3 inatukumbusha kama wageni wa Yehova hawatendee majirani wao mambo ya mubaya na hawaharibishie marafiki wao sifa. Tunaweza kuharibishia wengine sifa namna gani?

13 Bila kukusudia, tunaweza kuharibishia mutu sifa kwa kueneza habari zenye haziko za kweli juu yake. Kwa mufano: (1) dada anaacha upainia, (2) bibi na bwana hawatumikie tena ku beteli, ao (3) ndugu haiko tena mutumishi wa huduma ao muzee. Hauone kama haiko muzuri kuwazia-wazia sababu zenye zilifanya hali za wale watu zibadilike na kujaribu kuzielezea wengine? Pengine kuko sababu zenye zilifanya ile mabadiliko itokee zenye siye hatujue. Zaidi ya ile, mugeni mu hema ya Yehova “hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya, naye hawaharibishie marafiki wake sifa.”

Ni mwepesi kueneza habari zenye haziko za kweli juu ya wengine, pengine kwa kuwasingizia (Ona fungu ya 12-13)


HESHIMIA WALE WENYE KUMUOGOPA YEHOVA

14. Fasiria namna wageni wa Yehova wanaepuka “mutu yeyote mwenye kuzarauliwa”?

14 Zaburi 15:4 inasema kama rafiki ya Yehova “anamukataa mutu yeyote mwenye kuzarauliwa.” Tunaweza kufanya vile namna gani? Juu tuko wanadamu wenye hawakamilike, kwa uwezo wetu siye wenyewe hatuwezi kutambua ikiwa mutu fulani ni mwenye kuzaraulika ao hapana. Juu ya nini? Juu kwa kawaida tunavutiwaka na watu wenye wanatufurahisha na tunaepuka wenye hawatufurahishe. Lakini, tunapaswa kuepuka tu wale wenye Yehova anaona kuwa ‘wenye kuzarauliwa.’ (1 Ko. 5:11) Kwa mufano, tunapaswa kuepuka wale wenye wanafanya mambo ya mubaya lakini hawapende kutubu, wale wenye kuzarau imani yetu na mambo yenye tunaamini, ao wale wenye wanajaribu kuharibu hali yetu ya kiroho.—Mez. 13:20.

15. Ni mu njia gani tunaweza kuheshimia “wale wenye kumuogopa Yehova”?

15 Kwa upande mwingine, Zaburi 15:4 inatuomba tuheshimie “wale wenye kumuogopa Yehova.” Kwa hiyo tunatafuta njia za kuheshimia marafiki wa Yehova na kuwatendea mambo ya muzuri. (Ro. 12:10) Tunafanya vile namna gani? Njia moya inapatikana mu Zaburi 15:4 yenye kuonyesha kama mugeni mu hema ya Yehova “havunje ahadi yake, hata wakati inamuletea matatizo.” Kukosa kutimiza ahadi zetu kunaweza kuumiza wengine. (Mt. 5:37) Kwa mufano, Yehova anatazamia wageni wake waheshimie naziri ya ndoa. Pia anafurahi wakati wazazi wanajikaza kutimiza ahadi zenye wanafanyia watoto wao. Upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani utatuchochea tufanye yetu yote ili kutimiza ahadi zetu.

16. Tunaweza kufanya nini ingine ili kuheshimia marafiki wa Yehova?

16 Njia ingine ya kuonyesha kama tunaheshimia marafiki wa Yehova ni kuwa wakarimu na wakaribishaji-wageni. (Ro. 12:13) Wakati tunapitisha wakati pamoya na ndugu na dada ili kujifurahisha, ile inatia nguvu urafiki wetu pamoya nao na pamoya na Yehova. Zaidi ya ile, wakati tunakaribisha wengine, tunamuiga Yehova.

EPUKA KUPENDA FEZA

17. Juu ya nini feza inazungumuziwa mu Zaburi 15?

17 Zaburi 15 inaonyesha kama mugeni wa Yehova “hakopeshe feza zake kwa ajili ya faida, na hakubali rushwa ili kumutesa mwenye hana kosa.” (Zb. 15:5) Juu ya nini zaburi inazungumuzia feza ao makuta? Juu kuwa na maoni yenye haifae juu ya makuta kunaweza kuumiza wengine na kuharibu urafiki wetu pamoya na Mungu. (1 Ti. 6:10) Zamani, watu fulani walikuwa naonea ndugu zao maskini, walikuwa nawakopesha na kuwaomba faida. Pia, waamuzi fulani walikuwa wanakubali rushwa na kisha walikuwa nahukumu bila haki watu wenye hawakukuwa na kosa. Yehova anachukia matendo ya vile.—Eze. 22:12.

18. Ni maulizo gani inaweza kutusaidia kuchunguza namna yetu ya kuona makuta? (Waebrania 13:5)

18 Ni muzuri tuchunguze namna yetu ya kuona makuta. Ujiulize hivi: ‘Mara mingi ninajikutaka niko nafikiria makuta na vitu vyenye ninaweza kuuza? Kama wananikopesha makuta, ninachelewaka kulipa, na kuwaza kama mutu mwenye alinikopesha hana lazima ya ile makuta? Kuwa na makuta kunanifanya nijisikie kuwa mutu wa maana na kunanifanya nikuwe muchoyo? Ninahukumu ndugu na dada zangu kuwa wanapenda vitu vya kimwili juu tu wako na makuta? Ninafanyaka urafiki na matajiri na kuepuka maskini?’ Tuko na pendeleo kubwa sana ya kuwa wageni mu hema ya Yehova. Tunaweza kulinda ile pendeleo kwa kuendelea kuepuka kupenda makuta. Kama tunafanya vile, Yehova hatatuacha hata siku moya!—Soma Waebrania 13:5.

YEHOVA ANAPENDA MARAFIKI WAKE

19. Juu ya nini Yehova anatuomba tufanye mambo yenye kuwa mu Zaburi 15?

19 Zaburi 15 inaisha na hii maneno: “Mutu yeyote mwenye kufanya mambo hayo hatatikiswa hata kidogo.” (Zb. 1 5:5) Mu ile andiko, muandikaji wa Zaburi anaonyesha sababu yenye inafanya Yehova atuombe kufanya mambo yenye kuwa mu Zaburi 15. Anapenda tukuwe na furaha. Kwa hiyo, kama tunafuata muongozo wake, tutapata baraka na ulinzi.—Isa. 48:17.

20. Wageni wa Yehova wako na tumaini gani?

20 Wale wenye Yehova anakubali kuwa wageni wake, wako na tumaini ya muzuri ya wakati wenye kuya. Wakristo waaminifu watiwa-mafuta wataenda katika “makao mengi” yenye Yesu amewatayarishia mbinguni. (Yoh. 14:2) Wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi milele ku dunia wanangoya kwa hamu kutimizwa kwa ahadi zenye kuwa mu Ufunuo 21:3. Kwa kweli, siye wote tunaona kuwa ni pendeleo kubwa sana kualikwa na Yehova ili kuwa marafiki wake, ni kusema kuwa wageni milele mu hema yake!

WIMBO 39 Tujifanyie Jina ya Muzuri Mbele ya Mungu