Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 SIERRA LEONE NA GUINEA

Kitu Bora Zaidi Kuliko Almasi

Tamba Josiah

Kitu Bora Zaidi Kuliko Almasi
  • ALIZALIWA 1948

  • ALIBATIZWA 1972

  • MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Alifanya kazi kwenye migodi ya almasi kabla ya kupata kweli. Sasa ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi nchini Sierra Leone..

MNAMO 1970, nilifanya kazi katika kampuni ya Uingereza ya uchimbaji madini kwenye eneo la Tongo Fields lenye utajiri wa almasi ambalo liko kaskazini mwa Kenema. Pia, nilitumia muda wangu wa ziada kuchimba almasi zangu mwenyewe. Kila nilipopata almasi, ningevaa vizuri na kuelekea jijini Kenema kuuza vito hivyo na kujiburudisha.

Mwaka 1972, nilikutana na Mashahidi wa Yehova na nikaanza kujifunza Biblia. Miezi mitano baadaye, nilistahili kubatizwa. Kwa kuwa nilikuwa nimemaliza siku zangu za likizo, nilimwomba mfanyakazi mwenzangu anishikie zamu yangu ili niweze kuhudhuria kusanyiko la wilaya na kubatizwa. Alikubali, hata hivyo akanipa sharti moja kwamba nimpe mshahara wangu wa wiki moja. Ubatizo wangu ulikuwa na maana kubwa kuliko fedha, hivyo nilikubali ombi lake mara moja. Niliporudi kutoka kusanyikoni, akaniambia nisimlipe kwa sababu kumtumikia Mungu ni jambo la maana sana. Miezi sita baadaye, niliacha kazi yangu yenye mshahara mkubwa ili nijiwekee hazina mbinguni nikiwa painia wa pekee.—Mt.6:19, 20.

Kwa miaka 18 nilitumikia sehemu mbalimbali nchini nikiwa painia wa pekee na mwangalizi wa mzunguko. Wakati huohuo, nilimwoa Christiana, mwenzi mwaminifu na anayeniunga mkono, na tulibarikiwa kupata binti anayeitwa, Lynette.

Wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone, mimi na Christiana tulikuwa tukipainia jijini Bo, jiji hilo liko kwenye eneo lingine kubwa la uchimbaji wa almasi. Huko tulipata “almasi” nyingi za kiroho, yaani, wanafunzi wa kweli wa Kristo. Ndani ya miaka minne, kutaniko letu lilikua kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 60. Sasa jiji la Bo lina makutaniko matatu yanayosonga mbele vizuri.

Mnamo 2002, nilialikwa kuwa mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Sierra Leone. Mimi na Christiana tunaishi karibu na Betheli. Mimi huenda kufanya kazi Betheli na kurudi nyumbani kila siku, huku Christiana akiendelea na utumishi wa painia wa pekee. Lynette anafanya kazi Betheli kwenye timu ya utafsiri ya Krio.

Wakati fulani nilitafuta almasi halisi, lakini nilipata kitu bora zaidi—utajiri wa kiroho. Pia, nimechimbua “almasi” 18 za kiroho, yaani, wanafunzi wa kweli wa Kristo. Kwa kweli, Yehova amenibariki kwa kiwango kikubwa sana.

I Wakati fulani nilitafuta almasi halisi, lakini nilipata kitu bora zaidi—utajiri wa kiroho