Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 SIERRA LEONE NA GUINEA

Nimeazimia Kumtumikia Yehova

Philip Tengbeh

Nimeazimia Kumtumikia Yehova
  • ALIZALIWA 1966

  • ALIBATIZWA 1997

  • MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Mkimbizi ambaye alisaidia kujenga Majumba matano ya Ufalme.

MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Mkimbizi ambaye alisaidia kujenga Majumba matano ya Ufalme.

MNAMO 1991, mimi na mke wangu, Satta, tulikimbia ili kuokoa maisha yetu wakati wanajeshi waasi walipouvamia mji tulioishi, Koindu, nchini Sierra Leone. Kwa zaidi ya miaka nane, tuliishi katika kambi mbalimbali za wakimbizi. Katika kambi hizo, tulikabiliana na hali ngumu kama vile upungufu wa chakula, magonjwa na tulizungukwa na majirani waliojihusisha katika upotovu wa maadili.

Katika kila kambi, tuliziomba kiwanja mamlaka husika ili tujenge Jumba la Ufalme. Nyakati fulani maombi yetu yalikubaliwa au kukataliwa. Hata hivyo, siku zote tulipanga mahali pa kukutana kwa ajili ya ibada. Tulikuwa tumeazimia kumtumikia Yehova. Hatimaye, tulijenga Majumba ya Ufalme manne katika kambi hizo.

Vita vilipoisha, hatungeweza kurudi nyumbani. Mji wa Koindu ulikuwa umeharibiwa kabisa na mapigano hayo yaliyodumu kwa miaka kadhaa. Kwa hiyo tukapelekwa kwenye kambi nyingine ya wakimbizi iliyokuwa karibu na jiji la Bo. Tukiwa huko, ofisi ya tawi ilitoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa Jumba la Ufalme, hivyo tukajenga jumba la tano.