Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Andiko la Mwaka 2014

“Ufalme Wako na Uje.”Mathayo 6:10

Andiko la Mwaka 2014

Miaka mia moja hivi iliyopita, Yehova alimtawaza Yesu kuwa Mfalme mbinguni. Tangu wakati huo, watumishi wa Mungu wamekuwa na bidii ya kuwajulisha watu kuhusu baraka ambazo Ufalme wa Kristo utaleta. Hebu wazia! Chini ya utawala wa Yesu, Mfalme mwenye upendo, dunia itakuwa paradiso, na kujaa watu wanaopendana kikweli. Hakutakuwa na uhalifu, kupigana, magonjwa, kuteseka, na kifo.

Hivi karibuni, baraka hizo zitatimia. Ufalme wa Mungu ni utawala halisi, nao utakuja na kutimiza mambo yote ambayo Yehova amekusudia. Sali Ufalme wa Mungu uje, waambie wengine kuuhusu, na endelea kuthamini mambo ambayo Ufalme huo utakufanyia.