Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hii Ndiyo Nafasi Yetu ya Kufanyia Ibada

Hii Ndiyo Nafasi Yetu ya Kufanyia Ibada

‘Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanikula.’YOHANA 2:17.

NYIMBO: 127, 118

1, 2. (a) Zamani, watumishi wa Yehova walimuabudu wapi? (b) Yesu aliona hekalu la Yerusalemu namna gani? (c) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

TANGU zamani watumishi wa Mungu wamekuwa na nafasi kwa ajili ya ibada. Kwa mufano, wakati Abeli alimutolea Yehova zabihu, inawezekana alijenga mazabahu. (Mwanzo 4:3, 4) Noa, Abrahamu, Isaka, Yakobo, na Musa walijenga mazabahu. (Mwanzo 8:20; 12:7; 26:25; 35:1; Kutoka 17:15) Yehova aliwaambia Waisraeli wajenge tabenakulo ao hema la ibada. (Kutoka 25:8) Kisha, Yehova aliwaambia wajenge hekalu. (1 Wafalme 8:27, 29) Kisha watu wa Mungu kurudia kutoka katika utumwa wa Babiloni, walianza kukusanyika kwa ukawaida katika masinagogi. (Marko 6:2; Yohana 18:20; Matendo 15:21) Na Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanakusanyika katika nyumba. (Matendo 12:12; 1 Wakorintho 16:19) Leo, Watumishi wa Yehova katika dunia yote wanakusanyika katika maelfu ya Majumba ya Ufalme, ambamo wanajifunza juu ya Yehova na kumuabudu.

2 Yesu aliheshimu sana hekalu la Yehova la Yerusalemu. Upendo wa Yesu kwa ajili ya hekalu uliwakumbusha wanafunzi wake maneno haya ya mutunga-zaburi: ‘Bidii nyingi kwa ajili ya nyumba yako imenikula.’ (Zaburi 69:9; Yohana 2:17) Jumba la Ufalme ni “nyumba ya Yehova,” lakini haiko sawa na hekalu la Yerusalemu la zamani. (2 Mambo ya Nyakati 5:13; 33:4) Lakini tunapaswa kuheshimu sana nafasi yetu ya kufanyia ibada. Katika habari hii, tutazungumuzia kanuni za Biblia zenye kutufundisha namna tunapaswa kujiendesha wakati tuko kwenye Jumba la Ufalme, namna tunapaswa kulitunza, na namna tunaweza kusaidia ili Majumba mengine ya Ufalme ijengwe. *—Ona maelezo ya chini.

TUNAHESHIMU MIKUTANO YETU

3-5. Jumba la Ufalme ni nini, na namna gani tunapaswa kuona mikutano yetu?

3 Kwa kawaida tunakutana kwenye Jumba la Ufalme ili kumuabudu Yehova. Mikutano ni zawadi kutoka kwa Mungu, na inatia nguvu urafiki wetu pamoja naye. Kwenye mikutano yetu, tengenezo lake linatutolea muongozo na vitia-moyo vyenye tuko navyo lazima. Yehova na Mwana wake wanatualika tukule kwenye “meza ya Yehova” kila juma. (1 Wakorintho 10:21) Hilo ni pendeleo kubwa. Tusisahau hata kidogo kwamba mwaliko huo ni wa pekee sana.

4 Yehova anatuambia waziwazi kwamba anapenda tukusanyike ili kumuabudu na kutiana moyo. (Soma Waebrania 10:24, 25.) Tunakusanyika kwa ukawaida kwa sababu tunamuheshimu Yehova. Kwa hiyo, hatupaswe kukosa mikutano bila sababu fulani ya lazima. Tunaonyesha kwamba tunapendezwa na mikutano yetu wakati tunaitayarisha na kujikaza kutoa maelezo.—Zaburi 22:22.

5 Namna tunajiendesha kwenye mikutano na kutunza Majumba yetu ya Ufalme inaonyesha kwamba tunamuheshimu sana Yehova. Kwa kawaida jina la Yehova linaandikwa kwenye Jumba la Ufalme; kwa hiyo, tunapenda kutukuza jina hilo kupitia mwenendo wetu.—Linganisha na 1 Wafalme 8:17.

6. Watu fulani wamesema nini juu ya Majumba yetu ya Ufalme na juu ya wale wenye kufika kwenye mikutano yetu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Wakati tunaheshimu Majumba yetu ya Ufalme, watu wengine wanatambua jambo hilo. Kwa mufano, mwanaume mumoja katika inchi ya Uturuki alisema hivi: “Nilishangazwa sana na usafi na utaratibu wenye niliona kwenye Jumba la Ufalme. Watu walikuwa wamevaa vizuri, walikuwa na sura ya furaha, na walinisalimia kwa furaha sana. Jambo hilo lilinishangaza sana.” Mwanaume huyo alianza kufika kwenye mikutano yote na kisha muda mufupi akabatizwa. Katika muji moja wa inchi ya Indonesia, ndugu walialika majirani, kiongozi wa muji, na wakubwa wengine kwenye Jumba la Ufalme lenye lilitoka tu kujengwa. Kiongozi huyo alishangazwa sana na namna Jumba hilo lilikuwa limejengwa vizuri, na bustani yake nzuri sana. Alisema hivi: “Usafi wa jumba hili unaonyesha kabisa kwamba muko na imani ya kweli.”

Namna tunajiendesha wakati wa mikutano inaweza kuonyesha kwamba hatumuheshimu Mungu(Ona fungu la 7, 8)

7, 8. Wakati tuko kwenye Jumba la Ufalme, namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamuheshimu Yehova?

7 Yehova anatualika kwenye mikutano, na anapenda tukuwe na mwenendo muzuri na tuvae vizuri wakati tunahuzuria mikutano. Kwa hiyo, tunaepuka kuvuka ao kupitisha mipaka. Hatutajitilia sheria nyingi kuhusu namna ya kuvaa, lakini tutaepuka kujiachilia na kuvaa ovyoovyo. Yehova anapenda sisi na watu wenye tunaalika kwenye Jumba la Ufalme tujisikie muzuri. Lakini hatupendi hata kidogo kuzarau mikutano yetu kwa njia yoyote. Ndiyo sababu hatuvae mavazi yenye kuvuka mipaka ao ya ovyoovyo, na tunaepuka kutumiana ujumbe kwenye telefone, kuzungumuza, ao kula na kunywa wakati wa mikutano. Na wazazi wanapaswa kuwakataza watoto wao kukimbia-kimbia ao kuchezea katika Jumba la Ufalme.—Mhubiri 3:1.

8 Wakati Yesu aliona watu wanauzishia vitu katika hekalu la Mungu, alikasirika sana na aliwafukuza inje. (Yohana 2:13-17) Katika Majumba yetu ya Ufalme, tunamuabudu Yehova na kujifunza juu yake. Kwa hiyo, hatupaswe kuzungumuzia ao kufanya biashara kwenye Jumba la Ufalme.—Linganisha na Nehemia 13:7, 8.

TUNASAIDIA KUJENGA MAJUMBA YA UFALME

9, 10. (a) Namna gani watumishi wa Yehova wanafikia kujenga Majumba ya Ufalme, na hilo limekuwa na matokeo gani? (b) Namna gani tengenezo la Yehova linasaidia makutaniko yenye haina uwezo wa kujijengea Jumba la Ufalme?

9 Watumishi wa Yehova katika dunia yote wanatumika sana ili kujenga Majumba ya Ufalme. Ndugu na dada wenye kujitolea, wanachapa plan, wanajenga, na kutengeneza upya Majumba ya Ufalme. Wanafanya hivyo bila kulipwa. Kwa hiyo, kwa miaka 15 yenye imepita, tumejenga Majumba ya Ufalme mazuri sana zaidi ya 28000 katika dunia yote, ni kusema, karibu Majumba tano ya Ufalme kila siku.

10 Tengenezo la Yehova linatolea migawo ndugu na dada wenye kujitolea, na linatumia michango ili kujenga Majumba ya Ufalme kila mahali kwenye kuwa lazima. Tunafuata kanuni ya Biblia yenye kuonyesha kwamba wale wenye kuwa na uwezo wasaidie wale wenye kukosewa. (Soma 2 Wakorintho 8:13-15.) Kumekuwa matokeo gani? Majumba mengi ya Ufalme imejengwa kwa ajili ya makutaniko yenye haina uwezo wa kujijengea.

11. Ndugu na dada fulani wamesema nini kuhusu Jumba lao mupya la Ufalme, na hilo linakufanya ujisikie namna gani?

11 Katika kutaniko moja la Kosta Rika, ndugu mumoja alisema hivi: “Wakati tunasimama mbele ya Jumba letu la Ufalme, inakuwa kama vile tunaota ndoto! Hatuamini jambo hilo. Jumba letu nzuri sana lilijengwa kwa siku munane tu! Tulipata jumba hilo kwa sababu Yehova alitubariki, kwa sababu ya mipango ya tengenezo lake, na kwa sababu ndugu na dada zetu wapendwa walitusaidia. Kwa kweli, nafasi hii ya ibada ni zawadi yenye bei kubwa kutoka kwa Yehova. Tunafurahia sana jumba hili.” Ni jambo lenye kufurahisha sana wakati tunasikia namna ndugu na dada zetu wanamushukuru Yehova juu ya mambo yenye amewafanyia. Na tunafurahi kuona kwamba ndugu na dada katika dunia yote wanaweza kupata Jumba lao la Ufalme. Inaonekana wazi kwamba Yehova anaendelea kubariki kazi yetu ya kujenga Majumba ya Ufalme, kwa sababu kisha tu kujengwa, watu wengi wanaanza kuhuzuria mikutano na kujifunza juu ya Yehova.—Zaburi 127:1.

12. Namna gani unaweza kusaidia katika kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme?

12 Namna gani unaweza kusaidia katika kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme? Pengine unaweza kujitolea katika kazi hiyo. Pia, kila mumoja wetu anaweza kutoa michango ili kusaidia katika kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme. Wakati tunafanya nguvu yetu yote ili kutegemeza kazi hiyo, tunakuwa na furaha kwa sababu tumetoa, na jambo la lazima zaidi ni kwamba tunamuletea Yehova sifa. Tunafuata mufano wa watumishi wa zamani wa Mungu, wenye walikuwa tayari kutoa michango ili kujenga nafasi zao za ibada.—Kutoka 25:2; 2 Wakorintho 9:7.

TUNAFANYA JUMBA LETU LA UFALME LIENDELEE KUWA SAFI

13, 14. Namna gani Biblia inaonyesha kwamba Jumba letu la Ufalme linapaswa kuendelea kuwa safi na lenye kupangwa vizuri?

13 Yehova ni Mungu mwenye kuwa safi na mutakatifu. Anapenda utaratibu. Ndiyo sababu Jumba letu la Ufalme linapaswa kuendelea kuwa safi na lenye kupangwa vizuri. (Soma 1 Wakorintho 14:33, 40.) Ili tukuwe safi na watakatifu kama Yehova, ibada yetu, mawazo na matendo yetu, na mwili wetu vinapaswa kuwa safi.—Ufunuo 19:8.

14 Wakati Jumba letu la Ufalme linaendelea kuwa safi na lenye kupangwa vizuri, hatutasikia haya kualika watu kwenye mikutano yetu. Kwa hiyo, watu wataona kwamba tunatumikisha kabisa mambo yenye tunafundisha kuhusu dunia mupya yenye kuwa safi. Wataona pia kwamba tunaabudu Mungu mwenye kuwa safi na mutakatifu ambaye atafanya dunia hii kuwa paradiso.—Isaya 6:1-3; Ufunuo 11:18.

15, 16. (a) Sababu gani kila mara haiko mwepesi kufanya Jumba la Ufalme liendelee kuwa safi? Sababu gani linapaswa kuendelea kuwa safi? (b) Namna gani kazi ya kusafisha Jumba lenu la Ufalme imepangwa, na kila mumoja wetu iko na pendeleo gani?

15 Watu wako na maoni tofauti juu ya usafi. Sababu gani? Pengine ni kwa sababu ya namna walikomaa. Pia, watu fulani wanaishi nafasi ya vumbi ao nafasi kwenye barabara ziko na vumbi ao matope. Wengine hawapate maji mengi ao dawa za kufanya usafi. Lakini, iwe watu wa eneo letu wako na maoni gani juu ya usafi ao iwe tunaishi wapi, Jumba letu la Ufalme linapaswa kuendelea kuwa safi na lenye kupangwa vizuri. Ni nafasi yetu ya kumuabudu Yehova.—Kumbukumbu la Torati 23:14.

16 Ikiwa tunapenda Jumba letu la Ufalme liendelee kuwa safi kabisa, tunapaswa kufanya mipango. Wazee wanafanya programu kwa ajili ya kutaniko na kuhakikisha kwamba kuna vyombo na dawa ya kutosha ili kufanya usafi. Pia, wazee wanaongoza kazi hiyo ili ifanywe vizuri. Vitu fulani vinapaswa kusafishwa kisha kila mukutano, na vingine kisha muda fulani. Kila mumoja wetu iko na pendeleo la kusaidia katika kazi ya kusafisha Jumba la Ufalme.

TUNALINDA JUMBA LETU LA UFALME KATIKA HALI NZURI

17, 18. (a) Namna watumishi wa zamani wa Yehova walitunza hekalu, inatufundisha nini? (b) Sababu gani tunapaswa kutunza Jumba letu la Ufalme?

17 Tunafanya pia Jumba letu la Ufalme liendelee kuwa katika hali nzuri kwa kutengeneza nafasi ao vitu fulani vyenye kuharibika. Watumishi wa zamani wa Yehova walifanya hivyo. Kwa mufano, wakati wa utawala wa Mufalme Yehoashi wa Yuda, watu walitoa michango ya feza kwa ajili ya hekalu. Mufalme aliwaamuru makuhani watumie feza hizo ili kutengeneza kila nafasi yenye kuharibika katika hekalu. (2 Wafalme 12:4, 5) Zaidi ya miaka 200 kisha hapo, Mufalme Yosia alitumia pia michango yenye ilitolewa kwenye hekalu ili kulitengeneza.—Soma 2 Mambo ya Nyakati 34:9-11.

18 Halmashauri fulani za Tawi zimetambua kwamba watu katika inchi zao hawazoee kutunza vizuri majengo ao vitu vyenye kuwa ndani. Pengine ni kwa sababu katika inchi hizo ni watu wadogo sana ndio wanajua namna ya kufanya kazi hiyo. Ao inawezekana hawana feza za kutosha ili kutengeneza. Lakini ikiwa hatutengeneze Jumba letu la Ufalme wakati inaomba kufanya hivyo, litaanza kuonekana ovyoovyo na watu watatambua jambo hilo. Halitawatolea ushahidi muzuri. Lakini, ikiwa sisi wote tunajikaza kutunza Jumba letu la Ufalme, tunamuletea Yehova sifa na tunaepuka kutumia vibaya michango ya ndugu na dada zetu.

Tunapaswa kulinda Jumba letu la Ufalme safi na katika hali nzuri(Ona fungu la 16, 18)

19. Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kwamba unaheshimu nafasi yetu ya kufanyia ibada ya Yehova?

19 Jumba la Ufalme ni jengo lenye limetolewa kwa Yehova. Haiko nyumba ya mutu ao ya kutaniko fulani. Kama vile tumejifunza katika habari hii, kanuni za Biblia zitatusaidia tujiendeshe vizuri nafasi zetu za kufanyia ibada. Tunaonyesha kwamba tunamuheshimu Yehova kwa kuheshimu mikutano yetu na Jumba letu la Ufalme. Tunafurahi kutoa michango ili Majumba ya Ufalme ijengwe, na tunatumika sana ili majumba hayo iendelee kuwa safi na katika hali nzuri. Kama Yesu, tunatumika kwa bidii na kuheshimu nafasi yetu ya kufanyia ibada ya Yehova.—Yohana 2:17.

^ fu. 2 Habari hii inahusu Majumba ya Ufalme. Lakini mambo yenye tutazungumuzia inahusu pia Majumba ya Mikusanyiko na nafasi zingine zenye tunatumia ili kumuabudu Yehova.