Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Ni Mungu wa Upendo

Yehova Ni Mungu wa Upendo

“Mungu ni upendo.”1 Yohana 4:8, 16.

NYIMBO: 18, 91

1. Sifa kubwa ya Mungu ni gani, na kujua jambo hilo kunakufanya ujisikie namna gani juu yake?

BIBLIA inasema kwamba “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Lakini, maneno hayo inamaanisha nini kabisa? Yehova iko na sifa nyingi nzuri. Lakini, upendo ndio sifa yake kubwa. Yehova iko na upendo, lakini pia yeye ni upendo. Mambo yote yenye anafanya inaongozwa na upendo. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu upendo ulimuchochea Yehova aumbe ulimwengu wote na vitu vyote vyenye kuwa ndani!

2. Upendo wa Mungu unatuhakikishia nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Yehova anahangaikia viumbe wake na kuwasikilia huruma. Upendo wake unatuhakikishia kwamba atatimiza kabisa mambo yenye amepanga kuwafanyia wanadamu. Kwa hiyo, wale wote wenye kumutii watakuwa na furaha ya kweli. Kwa mufano, kwa sababu ya upendo, Yehova ‘ameweka siku ambayo katika hiyo anakusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayoikaliwa kupitia mwanaume ambaye amemuweka,’ ni kusema, Yesu Kristo. (Matendo 17:31) Tuko hakika kwamba hukumu hiyo itakuja. Hukumu hiyo itawaletea wanadamu watiifu wakati unaokuja muzuri zaidi na wa milele.

MAMBO YENYE HISTORIA IMEONYESHA

3. Maisha ingekuwa namna gani ikiwa Mungu hakuwa anawapenda wanadamu?

3 Maisha ya wanadamu ingekuwa namna gani ikiwa Mungu hangekuwa na sifa kubwa ya upendo? Wanadamu wangeendelea kutawala wengine na kuendelea kuchochewa na Shetani, mungu mwenye hana upendo na mwenye chuki. (2 Wakorintho 4:4; 1 Yohana 5:19; soma Ufunuo 12:9, 12.) Ikiwa Yehova hangekuwa anatupenda, wakati wetu unaokuja ungekuwa mubaya sana!

4. Sababu gani Yehova ameruhusu Shetani na wanadamu wapinge utawala wake?

4 Wakati Shetani alipinga utawala wa Mungu, alichochea pia wazazi wetu wa kwanza wafanye hivyo. Alipinga haki ya Mungu ya kuwa mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi. Shetani alionyesha kwamba utawala wake ungekuwa muzuri zaidi kuliko utawala wa Mungu. (Mwanzo 3:1-5) Hekima ya Yehova ilimuchochea amuachie Shetani wakati mufupi ili ajaribu kuonyesha ikiwa utawala wake ndio wa muzuri zaidi. Lakini matokeo inaonyesha wazi kwamba wanadamu ao Shetani hawawezi kuwa watawala wazuri.

Wakati Yehova aliumba wanadamu, hakuwapatia uwezo ao haki ya kujitawala ao kujiongoza wao wenyewe

5. Historia ya wanadamu imeonyesha wazi jambo gani?

5 Ulimwengu unaendelea kuharibika leo. Katika miaka 100 yenye imepita, vita imeua watu zaidi ya milioni 100. Biblia inasema kwamba “katika siku za mwisho,” ‘watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.’ (2 Timotheo 3:1, 13) Biblia inasema tena hivi: ‘Ninajua vema [muzuri], Ee Yehova, kwamba njia ya mutu wa udongo haiko katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua [njia] yake.’ (Yeremia 10:23) Historia imeonyesha kwamba maneno hayo ni ya kweli. Wakati Yehova aliumba wanadamu, hakuwapatia uwezo ao haki ya kujitawala ao kujiongoza wao wenyewe.

6. Sababu gani Mungu ameruhusu mambo mabaya?

6 Kwa kuacha mambo mabaya iendelee kwa muda fulani, Yehova ameonyesha pia kwamba utawala wake ndio wa muzuri zaidi. Wakati unaokuja, Mungu ataharibu watu wabaya wote. Kisha hapo, atatenda bila kukawia ikiwa mutu fulani atapinga utawala wake. Anaweza kutumia mambo yenye historia ya wanadamu imeonyesha ili kuhakikisha kwamba watu kama hao wanapaswa kuangamizwa bila kukawia. Na hataruhusu tena hata kidogo mambo mabaya.

NAMNA GANI MUNGU AMEONYESHA UPENDO WAKE?

7, 8. Namna gani Yehova ameonyesha upendo wake?

7 Yehova ameonyesha upendo wake mukubwa katika njia nyingi. Fikiria ukubwa na uzuri wa anga letu. Liko na mamiliare ya galaksi, na kila galaksi iko na mamiliare ya nyota na sayari (planètes). Jua ni nyota moja kati ya nyota za Kikundi cha Nyota cha Kilimia, ni kusema, galaksi yetu. Bila jua, uzima haungekuwa hapa duniani. Vitu vyote hivyo vinahakikisha kwamba Yehova ndiye Muumbaji wetu, na vinaonyesha sifa zake, kama vile nguvu, hekima, na upendo. Kwa kweli, “sifa [za Mungu] ambazo hazionekane, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu.”—Waroma 1:20.

Kila kitu chenye Yehova aliumba duniani kinaletea wanadamu na wanyama faida

8 Yehova aliumba dunia ili wanadamu na viumbe vingine waishi ndani. Dunia inaletea wanadamu na wanyama faida. Mungu aliwatayarishia wanadamu makao mazuri sana ili waishi ndani na aliwapatia akili na mwili mukamilifu wenye ungewasaidia waishi milele. (Soma Ufunuo 4:11.) Zaidi ya hilo, ‘anawapa chakula wote wenye mwili, kwa maana fazili zake zenye upendo ni za wakati usio na kipimo [za milele].’—Zaburi 136:25.

9. Hata kama Yehova ni Mungu wa upendo, anachukia mambo gani?

9 Yehova ni Mungu wa upendo, lakini anachukia mambo mabaya. Kwa mufano, Zaburi 5:4-6 inasema hivi juu ya yake: “Wewe si Mungu anayependezwa na uovu . . . Wewe unawachukia wote wanaozoea kufanya mambo yenye kuumiza.” Anachukia pia ‘mutu [mwenye jeuri] na mudanganyifu.’

MAMBO MABAYA ITAISHA HIVI KARIBUNI

10, 11. (a) Watu wabaya watapatwa na nini? (b) Yehova atawafanyia nini wanadamu wenye kumutii?

10 Kwa sababu Yehova ni Mungu wa upendo na anachukia mambo mabaya, kwa wakati wenye kufaa, atamaliza mambo mabaya katika ulimwengu wote. Neno la Mungu linaahidi hivi: ‘Watenda-maovu watakatiliwa mbali [wataharibiwa], bali wale wanaomutumaini Yehova ndio watakaoimiliki [watariti] dunia. Bado muda kidogo tu, na mutu muovu hatakuwa tena.’ Maadui wa Yehova watafikia mwisho wao kama moshi.—Zaburi 37:9, 10, 20.

11 Neno la Mungu linaahidi tena hivi: “Waadilifu [wenye haki] wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Wanadamu waaminifu “watapata furaha yao tele [nyingi] katika wingi wa amani.” (Zaburi 37:11) Sababu gani? Kwa sababu sikuzote Mungu wetu mwenye upendo anawafanyia watumishi wake mambo mazuri kabisa. Biblia inatuambia hivi: ‘Atafuta [atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwa tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’ (Ufunuo 21:4) Huo utakuwa ni wakati muzuri sana kwa wanadamu watiifu wenye kupendezwa na upendo wa Mungu!

12. ‘Mutu asiye na lawama’ ni nani?

12 Biblia inatuambia hivi: ‘Umuangalie mutu asiye na lawama na uendelee kumuangalia munyoofu, kwa maana wakati ujao wa mutu huyo utakuwa wenye amani. Lakini wakosaji hakika wataangamizwa pamoja; wakati ujao wa watu waovu hakika utakatiliwa mbali.’ (Zaburi 37:37, 38) ‘Mutu asiye na lawama’ anafikia kumujua Yehova na Mwana wake na anakubali kufanya mapenzi ya Mungu. (Soma Yohana 17:3.) Anaamini kwa moyo wake wote kwamba “ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:17) Kwa sababu mwisho wa ulimwengu huu unakaribia, tunapaswa kutenda bila kukawia kwa ‘kumutumaini Yehova na kuishika njia yake.’—Zaburi 37:34.

TENDO KUBWA ZAIDI LENYE KUONYESHA KWAMBA YEHOVA ANATUPENDA

13. Ni tendo gani kubwa zaidi lenye Mungu alifanya ili kuonyesha kwamba anatupenda?

13 Tunaweza kumutii Mungu hata kama hatukamilike. Tunaweza pia kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova kupitia tendo kubwa zaidi la kuonyesha kwamba anatupenda, ni kusema, zabihu ya Yesu ya ukombozi. Yehova alitoa zabihu hiyo ili wanadamu wenye kumutii wakombolewe kutoka katika zambi na kifo. (Soma Waroma 5:12; 6:23.) Yesu alikuwa muaminifu kwa Mungu kwa muda murefu sana mbinguni; kwa hiyo, Yehova alikuwa hakika kwamba Mwana wake ataendelea kuwa muaminifu kwake duniani. Yehova ni Baba mwenye upendo; kwa hiyo, aliumia katika moyo wake wakati aliona namna watu wanamutesa Mwana wake. Hata hivyo, Yesu alitegemeza kwa uaminifu haki ya Mungu ya kutawala na alionyesha kwamba mutu mukamilifu anaweza kubakia muaminifu kwa Mungu hata kama anapambana na majaribu makali sana.

Upendo wa Yehova ulimuchochea amutume Mwana wake (Picha hii inapatana na fungu la 13)

14, 15. Kifo cha Yesu kinaletea wanadamu faida gani?

14 Yesu alipambana na majaribu makali sana, lakini aliunga mukono haki ya Mungu ya kutawala. Tunapaswa kuwa wenye shukrani kwa sababu kupitia kifo chake, Yesu alilipa bei ya zabihu ya ukombozi kwa sababu inatolea wanadamu nafasi ya kuishi milele katika dunia mupya ya Mungu! Mutume Paulo alifasiria upendo wenye Yehova na Yesu walionyesha kupitia zabihu ya ukombozi. Alisema hivi: ‘Kwa kweli, tulipokuwa tungali bado zaifu, Kristo alikufa wakati uliowekwa kwa ajili ya watu wasiomuogopa Mungu. Kwa maana ni vigumu kwa yeyote kufa kwa ajili ya mutu mwadilifu; kwa kweli, labda, mutu anaweza kusubutu [kujaribu] kufa kwa ajili ya mutu mwema. Lakini Mungu anapendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.’ (Waroma 5:6-8) Mutume Yohana aliandika hivi: ‘Kwa hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwa habari yetu, kwa sababu Mungu alimutuma Mwana wake muzaliwa-pekee kuja ulimwenguni ili tupate uzima kupitia yeye. Hivi ndivyo upendo ulivyo, si kwamba sisi tumemupenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda akamutuma Mwana wake kuwa zabihu ya upatanisho kwa ajili ya zambi zetu.’—1 Yohana 4:9, 10.

15 Yesu alisema kwamba ‘Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe [asiharibiwe] bali akuwe na uzima wa milele.’ (Yohana 3:16) Yehova alimutoa Mwana wake kuwa zabihu ya ukombozi, hata kama ilikuwa vigumu sana kwake kufanya hivyo. Jambo hilo linaonyesha kwamba Yehova anawapenda sana wanadamu. Linaonyesha pia kwamba upendo wake ni wa milele. Mutume Paulo aliandika hivi: “Kwa maana nimesadiki kwamba wala kifo wala uzima wala malaika wala serikali wala mambo yaliyopo sasa wala mambo yatakayokuja wala nguvu wala kimo wala kina wala uumbaji mwingine wowote havitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”—Waroma 8:38, 39.

UFALME WA MUNGU UNATAWALA

16. Ufalme wa Masiya ni nini, na Yehova amechagua nani ili akuwe Mutawala wa Ufalme huo?

16 Guvernema ya Mungu, ni kusema, Ufalme wa Masiya, ni njia ingine yenye kuonyesha kwamba Yehova anawapenda wanadamu. Namna gani? Yehova amechagua Mutawala mwenye anapenda wanadamu na mwenye kustahili kutawala, ni kusema, Yesu Kristo. (Methali 8:31) Pia, Mungu amechagua wanadamu 144 000 ili watawale pamoja na Yesu mbinguni. Hata wakati wanafufuliwa, wanaendelea kuelewa vizuri hali ya wanadamu. (Ufunuo 14:1) Wakati Yesu alikuwa duniani, alizungumuzia sana Ufalme wa Mungu, na alifundisha wanafunzi wake kusali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litakaswe. Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’ (Mathayo 6:9, 10) Tunangojea kwa hamu kuona namna maneno ya sala hiyo itatimia, wakati Ufalme wa Mungu utaletea wanadamu baraka nyingi!

17. Kuko tofauti gani kati ya utawala wa Yesu na utawala wa wanadamu?

17 Utawala wa Yesu wenye upendo uko tofauti sana na utawala wa wanadamu. Utawala wa wanadamu umeleta vita yenye imeua mamilioni ya watu. Lakini Mutawala wetu, Yesu, anatupenda kabisa na anaiga sifa nzuri za Mungu, zaidi sana sifa yake ya upendo. (Ufunuo 7:10, 16, 17) Yesu alisema hivi: ‘Mukuje kwangu, nyote munaotaabika na kulemewa [munaoteseka na kushindwa] na mizigo, nami nitawaburudisha ninyi. Muchukue nira yangu na mujifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na munyenyekevu moyoni, nanyi mutapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu. Kwa maana nira yangu ni laini na muzigo wangu ni mwepesi.’ (Mathayo 11:28-30) Hiyo ni ahadi yenye upendo kabisa!

18.(a) Ni kazi gani yenye imefanywa tangu mwaka wa 1914? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

18 Biblia inaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni katika mwaka wa 1914. Kuanzia wakati huo, kumekuwa kazi kubwa ya kukusanya mabaki ya wale wenye watatawala mbinguni pamoja na Yesu, na mukutano mukubwa wa watu wenye wataokoka mwisho wa ulimwengu huu na kuingia katika dunia mupya. (Ufunuo 7:9, 13, 14) Leo, watu wa mukutano mukubwa wamefikia hesabu gani? Mungu anawaomba watu hao wafanye nini? Tutajibu maulizo hayo katika habari yenye kufuata.