Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme!

Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme!

Mungu wa amani . . . na awapatie ninyi vifaa vyema vya kila namna ili kufanya mapenzi yake.’—WAEBRANIA 13:20, 21.

NYIMBO: 136, 14

1. Yesu aliona namna gani kazi ya kuhubiri? Eleza.

YESU alifurahia kuzungumuzia Ufalme wa Mungu. Wakati alikuwa hapa duniani, alizungumuzia sana Ufalme kuliko habari ingine yoyote. Katika mahubiri yake, alitaja Ufalme zaidi ya mara 100. Yesu aliona kwamba Ufalme ni wa lazima sana.—Soma Mathayo 12:34.

2. Ni watu ngapi wenye walisikia amri yenye kupatikana kwenye Mathayo 28:19, 20, na sababu gani tunasema hivyo?

2 Muda mufupi kisha Yesu kufufuliwa, alikusanyika pamoja na watu zaidi ya 500 wenye wangekuwa wanafunzi wake. (1 Wakorintho 15:6) Pengine ni wakati huo ndio Yesu alitoa amri ya kuhubiri “watu wa mataifa yote.” Haingekuwa vyepesi kufanya kazi hiyo. * (Soma maelezo ya chini.) Aliwaambia kwamba kazi ya kuhubiri ingeendelea kwa muda murefu, ‘mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ Wakati unahubiri habari njema leo, unasaidia kutimiza unabii huo.​—Mathayo 28:19, 20.

3. Ni vifaa gani tatu vyenye vimetusaidia katika kazi yetu ya kuhubiri habari njema?

3 Kisha kuwatolea amri ya kuhubiri, Yesu aliwaambia hivi: ‘Niko pamoja nanyi.’ (Mathayo 28:20) Kwa hiyo, Yesu aliahidi wafuasi wake kwamba ataongoza kazi ya kuhubiri na kwamba atawasaidia wahubiri katika dunia yote. Yehova pia iko pamoja na sisi. Ametupatia “vifaa vyema vya kila namna” ili kutusaidia katika kazi yetu ya kuhubiri. (Waebrania 13:20, 21) Katika habari hii, tutazungumuzia vifaa tatu kati ya vifaa hivyo: (1) vyombo vyenye tumepewa, (2) njia zenye tumetumia, na (3) mazoezi yenye tumepata. Tuzungumuzie kwanza vyombo fulani kati ya vyombo vyenye tumetumia katika miaka 100 yenye imepita.

VYOMBO VYA KUSAIDIA WATU WA MUNGU KUHUBIRI

4. Namna gani vyombo mbalimbali vimetusaidia katika kazi yetu ya kuhubiri?

4 Yesu alilinganisha ujumbe wa Ufalme na mbegu yenye kupandwa katika aina mbalimbali za udongo. (Mathayo 13:18, 19) Mulimaji anatumia vyombo mbalimbali ili kutayarisha udongo. Vilevile, Mufalme wetu ametupatia vyombo vyenye tunaweza kutumia ili kusaidia watu wakubali ujumbe wetu. Tulitumia vyombo fulani kwa muda mufupi, lakini tunaendelea kutumia vyombo vingine mupaka leo. Lakini vyombo hivyo vyote vimetusaidia tukomalishe ufundi wetu wa kuhubiri.

Kadi ya kutoa ushahidi ilisaidia wengi waanze kuhubiri

5. Karte ya kutoa ushahidi ni nini, na ilitumiwa namna gani?

5 Katika mwaka wa 1933, wahubiri walianza kutumia karte ya kutoa ushahidi; karte hiyo ilisaidia wengi waanze kuhubiri. Karte hiyo ilikuwa ndogo na ilikuwa na ujumbe wa Biblia mufupi na mwepesi. Wakati fulani wahubiri walitumia karte mupya na zenye kuwa na ujumbe mupya. Ndugu Erlenmeyer alikuwa na miaka karibu 10, wakati alitumia kwa mara ya kwanza karte ya kutoa ushahidi. Alisema hivi: “Karte zote zilikuwa na maneno haya ya utangulizi: ‘Tafazali, unaweza kusoma ujumbe huu?’ Kisha mwenye-nyumba kusoma ujumbe huo, tulimutolea vichapo na kuondoka.”

6. Namna gani karte ya kutoa ushahidi ilisaidia wahubiri?

6 Karte ya kutoa ushahidi ilisaidia wahubiri katika njia mbalimbali. Kwa mufano, wahubiri fulani walipenda kabisa kuhubiri, lakini walikuwa wenye haya na hawakujua jambo la kusema. Wahubiri wengine walikuwa wenye bidii sana. Walikuwa na uwezo wa kumuambia mwenye-nyumba kwa dakika chache tu mambo yote yenye walijua, lakini, wakati fulani hawakutumia njia nzuri. Karte ya kutoa ushahidi ilisaidia wahubiri wote watoe ujumbe wenye kuwa wazi na mwepesi.

7. Wahubiri walipambana na magumu gani wakati walitumia karte ya kutoa ushahidi?

7 Lakini wahubiri walipata pia magumu fulani. Dada Grace Estep alisema hivi: “Wakati fulani, watu walikuwa wanauliza hivi: ‘Ujumbe huu unamaanisha nini? Unaweza tu kunielezea kwa kifupi?’ ” Pia, wenye-nyumba fulani walikuwa wanakataa kusoma ujumbe wenye ulikuwa kwenye karte hiyo. Wengine walikuwa wanachukua tu karte kisha wanafunga mulango. Watu fulani hawakuwa wanapendezwa na ujumbe wetu, kwa hiyo, walipasua-pasua karte hiyo. Hata kama wahubiri walipambana na magumu hayo, karte ya kutoa ushahidi iliwasaidia kuhubiria majirani wao, na kujulikana kuwa wahubiri wa Ufalme.

8. Namna gani wahubiri walitumia fonografe? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Chombo kingine chenye wahubiri walitumia kisha mwaka wa 1930 ni fonografe yenye kuwa mwepesi kubeba. Mashahidi fulani waliita fonografe Haruni kwa sababu ilikuwa inasema pa nafasi yao. (Soma Kutoka 4:14-16.) Ikiwa mwenye-nyumba alikubali kusikiliza ujumbe, muhubiri alimutilia rekodi ya hotuba fupi ya dakika ine na nusu yenye kutegemea Biblia na alimutolea vichapo fulani. Wakati fulani familia zilikusanyika pamoja ili kusikiliza hotuba hiyo! Katika mwaka wa 1934, Watch Tower Society ilianza kutengeneza fonografe za kutumia katika mahubiri. Mwishowe, ndugu walifikia kurekodi hotuba 92.

9. Wahubiri walipata matokeo gani wakati walitumia fonografe?

9 Wakati Hillary Goslin alisikiliza hotuba moja, aliomba muhubiri amuachie fonografe kwa muda wa juma moja ili asaidie pia majirani wake wasikilize ujumbe wa Biblia. Kwa hiyo, watu wengi walipendezwa na kweli na wakabatizwa. Kisha, binti wawili wa Ndugu Goslin walisoma Masomo ya Gileadi na kuwa wamisionere. Kama vile karte ya kutoa ushahidi, fonografe ilisaidia wengi waanze kuhubiri. Kisha, kupitia Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi, Mufalme angezoeza watu wake ili wakuwe walimu wazuri.

KUTUMIKISHA NJIA MBALIMBALI ILI KUHUBIRIA WATU WENGI ZAIDI

10, 11. Namna gani tulitumia magazeti ya kutangaza habari na radio ili kuhubiri habari njema, na sababu gani njia hizo zilileta matokeo mazuri?

10 Mufalme wetu ameongoza watu wa Mungu ili watumie njia mbalimbali za kufikia watu wengi zaidi katika kazi ya kuhubiri. Njia hizo zilikuwa za lazima, zaidi sana wakati kulikuwa wahubiri wadogo. (Soma Mathayo 9:37.) Kwa mufano, miaka mingi yenye imepita tulitumia magazeti ya kutangaza habari ili kuhubiri habari njema. Kila juma, Ndugu Russell alituma hotuba fulani yenye kutegemea Biblia kwenye shirika fulani la kutangaza habari. Kisha shirika hilo lilituma hotuba hiyo kwenye magazeti ya kutangaza habari katika Kanada, Ulaya, na États-Unis. Kufikia mwaka wa 1913, hotuba za Ndugu Russell zilichapishwa katika magazeti 2 000, na watu karibu 15 000 000 walisoma hotuba hizo!

Magazeti ya kutangaza habari na radio vilitusaidia kufikia watu wengi zaidi katika maeneo yenye haikuwa na wahubiri wengi

11 Tulitumia pia radio ili kuhubiri habari njema. Tarehe 16 Mwezi wa 4, 1922, Ndugu Rutherford alitoa moja kati ya hotuba zake za kwanza kwenye radio, na watu karibu 50 000 walisikiliza hotuba hiyo. Muda mufupi kisha hapo, tulianza kutumia radio yetu. Radio hiyo iliitwa WBBR. Watu walisikiliza programu ya radio hiyo kwa mara ya kwanza, tarehe 24 Mwezi wa 2, 1924. Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12, 1924 ulisema hivi: “Tunaamini kwamba radio ndiyo njia nzuri zaidi ya kueneza ujumbe wa ukweli na yenye haiombe feza nyingi. Tulikuwa hatujatumia njia hiyo.” Kama vile magazeti ya kutangaza habari, radio ilitusaidia kufikia watu wengi zaidi katika maeneo yenye haikuwa na wahubiri wengi.

Wahubiri wengi wa Ufalme wanafurahia kuhubiri mahali pa watu wengi na kuongoza watu kwenye adresi yetu ya Internete (Picha hii inapatana na fungu la 12, 13)

12. (a) Unafurahia zaidi kuhubiri mahali gani pa watu wengi? (b) Ni nini inaweza kutusaidia kumaliza woga wa kuhubiri mahali pa watu wengi?

12 Kuhubiri mahali pa watu wengi ni njia yenye matokeo mazuri yenye tunatumia leo ili kuhubiria watu. Tunajikaza sana ili kuhubiria nafasi ya kungojea bisi, nafasi kwenye treni zinazoea kusimama, nafasi ya kuegesha gari (parking), kwenye barabara zenye kuwa na watu wengi, na kwenye masoko. Je, unaogopa kuhubiri mahali pa watu wengi? Ikiwa unaogopa, usali ili kumuomba Yehova musaada na ufikirie maneno ya Ndugu Manera, mwangalizi mwenye kusafiri. Alisema hivi: “Tuliona kila njia mupya ya kuhubiri kuwa nafasi mupya ya kumutumikia Yehova, nafasi mupya ya kuonyesha uaminifu wetu kwake, jaribu lingine la ushikamanifu wetu, na tulikuwa na hamu ya kuonyesha kwamba tuko tayari kumutumikia katika njia yoyote yenye alituomba.” Ikiwa tunamaliza woga wetu na kutumia njia mupya za kuhubiri, hilo linatusaidia tumutegemee Yehova kabisa na kuwa wahubiri wazuri zaidi.—Soma 2 Wakorintho 12:9, 10.

13. Sababu gani kutumia adresi yetu ya Internete ni njia yenye kuleta matokeo mazuri katika mahubiri, na umepata matokeo gani kwa kufanya hivyo?

13 Wahubiri wengi wanafurahia kuongoza watu kwenye adresi yetu ya Internete, jw.org, ili wasome na kuchukua vichapo vya kutusaidia kuelewa Biblia, katika luga zaidi ya 700. Kila siku, watu zaidi ya milioni moja na nusu wanafungua adresi yetu ya Internete. Zamani, radio ilitusaidia kuhubiria watu habari njema katika maeneo ya mbali. Leo, adresi yetu ya Internete inatusaidia kufanya hivyo.

KUZOEZA WAHUBIRI WA HABARI NJEMA

14. Wahubiri walikuwa na lazima ya mazoezi gani, na ni nini imewasaidia wakuwe walimu wazuri?

14 Vyombo na njia za kuhubiri zenye tumezungumuzia vimeleta matokeo mazuri sana. Hata hivyo, katika miaka hiyo ya kwanza-kwanza wahubiri walikuwa na lazima ya mazoezi zaidi. Kwa mufano, wakati fulani mwenye-nyumba hakukubali ujumbe wenye alisikiliza kwenye fonografe. Wakati mwingine mwenye-nyumba alipendezwa na alikuwa tayari kujifunza mambo mengi. Wahubiri walikuwa na lazima ya kujua namna ya kutumia ufundi ili kumaliza vizuia-mazungumuzo na namna ya kuwa walimu wazuri zaidi. Ni wazi kwamba, roho takatifu ya Mungu ilimusaidia Ndugu Knorr atambue kwamba ilikuwa lazima wahubiri wajifunze namna ya kuzungumuza na watu katika mahubiri. Kwa hiyo, kuanzia mwaka wa 1943, Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi ilianzishwa katika makutaniko. Masomo hayo ilisaidia wahubiri wote kuwa walimu wazuri.

15. (a) Ndugu fulani walijisikia namna gani wakati walitoa hotuba yao ya kwanza kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi? (b) Namna gani umejionea kwamba ahadi ya Yehova kwenye Zaburi 32:8 ni ya kweli?

15 Ndugu wengi hawakuzoea kusema mbele ya watu. Ndugu Ramu anakumbuka wakati alitoa hotuba yake ya kwanza katika mwaka wa 1944. Hotuba hiyo ilikuwa inazungumuzia Doegi, mutu mwenye kutajwa katika Biblia. Ndugu Ramu alisema hivi: “Magoti na mikono yangu ilikuwa inatetemeka na nilikuwa ninapekenya meno yangu.” Aliongeza hivi: “Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kusema mbele ya watu, lakini sikuachia hapo.” Watoto pia walikuwa wanatoa hotuba kwenye masomo hayo, hata kama haikuwa vyepesi. Ndugu Manera anakumbuka jambo lenye lilitokea wakati mutoto moja mwanaume alitoa hotuba yake ya kwanza. Anasema hivi: “Alikuwa na woga sana wakati alianza hotuba yake na alianza kulia. Lakini alijikaza kuitoa, na alilia mupaka mwisho wa hotuba yake.” Pengine hautoe maelezo kwenye mikutano kwa sababu unasikia haya ao unawaza kwamba hauna uwezo wa kufanya hivyo. Ikiwa ni hivyo, umuombe Yehova akusaidie umalize woga wako. Atakusaidia kama vile tu alisaidia wanafunzi hao wa kwanza-kwanza wa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi.—Soma Zaburi 32: 8.

Tangu mwaka wa 1943, wanafunzi zaidi ya 8 500 wamezoezwa kwenye Masomo ya Gileadi na kutumwa katika inchi 170

16. Masomo ya Gileadi imekuwa na kusudi gani (a) zamani na (b) tangu mwaka wa 2011?

16 Masomo ya Gileadi ni njia ingine yenye tengenezo la Mungu limetumia ili kuzoeza watu wake. Kusudi kubwa la masomo hayo ni kusaidia wanafunzi wapendezwe sana na kazi ya kuhubiri habari njema. Masomo ya Gileadi ilianza katika mwaka wa 1943, na tangu wakati huo, wanafunzi 8 500 wamezoezwa na kutumwa katika inchi 170. Kuanzia mwaka wa 2011, mapainia wa pekee, waangalizi wenye kusafiri, Wanabeteli, na wamisionere wenye hawajasoma, ndio wanaalikwa kwenye Masomo ya Gileadi.

17. Masomo ya Gileadi imekuwa na matokeo gani?

17 Masomo ya Gileadi imeleta matokeo mazuri? Ndiyo. Tuchukue mufano wa inchi ya Japani. Katika Mwezi wa 8, 1949, katika inchi hiyo, hesabu ya wahubiri ilikuwa chini ya 10. Lakini, kufikia mwisho wa mwaka huo, wamisionere 13 walikuwa wanahubiri pamoja na ndugu na dada wa inchi hiyo. Leo, inchi ya Japani iko na wahubiri karibu 216 000, na karibu nusu ya hesabu hiyo ni mapainia!

18. Tuko na masomo mengine gani?

18 Tuko na masomo mengine mengi, kama vile Masomo ya Huduma ya Ufalme, Masomo ya Mapainia, Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, Masomo ya Waangalizi wa Muzunguko na Bibi Zao, na Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na Bibi Zao. Masomo hayo imewatolea ndugu na dada mazoezi mazuri sana na kufanya imani yao ikuwe yenye nguvu. Inaonekana wazi kwamba Yesu anaendelea kuzoeza watu wengi.

19. Ndugu Russell alisema nini juu ya kazi ya kuhubiri, na maneno hayo inatimia namna gani?

19 Ufalme wa Mungu umeanza kutawala kumepita miaka zaidi ya 100. Tangu wakati huo, Mufalme wetu, Yesu Kristo, amekuwa akiongoza kazi ya kuhubiri. Katika mwaka wa 1916, Ndugu Russell aliamini kwamba kazi ya kuhubiri habari njema itaenea katika dunia yote. Alisema hivi: “Kazi inaongezeka haraka, na itaendelea kuongezeka, kwa hiyo, kuko kazi kubwa ya kuhubiri ‘injili ya ufalme’ katika dunia yote. ” (La foi en marche cha Kiingereza chenye kiliandikwa na Macmillan, ukurasa wa 69) Kazi hiyo inaendelea kufanywa leo! Tunamushukuru Yehova, Mungu wa amani, kwa sababu anatupatia vifaa vyema vya kila namna vyenye tuko navyo lazima ili kufanya mapenzi yake!

^ fu. 2 Inawezekana kwamba wengi kati ya watu hao walifikia kuwa Wakristo. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu mutume Paulo anawaita “ndugu 500.” Anasema pia hivi: ‘Wengi kati yao wako mupaka sasa, lakini wengine wamelala usingizi katika kifo.’ Kwa hiyo, inaonekana kwamba mutume Paulo na Wakristo wengine walijua wengi kati ya watu wenye walimusikia Yesu anatoa amri ya kuhubiri.