Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uzoeze Kijana Wako Amutumikie Yehova

Uzoeze Kijana Wako Amutumikie Yehova

“Yesu akazidi [akaendelea] kufanya maendeleo katika hekima na ukuzi [ukomavu] wa kimwili, akipata kibali kwa Mungu na wanadamu.”LUKA 2:52.

NYIMBO: 41, 89

1, 2. (a) Wazazi fulani wenye kuwa na vijana wanaogopa nini? (b) Watoto wanaweza kupata faida gani katika miaka yao ya ujana?

WAZAZI wanafurahi sana wakati watoto wao wanabatizwa. Watoto wote ine wa dada Berenice walibatizwa mbele wafikie miaka 14. Anasema hivi: “Jambo hilo lilituletea furaha kubwa sana. Kwa kweli, tulikuwa wenye shukrani kwa sababu watoto wetu walipenda kumutumikia Yehova. Lakini tulijua pia kwamba wakati watakuwa vijana watapambana na magumu mengi.” Wewe pia unaweza kuogopa ao kuwa na wasiwasi ikiwa uko na kijana mwanaume ao mwanamuke ao ikiwa mutoto wako atafikia miaka ya ujana hivi karibuni.

2 Mutu moja mwenye kujifunza tabia za watoto anasema kwamba wakati watoto wanakuwa kati ya miaka 13 na 19, hilo linaleta magumu kwa wazazi na vijana wenyewe, lakini wazazi hawapaswe kufikiri kwamba vijana wao hawana akili sawa ao wanatenda kama watoto wadogo. Lakini anasema kwamba, vijana wanapenda kufanya mambo mapya, na wanapenda kila mara kujieleza namna wanajisikia katika moyo wao, na wako na lazima ya kupitisha wakati pamoja na marafiki wao. Kwa hiyo, wakati watoto wako wanafikia miaka ya ujana, wanaweza kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova, kama vile Yesu alifanya wakati alikuwa kijana. (Soma Luka 2:52.) Wanaweza pia kukomalisha ufundi wao wa kuhubiri na kupenda kabisa kufanya mengi katika kazi ya Mungu. Pia, wanaweza kuchukua maamuzi wao wenyewe, kama vile kutoa maisha yao kwa Yehova na kumutii. Lakini, ikiwa wewe ni muzazi unaweza kufanya nini ili umuzoeze kijana wako amutumikie Yehova? Unaweza kuiga namna Yesu alizoeza wanafunzi wake kwa upendo, kwa unyenyekevu, na kwa utambuzi.

UMUPENDE KIJANA WAKO

3. Ni nini iliwahakikishia mitume kwamba Yesu alikuwa rafiki yao?

3 Yesu hakuwa tu Bwana wa wanafunzi wake, lakini alikuwa pia rafiki yao. (Soma Yohana 15:15.) Wakati wa zamani, bwana hakuzoea kuwaambia watumwa wake mawazo yake na namna alikuwa anajisikia. Lakini Yesu hakuwaona mitume wake kuwa watumwa. Aliwapenda na alipitisha wakati pamoja nao. Alifurahia kuwaambia mawazo yake na namna alikuwa anajisikia, na alikuwa anawasikiliza kwa uangalifu wakati walimuelezea mawazo yao na namna walikuwa wanajisikia. (Marko 6:30-32) Mazungumuzo hayo iliwafanya wakuwe marafiki wa sana na ilitayarisha mitume wake kwa ajili ya kazi yenye wangefanya wakati unaokuja.

4. Wazazi, namna gani munaweza kufanya urafiki pamoja na watoto wenu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Unaweza pia kuwa rafiki ya watoto wako hata kama uko na mamlaka juu yao. Marafiki wanapitisha wakati pamoja. Pengine unaweza kupunguza wakati wenye unatumia ili kutumika ao kufanya mambo mengine ili upitishe wakati mwingi pamoja na watoto wako. Unapaswa kusali na kufikiri sana juu ya jambo hilo. Marafiki wanafurahia pia mambo yenye kupendeza kila mumoja wao. Kwa hiyo, ujikaze kujua mambo yenye kijana wako anafurahia, kama vile muziki, filme, ao michezo fulani. Kisha ujikaze kufurahia mambo hayo. Ilaria, dada mwenye kuishi Italia, anasema hivi: “Wazazi wangu walipendezwa na muziki wenye nilikuwa ninasikiliza. Kwa hiyo, baba yangu alikuwa rafiki yangu wa sana, na nilijisikia huru kuongea naye mambo yangu yote.” Wakati unakuwa rafiki wa watoto wako na unawasaidia wakuwe marafiki wa Yehova, haupoteze mamlaka yako. (Zaburi 25:14) Watoto wako wataona kwamba unawapenda na kuwaheshimu, na itakuwa vyepesi kwao kukuambia mambo yao yote.

5. Ni nini ingewasaidia wanafunzi wa Yesu wapate furaha katika kazi ya Yehova?

5 Yesu alijua kwamba ikiwa wanafunzi wake wanamutumikia Yehova na kuhubiri habari njema kwa bidii, wangepata furaha kweli-kweli. Kwa hiyo aliwatia moyo wahubiri kwa bidii, na aliwaahidi kwamba atawasaidia.—Mathayo 28:19, 20.

6, 7. Namna gani unaonyesha kwamba unawapenda watoto wako wakati unawafundisha kumutumikia Yehova kwa ukawaida?

6 Wazazi, munapenda watoto wenu wamukaribie Yehova. Yehova pia anapenda muwazoeze na kuwatia nizamu. Amewapatia mamlaka ya kufanya hivyo. (Waefeso 6:⁠4) Kwa hiyo, munapaswa kuhakikisha kwamba watoto wenu wanapata mazoezi kwa ukawaida. Mufikirie jambo hili: Munawatuma watoto wenu kwenye masomo kwa sababu munajua kwamba masomo ni ya lazima na kwa sababu munapenda wajifunze mambo mapya. Vilevile, munahakikisha kwamba watoto wenu wanahuzuria mikutano, mikusanyiko, na ibada ya familia. Zaidi ya yote, mafundisho yenye Yehova anawatolea inaweza kuokoa uzima wao. Kwa hiyo, muwasaidie wafurahie mambo yenye wanajifunza juu ya Yehova na waelewe kwamba anaweza kuwafundisha ili wakuwe wenye hekima kabisa. (Methali 24:14) Pia, muwazoeze watoto wenu kuhubiri kwa ukawaida. Muige mufano wa Yesu kwa kuwasaidia wafurahie kufundisha wengine Neno la Mungu.

7 Kumutumikia Yehova kwa ukawaida, ni kusema, kujifunza, kukusanyika, na kuhubiri kunaweza kusaidia namna gani vijana? Dada Erin, wa Afrika ya Kusini, anasema hivi: “Mara nyingi sisi watoto tulilalamika na kunungunika juu ya funzo la Biblia, mikutano, na kazi ya kuhubiri. Wakati fulani tuliamua kufanya makelele wakati wa funzo la familia ili tujaribu kuepuka funzo hilo. Lakini wazazi wetu hawakuchoka kufanya funzo.” Dada Erin anashukuru sana wazazi wake kwa sababu walimusaidia aelewe kwamba mambo hayo ni ya lazima sana. Sasa, kila mara wakati anakosa mukutano ao anashindwa kuenda katika kazi ya kuhubiri, anajikaza ili arudilie programu yake ya kawaida bila kukawia.

UKUWE MUNYENYEKEVU

8. (a) Namna gani Yesu alionyesha kwamba alikuwa munyenyekevu? (b) Unyenyekevu wa Yesu ulisaidia namna gani wanafunzi wake?

8 Yesu alikuwa mukamilifu, lakini alikuwa munyenyekevu na aliambia wanafunzi wake kwamba alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova. (Soma Yohana 5:19.) Je, hilo lilifanya wanafunzi wake wasiendelee kumuheshimu? Hapana. Wakati walimuona anaendelea kumutegemea Yehova, wao pia waliendelea kumutumainia Yesu. Kisha, wao pia waliiga mufano wake wa unyenyekevu.—Matendo 3:12, 13, 16.

Wakati unakubali makosa yako, watoto wako watakuheshimu

9. Wakati unakubali makosa yako na kuomba musamaha, hilo linaweza kusaidia kijana wako namna gani?

9 Yesu alikuwa mukamilifu, lakini sisi hatukamilike na tunafanya makosa. Kwa hiyo, ukuwe munyenyekevu. Uelewe kwamba hauna uwezo wa kufanya mambo yote, na ukubali makosa yako. (1 Yohana 1:8) Ukifanya hivyo, kijana wako atajifunza kukubali makosa yake, na atakuheshimu zaidi. Kwa kweli, unaheshimu zaidi mutu wa namna gani? Mukubwa wa kazi mwenye anakubali makosa yake ao ule mwenye haombake musamaha hata kidogo? Dada Rosemary, mama wa watoto watatu, anasema kwamba yeye na bwana yake walikuwa tayari kukubali makosa yao. Anasema hivi: “Jambo hilo lilichochea watoto wetu wakuwe tayari kutuelezea magumu yao.” Anaongeza hivi: “Tulionyesha watoto wetu nafasi kwenye wangepata mashauri mazuri sana ya kuwasaidia kumaliza magumu yao. Wakati walikuwa na lazima ya musaada, kila mara tuliwaomba wasome vichapo vyetu vyenye kutusaidia kuelewa Biblia, na tulisali pamoja nao.”

10. Wakati Yesu alikuwa anawaambia wanafunzi wake mambo yenye walipaswa kufanya, namna gani alionyesha unyenyekevu?

10 Yesu alikuwa na mamlaka ya kuambia wanafunzi wake mambo yenye walipaswa kufanya. Lakini, kwa sababu alikuwa munyenyekevu, kila mara aliwaambia sababu gani walipaswa kufanya mambo hayo. Kwa mufano, hakuwaambia tu wanafunzi wake kwamba watafute Ufalme wa Mungu na uadilifu wake. Lakini, aliwaambia pia hivi: ‘Na nyinyi mutaongezewa hivi vitu vingine vyote.’ Wakati Yesu aliwaambia kwamba waache kuhukumu wengine, aliwaambia pia hivi: ‘Ili musihukumiwe; kwa maana kwa hukumu munayohukumu, mutahukumiwa.’—Mathayo 6:31–7:2.

11. Namna gani unaweza kusaidia kijana wako ajue sababu gani unatia sheria fulani ao unachukua uamuzi fulani?

11 Chagua wakati wenye kufaa ili kumuelezea kijana wako sababu gani unatia sheria fulani ao unachukua uamuzi fulani. Wakati kijana wako anaelewa sababu gani unafanya hivyo, pengine atakuwa tayari kukutii. Ndugu Barry, mwenye iko na watoto ine, anasema hivi: “Kuwaambia vijana sababu gani mambo fulani inapaswa kufanywa, kunawasaidia wakutumainie.” Vijana wataelewa kwamba umetia sheria fulani ao umechukua uamuzi fulani si kwa sababu tu uko na mamlaka ya kufanya hivyo, lakini kwa kuwa uko na sababu nzuri ya kufanya hivyo. Pia ukumbuke kwamba vijana hawako tena watoto wadogo. Wanajifunza namna ya kufikiri, na wanapenda kuchukua maamuzi yao wenyewe. (Waroma 12:1) Ndugu Barry anaeleza hivi: “Vijana wanapaswa kujifunza namna ya kuchukua maamuzi yenye hekima na yenye kutegemea sababu fulani kuliko kuamua kulingana na namna wanajisikia.” (Zaburi 119:34) Kwa hiyo, ukuwe munyenyekevu na umuambie kijana wako sababu gani unachukua uamuzi fulani. Kwa kufanya hivyo, kijana wako atajifunza kuchukua maamuzi yake mwenyewe, na atajua kwamba unamuheshimu na kwamba unaelewa kuwa anaendelea kukomaa.

UKUWE NA UTAMBUZI

12. Yesu alitumia utambuzi namna gani wakati alimusaidia Petro?

12 Yesu alikuwa na utambuzi na alijua musaada wenye wanafunzi wake walikuwa nao lazima. Kwa mufano, wakati aliwaambia wanafunzi wake kwamba anakaribia kufa, Petro alimuambia kwamba ajitendee kwa wema. Yesu alijua kwamba Petro alimupenda, lakini alielewa pia kwamba mawazo ya Petro ilikuwa ya mubaya. Namna gani Yesu alimusaidia Petro na wanafunzi wengine? Kwanza kabisa alimushauria Petro. Pia, Yesu alieleza mambo yenye itawapata wale wenye kukataa kufanya mapenzi ya Yehova wakati inakuwa vigumu kufanya hivyo. Yesu alisema pia kwamba Yehova atawabariki wale wenye kuhangaikia wengine. (Mathayo 16:21-27) Mashauri hayo ilimusaidia Petro.1 Petro 2:20, 21.

13, 14. (a)Ni nini inaweza kuonyesha kwamba kijana wako anapaswa kutia nguvu imani yake? (b) Namna gani unaweza kujua mambo yenye kijana wako iko nayo lazima kabisa?

13 Umuombe Yehova akupatie utambuzi ili ujue mambo yenye kijana wako anaweza kuwa nayo lazima. (Zaburi 32:8) Pengine unaona kwamba kijana wako hana tena furaha ao anasema mubaya juu ya ndugu na dada. Pengine unatambua kwamba anakuficha jambo fulani. Usifikiri mara moja kwamba kijana wako anafanya mambo fulani mabaya sana kwa uficho. * (Soma maelezo ya chini.) Lakini usizarau magumu yake ao kufikiri tu kwamba itaisha. Pengine unaweza kumusaidia atie nguvu imani yake.

Umusaidie kijana wako apate marafiki wazuri katika kutaniko (Picha hii inapatana na fungu la 14)

14 Ili ujue namna unaweza kumusaidia kijana wako, umuulize maulizo kwa upole na kwa heshima. Ni kama vile kushota maji katika shimo murefu. Ikiwa unashota mbiombio, hautapata maji mengi. Vilevile, ikiwa unakosa uvumilivu wakati unamuuliza kijana wako maulizo ao kujaribu kumukaza ajieleze, hautajua kabisa mawazo yake na namna anajisikia. (Soma Methali 20:5.) Dada Ilaria anakumbuka kwamba wakati alikuwa kijana, alipenda kupitisha wakati mwingi pamoja na wanafunzi wenzake, lakini alijua kwamba ilikuwa mubaya kufanya hivyo. Wazazi wake walitambua kwamba alikuwa mwenye wasiwasi. Dada Ilaria anasema hivi: “Mangaribi moja, waliniambia tu kwamba walitambua kuwa nilikuwa na huzuni, na waliniuliza sababu gani. Nilianza kulia na kuwaelezea magumu yangu, na niliwaomba musaada. Walinikumbatia, waliniambia kwamba wananielewa, na walisema kwamba watanisaidia.” Mara moja wazazi wa dada Ilaria walianza kumusaidia apate marafiki wazuri katika kutaniko.

Ujikaze kuona sifa nzuri za kijana wako na umupongeze

15. Yesu alitumia njia gani ingine ili kuonyesha kwamba alikuwa na utambuzi.

15 Yesu alitumia pia utambuzi ili kuona sifa nzuri za wanafunzi wake. Kwa mufano, wakati Nathanaeli alisikia kwamba Yesu alikuwa wa Nazareti, alisema hivi: “Je, kitu chochote kilicho chema kinaweza kutoka Nazareti?” (Yohana 1:46) Ikiwa ungekuwa hapo, je, ungefikiri kwamba Nathanaeli alikuwa na mawazo mabaya juu ya Yesu, alikuwa na ubaguzi, ao hakuwa na imani? Yesu hakuwa na mawazo kama hayo. Lakini, alikuwa na utambuzi na alijua kwamba Nathanaeli alikuwa mutu muzuri, kwa hiyo, alisema kwamba Nathanaeli ni ‘Mwisraeli [wa kweli], ambaye hamuna udanganyifu ndani yake.’ (Yohana 1:47) Yesu alikuwa na uwezo wa kusoma katika mioyo ya watu, na alitumia uwezo huo ili kuona sifa nzuri zao.

16. Namna gani unaweza kumusaidia kijana wako afanye maendeleo?

16 Hauna uwezo wa kusoma katika mioyo ya watu kama vile Yesu alifanya, lakini unaweza kutumia utambuzi. Yehova ­anaweza kukusaidia utambue sifa nzuri za kijana wako. Hata kama kijana wako anakukosea, usimuambie hata kidogo kwamba yeye ni mutu mubaya ao mwenye kuleta muvurugo. Usikuwe na mawazo ya namna hiyo juu yake. Lakini, umuambie kwamba unaona sifa nzuri zake na kwamba uko hakika kama anapenda kufanya mambo mazuri. Utambue maendeleo yenye amefanya, kisha umupongeze. Ikiwa inawezekana, umusaidie akomalishe sifa nzuri kwa kumupatia mambo mengi ya kufanya. Yesu alifanya hivyo kwa wanafunzi wake. Mwaka moja na nusu kisha kukutana na Nathanaeli (mwenye anaitwa pia Bartholomayo), Yesu alimupatia daraka la maana. Alimuchagua kuwa mutume, naye alitimiza kwa uaminifu daraka hilo. (Luka 6:13, 14; Matendo 1:13, 14) Kuliko kumufanya kijana wako ajisikie kuwa hafanyake mambo ya muzuri kabisa, umupongeze na umutie moyo. Umusaidie aone kwamba anaweza kukufurahisha wewe na Yehova, na kwamba anaweza kutumia uwezo wake katika kazi ya Yehova.

UTAPATA FURAHA KUBWA IKIWA UNAWAZOEZA WATOTO WAKO

17, 18. Mutapata matokeo gani ikiwa munaendelea kuzoeza vijana wenu wamutumikie Yehova?

17 Unaweza kujisikia kama mutume Paulo. Alihangaikia wale wenye aliona kuwa watoto wake kiroho. Watu hao ni wale wenye alisaidia wajifunze kumujua Yehova, na aliwapenda sana. Hakufikiri kwamba watu fulani kati ya hao wataacha kumutumikia Yehova. (1 Wakorintho 4:15; 2 Wakorintho 2:4) Ndugu Victor, mwenye alilea watoto watatu, anasema hivi: “Ilikuwa vigumu kwangu wakati watoto wangu walikuwa vijana. Lakini, wakati muzuri wenye tumepata ni mwingi kuliko magumu yenye tulipambana nayo. Yehova ametusaidia tukuwe na urafiki muzuri pamoja na watoto wetu.”

18 Wazazi, munatumika sana ili kuzoeza watoto wenu kwa sababu munawapenda sana. Musichoke. Mufikirie furaha kubwa yenye mutapata wakati mutaona watoto wenu wanachukua uamuzi wa kumutumikia Mungu kwa uaminifu.—3 Yohana 4.

^ fu. 13 Wazazi wanaweza kupata musaada kwa kusoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, ukurasa wa 317, na Buku la 2, ukurasa wa 136-141.