Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Watu wenye kuchimba vitu vya zamani wamepata nini yenye kuonyesha kwamba muji wa Yeriko ulikamatwa kisha kuzungukwa kwa muda mufupi?

Andiko la Yoshua 6:10-15, 20 linasema kwamba maaskari Waisraeli walizunguka muji wa Yeriko mara moja kwa siku kwa muda wa siku sita. Siku ya saba, walizunguka muji huo mara saba. Kisha, Mungu akaangusha kuta zenye nguvu za Yeriko, na maaskari Waisraeli wakakamata muji huo. Je, watu wenye kuchimba vitu vya zamani wamepata mambo fulani yenye kuonyesha kwamba muji wa Yeriko ulikamatwa kisha kuzungukwa kwa muda mufupi, kama vile tu Biblia inasema?

Wakati wa zamani, muji ulikamatwa wakati maaskari waliuzunguka na kuwa tayari kuushambulia. Ikiwa maaskari walizunguka muji kwa muda murefu, watu wa muji huo walipaswa kula sehemu kubwa zaidi ya chakula chenye walikuwa wameweka. Kisha, wakati maaskari walikamata muji, walichukua kila kitu chenye walipenda, na pia chakula chenye watu waliacha. Ndiyo sababu watu wenye kuchimba vitu vya zamani walipata chakula kidogo sana ao hawakupata chakula chochote nafasi penye palikuwa miji ya zamani katika Palestina yenye maaskari walizunguka kwa muda murefu mbele waikamate. Lakini, mambo ilikuwa tofauti juu ya muji wa Yeriko. Kitabu Biblical Archaeology Review kinasema hivi: “Kati ya vitu vyenye vilivumbuliwa, kulikuwa vyombo vya udongo, lakini nafaka (mbegu) ndiyo ilikuwa nyingi sana.” Kitabu hicho kinaongeza hivi: “Ilikuwa jambo la pekee sana kupata kiasi kikubwa sana cha mbegu.”

Biblia inasema kwamba Waisraeli hawakuchukua chakula chenye kilikuwa katika muji wa Yeriko kwa sababu Yehova alikuwa amewakataza kufanya hivyo. (Yoshua 6:17, 18) Biblia inasema tena kwamba Waisraeli walikamata muji wa Yeriko katika majira ya kuchipua, kisha tu wakati wa mavuno, wakati watu wa Yeriko walikuwa wameweka mbegu nyingi sana. (Yoshua 3:15-17; 5:10) Kwa hiyo, kwa sababu kulikuwa mbegu nyingi sana wakati muji wa Yeriko ulikamatwa, hilo linahakikisha kwamba ulikamatwa kisha kuzungukwa kwa muda mufupi, kama vile tu Biblia inasema.