Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Muazimie Kuendeleza “Upendo Wenu wa Kindugu”!

Muazimie Kuendeleza “Upendo Wenu wa Kindugu”!

“Upendo wenu wa kindugu na uendelee.”WAEBRANIA 13:1.

NYIMBO: 72, 119

1, 2. Sababu gani mutume Paulo aliandikia Wakristo Waebrania?

KATIKA mwaka wa 61, makutaniko yote ya Israeli ilikuwa na amani kwa kadiri fulani. Hata kama mutume Paulo alikuwa katika gereza huko Roma, alitumaini kwamba ataachiliwa kisha muda mufupi. Timotheo, mwenye walikuwa wanasafiri pamoja naye alikuwa ameachiliwa tu kutoka katika gereza, na wote wawili walitumaini kutembelea ndugu na dada wa Yudea. (Waebrania 13:23) Kulikuwa kunabakia tu miaka tano ili Wakristo wa Yudea, zaidi sana wale wenye kuishi katika Yerusalemu, wafanye haraka. Sababu gani? Kwa sababu Yesu alikuwa ameambia wafuasi wake kwamba wakati tu wangeona maaskari wanazunguka muji wa Yerusalemu, walipaswa kukimbia.—Luka 21:20-24.

2 Miaka 28 ilikuwa imepita tangu Yesu atolee wafuasi wake onyo hilo. Wakati huo, Wakristo katika Israeli walibakia waaminifu hata kama walipatwa na magumu na majaribu mengi. (Waebrania 10:32-34) Lakini, mutume Paulo alipenda kuwatayarisha juu ya mambo yenye ingetokea wakati unaokuja. Walikuwa karibu kupata jaribu kubwa zaidi la imani yao. (Mathayo 24:20, 21; Waebrania 12:4) Kuliko wakati mwingine wowote, walipaswa kuonyesha uvumilivu na imani ili kutii onyo la Yesu la kukimbia ili kuokoa uzima wao. (Soma Waebrania 10:36-39.) Kwa hiyo, Yehova alitumia roho yake takatifu ili kumuongoza mutume Paulo aandikie ndugu na dada hao wapendwa. Barua hiyo inaitwa kitabu cha Waebrania; iliandikwa ili kuwatia nguvu wavumilie mambo yenye ingetokea.

3. Sababu gani leo tunapaswa kupendezwa na kitabu cha Waebrania?

3 Sisi watu wa Mungu, tunapaswa kupendezwa leo na kitabu cha Waebrania. Sababu gani? Kwa sababu hali yetu inafanana na ile ya Wakristo wa Yudea. Tunaishi katika “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” na ndugu na dada wengi wamevumilia kwa uaminifu majaribu ao mateso makali. (2 Timotheo 3:1, 12) Lakini wamoja kati yetu wanaishi kwa amani na hawapatwe na mateso ya moja kwa moja. Kwa hiyo, tunapaswa kukesha kama vile Wakristo wa wakati wa mutume Paulo. Sababu gani? Kwa sababu hivi karibuni, tutapata jaribu kubwa zaidi la imani!—Soma Luka 21:34-36.

4. Andiko letu la mwaka wa 2016 ni gani, na sababu gani andiko hilo linafaa?

4 Ni nini itatusaidia tujitayarishe kwa ajili ya tukio hilo la wakati unaokuja? Katika kitabu cha Waebrania, mutume Paulo alizungumuzia mambo mengi ya kutusaidia kutia nguvu imani yetu. Jambo moja la maana sana linapatikana kwenye Waebrania 13:1. Andiko hilo linatutia moyo hivi: “Upendo wenu wa kindugu na uendelee.” Andiko hilo limechaguliwa ili kuwa andiko letu la mwaka wa 2016.

Andiko letu la mwaka wa 2016: “Upendo wenu wa kindugu na uendelee.” —Waebrania 13:1

UPENDO WA KINDUGU NI NINI?

5. Upendo wa kindugu ni nini?

5 Upendo wa kindugu ni nini? Neno la Kigiriki lenye mutume Paulo alitumia linamaanisha moja kwa moja “kumupenda ndugu.” Upendo wa kindugu ni upendo wenye nguvu, ao upendo muchangamufu kati ya watu wa familia moja ao kati ya marafiki wa sana. (Yohana 11:36) Hatujiite tu ndugu na dada. Lakini Tuko ndugu na dada. (Mathayo 23:8) Mutume Paulo alisema hivi: ‘Katika upendo wa kindugu mukuwe na upendo mwororo kwa mutu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima, mukuwe wa kwanza.’ (Waroma 12:10) Maneno hayo inaonyesha kwamba upendo wetu kwa ndugu na dada ni wenye nguvu sana. Upendo huo wa kindugu, pamoja na upendo wenye kuongozwa na kanuni za Maandiko, unasaidia watu wa Mungu wakuwe marafiki wa sana na wakuwe na umoja.

6. Wakristo wa kweli wanaelewa namna gani maneno “upendo wa kindugu”?

6 Maneno “upendo wa kindugu” inapatikana sana katika maandiko ya Kikristo. Wayahudi wa zamani walitumia neno “ndugu” kwa ukawaida ili kuzungumuzia mutu wa jamaa na wakati fulani ili kuzungumuzia mutu mwenye haiko wa jamaa yao. Lakini hawakutumia hata kidogo neno hilo ili kuzungumuzia watu wenye hawakuwa Wayahudi. Lakini, kwa sababu sisi ni Wakristo wa kweli, “ndugu” yetu ni kila Mukristo wa kweli, hata kama ni wa inchi ingine. (Waroma 10:12) Yehova ametufundisha tupendane kama ndugu na dada. (1 Wathesalonike 4:9) Lakini, sababu gani ni jambo la maana tuendelee kuonyesha upendo wa kindugu?

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA SANA TUENDELEE KUONYESHA UPENDO WA KINDUGU?

7. (a) Ni sababu gani kubwa zaidi yenye kutuchochea tuonyeshe upendo wa kindugu? (b) Toa sababu ingine yenye kuonyesha kwamba ni jambo la maana kutia nguvu upendo wetu wa kindugu.

7 Sababu kubwa zaidi yenye kutuchochea tuonyeshe upendo wa kindugu ni kwamba Yehova anatuomba tufanye hivyo. Hatuwezi kabisa kumupenda Yehova ikiwa tunakataa kupenda ndugu na dada zetu. (1 Yohana 4:7, 20, 21) Sababu ingine ni kwamba kila mumoja wetu iko na lazima ya mwengine, zaidi sana wakati wa magumu. Wakati mutume Paulo aliandikia Wakristo Waebrania, alijua kwamba wamoja kati yao walikuwa karibu kuacha nyumba zao na vitu vyao vingine. Yesu alikuwa ameeleza magumu yenye ingetokea wakati huo. (Marko 13:14-18; Luka 21:21-23) Kwa hiyo, mbele wakati huo ufike, Wakristo hao walipaswa kutia nguvu upendo wao.—Waroma 12:9.

Tunapaswa kutia nguvu upendo wetu wa kindugu leo kwa sababu upendo huo utatusaidia kuvumilia majaribu yenye tunaweza kupata wakati unaokuja

8. Mbele ziki kubwa ianze, tunapaswa kufanya nini leo?

8 Ziki kubwa yenye haijatokeaka katika historia yote ya wanadamu, itafika hivi karibuni. (Marko 13:19; Ufunuo 7:1-3) Tutakuwa na lazima ya kutii amri hii: ‘Muende, watu wangu, ingia katika vyumba vyako vya ndani, na ufunge milango nyuma yako. Ujifiche kwa kitambo [muda] kidogo mupaka hukumu itakapopita.’ (Isaya 26:20) Vyumba hivyo vya ndani vinaweza kumaanisha makutaniko yetu. Tunakusanyika humo pamoja na ndugu na dada zetu ili kumuabudu Yehova. Lakini tunapaswa kufanya mengi zaidi kuliko tu kukusanyika kwa ukawaida. Mutume Paulo aliwakumbusha Wakristo Waebrania kwamba walipaswa kuchocheana ili kuonyeshana upendo na kutendeana mema. (Waebrania 10:24, 25) Tunapaswa kutia nguvu upendo wetu wa kindugu leo kwa sababu upendo huo utatusaidia kuvumilia majaribu yenye tunaweza kupata wakati unaokuja.

9. (a) Tuko na nafasi gani za kuonyesha upendo wa kindugu? (b) Toa mifano yenye kuonyesha namna watu wa Yehova wameonyesha upendo wa kindugu.

9 Mbele ziki kubwa ianze, tuko na nafasi nyingi za kuonyesha upendo wa kindugu leo. Ndugu na dada zetu wengi wanateseka kwa sababu ya mambo kama vile, matetemeko ya inchi, mafuriko ao maji mengi yenye kubeba nyumba na vitu, na tsunami. Ndugu na dada wanaendelea kuvumilia mateso. (Mathayo 24:6-9) Pia, maisha katika ulimwengu huu muovu inafanya ikuwe vigumu kupata feza. (Ufunuo 6:5, 6) Hata hivyo, kadiri ndugu na dada zetu wanaendelea kupata magumu mengi, tunakuwa na nafasi nyingi za kuonyesha kwamba tunawapenda sana. Watu wa ulimwengu huu hawapendane, lakini sisi tunapaswa kuendelea kuonyesha upendo wa kindugu. (Mathayo 24:12) [1]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUFANYA UPENDO WETU WA KINDUGU UENDELEE?

10. Tutazungumuzia nini sasa?

10 Hata kama tuko na magumu, namna gani tunaweza kuhakikisha kwamba tunaendelea kuonyesha upendo wa kindugu? Namna gani tunaweza kuonyesha ndugu na dada zetu upendo huo? Kisha kusema, “upendo wenu wa kindugu na uendelee,” mutume Paulo alitaja njia mbalimbali zenye Wakristo wanaweza kutumia ili kuonyesha upendo huo. Tuzungumuzie sasa njia sita kati ya njia hizo.

11, 12. Kukaribisha wageni kunamaanisha nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 ‘Musisahau ukaribishaji-wageni.’ (Soma Waebrania 13:2.) Maneno “ukaribishaji-wageni” inamaanisha nini? Maneno yenye mutume Paulo alitumia inamaanisha moja kwa moja “kuonyesha wageni wema.” Pengine maneno hayo inatukumbusha Abrahamu na Loti. Wanaume hao wawili walionyesha wema watu wenye hawakuwa wanajua. Kisha, Abrahamu na Loti walitambua kabisa kwamba watu hao walikuwa malaika. (Mwanzo 18:2-5; 19:1-3) Mifano hiyo ilitia moyo Wakristo Waebrania waonyeshe upendo wa kindugu kwa kukaribisha wageni.

12 Namna gani tunaweza kuonyesha wengine ukaribishaji? Tunaweza kualika ndugu na dada nyumbani kwetu ili kula chakula pamoja ao kutiana moyo. Hata kama hatufahamie muzuri mwangalizi wa muzunguko na bibi yake, tunaweza kuwaalika wakati wanatembelea kutaniko letu. (3 Yohana 5-8) Haiko lazima kupika chakula mingi ao kutumia feza nyingi sana. Kusudi letu ni kutia ndugu na dada zetu moyo, lakini hatutafute kuwashangaza na vitu vyenye tuko navyo. Tena, hatutaalika tu wale wenye kuwa na uwezo wa kutualika pia. (Luka 10:42; 14:12-14) Jambo la maana zaidi ni kuhakikisha kwamba hatuhangaikie mambo mengi sana mupaka tufikie kusahau kuonyesha wengine ukaribishaji!

13, 14. Namna gani tunaweza ‘kuwakumbuka wale walio katika gereza’?

13 ‘Muwakumbuke wale walio katika gereza.’ (Soma Waebrania 13:3.) Wakati mutume Paulo aliandika maneno hayo, alikuwa anazungumuzia ndugu wenye walifungwa kwa sababu ya imani yao. Mutume Paulo alipongeza ndugu na dada wa kutaniko hilo kwa sababu ‘waliwasikitikia [waliwasikilia huruma] wale waliokuwa gerezani.’ (Waebrania 10:34) Ndugu fulani walimusaidia mutume Paulo kwa muda wa miaka ine yenye alifungwa katika gereza, lakini wengine walikuwa wanaishi mbali sana. Namna gani wangemusaidia mutume Paulo? Kwa kuendelea kusali kwa bidii kwa ajili yake.—Wafilipi 1:12-14; Waebrania 13:18, 19.

Tunaweza kusali kwa ajili ya ndugu, dada, na watoto wenye wamefungwa katika gereza huko Eritrea

14 Leo, Mashahidi wengi wa Yehova wamefungwa katika gereza kwa sababu ya imani yao. Ndugu na dada wenye kuishi karibu nao wanaweza kuwasaidia moja kwa moja. Lakini wengi kati yetu tunaishi mbali nao. Namna gani tunaweza kuwakumbuka na kuwasaidia? Upendo wa kindugu utatuchochea tusali kwa bidii kwa ajili yao. Kwa mufano, tunaweza kusali kwa ajili ya ndugu, dada, na watoto wenye wamefungwa katika gereza huko Eritrea, kati yao kuko ndugu Paulos Eyassu, Isaac Mogos, na Negede Teklemariam, wenye wamefungwa zaidi ya miaka 20.

15. Namna gani tunaweza kuheshimia ndoa yetu?

15 ‘Ndoa iheshimiwe kati ya wote.’ (Soma Waebrania 13:4.) Tunaweza pia kuonyesha upendo wa kindugu kwa kuwa na mwenendo safi. (1 Timotheo 5:1, 2) Kwa mufano, ikiwa tunafanya uasherati na ndugu ao dada fulani, tutamuumiza yeye na familia yake. Hilo linaweza kufanya tukose kutumainiana. (1 Wathesalonike 4:3-8) Fikiria pia namna bibi anaweza kujisikia ikiwa anavumbua kwamba bwana yake anaangaliaka pornografia. Je, atajisikia kuwa bwana yake anamupenda kabisa na anaheshimia mupango wa ndoa?—Mathayo 5:28.

16. Namna gani kutosheka kunatusaidia tuonyeshe upendo wa kindugu?

16 ‘Murizike [mutosheke] na vitu vya sasa.’ (Soma Waebrania 13:5.) Kumutegemea Yehova kutatusaidia tutosheke, ni kusema, kufurahia vitu vyenye tuko navyo. Namna gani kufanya hivyo kunatusaidia tuonyeshe upendo wa kindugu? Ikiwa tunatosheka, tutakumbuka kwamba ndugu na dada zetu ni wa maana zaidi kuliko feza ao vitu. (1 Timotheo 6:6-8) Hatutanungunikia ndugu na dada zetu ao hali yetu katika maisha. Tutaepuka pia kusikilia wengine wivu ao kuwa wenye pupa (tamaa kubwa). Lakini, ikiwa tunatosheka, tutakuwa wakarimu.—1 Timotheo 6:17-19.

17. Namna gani ‘kuwa hodari’ kunatusaidia tuonyeshe upendo wa kindugu?

17 ‘Mukuwe hodari.’ (Soma Waebrania 13:6.) Kumutegemea Yehova kunatupatia uhodari ao nguvu ya kuvumilia majaribu. Nguvu hiyo inatusaidia kuwa na maoni mazuri. Na wakati tunakuwa na maoni mazuri, tunaweza kuonyesha upendo wa kindugu kwa kutia moyo na kufariji ndugu na dada zetu. (1 Wathesalonike 5:14, 15) Hata wakati wa ziki kubwa, tunaweza kuwa na ujasiri, kwa sababu tunajua kwamba wokovu wetu unakaribia.—Luka 21:25-28.

Tunaweza kuwa na ujasiri, kwa sababu tunajua kwamba wokovu wetu unakaribia

18. Ni nini inaweza kutuchochea tuendelee kuwapenda wazee?

18 ‘Muwakumbuke wale ambao wanaongoza katikati yenu.’ (Soma Waebrania 13:7, 17.) Wazee wa kutaniko wanatumia sana wakati wao ili kutusaidia. Wakati tunafikiria mambo yote yenye wanatufanyia, hilo linatuchochea tuendelee kuwapenda na kuwaonyesha shukrani. Hatupendi hata kidogo matendo yetu iwafanye wapoteze furaha yao ao wakasirike. Lakini, tunapenda kuwa tayari kutii. Kwa kufanya hivyo, ‘tunawafikiria kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.’—1 Wathesalonike 5:13.

Unaonyesha shukrani juu ya kazi yenye wazee wanatufanyia?(Picha hizi zinapatana na fungu la 18)

MUENDELEE KUFANYA HIVYO KWA NJIA KUBWA ZAIDI

19, 20. Namna gani tunaweza kuendelea kuonyesha upendo wa kindugu kwa njia kubwa zaidi?

19 Watu wa Yehova wanajulikana kwa sababu ya upendo wao wa kindugu. Ilikuwa hivyo pia wakati wa mutume Paulo. Lakini mutume Paulo alichochea ndugu na dada waonyeshe upendo kwa njia kubwa zaidi. Alisema hivi: ‘Muendelee kufanya hivyo kwa kipimo kamili zaidi [njia kubwa zaidi].’ (1 Wathesalonike 4:9, 10) Ni wazi kwamba tungali na mengi ya kufanya ili kuonyesha upendo kwa njia kubwa zaidi!

20 Kwa hiyo, katika mwaka huu, wakati tutakuwa tunaona andiko letu la mwaka katika Jumba letu la Ufalme, tunapaswa kufikiri sana juu ya maulizo haya: Ninaweza kuonyesha ukaribishaji kwa njia kubwa zaidi? Namna gani ninaweza kusaidia ndugu na dada wenye kufungwa katika gereza? Ninaheshimia ndoa, mupango wa Mungu? Ninaweza kufanya nini ili nitosheke kabisa? Namna gani ninaweza kumutegemea Yehova zaidi? Namna gani ninaweza kutii kabisa wale wenye kuongoza? Tukifanya mabadiliko katika mambo hayo sita, andiko letu la mwaka halitakuwa tu alama katika Jumba la Ufalme; lakini litatuchochea kutii maneno haya ya mutume Paulo: “Upendo wenu wa kindugu na uendelee.”—Waebrania 13:1.

^ [1] (fungu la 9) Ili kujua namna Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo wa kindugu wakati wa misiba, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2002 ukurasa wa 8-9, na kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu, sura ya 19.