Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni wakati gani watu wa Mungu walikuwa watumwa, ao wafungwa, wa Babiloni Mukubwa?

Utumwa huo ulianza wakati fulani kisha mwaka wa 100 na uliisha katika mwaka wa 1919. Sababu gani mafasirio haya ya mupya ni ya lazima?

Ushuhuda mwingi unaonyesha kwamba katika mwaka wa 1919, Wakristo watiwa-mafuta walikombolewa kutoka katika Babiloni Mukubwa na walikuwa wamekusanywa katika kutaniko lenye kuwa safi. Ufikirie jambo hili: Kisha tu Ufalme wa Mungu kuanza kutawala huko mbinguni katika mwaka wa 1914, watu wa Mungu walichunguzwa na kusafishwa polepole na kuacha ibada ya uongo. * (Soma maelezo ya chini.) (Malaki 3:1-4) Kisha, katika mwaka wa 1919, Yesu alimuweka ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ ili apatie watu wa Mungu “chakula chao kwa wakati unaofaa.” (Mathayo 24:45-47) Katika mwaka huo, watu wa Mungu waliachiliwa kutoka katika utumwa wa mufano wa Babiloni Mukubwa. (Ufunuo 18:4) Lakini, ni wakati gani watu wa Mungu waliingia katika utumwa huo?

Zamani, tulifasiria kwamba watu wa Mungu walikuwa watumwa wa Babiloni Mukubwa kwa muda mufupi kuanzia mwaka wa 1918. Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 3, 1992 ulisema kwamba kama vile tu Waisraeli walipelekwa katika utumwa huko Babiloni, katika mwaka wa 1918 watumishi wa Yehova walikuwa watumwa katika Babiloni Mukubwa. Kujifunza maandiko zaidi kumeonyesha kwamba watu wa Mungu walikuwa watumwa miaka mingi mbele ya mwaka wa 1918.

Unabii wenye kupatikana kwenye Ezekieli 37:1-14 ulisema kwamba watu wa Mungu wangekuwa watumwa na mwishowe wangeachiliwa. Nabii Ezekieli aliona katika maono bonde lenye kujaa mifupa. Yehova alimuambia hivi: “mifupa hii, hii ni nyumba nzima ya Israeli.” (Mustari wa 11) Unabii huo ulizungumuzia taifa la Israeli na mwishowe “Israeli wa Mungu,” wenye kutiwa mafuta. (Wagalatia 6:16; Matendo 3:21) Katika maono hayo, mifupa ilianza kuishi tena na kuwa jeshi kubwa sana. Hilo linaeleza namna watu wa Mungu waliachiliwa kutoka katika Babiloni Mukubwa katika mwaka wa 1919. Lakini, namna gani unabii huo unaonyesha kwamba walikuwa watumwa kwa miaka mingi?

Kwanza, nabii Ezekieli aliona kwamba mifupa ya watu hao wenye walikufa ilikuwa “mikavu [yenye kukauka] sana.” (Ezekieli 37:2, 11) Hilo linamaanisha kwamba watu hao walikuwa wamekufa zamani. Pili, nabii Ezekieli aliona watu wenye walikuwa wamekufa wanarudia polepole kwenye uzima, lakini haikuwa mara moja. Alisikia ‘sauti ya kugongana, nayo mifupa ikaanza kukaribiana, mufupa kwa mufupa wake.’ Kisha, aliona “kano na nyama zikaja juu yake na ngozi.” Kisha, ngozi ikafunika nyama. Kisha hapo, ‘pumuzi ikaanza kuingia ndani yao, nao wakaanza kuishi.’ Mwishowe, watu hao walianza kuishi tena; kisha Yehova aliwapatia inchi yao ili waishi ndani yake. Mambo hayo yote yangechukuwa wakati fulani.—Ezekieli 37:7-10, 14.

Kama vile unabii ulisema, Waisraeli walikuwa watumwa kwa muda murefu. Utumwa huo ulianza katika mwaka wa 740 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati makabila kumi ya Israeli, ni kusema, ufalme wa kaskazini, yalihamishwa kwa nguvu kutoka katika inchi yao. Kisha, katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Wababiloni waliharibu muji wa Yerusalemu, na makabila mengine mawili, ni kusema, ufalme wa kusini wa Yuda, yalihamishwa kwa nguvu kutoka katika inchi yao. Kisha, katika mwaka wa 537 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, utumwa huo ukaisha wakati hesabu kidogo ya Wayahudi walirudia kujenga tena hekalu na kumuabudu Yehova katika Yerusalemu.

Kwa hiyo, maelezo hayo yanaonyesha kwamba Wakristo walikuwa watumwa wa Babiloni Mukubwa kwa muda murefu, haiko tu kuanzia mwaka wa 1918 mupaka 1919. Yesu alizungumuzia kipindi hicho kirefu wakati alisema kwamba Wakristo wa uongo, ni kusema, magugu, wangekomalia pamoja na “wana wa ufalme,” ni kusema, ngano. (Mathayo 13:36-43) Katika kipindi hicho, kulikuwa hesabu kidogo ya Wakristo wa kweli. Wengi kati ya wale wenye walijiita kuwa Wakristo walikubali mafundisho ya uongo na kuwa waasi-imani. Ndiyo sababu tunaweza kusema kwamba Babiloni Mukubwa alitia kutaniko la Kikristo katika utumwa. Utumwa huo ulianza wakati fulani kisha mwaka wa 100 na kuendelea mupaka wakati hekalu la kiroho la Mungu lilisafishwa wakati wa mwisho.—Matendo 20:29, 30; 2 Wathesalonike 2:3, 6; 1 Yohana 2:18, 19.

Katika miaka mingi hiyo, viongozi wa kanisa na viongozi wa politike walikuwa na nguvu ya kutawala watu sana. Kwa mufano, watu hawakuruhusiwa kuwa na Biblia ao kuisoma katika luga yenye wangeweza kuelewa. Watu fulani wenye walisoma Biblia walifungwa kwenye muti na kuunguzwa. Na wale wenye walipinga mafundisho ya viongozi wa kanisa waliteswa sana. Ilikuwa vigumu sana watu wajifunze kweli ao kuifundisha watu wengine.

Maono ya nabii Ezekieli inatufundisha pia kwamba watu wa Mungu walianza kuishi tena na waliachiliwa polepole kutoka katika dini ya uongo. Kwa hiyo, ni wakati gani jambo hilo lilianza kutokea, na namna gani? Maono inataja “sauti ya kugongana.” Hilo lilianza kufanyika miaka kidogo mbele wakati wa mwisho uanze. Katika miaka hiyo, kulikuwa watu fulani waaminifu wenye walipenda kupata kweli na kumuabudu Mungu hata kama walizungukwa na mafundisho mengi ya uongo. Walijifunza Biblia na walifanya yao yote ili kuambia watu mambo yenye walikuwa wanajifunza. Wengine walitumika sana ili kutafsiri Biblia katika luga zenye watu walikuwa wanaelewa.

Kisha, karibu na mwisho wa miaka ya 1800, ilikuwa kama vile mifupa ilianza kuwa na nyama na ngozi. Charles Taze Russell na marafiki wake walitumika sana ili kupata kweli ya Biblia na kumutumikia Yehova. Walisaidia pia wengine kuelewa kweli kwa kutumia Le Phare de la Tour de Sion na vichapo vingine. Kisha, walitumia “Foto-Drama ya Uumbaji” katika mwaka wa 1914, na kitabu Le mystère de Dieu accompli katika mwaka wa 1917, ili kusaidia watu wa Yehova watie nguvu imani yao. Mwishowe, katika mwaka wa 1919, ilikuwa kama vile watu wamepewa uzima na inchi mupya. Tangu wakati huo, wale wenye kuwa na tumaini la kuishi milele katika dunia wamejiunga na watiwa-mafuta. Wote wanamuabudu Yehova, na wamekuwa “jeshi kubwa, naam, kubwa sana.”—Ezekieli 37:10; Zekaria 8:20-23. *—Soma maelezo ya chini.

Kwa hiyo, ni wazi kwamba watu wa Mungu walikuwa katika utumwa wa Babiloni Mukubwa kisha mwaka wa 100. Wakati huo watu waligeuka na kuwa waasi-imani kwa kukubali mafundisho ya uongo na kuacha mafundisho ya kweli. Kwa miaka mingi, ilikuwa vigumu sana kumutumikia Yehova, kama vile ilikuwa kwa Waisraeli wakati walikuwa watumwa ao katika gereza. Lakini leo kweli inahubiriwa kwa kila mutu. Tunafurahi sana kwa sababu tunaishi wakati wale wenye “walio na ufahamu watangaa . . . kama mwangaza”! Leo wengi wanaweza ‘kujitakasa [kujisafisha],’ “kusafishwa,” na kukubali ibada safi!—Danieli 12:3, 10.

Wakati Shetani alipenda kumujaribu Yesu, alimupeleka moja kwa moja kwenye hekalu, ao alimuonyesha hekalu katika maono?

Hatujue kabisa njia yenye Shetani alitumia ili kumuonyesha Yesu hekalu.

Mathayo na Luka, waandikaji wa Biblia waliandika habari juu ya mambo yenye ilifanyika. Mathayo anasema kwamba ‘Ibilisi akamuchukua’ Yesu huko Yerusalemu na ‘kumusimamisha juu ya munara wa hekalu,’ ni kusema, “sehemu ya juu sana” ya hekalu. (Mathayo 4:5) Luka anasema kwamba Ibilisi ‘akamuongoza kuingia Yerusalemu, akamusimamisha juu ya munara wa hekalu.’—Luka 4:9.

Zamani, vichapo vyetu vilisema kwamba pengine Shetani hakumupeleka Yesu moja kwa moja kwenye hekalu ili kumujaribu. Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 1961, ulilinganisha hilo na wakati Shetani alimujaribu Yesu kwa kumupandisha kwenye mulima murefu sana ili kumuonyesha falme zote za dunia. Gazeti hilo lilisema kwamba hakuna mulima wenye kuwa murefu zaidi kwenye mutu anaweza kupanda ili kuona falme zote za dunia. Kisha gazeti hilo lilisema kwamba, vilevile pengine Shetani hakumupeleka moja kwa moja kwenye hekalu la kweli. Hata hivyo, habari zingine zenye zilitokea katika Munara wa Mulinzi kisha hapo zilisema kwamba ikiwa Yesu angeruka kutoka kwenye hekalu, angejiua.

Watu fulani wanasema kwamba kwa sababu Yesu hakuwa Mulawi, hangeruhusiwa kupanda juu ya patakatifu pa hekalu. Kwa hiyo, watu hao wanasema kwamba pengine Shetani alipenda kumujaribu Yesu kwa kutumia maono. Mamia ya miaka mbele ya hapo, Ezekieli alipelekwa pia kwenye hekalu katika maono.—Ezekieli 8:3, 7-10; 11:1, 24; 37:1, 2.

Lakini, ikiwa Yesu alipelekwa kwenye hekalu katika maono, watu fulani wanaweza kujiuliza hivi:

  • Je, angejaribu kabisa kuruka kutoka kwenye hekalu?

  • Mara ingine wakati Shetani alipenda tena kumujaribu Yesu, alimuomba ageuze majiwe ya kweli ikuwe mikate na alipenda Yesu amufanyie tendo la kweli la ibada. Kwa hiyo, inawezekana pia Shetani alipenda Yesu aruke kutoka kwenye hekalu la kweli-kweli?

Sasa, ikiwa Shetani hakutumia maono lakini alimupeleka Yesu kwenye hekalu la kweli-kweli, watu wengine wanaweza kujiuliza hivi:

  • Wakati Yesu alisimama kwenye sehemu ya juu ya patakatifu pa hekalu, je, alivunja Sheria?

  • Namna gani Yesu alitoka katika jangwa na kufika kwenye hekalu katika Yerusalemu?

Tuchunguze basi habari fulani zingine zenye zitatusaidia kujibu maulizo hayo mawili.

Profesa Carson aliandika kwamba inawezekana neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “hekalu,” lenye Mathayo na Luka walitumia linaweza kumaanisha eneo lote la hekalu na haiko tu mahali patakatifu, ni kusema, mahali kwenye Walawi tu ndio waliruhusiwa kufika. Pembe ya kusini-mashariki ya hekalu ilikuwa na dari yenye kuwa tambarare (plat); dari hiyo ndiyo ilikuwa ya juu sana katika hekalu. Pengine Yesu alisimamishwa kwenye dari hiyo. Kutoka pale mupaka mwisho wa bonde la Kidroni, kulikuwa metre 140 hivi. Mwanahistoria Josèphe alisema kwamba mahali hapo palikuwa juu sana, na kwamba ikiwa mutu angesimama hapo na kuangalia chini, “angesikia kizunguzungu.” Hata kama Yesu hakuwa Mulawi, angesimama mahali hapo, na hakuna mutu mwenye angemuzuia.

Lakini, namna gani Yesu alitoka katika jangwa na kufika kwenye hekalu katika Yerusalemu? Hatujue kabisa. Biblia inasema tu kwamba Yesu alipelekwa huko Yerusalemu. Haiseme ikiwa Yesu alikuwa mbali ao karibu na Yerusalemu, ao muda wenye Shetani alimujaribu. Kwa hiyo, inawezekana Yesu alitembea mupaka Yerusalemu, hata kama hilo lingemuchukua wakati mwingi.

Wakati Shetani alimuonyesha Yesu “falme zote za dunia,” inawezekana ilikuwa katika maono, kwa sababu katika dunia yote, hakuna mulima fulani kwenye mutu anaweza kupanda ili aone falme hizo zote. Tunaweza kufananisha jambo hilo na namna tunaweza kutumia televizyo ili kumuonyesha mutu picha za sehemu zingine za dunia. Pengine Shetani alitumia maono, lakini alimuomba kwa kweli Yesu amuinamie ili kumuabudu. (Mathayo 4:8, 9) Kwa hiyo, wakati Shetani alimubeba Yesu kwenye hekalu, inawezekana alipenda kwa kweli Yesu atie uzima wake katika hatari kwa kuruka kutoka kwenye hekalu. Lakini Yesu alikataa. Ingekuwa jaribu kubwa sana ikiwa angejaribiwa tu kupitia maono!

Kwa hiyo, inawezekana kwamba Yesu alienda kabisa Yerusalemu na kusimama kwenye sehemu ya juu sana ya hekalu. Kwa kweli, kama vile tulisema kwenye mwanzo wa habari hii, hatujue muzuri kabisa namna Shetani alimuonyesha Yesu hekalu. Lakini, tunaweza kuwa hakika kwamba Shetani aliendelea kumujaribu Yesu ili afanye jambo fulani la mubaya, lakini Yesu aliendelea kukataa kabisa jaribu hilo.

^ fu. 2 Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013 ukurasa wa 10-12, fungu la 5-8, 12.

^ fu. 2 Andiko la Ezekieli 37:1-14 na Ufunuo 11:7-12 yote yanazungumuzia jambo fulani lenye lilitokea katika mwaka wa 1919. Unabii wenye kupatikana kwenye Ezekieli 37:1-14 unazungumuzia namna watu wote wa Mungu walirudilia ibada ya kweli katika mwaka wa 1919, kisha kuwa katika utumwa kwa miaka mingi. Lakini andiko la Ufunuo 11:7-12 linazungumuzia mwaka wa 1919, wakati kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta wenye kuongoza katikati ya watu wa Mungu walianza tena kuishi. Ndugu hao walikuwa wamezuiwa kutenda kwa muda fulani.