Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’

‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’

‘Muende mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, muwabatize . . . , na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’MATHAYO 28:19, 20.

NYIMBO: 141, 97

1, 2. Maneno ya Yesu katika Mathayo 24:14 yanaleta maulizo gani?

YESU alitabiri kama katika siku za mwisho, habari njema ya Ufalme itahubiriwa kwa watu wote. (Mathayo 24:14) Sisi Mashahidi wa Yehova tunajulikana katika dunia yote kwa sababu ya kazi yetu ya kuhubiri. Watu fulani wanapendezwa na ujumbe wenye tunahubiri, na wengine hawapendezwe na ujumbe huo. Lakini hata watu fulani wenye hawapendezwe na ujumbe wetu wanatuheshimia kwa sababu ya kazi yetu. Tunasema kama sisi ndio tunafanya kazi yenye Yesu alitabiri. Tuko na haki ya kusema hivyo? Namna gani tunaweza kuwa hakika kama kazi yetu ya kuhubiri ndiyo kazi yenye Yesu alitabiri?

2 Watu wa dini nyingi wanasema kama wanahubiri ujumbe wa Yesu. Lakini wanahubiri tu katika kanisa, kwenye televizyo, ao kwenye Internete, ao wanaweza tu kuambia wengine namna walijua Yesu. Wengine wanafikiri kwamba kusaidia watu wenye wako na lazima ya musaada kwa kufanya kazi kama vile kuwa munganga, ao mwalimu, ndio namna yao ya kuhubiri. Lakini, kufanya hivyo ndiyo kazi ya kuhubiri yenye Yesu alizungumuzia?

3. Kulingana na Mathayo 28:19, 20, wanafunzi wa Yesu wanapaswa kufanya mambo gani ine?

3 Yesu alitaka wanafunzi wake wangojee watu wakuje kwao? Hapana! Kisha ufufuo wake, Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Muende mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, muwabatize. . . , na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’ (Mathayo 28:19, 20) Kwa hiyo, sisi wanafunzi wa Yesu, tunapaswa kufanya mambo ine. Tunapaswa kufanya wanafunzi, kuwabatiza, na kuwafundisha. Lakini kwanza, tunapaswa kuenda kutembelea watu. Mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia anasema kama kila mutu mwenye kuamini anapaswa ‘kuenda’ ikuwe ataenda katika maeneo ya mbali ao ya karibu ili kuhubiri.—Mathayo 10:7; Luka 10:3.

4. Kazi ya ‘kuvua watu,’ inaomba nini?

4 Yesu alipenda wanafunzi wake wafanye nini? Alitaka kila mutu ahubiri vile anapenda, ao alitaka wakuwe kikundi chenye kupangwa muzuri? Kwa sababu mutu moja hangeweza kuhubiria watu wa “mataifa yote,” wanafunzi wake walipaswa kuwa kikundi chenye kupangwa muzuri. Ni hivyo Yesu alipenda kusema wakati alialika wanafunzi wake wakuwe “wavuvi wa watu.” (Soma Mathayo 4:18-22.) Yesu hakuwa anazungumuzia mutu mwenye kuloa samaki kwa kutumia ndoano na chambo, na kungojea samaki yenye itakula chambo hicho. Lakini, Yesu alikuwa anazungumuzia kazi ya kuvua samaki kwa kutumia wavu (filet). Kazi hiyo inaomba kutumika sana, kupangwa muzuri, na inaomba watu wengi watumike pamoja.—Luka 5:1-11.

5. Ni maulizo gani ine yenye tunapaswa kujibia, na sababu gani?

5 Ili tujue ni nani wanahubiri habari njema leo, tunapaswa kujibia maulizo haya ine:

  • Wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuhubiri ujumbe gani?

  • Wanapaswa kuchochewa na nia gani?

  • Wanapaswa kutumia njia gani?

    Kazi yao inapaswa kufika wapi, na inapaswa kuendelea mupaka wakati gani?

Majibu ya maulizo hayo yatatusaidia tujue ni nani wanafanya kazi hiyo ya kuokoa uzima, na yatatusaidia tukuwe na bidii ya kuendelea kuhubiri.—1 Timotheo 4:16.

WANAFUNZI WA YESU WANAPASWA KUHUBIRI UJUMBE GANI?

6. Sababu gani unaweza kuwa hakika kama Mashahidi wa Yehova wanahubiri ujumbe wenye unastahili kuhubiriwa?

6 Soma Luka 4:43. Yesu alihubiri “habari njema ya ufalme wa Mungu,” na alipenda wanafunzi wake wafanye pia hivyo. Ni watu gani wenye kuhubiri ujumbe huo kwa watu wote? Ni Mashahidi wa Yehova tu! Hata watu fulani wenye wanatuchukia wanajua hivyo. Kwa mufano, ona namna padri mumoja misionere mwenye aliishi katika inchi mbalimbali aliambia Shahidi wa Yehova mumoja. Katika kila inchi, padri huyo aliuliza Mashahidi wa Yehova ni ujumbe gani walikuwa wanahubiri. Alisema hivi: “Wote walikuwa wapumbavu sana, kwa sababu walitoa jibu lilelile: ‘Habari njema ya Ufalme.’” Maneno ya padri huyo yanaonyesha kabisa kama hatuko wapumbavu lakini tuko na umoja kwa sababu tuko Wakristo wa kweli. (1 Wakorintho 1:10) Pia, Ufalme wa Mungu ndio ujumbe mukubwa wa gazeti letu Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Gazeti hilo linapatikana katika luga 254 na karibu kopi 59000000 za kila gazeti zinachapishwa. Kwa hiyo, gazeti hilo ndilo gazeti lenye kugawanywa sana katika dunia!

Mashahidi wa Yehova tu ndio wanahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu

7. Tunajua namna gani kama viongozi wa dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hawahubiri ujumbe wenye unastahili kuhubiriwa?

7 Viongozi wa dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hawahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Kama wanazungumuza juu ya Ufalme, wengi kati yao wanasema kwamba ni hali yenye kuwa katika moyo wa mutu. (Luka 17:21) Hawafundishe watu kama Ufalme ni serikali ya mbinguni yenye Yesu anaongoza. Lakini, wanazungumuza juu ya Yesu mara nyingi siku ya Noeli ao siku ya Pasaka. Hawaambie watu kama Ufalme wa Mungu ndio utamaliza magumu yote ya wanadamu na kama hivi karibuni utaondoa mambo yote ya mubaya kwenye dunia. (Ufunuo 19:11-21) Kwa kweli, viongozi wa dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hawajue mambo yenye Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, atafanya. Na kwa sababu hawaelewe ujumbe wa Yesu, hawaelewe sababu gani wanapaswa kuhubiri.

TUNAPASWA KUCHOCHEWA NA NIA GANI WAKATI TUNAFANYA KAZI YA KUHUBIRI?

8. Makanisa mengi yanachochewa na nia gani ya mubaya wakati yanafanya kazi ya kuhubiri?

8 Wanafunzi wa Yesu hawapaswe kuhubiri ili kupata feza ao kujenga nyumba kubwa zenye kushangaza. Yesu alisema hivi: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’ (Mathayo 10:8) Kwa hiyo, kazi ya kuhubiri haipaswe kuwa biashara ao kazi ya kutafuta feza. (2 Wakorintho 2:17) Wanafunzi wa Yesu hawapaswe kuomba malipo kwa ajili ya kazi yao. (Soma Matendo 20:33-35.) Agizo la Yesu liko wazi sana, lakini makanisa mengi yanafuatilia tu kukusanya feza ili kuendeleza kazi za makanisa yao na kulipa viongozi wa kanisa na wafanyakazi wengine. Hilo limefanya viongozi wengi wa dini zenye kujiita kuwa za Kikristo wakuwe matajiri sana.—Ufunuo 17:4, 5.

Kazi ya kuhubiri haipaswe kuwa biashara ao kazi ya kutafuta feza

9. Namna gani Mashahidi wa Yehova wameonyesha kama wanachochewa na nia ya muzuri wakati wanafanya kazi ya kuhubiri?

9 Je, Mashahidi wa Yehova wanakusanya sadaka kwenye Majumba yao ya Ufalme ao kwenye mikusanyiko yao? Hapana! Kazi yao inategemezwa na michango ya kujipendea. (2 Wakorintho 9:7) Hata hivyo, mwaka jana, Mashahidi wa Yehova walipitisha saa karibu miliare mbili katika kazi ya kuhubiri habari njema na waliongoza mafunzo ya Biblia zaidi ya milioni kenda kila mwezi. Hawapate malipo kwa ajili ya kazi yao ya kuhubiri, lakini wanafurahia kutumia feza zao wenyewe ili kufanya kazi hiyo. Juu ya kazi ya Mashahidi wa Yehova, mutu mumoja mwenye kutafuta habari alisema hivi: “Kusudi lao kubwa ni kuhubiri na kufundisha.” Pia alisema kama Mashahidi wa Yehova hawana viongozi wa dini wenye kupokea mushahara. Sasa, ikiwa hatuhubiri ili kupata feza, ni nia gani yenye inatuchochea kuhubiri? Tunafanya kazi hiyo kwa kujipendea kwa sababu tunamupenda Yehova na tunapenda watu. Hilo linatimiza unabii wenye kuwa katika andiko la Zaburi 110:3. (Soma.)

WANAPASWA KUTUMIKISHA NJIA GANI?

Tunahubiri kila mahali kwenye tunapata watu (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10. Yesu na wanafunzi wake walitumikisha njia gani ili kuhubiri?

10 Yesu na wanafunzi wake walitumikisha njia gani ili kuhubiri? Walienda kila nafasi kwenye wangeweza kupata watu. Kwa mufano, walihubiri katika barabara na katika soko. Pia, walitembelea watu kwenye nyumba zao. (Mathayo 10:11; Luka 8:1; Matendo 5:42; 20:20) Kuhubiri nyumba kwa nyumba ilikuwa njia yenye kupangwa muzuri ili kufikia watu wa namna zote.

11, 12. Juu ya kazi ya kuhubiri habari njema, kuna tofauti gani kati ya Mashahidi wa Yehova na watu wenye kujiita kuwa Wakristo?

11 Makanisa yenye kujiita kuwa ya Kikristo yanahubiri habari njema kama vile Yesu alifanya? Mara nyingi, viongozi wa dini wenye kulipwa ndio wanahubiria watu wa makanisa yao. Viongozi hao hawafanye wanafunzi wapya, lakini wanajikaza tu kubakia na watu wenye wamekwisha kuamini. Wakati fulani, wamejaribu kutia moyo watu wa makanisa yao wahubiri. Kwa mufano, katika mwaka wa 2001, Papa Jean Paul wa 2 alisema katika barua moja kama watu wa kanisa wanapaswa kuhubiri Injili na kuwa na bidii kama ya mutume Paulo, mwenye alisema hivi: “Ole wangu kama sihubiri Injili.” Kisha, Papa huyo alisema kama kazi ya kuhubiri haipaswe kufanywa tu na watu kidogo wenye wamepata mazoezi, lakini watu wote wa kanisa wanapaswa kufanya kazi hiyo. Lakini, ni watu kidogo tu ndio wamefuata maneno hayo.

12 Halafu Mashahidi wa Yehova? Ni wao tu ndio wanahubiri kama Yesu ameanza kutawala akiwa Mufalme tangu mwaka wa 1914. Wanamutii Yesu na wanatia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. (Marko 13:10) Kitabu kimoja (Pillars of Faith—American Congregations and Their Partners) kilisema kama Mashahidi wa Yehova wanaona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana sana kwao. Kitabu hicho kilisema pia kama wakati wanakutana mutu mwenye kuwa na njaa, mutu mwenye kujisikia kuwa pekee yake, na mutu mwenye kuwa mugonjwa, wanajikaza kumusaidia, lakini hawasahau hata kidogo kama kazi yao ya maana zaidi ni kuhubiria watu juu ya mwisho wa ulimwengu huu na juu ya wokovu. Mashahidi wa Yehova wanaendelea kuhubiri ujumbe huo na kutumikisha njia zenye Yesu na wanafunzi wake walitumikisha.

KAZI YA KUHUBIRI INAPASWA KUFIKA WAPI, NA INAPASWA KUENDELEA MUPAKA WAKATI GANI?

13. Kazi ya kuhubiri inapaswa kufika wapi?

13 Yesu alisema kama wanafunzi wake wangepaswa kuhubiri na kufundisha habari njema “katika dunia yote inayokaliwa.” Yesu aliwaagiza wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa “mataifa yote.” (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Ni kusema kama habari njema ingepaswa kuhubiriwa katika dunia yote.

14, 15. Ni nini inaonyesha kama Mashahidi wa Yehova wametimiza unabii juu ya mahali kwenye kazi ya kuhubiri inapaswa kufika? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

14 Ni Mashahidi wa Yehova tu ndio wametimiza unabii wa Yesu wenye ulionyesha kama habari njema inapaswa kuhubiriwa katika dunia yote. Sababu gani tunasema hivyo? Katika inchi ya Amerika, kuko viongozi wa dini karibu 600000 katika dini zenye kujiita kuwa za Kikristo, lakini kuko Mashahidi wa Yehova 1200000 hivi wenye kuhubiri habari njema katika inchi hiyo. Katika dunia yote, kuko mapadri Wakatoliki karibu 400000, lakini kuko Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni 8 wenye wanahubiri habari njema katika inchi 240. Kwa kweli, Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema katika dunia yote, na hilo linamuletea Yehova sifa na utukufu!—Zaburi 34:1; 51:15.

15 Sisi Mashahidi wa Yehova tuko na kusudi la kuhubiria watu wengi zaidi habari njema mbele mwisho ufike. Ili kufanya kazi hiyo, tumetafsiri na kuchapisha mamilioni ya vitabu, magazeti, trakte, na mialiko ya kuita watu kwenye mikusanyiko na Ukumbusho katika luga zaidi ya 700. Tunatolea watu vichapo hivyo bila kuwaomba feza. Mwaka jana tu, tulichapisha vichapo karibu milioni 4 na nusu vyenye kuzungumuzia Biblia. Pia, tulichapisha Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya zaidi ya milioni 200 katika luga zaidi ya 130. Na adresi yetu ya Internete iko na habari katika zaidi ya 750. Ni Mashahidi wa Yehova tu ndio wanafanya kazi hiyo kubwa yenye kushangaza.

16. Namna gani tunajua kama Mashahidi wa Yehova wako na roho ya Mungu?

16 Kazi ya kuhubiri itaendelea kufanywa mupaka wakati gani? Yesu alisema kama habari njema itahubiriwa mupaka mwisho ufike. Sisi Mashahidi wa Yehova, tumeweza kuendelea kuhubiri habari njema katika siku hizi za mwisho kwa sababu tuko na roho takatifu ya Yehova. (Matendo 1:8; 1 Petro 4:14) Watu wa dini fulani wanaweza kusema kama wako na roho takatifu. Lakini, wanaweza kufanya kazi yenye Mashahidi wa Yehova wanafanya katika siku hizi za mwisho? Watu wa dini fulani wamejaribu kuhubiri kama vile tunafanya, lakini wameshindwa. Wengine wanahubiri, lakini kwa wakati kidogo tu. Na wengine wanaweza kuhubiri nyumba kwa nyumba, lakini hawahubiri habari njema ya Ufalme. Kwa hiyo, hawafanye kazi yenye Yesu alianzisha.

NI NANI KABISA WANAHUBIRI HABARI NJEMA LEO?

17, 18. (a) Sababu gani tunaweza kuwa hakika kama Mashahidi wa Yehova ndio wanahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu leo? (b) Ni nini inatusaidia tuendelee kufanya kazi hiyo?

17 Sasa, ni nani wanahubiri habari njema ya Ufalme leo? Ni Mashahidi wa Yehova tu! Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu tunahubiri ujumbe wenye unastahili, ni kusema, habari njema ya Ufalme. Katika kazi yetu, tunatembelea watu, kwa hiyo tunatumikisha njia zenye kustahili. Tunachochewa na nia yenye kustahili, ni kusema, tunamupenda Yehova na tunapenda watu. Kazi yetu ya kuhubiri inafika mbali sana, kwa sababu tunahubiria watu wa mataifa yote na luga zote. Na tutaendelea kuhubiri habari njema ya Ufalme mupaka mwisho ufike!

18 Inashangaza kabisa kuona kazi kubwa sana yenye watu wa Yehova wanafanya ili kuhubiri habari njema katika siku hizi za mwisho. Lakini, ni nini inatusaidia kufanya kazi hiyo yote? Mutume Paulo alisema hivi: ‘Mungu ndiye ambaye, kwa ajili ya mapenzi yake mema, anatenda ndani yenu ili ninyi mukuwe na nia na kutenda.’ (Wafilipi 2:13) Yehova na aendelee kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tujikaze kuendelea kuhubiri habari njema!—2 Timotheo 4:5.