Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inaendelea Kubadilisha Maisha Yako?

Biblia Inaendelea Kubadilisha Maisha Yako?

‘Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu.’WAROMA 12:2.

NYIMBO: 61, 52

1-3. (a) Kisha kubatizwa, inaweza kuwa vigumu kwetu kufanya mabadiliko gani? (b) Wakati inakuwa vigumu kwetu kufanya maendeleo kuliko namna tuliwazia, ni maulizo gani tunaweza kujiuliza? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

KWA miaka mingi, Kevin alicheza michezo ya feza, alivuta tumbako, alikunywa pombe sana, na kutumia dawa za kulewesha. [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) Kisha, alijifunza juu ya Yehova na alipenda akuwe rafiki yake. Lakini, ili akuwe rafiki ya Yehova, alipaswa kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yake. Aliweza kufanya mabadiliko hayo kupitia musaada wa Yehova na nguvu za Neno lake, Biblia.—Waebrania 4:12.

2 Kisha kubatizwa, Kevin alipaswa kuendelea kubadilisha tabia yake ya zamani ili akuwe Mukristo mwenye sifa za muzuri. (Waefeso 4:31, 32) Kwa mufano, alikuwa anakasirika haraka. Alishangaa wakati alitambua namna ilikuwa vigumu kwake kujifunza kuzuia hasira yake. Kevin alisema kama kujifunza kuzuia tabia yake ya kukasirika ilikuwa vigumu sana kwake kuliko kuacha mambo ya mubaya yenye alikuwa anafanya mbele ya kubatizwa! Lakini aliweza kufanya mabadiliko kwa sababu aliendelea kumuomba Yehova amusaidie na kujifunza Biblia kwa uangalifu.

3 Mbele ya kubatizwa, wengi kati yetu walipaswa kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yao ili waishi kama vile Biblia inatuomba. Lakini hata leo, tunatambua kama tunapaswa kufanya mabadiliko madogo-madogo ili tuendelee kumuiga Mungu na Yesu. (Waefeso 5:1, 2; 1 Petro 2:21) Kwa mufano, tunaweza kutambua kama tunanungunika sana juu ya wengine ao mara nyingi tunafanya porojo na kusema wengine mubaya. Ao wakati fulani, tunaweza kuogopa sana kama wengine wanaweza kuwaza ao kusema kwamba hatufanye mambo ya muzuri. Pengine tumejikaza kwa miaka mingi ili kufanya mabadiliko lakini tunaendelea kufanya makosa yaleyale. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Sababu gani ni vigumu kwangu kufanya mabadiliko haya madogo-madogo? Ninapaswa kufanya nini ili nitumikishe mambo Biblia inasema na niendelee kuwa na sifa za muzuri?’

UNAWEZA KUMUFURAHISHA YEHOVA

4. Sababu gani hatuwezi kumufurahisha Mungu katika mambo yote yenye tunafanya?

4 Tunamupenda Yehova, na tunapenda kwa moyo wote kumufurahisha. Lakini jambo la kuhuzunisha ni hili: hatuwezi kumufurahisha wakati wote, kwa sababu hatukamilike. Mara nyingi, tunajisikia kama mutume Paulo. Alisema hivi: ‘Kwa maana nina uwezo wa kutaka, bali uwezo wa kufanya yaliyo mazuri haupo.’—Waroma 7:18; Yakobo 3:2.

5. Ni mabadiliko gani tulifanya mbele ya kubatizwa, lakini ni uzaifu gani wenye tunaweza kuendelea kupiganisha?

5 Mbele ya kubatizwa na kuwa katika kutaniko, tulipaswa kuacha kufanya mambo yenye Yehova anachukia. (1 Wakorintho 6:9, 10) Lakini hatujakuwa wakamilifu. (Wakolosai 3:9, 10) Kwa hiyo, tunaendelea kufanya makosa hata kama tumebatizwa kumepita miaka mingi. Mara nyingi, tunaweza kuwa na tamaa na mawazo ya mubaya, ao inaweza kuwa vigumu kwetu kuachana na uzaifu fulani wenye tuko nao. Kwa kweli, pengine tunapaswa kupiganisha uzaifu uleule kwa miaka mingi.

6, 7. (a) Ni nini inatusaidia tukuwe marafiki wa Yehova hata kama hatukamilike? (b) Sababu gani hatupaswe kujizuia kuomba Yehova musamaha?

6 Hata kama hatukamilike, tunaweza kufanya urafiki pamoja na Yehova na kumutumikia. Usisahau namna ulianzisha urafiki wako pamoja na Yehova. Yeye ndiye aliona mema katika moyo wako na alipenda umujue. (Yohana 6:44) Pia, alijua kama uko na makosa na uzaifu na kama utafanya makosa. Lakini, Yehova alipenda ukuwe rafiki yake.

7 Yehova alitupenda sana na kwa hiyo alitupatia zawadi ya maana zaidi. Alituma Mwana wake Yesu duniani ili atoe uzima wake kuwa zabihu ya ukombozi kwa ajili ya zambi zetu. (Yohana 3:16) Wakati tunafanya kosa fulani, tunaweza kumuomba Yehova atusamehe. Kupitia zabihu ya ukombozi, tunaweza kuwa hakika kama atatusamehe na kama tutaendelea kuwa marafiki wake. (Waroma 7:24, 25; 1 Yohana 2:1, 2) Kumbuka kama Yesu alikufa kwa ajili ya watenda-zambi wenye kutubu. Kwa hiyo, hata kama tunaona kuwa tulifanya jambo fulani la mubaya sana, tunapaswa kuendelea tu kumuomba Yehova atusamehe. Ikiwa hatumuombe musamaha, itakuwa kama vile tunakataa kunawa mikono yetu wakati inachafuka. Sisi ni wenye shukrani sana kwa Yehova kwa sababu ametusaidia tukuwe marafiki wake hata kama hatukamilike!—Soma 1 Timotheo 1:15.

Ikiwa tunapenda kumukaribia Yehova zaidi, tunapaswa kuendelea kujikaza kumuiga yeye na Mwana wake

8. Sababu gani hatupaswe kukataa uzaifu wetu?

8 Kwa kweli, hatuwezi kukataa uzaifu wetu ao kuutetea. Yehova ametuambia namna marafiki wake wanapaswa kuwa. (Zaburi 15:1-5) Kwa hiyo ikiwa tunapenda kumukaribia zaidi, tunapaswa kuendelea kujikaza kumuiga yeye na Mwana wake. Tunapaswa pia kujikaza kuzuia tamaa za mubaya zenye tuko nazo, na tunaweza hata kuachana nazo. Hata kama tumebatizwa kumepita miaka mingi ao hivi karibuni, tunapaswa kuendelea kuwa na sifa za muzuri.—2 Wakorintho 13:11.

9. Sababu gani tunasema kama tunaweza kuendelea kuvaa utu mupya?

9 Mutume Paulo aliandikia Wakristo hivi: ‘Munapaswa kuuondolea mbali utu wa zamani unaolingana na mwenendo wenu wa kwanza na ambao unaharibiwa kulingana na tamaa zake za udanganyifu. Bali kwamba munapaswa [kuendelea] kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili yenu, na munapaswa kuvaa utu mupya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu.’ (Waefeso 4:22-24) Maana yake tunapaswa kujikaza ili kufanya mabadiliko na ‘kuvaa utu mupya.’ Kwa hiyo, hata kama tumetumikia Yehova kwa miaka mingi ao hapana, tunaweza kuendelea kujifunza mengi juu ya sifa zake. Na Biblia inaweza kutusaidia tuendelee kufanya mabadiliko ili tuendelee kumuiga.

SABABU GANI NI VIGUMU SANA?

10. Tunapaswa kufanya nini ili Biblia itusaidie tuendelee kufanya mabadiliko, na tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

10 Sisi wote tunapenda kufuata mambo yenye Biblia inasema. Lakini tunapaswa kujikaza sana ikiwa tunapenda kuendelea kufanya mabadiliko. Sababu gani tunapaswa kujikaza? Sababu gani Yehova hatuwezeshe kufanya mambo ya muzuri bila kujikaza?

11-13. Sababu gani Yehova anatuomba tujikaze sana ili kupiganisha uzaifu wetu?

11 Wakati tunafikiri juu ya ulimwengu wote na mambo yote yenye kuwa ndani yake, tunaona kabisa kama Yehova ana nguvu ya kufanya kila kitu. Kwa mufano, aliumba jua lenye kuwa na nguvu nyingi sana. Kila segonde, jua linatoa mwangaza mwingi na joto nyingi sana, lakini ni sehemu kidogo tu ya nguvu hiyo ndiyo inawezesha uzima uendelee katika dunia. (Zaburi 74:16; Isaya 40:26) Pia, Yehova anapatia watumishi wake wenye kuwa duniani nguvu wakati wako nayo lazima. (Isaya 40:29) Kwa kweli, ikiwa Yehova angependa, angefanya ikuwe vyepesi sana kwetu kupiganisha uzaifu wetu na kuachana na tamaa za mubaya. Sasa, sababu gani hafanye hivyo?

12 Yehova ametupatia uhuru wa kuchagua. Anaacha sisi wenyewe tuchague ikiwa tutamutii ao hapana. Wakati tunachagua kumutii na kujikaza sana kufanya mapenzi yake, tunaonyesha kama tunamupenda na tunapenda kumufurahisha. Shetani anasema kama Yehova hana haki ya kutawala. Lakini wakati tunamutii Yehova, tunaonyesha kama tunapenda akuwe Mutawala wetu. Na tunaweza kuwa hakika kama Baba yetu mwenye upendo anapendezwa sana na nguvu yote yenye tunafanya ili kumutii. (Ayubu 2:3-5; Methali 27:11) Wakati tunajikaza sana kuachana na uzaifu wetu hata kama ni vigumu kufanya hivyo, tunashikamana na Yehova na kuonyesha kama tunapenda akuwe Mutawala wetu.

13 Yehova anatuambia kama tunapaswa kujikaza sana ili kuiga sifa zake. (Wakolosai 3:12; soma 2 Petro 1:5-7.) Anapenda pia tujikaze sana kuzuia mawazo yetu na namna tunajisikia katika moyo. (Waroma 8:5; 12:9) Kila wakati tunajikaza sana ili kufanya badiliko fulani na tunaweza kufanya hivyo, hilo linatuletea furaha kabisa.

ACHA NENO LA MUNGU LIENDELEE KUKUBADILISHA

14, 15. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa na sifa zenye kumupendeza Yehova? (Soma kisanduku “Biblia na Sala Vilibadilisha Maisha Yao.”)

14 Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa na sifa zenye kumupendeza Yehova? Kuliko tu kuamua sisi wenyewe mambo yenye tunapaswa kubadilisha, ni lazima tufuate muongozo wa Mungu. Andiko la Waroma 12:2 linasema hivi: ‘Muache kufanyizwa kulingana na mufumo huu wa mambo, bali [lakini] mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’ Kwa hiyo, ili kujua mambo Yehova anapenda, tunapaswa kutegemea musaada wenye ametupatia. Tunapaswa kusoma Biblia kila siku, kufikiri sana juu ya mambo tunasoma, na kumuomba Yehova roho takatifu yake. (Luka 11:13; Wagalatia 5:22, 23) Kama tunafanya hivyo, Yehova anaweza kutusaidia tuelewe mambo yenye kumupendeza, na tunaweza kuwa na mawazo kama yake. Kwa hiyo, mambo tunawaza, tunasema, na kufanya yatamufurahisha Yehova zaidi, na tutajifunza namna ya kuachana na uzaifu wetu. Lakini, hata kama tunafanya hivyo, tunapaswa kuendelea kupiganisha uzaifu huo.—Methali 4:23.

Weka pamoja habari zenye unapata katika vichapo vyetu ao maandiko fulani ya Biblia yenye kukusaidia kupiganisha uzaifu wako, na usome habari ao maandiko hayo mara kwa mara (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15 Zaidi ya kusoma Biblia kila siku, tunapaswa kujifunza Biblia kwa kutumia vichapo vyetu, kama vile Munara wa Mulinzi na Amuka! Habari nyingi katika magazeti hayo zinatufundisha namna tunaweza kuiga sifa za Yehova na namna ya kupiganisha uzaifu wetu. Tunaweza kupata habari fulani ao maandiko yenye yanaweza kutusaidia kabisa. Tunaweza kuweka pamoja maandiko ao habari hizo ili tuzisome mara kwa mara.

16. Sababu gani hatupaswe kuvunjika moyo ikiwa hatufanye mabadiliko haraka?

16 Inaomba wakati ili kujifunza kuiga sifa za Yehova. Kwa hiyo, ikiwa unaona kwamba haujafanya mabadiliko mengi yenye ungependa kufanya, usivunjike moyo. Mwanzoni, unaweza kujikaza sana ili kufanya mambo yenye Biblia inasema. Lakini, ikiwa unajikaza kuwaza na kutenda mambo Yehova anataka, haitakuwa vigumu kwako kuwa na mawazo kama yake na kufanya mambo ya muzuri.—Zaburi 37:31; Methali 23:12; Wagalatia 5:16, 17.

FIKIRIA WAKATI MUZURI SANA UNAOKUJA

17. Ikiwa tuko washikamanifu kwa Yehova, tunaweza kungojea kwa hamu wakati gani muzuri unaokuja?

17 Tunangojea kwa hamu wakati tutakuwa wakamilifu na kumutumikia Yehova milele. Wakati huo, hatutakuwa na lazima ya kupiganisha uzaifu wowote, na itakuwa vyepesi sana kwetu kumuiga Yehova. Lakini hata leo tuko na uwezo wa kumuabudu Yehova kwa sababu ametupatia zawadi ya zabihu ya ukombozi. Hata kama hatukamilike, tunaweza kumufurahisha ikiwa tunaendelea kujikaza sana ili kufanya mabadiliko na kufuata mambo yenye anatufundisha katika Biblia.

18, 19. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kama Biblia iko na nguvu ya kuendelea kubadilisha maisha yetu?

18 Kevin alifanya nguvu yake yote ili ajifunze kuzuia hasira yake. Alifikiri sana juu ya mambo yenye alisoma katika Biblia na alijikaza sana kufanya mabadiliko katika maisha yake. Alifuata pia mashauri yenye Wakristo wenzake walimupatia. Hata kama ilimuomba miaka fulani ili akuwe na sifa za muzuri, alifikia kuwa mutumishi wa huduma. Na amekuwa muzee katika kutaniko kwa miaka 20 yenye imepita. Lakini hata leo, anajua kuwa anapaswa kuendelea kupiganisha uzaifu wake.

19 Kama Kevin, tunaweza kuendelea kufanya mabadiliko katika maisha yetu. Ikiwa tunafanya hivyo, tutaendelea kumukaribia Yehova zaidi. (Zaburi 25:14) Na wakati tunafanya nguvu yetu yote kufanya mabadiliko hayo ili kumufurahisha, atatusaidia tuweze. Tunaweza kuwa hakika kama Biblia inaweza kutusaidia tuendelee kufanya mabadiliko katika maisha yetu.—Zaburi 34:8.

^ [1] (fungu la 1) Jina limebadilishwa.