Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tafuta Ufalme, Usitafute Vitu vya Kimwili

Tafuta Ufalme, Usitafute Vitu vya Kimwili

‘Mutafute Ufalme [wa Mungu] sikuzote, na mambo hayo mutaongezewa.’LUKA 12:31.

NYIMBO: 40, 98

1. Kuko tofauti gani kati ya vitu vyenye tuko navyo lazima na vitu vyenye tunapenda kuwa navyo?

KUKO vitu vidogo tu vyenye tuko navyo lazima ili tuendelee kuishi. Kwa mufano, tuko na lazima ya chakula, manguo, na nafasi ya kuishi. Lakini vitu vyenye tunapenda kuwa navyo ni vingi sana ao havina mwisho. Watu wengi hawatambue kama hawana lazima kabisa ya vitu vyote vyenye wanapenda kuwa navyo.

2. Watu wanapenda kuwa na vitu gani?

2 Mutu mwenye kuishi katika inchi masikini, anaweza kupenda kuwa na kitu fulani chenye kuwa tofauti kabisa na kile mutu mwenye kuishi katika inchi tajiri anaweza kupenda kuwa nacho. Katika maeneo fulani ya dunia, watu wanaweza kupenda kuwa na telefone, pikipiki (moto), ao sehemu kidogo ya udongo. Katika maeneo mengine, watu wanapenda kuwa na manguo mengi ya bei kali, nyumba kubwa, ao motokari ya bei kali. Iwe tunaishi wapi ao tuko na feza nyingi ao kidogo, tunaweza kuanza kupenda kuwa na vitu vingi sana vya kimwili vyenye hatuko navyo lazima ao vyenye hatuwezi kupata.

KUPENDA VITU VYA KIMWILI KUNAWEZA KUWA NA MATOKEO GANI JUU YETU?

3. Kupenda vitu vya kimwili, maana yake nini?

3 Kupenda vitu vya kimwili, maana yake nini? Ni tabia ya mutu ya kuhangaikia sana kupata vitu vingi kuliko kuhangaikia urafiki wake pamoja na Mungu. Hatosheke tu na vitu vya lazima vyenye iko navyo, lakini anaendelea kutafuta vingi zaidi. Hata wale wenye hawana feza nyingi ao wale wenye hawauze vitu vya bei kali wanaweza kupenda sana vitu vya kimwili. Wanaweza kuacha kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yao.—Waebrania 13:5.

4. Namna gani Shetani anatumia “tamaa ya macho”?

4 Shetani anapenda tuamini kama tunaweza kuwa na furaha katika maisha ikiwa tu tuko na vitu vingi vya kimwili. Kwa hiyo, anatumia ulimwengu wake na “tamaa ya macho” ili kujaribu kutufanya sikuzote tupende kuwa na vitu vingi vya kimwili. (1 Yohana 2:15-17; Mwanzo 3:6; Methali 27:20) Kila mara tunaona ao kusikia matangazo ya biashara yenye kutuchochea tuuze vitu vya mupya. Umekwisha kuuza kitu fulani kwa sababu tu kilionekana kuwa chenye kupendeza katika soko ao kwa sababu ulikiona kwenye matangazo ya biashara? Ikiwa ni hivyo, pengine kisha ulitambua kama haukukuwa kabisa na lazima ya kitu hicho. Wakati tunaendelea kuuza vitu vyenye hatuko navyo lazima, tunafanya maisha yetu yakuwe magumu. Vitu hivyo vinaweza kutukengeusha kumutumikia Yehova. Kwa mufano, tunaweza kukosa wakati wa kusoma Biblia, kutayarisha na kuenda kwenye mikutano, na hata kuhubiri kwa ukawaida. Usisahau onyo hili la mutume Yohana: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake.”

5. Ni nini inaweza kufikia wale wenye wanatumikisha nguvu zao zote ili kupata vitu vya kimwili?

5 Shetani anapenda tutumikishe nguvu zetu ili kupata feza nyingi na vitu vingi vya kimwili kuliko kuzitumikisha katika kazi ya Yehova. (Mathayo 6:24) Lakini, kama tunahangaikia tu kupata vitu vingi vya kimwili, maisha yetu hayatakuwa na maana. Tunaweza kuvunjika moyo na kuwa na magumu ya feza. Na jambo la mubaya zaidi, tunaweza kupoteza imani yetu katika Yehova na Ufalme wake. (1 Timotheo 6:9, 10; Ufunuo 3:17) Yesu alisema kama “tamaa za mambo yale mengine” ziko kama miiba yenye inaweza kuzuia mbegu kukomaa na kuzaa matunda.—Marko 4:14, 18, 19.

6. Mufano wa Baruku unatufundisha nini?

6 Fikiria kidogo mufano wa Baruku, mwandishi wa nabii Yeremia. Wakati Baruku alianza ‘kujitafutia mambo makubwa’, Yehova alimukumbusha kama hivi karibuni muji wa Yerusalemu ungeharibiwa. Lakini alimuahidi Baruku kama angeokoa uzima wake. (Yeremia 45:1-5) Baruku hangengojea kupata mambo mengi zaidi. Yehova hangeokoa vitu vya kimwili vyenye watu walikuwa navyo. (Yeremia 20:5) Leo, tunaishi siku za mwisho za ulimwengu wa Shetani. Kwa hiyo, huu si wakati wa kuendelea kujitafutia vitu vingi zaidi. Na hatupaswe kufikiri kama kisha ziki (taabu) kubwa, tutaendelea kuwa na vitu vyenye tuko navyo leo, hata kama ni vya maana sana kwetu.—Methali 11:4; Mathayo 24:21, 22; Luka 12:15.

Huu si wakati wa kuendelea kujitafutia vitu vingi zaidi

7. Tutazungumuzia nini katika habari hii, na sababu gani?

7 Sasa, namna gani tunaweza kutimiza mambo yetu ya lazima na ya watu wa familia yetu na kuendelea kukaza akili juu ya mambo ya maana zaidi? Namna gani tunaweza kuepuka kupenda vitu vya kimwili? Ni nini inaweza kutusaidia tuache kuhangaika sana juu ya vitu vyenye tuko navyo lazima? Katika Mahubiri yake ya Mulimani, Yesu alitutolea shauri la muzuri zaidi juu ya jambo hilo. (Mathayo 6:19-21) Tusome basi na kuzungumuzia Mathayo 6:25-34. Kufanya hivyo kutatuhakikishia kama tunapaswa kuendelea kutafuta Ufalme, lakini tusitafute vitu vya kimwili.—Luka 12:31.

YEHOVA ANATUPATIA VITU VYENYE TUKO NAVYO LAZIMA

8, 9. (a) Sababu gani hatupaswe kuhangaika sana juu ya mambo yenye tuko nayo lazima? (b) Yesu alijua nini juu ya wanadamu na mambo yenye wako nayo lazima?

8 Soma Mathayo 6:25. Yesu alijua kama wanafunzi wake walihangaika juu ya mambo kama vile kula, kunywa, na kuvaa, ndiyo sababu, katika Mahubiri yake ya Mulimani, aliwaambia hivi: ‘Muache kuhangaika juu ya nafsi zenu.’ Yesu alipenda kuwasaidia waelewe sababu gani hawakupaswa kuhangaika juu ya mambo yote hayo. Alijua kama ikiwa wanahangaika sana, hata juu ya vitu vyenye walikuwa navyo lazima kabisa, hilo lingewafanya wasahau mambo ya maana zaidi katika maisha. Yesu alihangaikia sana wanafunzi wake, kwa hiyo, katika mahubiri yake aliwaonya tena mara ine juu ya hatari hiyo.—Mathayo 6:27, 28, 31, 34.

9 Lakini, sababu gani Yesu anatushauria tusihangaike juu ya mambo kama vile kula, ao kunywa, ao kuvaa? Hatuna lazima ya chakula na manguo? Kwa kweli, tuko na lazima ya vitu hivyo! Na kama hatuna feza za kupata vitu hivyo, ni jambo la kawaida kuhangaika. Yesu alijua jambo hilo. Alijua mambo yenye watu walikuwa nayo lazima. Na alijua kama “katika siku za mwisho,” wanafunzi wake wangeishi katika nyakati za magumu sana. (2 Timotheo 3:1) Kwa kweli, leo watu wengi hawana kazi, na vitu vinaendelea kupanda bei sana. Katika maeneo mengi, watu ni masikini sana na wanapata chakula kidogo ao wanakosa chakula. Lakini pia, Yesu alijua kama uzima wa mutu ndio wa maana zaidi ya chakula na mwili zaidi ya manguo.

Yesu alisema kama uzima wa mutu ndio wa maana zaidi ya chakula na mwili zaidi ya manguo

10. Wakati Yesu alifundisha wanafunzi wake namna ya kusali, ni mambo gani yenye alisema yanapaswa kuwa ya maana zaidi katika maisha yao?

10 Mbele ya hapo, Yesu alikuwa amefundisha wanafunzi wake kama wakati wanasali, walipaswa kumuomba Baba yao wa mbinguni awapatie mambo yenye walikuwa nayo lazima. Walipaswa kusali hivi: ‘Utupe leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii.’ (Mathayo 6:11) Wakati mwingine, aliwaambia wasali hivi: ‘Utupe mukate wetu kwa ajili ya siku kulingana na mahitaji [mambo ya lazima] ya siku hiyo.’ (Luka 11:3) Lakini hilo halimaanishe kama tunapaswa kuendelea kukaza akili yetu juu ya namna ya kupata mambo yenye tuko nayo lazima. Kwa kweli, Yesu aliwaambia wanafunzi wake kama kusali ili Ufalme wa Mungu ukuje, ndilo jambo la maana zaidi kuliko kusali juu ya mambo yenye wako nayo lazima. (Mathayo 6:10; Luka 11:2) Ili kusaidia wanafunzi wake waache kuhangaika, Yesu aliwatuliza kwa kuwakumbusha namna Yehova anahangaikia viumbe wake wote.

11, 12. Namna Yehova anahangaikia ndege wa mbinguni, inatufundisha nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 Soma Mathayo 6:26. Tunapaswa ‘kuangalia kwa makini [uangalifu] ndege wa mbinguni.’ Ndege ni viumbe wadogo-wadogo, lakini wanakula chakula mingi. Kwa kweli, ikiwa ndege angekuwa na ukubwa sawa na wa mwanadamu, angekula chakula mingi kuliko mwanadamu. Ndege wanakula matunda, mbegu, vidudu, na vitu vingine. Lakini hawapande mbegu na kukomalisha chakula chenye watakula. Yehova anawapatia kila kitu chenye wako nacho lazima. (Zaburi 147:9) Kwa kweli, hatie chakula katika midomo yao! Lakini wanapaswa kuenda na kutafuta chakula kwenye wanaweza kukipata.

12 Yesu alikuwa hakika kama kwa sababu Baba yake anahangaikia ndege, atahangaikia pia watu. [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) (1 Petro 5:6, 7) Kwa kweli, kama vile ndege, hatupaswe kuwa wavivu. Tunapaswa kutumika ili kukomalisha chakula chetu ao kutafuta feza ili kuuza chakula. Yehova atabariki bidii yetu. Na hata kama hatuna feza ao chakula cha kutosha, anaweza kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima. Kwa mufano, wengine wanaweza kutusaidia. Pia, Yehova anapatia ndege nafasi ya kuishi. Amepatia ndege uwezo wa kujijengea nafasi ya kulala, na amefanya vitu vyenye wanaweza kutumia ili kujenga. Vilevile Yehova anaweza kutusaidia ili tupate nafasi yenye kufaa ya kuishi kwa ajili ya familia yetu.

13. Ni nini inaonyesha kama tuko wa maana sana kuliko ndege wa mbinguni?

13 Kisha Yesu kuwakumbusha wanafunzi wake kama Yehova anakulisha ndege, aliwauliza hivi: “Je, ninyi si bora [wa maana sana] kuliko wao?” (Linganisha na Luka 12:6, 7.) Wakati Yesu alisema maneno hayo, pengine alifikiria namna angetoa uzima wake kwa ajili ya wanadamu. Ndiyo, Yesu hakukufa kwa ajili ya ndege ao kwa ajili ya munyama mwengine yeyote. Alikufa kwa ajili yetu ili tuishi milele.—Mathayo 20:28.

14. Mutu mwenye kuhangaika hawezi kufanya nini hata kidogo?

14 Soma Mathayo 6:27. Yesu alipenda kusema nini wakati alisema kama hatuwezi kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye uzima wetu wakati tunahangaika? Alipenda kusema kama hatuwezi kurefusha uzima wetu hata kidogo wakati tunahangaika juu ya mambo yenye tuko nayo lazima. Kwa kweli, ikiwa tuko na mahangaiko mengi, tunaweza kupata magonjwa na hata kufa.

15, 16. (a) Namna Yehova anahangaikia mayungiyungi ya shambani, inatufundisha nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Ni maulizo gani tunapaswa kujiuliza, na sababu gani?

15 Soma Mathayo 6:28-30. Tunafurahi wakati tuko na nguo ya muzuri ya kuvaa, zaidi sana wakati tunaenda katika mahubiri ao kwenye mikutano na mikusanyiko yetu. Lakini, tunapaswa kuhangaika juu ya manguo? Tena, Yesu aliwakumbusha wanafunzi wake namna Yehova anahangaikia viumbe wake. Yesu alitumia mufano wa “mayungiyungi [maua] ya shamba.” “Mayungiyungi” hayo yanaweza kuwa maua kama vile muzambarausime, magugu-maji, mutakawa, na iris. Maua hayo yote hayajishonee manguo ya kuvaa. Lakini ni ya muzuri sana, ndiyo sababu Yesu alisema kama “hata Sulemani katika utukufu wake wote hakupambwa kama moja la haya”!

16 Fikiria mambo yenye Yesu alisema kisha hapo. Alisema hivi: ‘Ikiwa Mungu anavika [anavalisha] hivyo mimea ya shambani . . . , yeye hataona ni afazali [muzuri] zaidi awavike, ninyi wenye imani kidogo?’ Kwa kweli atafanya hivyo! Lakini wanafunzi wa Yesu walipaswa kuwa na imani zaidi. (Mathayo 8:26; 14:31; 16:8; 17:20) Walipaswa kuwa na tumaini kama Yehova anapenda kuwahangaikia na kama angefanya hivyo kabisa. Halafu sisi? Tunaamini kama Yehova atatuhangaikia?

Tunaamini kama Yehova atatuhangaikia?

17. Ni nini inaweza kuharibu urafiki wetu pamoja na Yehova?

17 Soma Mathayo 6:31, 32. Watu wengi wenye hawamujue Yehova wanakaza maisha yao juu ya feza na vitu vingi zaidi vya kimwili. Kama tunawaiga, tunaweza kuharibu urafiki wetu pamoja na Yehova. Tunajua kama Yehova ni Baba yetu na kama anatupenda. Na tuko hakika kama ikiwa tunafanya mambo yenye anatuomba na kutia Ufalme wake pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu, atatupatia mambo yote yenye tuko nayo lazima na hata zaidi. Pia, tunatambua kama urafiki wa muzuri pamoja na Yehova ndio wenye kutuletea furaha, na hilo linatusaidia kuwa wenye kutosheka ikiwa tuko na mambo ya lazima kama vile “chakula na kitu cha kujifunika.”—1 Timotheo 6:6-8.

UNATIA UFALME WA MUNGU PA NAFASI YA KWANZA KATIKA MAISHA YAKO?

18. Yehova anajua nini juu ya kila mumoja wetu, na atafanya nini kwa ajili yetu?

18 Soma Mathayo 6:33. Ikiwa tunatia Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu, Yehova atatupatia vitu vyote vyenye tuko navyo lazima. Yesu alieleza sababu gani tunapaswa kuamini kabisa ahadi hiyo. Alisema hivi: ‘Baba yenu wa mbinguni anajua munahitaji [muko na lazima ya] vitu hivi vyote.’ Yehova anajua mambo yenye uko nayo lazima hata mbele utambue jambo hilo. (Wafilipi 4:19) Anajua manguo yenye tutakuwa nayo lazima. Anajua tutakuwa na lazima ya chakula gani. Na anajua kama wewe na watu wa familia yako muko na lazima ya nafasi ya kuishi. Yehova atahakikisha kama umepata mambo yenye uko nayo lazima kabisa.

19. Sababu gani hatupaswe kuhangaika juu ya mambo yenye yanaweza kutokea wakati unaokuja?

19 Soma Mathayo 6:34. Tena, Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Musihangaike kamwe [hata kidogo].’ Yehova atatupatia vitu vyote vyenye tuko navyo lazima kila siku. Kwa hiyo, hatupaswe kuhangaika sana juu ya mambo yenye yatatufikia wakati unaokuja. Ikiwa tunafanya hivyo, tunaweza kuanza kujitumainia sisi wenyewe, na hilo linaweza kuharibu urafiki wetu pamoja na Yehova. Lakini, tunapaswa kumutegemea kabisa yeye.—Methali 3:5, 6; Wafilipi 4:6, 7.

TAFUTA KWANZA UFALME, NA YEHOVA ATAKUHANGAIKIA

Unaweza kufanya maisha yako yakuwe mepesi ili ukaze akili yako juu ya Ufalme? (Picha hii inapatana na fungu la 20)

20. (a) Unaweza kujiwekea muradi gani katika kazi ya Yehova? (b) Unaweza kufanya nini ili maisha yako yakuwe mepesi?

20 Litakuwa jambo lenye kuhuzunisha sana ikiwa tunakosa nguvu za kumutumikia Yehova kabisa kwa sababu tunajikaza kupata vitu vingi sana vya kimwili! Kuliko kufanya hivyo, tunapaswa kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote. Kwa mufano, unaweza kuhamia katika kutaniko lenye kuwa na lazima ya wahubiri zaidi? Unaweza kuwa painia? Ao ikiwa tayari uko painia, umefikiria kusoma Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme? Unaweza pengine kupitisha siku fulani katika juma ili kusaidia kwenye Beteli ao kwenye biro ya kutafsiri? Ao pengine unaweza kuwa Mujenzi Mwenye Kujitolea wa Mahali na kutumia sehemu ya wakati wako ili kusaidia kujenga Majumba ya Ufalme. Fikiria mambo yenye unaweza kufanya ili maisha yako yakuwe mepesi na ukuwe na wakati mwingi na nguvu nyingi za kutumia katika kazi za Ufalme. Kisanduku “ Namna ya Kufanya Maisha Yako Kuwa Mepesi” kinatoa mashauri fulani. Umuombe Yehova akusaidie ujue mambo yenye unapaswa kufanya. Kisha uanze kufanya mabadiliko yenye kufaa.

21. Ni nini itakusaidia umukaribie sana Yehova?

21 Yesu alitufundisha kama tunapaswa kutafuta Ufalme kwanza. Wakati tunafanya hivyo, tunaepuka kuhangaika sana juu ya mambo yenye tuko nayo lazima. Tunamukaribia Yehova zaidi kwa sababu tunatumaini kama atatuhangaikia. Tunajifunza kujizuia na hatuuze kila kitu chenye tunapenda ao kila kitu chenye ulimwengu unatutolea, hata kama tuko na uwezo wa kukiuza. Ikiwa tunafanya maisha yetu kuwa mepesi leo, itakuwa vyepesi kwetu kubakia waaminifu kwa Yehova na ‘kuushika imara uzima ulio wa kweli’ wenye ametuahidi.—1 Timotheo 6:19.

^ [1] (fungu la 12) Wakati mwingine, watumishi fulani wa Yehova wanakosa chakula cha kutosha. Ili kuelewa sababu gani Yehova anaweza kuacha hali hiyo ifike, soma “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika gazeti la kawaida la Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi 9, 2014, ukurasa wa 22.