Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Kazi Yangu ya Mauaji na Kupenda Makuta Kuliniletea Maumivu Mingi”

“Kazi Yangu ya Mauaji na Kupenda Makuta Kuliniletea Maumivu Mingi”
  • Alizaliwa Mwaka wa: 1974

  • Inchi: Albania

  • Alikuwa: Mwizi, muuzishaji wa dawa za kulewesha, na mufungwa

MAISHA YANGU YA ZAMANI

 Nilizaliwa mu familia maskini katika Tirani, muji mukubwa wa inchi ya Albania. Baba yangu alikuwa mutu muzuri mwenye alitumika sana juu ya kutuhangaikia. Lakini hatukukuwa kabisa na makuta mingi juu ya kuishi. Wakati nilikuwa mutoto, nilihuzunika kuona vile tulikuwa maskini. Karibu maisha yangu yote ya utoto, sikukuwa na viatu na kila mara sikukuwa na chakula ya kutosha.

 Nilianza kuiba wakati nilikuwa mutoto sana. Niliwaza tu kama nilikuwa nasaidia familia yetu. Lakini, kisha wakati fulani polisi ikanikamata. Mu mwaka wa 1988, wakati nilikuwa na miaka 14, baba yangu alinituma ku masomo ya kunisaidia nibadilishe tabia yangu. Nilipitisha miaka mbili mule na nikajifunza kuwa soudeur. Wakati nilitoka mule sikupenda tena kuishi maisha yenye nilikuwa nayo, lakini, sikukuwa napata kazi. Ilikuwa nguvu sana mu ile wakati mu Albania kupata kazi juu kulikuwa fujo mu mambo ya politike. Nilivunjika moyo, na nikaanza kupitisha wakati pamoya na wale marafiki wangu wa zamani na nikaanza tena kuiba. Kisha, miye na marafiki wangu tulifungwa na wakatutia mu gereza kwa miaka tatu.

 Kisha kutoka mu gereza, niliendelea na kazi yangu ya mauaji. Hali ya uchumi ya Albania haikukuwa tena muzuri, na kulikuwa muvurugo mu inchi yote. Mu zile kipindi, nilipata makuta mingi sana lakini mu njia ya mubaya. Kisha kuenda kuiba tukiwa na bunduki, marafiki wangu wawili walikamatwa, kisha miye nilikimbia mu inchi ingine juu wasinitie mu gereza. Ile wakati, nilikuwa nilishafunga ndoa na Julinda, na tulikuwa na mutoto mwanaume.

 Kisha tukafika Uingereza. Nilikuwa nilishapanga kuanza maisha ya mupya pamoya na bibi yangu na mutoto wetu mwanaume, lakini ilikuwa nguvu kubadilisha tabia zangu za zamani. Nilirudilia tena maisha yangu ya mubaya, lakini mara hiyo, nilianza sasa kuuzisha dawa za kulewesha, na nilikuwa napata makuta mingi sana.

 Julinda alijisikia namna gani kuhusu kazi yangu ya kuuzisha dawa za kulewesha? Muache yeye mwenyewe awaelezee: “Wakati nilikuwa nakomala mu Albania, nilikuwa nawaza namna ya kutoka mu umaskini. Nilikuwa tayari kufanya kila kitu juu tu tukuwe na maisha ya muzuri. Niliwaza kama kuwa na makuta kungefanya tukuwe na maisha ya muzuri, njo maana nilimutegemeza Artan mu bongo yake, mu bwizi, na mu kazi yake ya kuuzisha dawa za kulewesha, ni kusema, nilikuwa tayari kufanya kila kitu juu tu ya kupata makuta.”

“Nilimuungaka Artan mukono kwa uongo wake, wizi, na kuuzisha dawa za kulewesha.”—Julinda

 Mu 2002, maisha yetu ilibadilika na mipango yote yenye tulikuwa nayo juu ya makuta yetu na ndoto zenye tulikuwa nazo, yote ikasimamia pale. Balinikamata na niko na muzigo mukubwa sana wa dawa za kulewesha na nilifungwa tena.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

 Biblia ilianzaka kubadilisha maisha yangu mbele hata nitambue ile jambo. Mbele ya pale, mu 2000, Julinda alikutanaka na bibi na bwana Mashahidi wa Yehova na kuanza kujifunza Biblia pamoya nao. Sikukuwaka napenda kuzungumuza juu ya Biblia juu niliwaza kama ilikuwa inachokesha. Lakini Julinda alipenda sana. Anasema hivi: “Nilizaliwa mu familia ya watu wenye kupenda mambo ya dini, na nilipenda na kuheshimia Biblia. Kila wakati nilipenda kujua mambo yenye Biblia inafundisha, na nilifurahia sana kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi. Mafundisho mingi ya Biblia ilinipatia tumaini kabisa. Mambo yenye nilijifunza ilinisaidia kufanya mabadiliko fulani mu maisha yangu. Lakini, niliendelea tu kuwaza kama makuta ingetuletea furaha, mupaka wakati walimukamata Artan, njo nilifikia kubadilisha mawazo yangu. Bila kukawia, nilitambua kama mambo yenye Biblia inasema juu ya makuta ni ya kweli. Tulikuwa tunaitafuta kwa nguvu yetu yote, lakini haikufanya tukuwe na furaha. Kisha, nilielewa kama nilikuwa kabisa na lazima ya kufuata kanuni za Mungu.”

 Mu mwaka wa 2004, niliachiliwa huru kutoka mu gereza, na bila kukawia nilirudilia tena kazi ya kuuzisha dawa za kulewesha. Hata vile, mawazo ya Julinda ilibadilika, na jambo yenye alisemaka ilinifanya niwaze sana. Alisemaka hivi: “Sipende makuta yako tena. Napenda bwana yangu arudie, na napenda baba ya watoto wangu akuwe hapa juu ya kuwahangaikia.” Wakati nilisikia vile, roho yangu ililuma sana, lakini alikuwa na haki ya kusema vile. Niliishi mbali na familia yangu kwa miaka mingi. Nilifikiria pia juu ya maumivu mingi ya moyo yenye nilipataka juu tu ya kutafuta makuta mu njia ya mubaya. Kwa hiyo, niliamua kubadilisha njia yangu na kuachana na marafiki wangu wa zamani.

 Jambo yenye ilinigusa sana ni wakati tuliendaka miye, bibi yangu na watoto wetu wawili ku mukutano wa Mashahidi wa Yehova. Nilifurahiaka kuona watu waaminifu na wenye kufanya urafiki. Kisha, nikaanza kujifunza Biblia.

Nilikuwaka nawaza kama ikiwa tuko na makuta mingi, tungepata furaha

 Nilijifunzaka mu Biblia kama “kupenda feza ni chanzo cha mambo ya mubaya ya namna zote, na kwa kujikaza kufikia upendo huo, watu wengine . . . wamejitoboa wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” (1 Timoteo 6:9, 10) Nilielewa muzuri kweli ya hii andiko! Nilihuzunika sana juu ya makosa ya maisha yangu ya zamani na namna iliniumiza na kuumiza pia familia yangu. (Wagalatia 6:7) Wakati nilijifunza juu ya upendo wenye Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo, wako nayo juu yetu nilianza kubadilisha utu wangu wa zamani. Na nilianza kuwazia wengine zaidi kuliko kujiwazia miye peke, na zaidi sana kupitisha wakati mingi pamoya na familia yangu.

FAIDA YENYE NIMEPATA

 Nimepata faida kwa kufuata hii shauri ya Biblia: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.” (Waebrania 13:5) Sasa niko na amani ya akili na zamiri safi. Ile, imenipatia furaha yenye siyapataka. Ndoa yangu inakuwa nguvu zaidi na familia yangu inakuwa na umoja.

 Nilikuwaka nawaza kama ikiwa tuko na makuta mingi, tungepata furaha. Sasa najionea namna mauaji na kupenda makuta kuliniletea maumivu mingi. Siye hatuko matajiri, lakini ninajisikia kama tumepata jambo fulani yenye ni ya maana zaidi mu maisha yetu, ni kusema, kuwa rafiki wa Yehova Mungu. Kumuabudu Mungu kwa umoja tukiwa familia kunatufanya tukuwe na furaha ya kweli.

Pamoya na familia yangu ku mukusanyiko wa eneo wa Mashahidi wa Yehova