Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUENDELEE KUKESHA!

Mamilioni ya Watu Wanakimbia Ukraine

Mamilioni ya Watu Wanakimbia Ukraine

 Tarehe 24, Mwezi wa 2, 2022, maaskari wa Urusi walianza kushambulia Ukraine. Ile ilifanya mamilioni ya watu wakuwe mu hatari, na waanze kukimbia maeneo ya vita. a

 “Kulikuwa mabombe na milipuko mingi. Ni nguvu kufasiria ile hali juu ilikuwa ya kuogopesha sana. Wakati tulisikia kuko treni za kupeleka watu fasi kwenye kuko usalama, tuliamua kuondoka. Tulilazimika kuacha kila kitu juu kila mutu angeweza tu kubeba sakoshe moya ya kidogo. Tuliweza tu kubeba dokima zetu, dawa, maji, na chakula kidogo. Tuliacha vitu vingine vyote na tukaenda fasi ya kuchungia treni wakati bombe zilikuwa nalia.”​—Nataliia, wa Kharkiv, Ukraine.

 “Kufikia dakika ya mwisho, hatukuwazia kama vita itatokea. Nilisikia mulio wa bunduki mu sehemu fulani za muji, na madirisha ilikuwa natingizika. Kwa hiyo, niliamua kuondoka na nikabeba vitu vya lazima kabisa. Nilitoka ku nyumba na saa mbili ya asubui, na nikakamata treni ya kuenda Lviv na kisha nikapanda bisi ya kuenda Pologne.”​—Nadija, wa Kharkiv, Ukraine.

Mu hii habari, utapata majibu ya hii maulizo:

 Juu ya nini mamilioni ya watu walikimbia Ukraine?

 Hata kama mamilioni ya watu walikimbia Ukraine juu maaskari wa Urusi walishambulia Ukraine, Biblia inaonyesha sababu kubwa zenye zinafanya ile hali itokee:

  •   Serikali za wanadamu zimeshindwa kupatia wanadamu mambo yenye wako nayo lazima. Mara mingi wenye mamlaka wanaitumiaka juu ya kutesa watu.​—Muhubiri 4:1; 8:9.

  •   Shetani Ibilisi, “mutawala wa ulimwengu,” anachochea watu watende mubaya. Njo maana Biblia inasema: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.”​—Yohana 14:30; 1 Yohana 5:19.

  •   Zaidi ya magumu yenye wanadamu wamekuwa nayo kwa miaka mingi, kwa sasa tunaishi mu kipindi yenye Biblia ilizungumuziaka kwa kusema hivi: “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Timoteo 3:1) Mu ile kipindi mulipaswa kuwa vita, misiba ya asili, njala, na magonjwa ya kuambukiza, mambo yenye inafanya watu wakimbie.​—Luka 21:10, 11.

 Wapi njo wakimbizi wanaweza kupata tumaini?

 Biblia inaonyesha kama Muumbaji wetu, Yehova, b ni Mungu mwenye anapenda na kusikilia huruma wakimbizi. (Kumbukumbu la Torati 10:18) Anaahidi kama atatosha magumu ya wakimbizi kupitia serikali yake ya mbinguni. Ile serikali inaitwa Ufalme wa Mungu na itakamata nafasi ya serikali zote za wanadamu. (Danieli 2:44; Matayo 6:10) Yehova atatumia Ufalme wake juu ya kuharibu Shetani Ibilisi. (Waroma 16:20) Ufalme wake utatawala dunia yote. Utatosha migawanyiko yenye imeletwa na mipaka ya kila inchi. Watu wote mu dunia watakuwa familia yenye umoja. Hakuna mutu mwenye atalazimika kuwa mukimbizi. Biblia inaahidi: “Watakaa, kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini, na hakuna mutu mwenye atawaogopesha, kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema.”​—Mika 4:4.

 Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kumaliza kabisa magumu yenye wakimbizi wako napata leo. Yehova atatumia Ufalme wake ili kumaliza magumu yenye inalazimisha watu kukimbia inchi yao. Kwa mufano:

 Biblia inaweza kusaidia wakimbizi leo?

 Ndiyo. Kwanza, Biblia inapatia wakimbizi tumaini. Kisha, inaweza kuwasaidia kupambana na magumu yenye wako nakutana nayo leo.

 Kanuni ya Biblia: “Mujinga anaamini kila neno, lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.”​—Mezali 14:15.

 Maana: Fikiria mbele ya wakati hatari zenye zinaweza kukupata na uone namna unaweza kujilinda. Kwa kawaida wakimbizi wanakuwaka na wasiwasi na hawajue muzuri fasi kwenye wako. Kwa hiyo, ufanye angalisho na watu wenye wanatafutaka kutendea mubaya wakimbizi.

 Kanuni ya Biblia: “Kama tuko na chakula na nguo, tutatosheka na vitu hivyo.”​—1 Timoteo 6:8.

 Maana: Uepuke kukaza akili juu ya vitu vya kimwili. Kama unatosheka na mambo ya lazima, utakuwa na furaha zaidi.

 Kanuni ya Biblia: “Kwa hiyo, mambo yote yenye munataka watu wawatendee, ninyi pia lazima muwatendee wao.”​—Matayo 7:12.

 Maana: Ukuwe muvumilivu na utendee wengine mambo ya muzuri. Kama unafanya vile, majirani wako wapya watakuheshimia na watafurahia kuishi na weye.

 Kanuni ya Biblia: “Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu.”​—Waroma 12:17.

 Maana: Kama mutu anakutendea mubaya, usiache kasirani ikusukume kumutendea vile alikutendea. Ile haitasaidia kitu.

 Kanuni ya Biblia: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”​—Wafilipi 4:13.

 Maana: Umutie Mungu pa nafasi ya kwanza mu maisha yako na usali kwake. Atakupatia nguvu.

 Kanuni ya Biblia: “Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.”​—Wafilipi 4:6, 7.

 Maana: Umuombe Mungu akupatie amani ya akili na ya moyo mu hali yoyote yenye unaweza kujikuta ndani. Ona habari “Wafilipi 4:6, 7​—‘Msihangaike Kuhusiana na Jambo Lolote.’”

a Siku moya kisha Urusi kuanza kushambulia Ukraine, shirika ya umoja wa mataifa yenye kuhangaikia wakimbizi (UNHCR) ilisema kama ile hali iko hatari sana kwa watu. Mu siku 12 tu, zaidi ya watu milioni mbili walitoka Ukraine na kukimbilia mu inchi za karibu-karibu, na wengine watu milioni moya walikimbilia mu maeneo ingine ya Ukraine.

b Yehova njo jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Ona habari “Yehova Ni Nani?