Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Comstock Images/Stockbyte via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Utachagua Nani ili Akuwe Kiongozi?​—Biblia Inasema Nini?

Utachagua Nani ili Akuwe Kiongozi?​—Biblia Inasema Nini?

 Mu majuma kidogo yenye iko nakuya, kutakuwa uchaguzi mu inchi mbalimbali mu dunia yote. Watu wako nafikiria kwa uzito ni nani mwenye watachagua ili akuwe kiongozi.

 Biblia inasema nini?

Wanadamu wenye wako naongoza wako na mipaka

 Biblia inaonyesha kama wanadamu wote wenye wako naongoza wako na mipaka.

  •   “Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu. Roho yake inatoka, anarudia kwenye udongo; siku ileile mawazo yake yanapotea.”​—Zaburi 146:3, 4, maelezo ya chini.

 Hata viongozi wenye wanaonekana kuwa na uwezo sana, ku mwisho watafikia tu kufa. Zaidi ya ile, hakuna jambo yenye wanaweza kufanya ili kuhakikisha kama wale wenye wataongoza kisha wao wataendeleza mambo ya muzuri yenye wako nafanya.​—Muhubiri 2:18, 19.

 Kusema kweli, Biblia inaonyesha wazi kama wakati Mungu aliumba wanadamu hakupanga hata kidogo wakuwe najiongoza wao wenyewe.

  •   “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

 Kuko mutu mwenye anaweza kuongoza muzuri leo?

Kiongozi mwenye Mungu anakubali

 Biblia inaonyesha kama Mungu ameweka kiongozi mwenye kuwa na uwezo sana na mwenye kutumainika. Ule kiongozi ni Yesu Kristo. (Zaburi 2:6) Yesu njo Mufalme wa Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali yenye kuwa mbinguni.​—Matayo 6:10.

 Utachagua Yesu ili akuwe kiongozi wako? Biblia inaonyesha juu ya nini ile ulizo ni ya maana.

  •   “Mumuheshimie mwana [Yesu Kristo], kama hamufanye vile Mungu atakasirika sana na ninyi mutaangamia kutoka katika njia, kwa maana kasirani Yake inawaka haraka. Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.”​—Zaburi 2:12.

 Sasa njo wakati ya kuamua ni nani utachagua. Unabii wa Biblia unaonyesha kama Yesu alianza kutawala mu mwaka wa 1914 na kama hivi karibuni Ufalme wa Mungu utaanza kutawala pa nafasi ya serikali zote za wanadamu.​—Danieli 2:44.

 Ili ujifunze mambo mingi zaidi juu ya namna unaweza kutegemeza uongozi wa Yesu, soma habari “Chagua Kuunga Mukono Ufalme wa Mungu Leo!