Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

E+/taseffski/via Getty Images (Stock photo. Posed by model.)

MUENDELEE KUKESHA!

Hesabu ya Vijana Wenye Kuwa na Matatizo ya Akili Inaongezeka​—Biblia Inasema Nini?

Hesabu ya Vijana Wenye Kuwa na Matatizo ya Akili Inaongezeka​—Biblia Inasema Nini?

 Siku ya Kwanza, tarehe 13 Mwezi wa 2, 2023, Kituo ya mu Amerika yenye inashugulikiaka magonjwa ya kuambukiza (CDC) ilitoa ripoti kuhusu matatizo ya akili ya vijana wa mu Amerika. Ile ripoti ilionyesha kama zaidi ya asilimia 40 (40%) ya wanafunzi wa masomo ya segondere walikuwa na huzuni na walikosa tumaini kwa wakati murefu.

 Dr. Kathleen Ethier, musimamizi wa idara ya CDC yenye inashugulikiaka vijana na afya ku masomo (DASH) alisema hivi: “Kwa zaidi ya miaka 10 yenye ilipita, tulijionea vile hali ya vijana wenye kuwa na matatizo ya akili iliendelea kuwa mubaya. Lakini, ile hali inaendelea kuwa mubaya hata zaidi kwa vijana wanamuke, na wengi kati yao wako nawaza kujiua na wengine wako hata najiua.”

 Ile ripoti ilisema hivi:

  •   Kijana 1 mwanamuke ao zaidi kati ya 10 (14%) alikazwa kufanya ngono. Dr. Ethier anasema hivi: “Ile ni jambo ya kuogopesha sana. Kati ya vijana wanamuke 10 wenye unajua, pengine moya ao zaidi alishakalalwa kinguvu.”

  •   Karibu kijana 1 mwanamuke kati ya 3 (30%) alifikiria sana kujiua.

  •   Karibu vijana 3 wanamuke kati ya 5 (57%) wako na huzuni ao wanakosa tumaini kwa wakati murefu.

 Zile ripoti ni za kuhuzunisha sana juu, kwa kawaida, wakati wa ujana ni kipindi yenye mutu anapaswa kuwa na furaha. Nini njo inaweza kusaidia vijana wapambane na mahangaiko yenye wako napata leo? Biblia inasema nini?

Biblia njo inaweza kusaidia vijana

 Biblia inaonyesha waziwazi kama leo tuko naishi wakati wa nguvu. Na inaiita “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Timoteo 3:1-5) Hata vile, mu Biblia muko mashauri yenye iko nasaidia mamilioni ya vijana mu dunia yote wavumilie magumu yenye wako napambana nayo. Fikiria habari zenye kufuata zenye kutegemea Biblia.

 Musaada kwa vijana wenye wako nawaza kujiua

 Musaada kwa vijana wenye kushuka moyo, wenye kuwa na huzuni, ao wenye kuwa na mawazo yenye haifae

 Musaada kwa vijana wenye kuonewa

 Musaada kwa vijana wenye wanakazwa kufanya ngono

Biblia inapatia wazazi mashauri ya muzuri

 Biblia iko pia na mashauri ya muzuri yenye wazazi wanaweza kutumia ili kusaidia vijana wao wavumilie magumu ya maisha. Fikiria habari zenye kufuata zenye kutegemea Biblia.