Ona video zinazopatikana

Je, Mashahidi wa Yehova Wanavumilia Dini Zingine?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanavumilia Dini Zingine?

 Tunatii shauri la Biblia la ‘kuwaheshimu watu wa namna zote’ hata wawe wa dini gani. (1 Petro 2:17) Kwa mufano, katika inchi fulani kuna Mashahidi wa Yehova wengi sana. Hata hivyo, hatuwachochee wakubwa wa serikali ao wale wanaotunga sheria wakataze dini zingine ao kuzitilia vizuizi. Wala hatufanye kampanye ili serikali itunge sheria za kuwalazimisha watu kufuata kanuni zetu na mambo tunayoamini. Lakini, tunawavumilia wengine namna tunavyotaka wao pia watuvumilie.—Mathayo 7:12.