Hamia kwenye habari

Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, Ibilisi ni kiumbe halisi. Yeye ni “mtawala wa ulimwengu,” kiumbe wa roho aliyegeuka kuwa mwovu na kumwasi Mungu. (Yohana 14:30; Waefeso 6:11, 12) Biblia inafunua utu au tabia ya Ibilisi kupitia majina yake yafuatayo:

Si uovu tu au tabia fulani ya uovu

 Wengine wana maoni kwamba Shetani Ibilisi ni uovu tu au tabia fulani ya uovu iliyo ndani yetu. Hata hivyo, Biblia inasimulia mazungumzo kati ya Mungu na Shetani. Kwa kuwa Mungu ni mkamilifu, ni jambo lisilowezekana kwamba alizungumza na sehemu fulani ovu iliyo ndani yake. (Kumbukumbu la Torati 32:4; Ayubu 2:1-6) Pia, Shetani alimshawishi Yesu asiye na dhambi. (Mathayo 4:8-10; 1 Yohana 3:5) Kwa hiyo, Biblia inaonyesha kwamba Ibilisi ni kiumbe halisi wala si sifa ya uovu tu.

 Je, tushangae kwa kuwa watu wengi hawaamini kwamba Ibilisi ni kiumbe halisi? Bila shaka la, kwa kuwa Biblia inasema kwamba Shetani hutumia udanganyifu ili kutimiza malengo yake. (2 Wathesalonike 2:9, 10) Mojawapo ya mbinu zake kuu ni kuwapofusha watu wengi waamini kwamba hayupo.—2 Wakorintho 4:4.

Maoni mengine yenye makosa kuhusu Ibilisi

  Uwongo: Jina lingine la Ibilisi ni Lusifero.

 Ukweli: Neno la Kiebrania linalotafsiriwa katika baadhi ya Biblia kuwa “Lusifero” linamaanisha “mwenye kung’aa.” (Isaya 14:12) Muktadha unaonyesha kwamba usemi huo unarejelea utawala, au wafalme wa Babiloni, ambao Mungu angewaibisha kwa sababu ya kiburi chao. (Isaya 14:4, 13-20) Usemi “mwenye kung’aa” ulitumiwa kudhihaki Babiloni baada ya ufalme wao kupinduliwa.

  Uwongo: Shetani anatumiwa na Mungu akiwa “kiongozi wa mashtaka.”

 Ukweli: Ibilisi ni adui wala si mtumishi wa Mungu. Shetani Ibilisi anawapinga na kuwashtaki kwa uwongo watu wanaomtumikia Mungu.​—1 Petro 5:8; Ufunuo 12:10.