Hamia kwenye habari

Kitabu cha Ufunuo​—Kinamaanisha Nini?

Kitabu cha Ufunuo​—Kinamaanisha Nini?

Jibu la Biblia

 Neno A·po·kaʹly·psis (apokalipsi) ni neno la Kigiriki la kitabu cha Ufunuo ambalo linamaanisha “Kufunua” au “Kufichua.” Neno hilo linatusaidia kuelewa maana ya kitabu cha Ufunuo kwamba kinafichua mambo ambayo yalikuwa yamefichwa na kinafunua matukio yatakayotendeka muda mrefu baada ya kuandikwa. Unabii mwingi ulioandikwa katika kitabu cha Ufunuo bado haujatimizwa.

Muhtasari wa kitabu cha Ufunuo

Mambo yanayoweza kutusaidia kuelewa kitabu cha Ufunuo

  1.   Kitabu cha Ufunuo kina ujumbe wenye kutia moyo na ujumbe huo hauwaogopeshi wale wanaomtii Mungu. Ingawa watu wengi hulihusianisha neno “apokalipsi” na msiba mkubwa, kitabu cha Ufunuo kinaanza kwa kusema kwamba wale wanaosoma, wanaoelewa na kutenda kupatana na mambo yaliyoandikwa humo watakuwa na furaha wanapofanya hivyo.​—Ufunuo 1:3; 22:7.

  2.   Kitabu cha Ufunuo kinatumia “ishara” nyingi au mifano.​—Ufunuo 1:1.

  3.   Majina ya cheo au sifa zinazowakilisha watu au vitu vinavyotajwa katika kitabu cha Ufunuo zinapatikana katika sehemu nyingine za Biblia:

  4.   Maono hayo yanahusu “Siku ya Bwana” ambayo ilianza mwaka wa 1914 Mungu alipomweka Yesu rasmi kuwa Mfalme wa Ufalme wake. (Ufunuo 1:​10) Kwa hiyo basi utimizo mkubwa wa unabii wa kitabu cha Ufunuo unahusu wakati wetu.

  5.   Ili tukielewe kitabu cha Ufunuo tunahitaji mambo yaleyale yanayohitajika tunaposoma sehemu nyinginezo za Biblia, yaani, hekima kutoka kwa Mungu na mwongozo kutoka kwa wale ambao tayari wanakielewa.​—Matendo 8:​26-​39; Yakobo 1:5.