Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ninaonekana Namna Gani?

Ninaonekana Namna Gani?

 Juu ya nini tunapaswa kuhangaikia namna yetu ya kuvala? Juu namna yetu ya kuvala inaonyesha kama tuko watu wa namna gani. Manguo yako inafanya watu wakuwe na mawazo gani juu yako?

 Makosa tatu kuhusu namna ya kuvala na namna unaweza kuiepuka

Kosa ya #1: Kuacha vyombo vya habari vichochee namna yako ya kuvala.

 Kijana fulani mwenye kuitwa Theresa anasema hivi: “Wakati fulani, ninafurahiaka namna fulani ya kuvala juu vyombo vya habari vimeizungumuzia sana. Wakati akili yako inayala picha za watu wenye wanavala nguo fulani, ni mwepesi kupenda kuwa nayo.”

 Haiko vijana wanamuke tu njo wanachochewa na matangazo ya vyombo vya habari. Kitabu The Everything Guide to Raising Adolescent Boys inasema hivi: “Vijana wanaume pia wanavutiwaka na namna mupya za kuvala. Hata wakati wangali wadogo, wafanyabiashara wanajaribu kuwavutia.”

 Jambo ya muzuri ya kufanya: Biblia inasema hivi: “Mujinga anaamini kila neno, lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.” (Mezali 14:15) Kulingana na ile kanuni ya Biblia, usikuwe haraka kufuata mambo yote yenye unaona mu matangazo ya biashara. Kwa mufano, kama matangazo ya biashara inasema kama nguo fulani “inavutia sana” ao iko “sexy,” ujiulize hivi:

  •  ‘Nani njo atapata faida kama ninauza ile nguo?’

  •  ‘Itafanya nionekane kuwa mutu wa namna gani?’

  •  ‘Inapatana na vile niko kabisa, na inapatana na kanuni zenye ninaheshimia?’

 Shauri: Kwa juma moya, chunguza muzuri matangazo ya biashara kuhusu namna ya kuvala. Inachochea watu wakuwe na maisha ya namna gani? Mu ile matangazo munajificha mawazo yenye imekusudiwa kukufanya uone kama unapaswa kufuata namna fulani ya kuvala? Kijana mwenye kuitwa Karen anasema hivi: “Watu wanatiwa moyo sana wajikaze kuonekana muzuri sana, kuvala muzuri sana, na kuonyesha mwili wenye kuvutia wenye wako nao. Watu wenye kufanya matangazo ya biashara wenye wanajua ile jambo, wanafanyaka yao yote juu ya kuchochea vijana.”

Kosa ya #2: Kufuata namna ya kuvala yenye imeenea sana juu tu wengine wakukubali.

 Kijana mwenye kuitwa Manuel anasema hivi: “Kama nguo fulani njo inapendwa sana, kila mutu ataivala. Kama hauivale, watu watakusema mubaya.” Kijana mwenye kuitwa Anna naye anasema hivi: “Jambo yenye watu wanahangaikia sana haiko manguo, lakini ni kukubaliwa na wengine.

 Jambo ya muzuri ya kufanya: Biblia inasema hivi: “Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.” (Waroma 12:2) Kulingana na ile shauri, angalia manguo yako na ujiulize hivi:

  • ‘Ni mambo gani inanichocheaka sana wakati niko nachagua manguo?’

  • ‘Ninaonaka kama ni jambo ya maana sana kuwa na manguo yenye kutengenezwa na watu wenye kujulikana sana ao kompanyi zenye kujulikana sana?’

  • ‘Ninavalaka juu wengine wanione?’

 Shauri: Kuliko kuona kama kuko tu mambo mbili, ni kusema, kuvala manguo yenye kupendwa sana (juu ukubaliwe) ao kuvala mu njia yenye ilishapitwa na wakati (yenye watu hawafurahie), fikiria jambo ingine ya tatu: Kuvala mu njia yenye inafanya ujitumainie na ujisikie muzuri, juu kama unajitumainia, hautafuata-fuata namna ya wengine ya kuvala.

Kosa ya #3: Kuwaza kama nguo ya kuvutia sana wengine njo ya muzuri zaidi.

 Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Jennifer anasema hivi: “Kusema kweli, wakati fulani mutu anaweza penda avale manguo ya kuvutia sana, kwa mufano manguo ya mufupi sana ao ya kubana sana.”

 Jambo ya muzuri ya kufanya: Biblia inasema hivi: “Kujipamba kwenu kusikuwe kwa inje . . . lakini kukuwe ule mutu wa siri wa ndani ya moyo.” (1 Petro 3:3, 4) Kulingana na ile andiko, ujiulize hivi: Nini njo ya kuvutia zaidi, nguo yenye kufanya watu watuangalie sana ao sifa za muzuri?

 Shauri: ‘Nguo’ ya muzuri zaidi yenye unapaswa kuvala ni sifa ya kiasi. Ni kweli kwamba leo watu wengi hawana ile sifa. Lakini waza kidogo:

 Ulishakazungumuza na mutu mwenye anasemaka mingi, na mazungumuzo yake yote inahusu tu maisha yake? Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, pengine ule mutu hajue kama wakati iko nafanya vile, iko nakukimbiza!

Sawa tu vile mazungumuzo, namna ya mutu ya kuvala inaweza kuonyesha kama anajifikiria sana na kufanya wengine wasipende kumukaribia

 Wakati unavala bila kiasi, unakuwa sawa ule mutu. Manguo yako iko naambia watu, ‘muniangalie,’ na ile inaweza kufanya watu waone kama haujitumainie ao unajifikiria sana, ao yote mbili. Tena, inaweza kuonekana kama uko tayari kufanya jambo yoyote juu tu watu wakuone, hata jambo ya mubaya.

 Kuliko kuonyesha-onyesha kitu yenye hauko nauzisha, ujikaze kuwa na kiasi. Kijana mwenye kuitwa Monica anasema hivi: “Kuwa na kiasi haimaanishe kama utakuwa navala sawa tate yako. Inamaanisha tu kama unajiheshimia na unaheshimia wengine.”