Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Ni Mubaya kwa Mwanaume Kufanya Ngono na Mwanaume na Mwanamuke Kufanya Ngono na Mwanamuke?

Ni Mubaya kwa Mwanaume Kufanya Ngono na Mwanaume na Mwanamuke Kufanya Ngono na Mwanamuke?

 “Wakati nilikuwa nakomala, nilikuwa napendezwa kimapenzi na wanaume wenzangu. Ile ilikuwa kati ya mambo yenye ilikuwa nanihangaisha sana. Nilikuwa nawaza kama ile mawazo itapita kisha wakati fulani. Lakini iliendelea kunisumbua.”​—David, 23.

 David ni Mukristo mwenye anapenda kumufurahisha Mungu. Anaweza kumufurahisha Mungu hata kama iko napendezwa kimapenzi na wanaume wenzake? Mungu Iko na mawazo gani kuhusu ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke?

 Biblia inasema nini?

 Mu kila eneo watu wako na mawazo tofauti juu ya ngono kati ya wanaume na wanaume na ngono kati ya wanamuke na wanamuke. Na ile mawazo inaweza kubadilika vile siku ziko zinapita. Lakini Wakristo hawafuatake mawazo ya watu wengi ao “kupeperushwa huku na huku na kila upepo wa mafundisho.” (Waefeso 4:14) Wanaacha kanuni za Biblia ziongoze mawazo yao kuhusu ngono kati ya wanaume na wanaume na ngono kati ya wanamuke na wanamuke, na pia kuhusu tabia ingine yoyote.

 Mawazo ya Biblia juu ya ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke iko wazi.

  •  Biblia inasema hivi: “Haupaswe kulala na mwanaume kama vile unalala na mwanamuke. Hilo ni tendo lenye kuchukiza.”​—Walawi 18:22.

  •  “Kwa kupatana na tamaa za mioyo yao, Mungu, . . . aliwaacha katika tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe, kwa maana wanamuke wao walibadilisha matumizi yao ya asili kuwa kinyume cha asili.”​—Waroma 1:24, 26.

  •  “Musidanganywe. Waasherati, waabudu-sanamu, wazinifu, wanaume wenye wanakubali matendo ya kulalwa na wanaume wenzao, wanaume wenye kulala na wanaume wenzao, wezi, watu wenye kuwa na pupa, walevi, watukanaji, wanyanganyi hawatariti Ufalme wa Mungu.”​​—1 Wakorinto 6:9, 10.

 Ile mawazo ya Biblia inahusu watu wote. Haiko tu wanaume wenye kuwa na hamu ya kufanya ngono na wanaume ao wanamuke wenye kuwa na hamu ya kufanya ngono na wanamuke. Kila mutu anapaswa kuzuia tamaa ya kufanya mambo yenye Mungu anachukia.​​—Wakolosai 3:5.

 Ile inamaanisha kama . . . ?

 Biblia inapenda tuchukie wanaume wenye kufanya ngono na wanaume na wanamuke wenye kufanya ngono na wanamuke?

 Hapana. Biblia haitutie moyo tuchukie mutu yeyote, ukuwe iko na ile tabia ao hapana. Inatuambia ‘tufuatie amani pamoja na watu wote.’ (Waebrania 12: 14) Hata wakuwe na tabia ya namna gani. Kwa hiyo, ni kosa kuchukia ao kutendea mubaya wanaume wenye kufanya ngono na wanaume na wanamuke wenye kufanya ngono na wanamuke.

 Ile inamaanisha kama Wakristo wanapaswa kupinga sheria zenye zinaruhusu ndoa kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke?

 Biblia inaonyesha kama ndoa inapaswa kuwa kati ya mwanaume na mwanamuke. (Matayo 19:4-6) Lakini, mabishano ya sheria za wanadamu juu ya ndoa kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke inahusiana na mambo ya politique, hapana kanuni za mema na mabaya. Biblia inaambia Wakristo wasijiingize mu mambo ya politike. Njo maana hawateteake wala kupinga sheria za serikali kuhusu ndoa ao ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke.

 Lakini namna gani kama . . . ?

 Lakini namna gani kama mwanaume fulani anafanyaka ngono na mwanaume mwenzake ao mwanamuke fulani anafanyaka ngono na mwanamuke mwenzake? Ule mutu anaweza kubadilika?

 Ndiyo, juu watu fulani wa wakati wa mitume walikuwa vile. Kisha kusema wanaume wenye kufanya ngono na wanaume hawatariti Ufalme wa Mungu, Biblia inasema: “Na bado wengine wenu mulikuwa vile.”​—1 Wakorinto 6:11

 Ni kusema wale wanaume wenye waliacha kufanya ngono na wanaume hawakusikiaka tena hamu ya kurudilia maisha yao ya zamani? Inawezekana walisikia tena ile hamu wakati fulani. Biblia inasema hivi: Muvae utu mupya, wenye kupitia ujuzi wenye hauna makosa unafanywa kuwa mupya kulingana na mufano wa Ule mwenye aliuumba.” (Wakolosai 3:10) Mutu habadilikake mu siku moya.

 Lakini namna gani ikiwa mutu mwenye anapenda kufuata kanuni za Mungu angali na tamaa ya kufanya ngono na mwanaume mwenzake ao mwanamuke mwenzake?

 Ikuwe tamaa ni ya namna gani, mutu njo anaweza kuamua kama hataikomalisha ao kuitimiza. Anaweza kufanya vile namna gani? Biblia inasema hivi: “Muendelee kutembea kwa roho na hamutatenda tamaa yoyote ya mwili hata kidogo.”​—Wagalatia 5:16.

 Ile andiko haiseme kama mutu hatakuwa na tamaa yoyote ya mwili. Lakini, kama iko anazoea kujifunza Biblia na kusali, atakuwa na nguvu ya kupinga zile tamaa.

 David mwenye tulizungumuzia ku mwanzo alifikia kujionea vile. Zaidi sana wakati aliambia wazazi wake tatizo yenye alikuwa nayo. Anasema hivi: “Ilikuwa sawa vile muzigo ya muzito sana inatoka ku mabega yangu. Na kama pengine ningewaambiaka zamani, ningekuwaka na furaha zaidi wakati nilikuwa kijana.”

 Tunakuaka tu na furaha sana kama tunafuata kanuni za Yehova. Tuko hakika kama zile kanuni “ni za haki, zinafanya moyo ushangilie,” na kama “katika kuzishika, kuko zawabu kubwa.”​—Zaburi 19:8, 11.