JANUARI 21, 2015
FILIPINO
Mwaka Mmoja Baada ya Kimbunga Haiyan, Waathiriwa Wapata Makao Mapya
MANILA, Filipino—Mashahidi wa Yehova walianzisha mradi mkubwa wa ujenzi baada ya Kimbunga Haiyan ili kurekebisha au kujenga upya nyumba 750 hivi katika muda usiozidi mwaka mmoja.
Dean Jacek, msemaji wa Mashahidi wa Yehova nchini Filipino, anaeleza hivi: “Tulijiwekea mradi wa kumaliza kazi kufikia Septemba 2014. Ujenzi ulianza mapema mwaka huo na kwa msaada wa wajitoleaji wengi, ujenzi ulikamilika kabla ya mwisho wa mwezi wa Agosti.”
Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova liliweka kando michango iliyotumwa na Mashahidi wengine kutoka ulimwenguni pote ili kutegemeza mradi huo. Ofisi ya tawi ya Mashahidi iliyoko Manila ilianzisha halmashauri za kupanga kazi hiyo ya ujenzi katika maeneo yaliyoathiriwa. Kazi hiyo ilitia ndani kurekebisha au kujenga upya nyumba 167 katika Jiji la Tacloban, nyumba 256 katika Jiji la Ormoc, nyumba 101 katika Jiji la Cebu, na nyumba 218 katika Jiji la Roxas. Mashahidi 522 waliojitolea kutoka Filipino na wengine 90 kutoka nchi nyingine, walishiriki katika kazi hiyo.
Bw. Ferdinand Martin G. Romualdez, mwakilishi wa Wilaya ya Kwanza ya Leyte, alisema hivi: “Mashahidi wa Yehova ndio waliokuwa shirika la kwanza lisilo la kiserikali kuanzisha mpango huo wa kujenga nyumba upya . . . . Siwezi kueleza uthamini na shukrani za familia yangu na jamaa zetu.”
Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:
J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000
Filipino: Dean Jacek, simu +63 2 411 6090