Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 14, 2017
INDIA

Mvua Kubwa Zapiga Mumbai

Mvua Kubwa Zapiga Mumbai

Mvua nyingi ilinyesha Mumbai, India, katika juma la Agosti 28, na kusababisha vifo vya watu 14.

Ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini India imeripoti kwamba hakuna Shahidi yeyote aliyekufa au kujeruhiwa vibaya. Hata hivyo, nyumba kadhaa za Mashahidi zilikumbwa na mafuriko. Mashahidi waliandaa chakula na kusaidia kusafisha nyumba zilizoharibiwa za Mashahidi wenzao.

Ofisi ya tawi inaendelea kufuatilia hali huko Mumbai na vilevile katika maeneo mengine ya India yaliyoathiriwa na mafuriko.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1-845-524-3000

India: Tobias Dias, simu +91-9845476425