Hamia kwenye habari

Hali baada ya maporomoko ya ardhi huko Natonin, Wilaya ya Mountain

AGOSTI 14, 2019
FILIPINO

Mvua Kubwa za Masika Zanyesha Ufilipino

Mvua Kubwa za Masika Zanyesha Ufilipino

Mwanzoni mwa mwezi Agosti 2019, mvua kubwa za masika na upepo mkali ulisababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi nchini Ufilipino. Kwa kusikitisha, ndugu mmoja aliyekuwa akitumikia akiwa painia wa pekee wa muda alikufa katika maporomoko hayo yaliyotokea huko Natonin, Wilaya ya Mountain. Ndugu mwingine pia ambaye anatumikia akiwa painia wa pekee wa muda alipata majeraha madogo katika maporomoko hayohayo. Katika tukio lingine, mvulana wa miaka kumi alijeruhiwa na kifusi lakini alipata matibabu yanayofaa.

Hakuna nyumba ya akina ndugu iliyoharibiwa vibaya. Hata hivyo, Jumba moja la Ufalme lililo huko Negros Occidental limeharibika kwa kiasi fulani kutokana na upepo mkali uliosababisha sehemu fulani ya dari kuanguka.

Ofisi ya tawi ya Ufilipino na mwangalizi wa mzunguko wanatoa msaada wa kiroho na wa kihisia kwa familia za akina ndugu waliothiriwa.

Tunasikitika kusikia kuhusu msiba huo mkubwa na tunasali kwa ajili ya wale wanaoomboleza kifo cha ndugu yetu. Tunatazamia wakati ambao mambo yenye kuumiza kama hayo “hayataingia tena akilini.”—Isaya 65:17..