Hamia kwenye habari

Apex, jamii ndogo ya Iqaluit iliyo katika Kisiwa cha Baffin huko Nunavut, Kanada

APRILI 17, 2020
KANADA

Mwadhimisho wa Ukumbusho wa 2020—Kanada

Kuadhimisha Ukumbusho Katika Eneo la Kaskazini Zaidi la Dunia

Mwadhimisho wa Ukumbusho wa 2020—Kanada

Wahubiri 27 katika Kutaniko la Iqaluit, kwenye Visiwa Aktiki vya Kanada, waliadhimisha ukumbusho kupitia video iliyounganishwa kwenye mtandao. Wanafunzi 12 wa Biblia kati ya 55 walitazama hotuba hiyo na walishukuru sana kwamba waliunganishwa.

Kwa wengi wa wanafunzi hao, isingalikuwa rahisi kuhudhuria ukumbusho, au huenda wangeshindwa kabisa. Wanaishi katika maeneo ya mbali sana ya kutaniko hilo, lenye ukubwa wa kilomita milioni mbili hivi za mraba, kuanzia Kimmirut hadi Grise Fiord—eneo la kaskazini zaidi la Kanada.

Ndugu Isaac Demeester, mzee wa Kutaniko la Iqaluit anasema hivi: “Mwaka huu kwa mara ya kwanza wanafunzi wetu wa Biblia walifaulu kujiunga nasi kwa ajili ya programu ya Ukumbusho. Mwanafunzi mmoja wa Biblia anayeishi Grise Fiord aliwaalika wengine wanne watazame programu hiyo pamoja naye, kwa hiyo, jumla ya watu watano kutoka eneo la kaskazini zaidi la dunia walijiunga nasi kwa ajili ya ukumbusho.”

Changamoto za pekee zilizotokezwa na ugonjwa wa virusi vya corona zimewasaidia ndugu na dada wengi katika Kutaniko la Iqaluit wamejionea manufaa ya kubadilika kulingana na hali.

Dada Kathy Burechailo anasema hivi: “Tulifaulu kuwahubiria watu wanaoishi katika maeneo ya mashariki ya Aktiki kupitia simu. Nilifurahia kuzungumza na watu katika maeneo ya mbali zaidi ya eneo letu. Watu hawawezi kutoka nyumbani na wanahitaji faraja.”

Dada Laura McGregor anasema hivi: “Kutengwa kumefanya tuwe na mkazo sana huku Iqaluit tunapokabiliana na matatizo ya kiuchumi na pia hatujui kitakachotokea. Ilikuwa mara ya kwanza kwa familia yetu kutengeneza mkate wa Ukumbusho. Tulifurahia sana pindi hiyo pamoja. Ilitusaidia kuthamini jinsi mwadhimisho huo ulivyo rahisi sana, na ni baraka kwamba tunaweza kupata kila kitu kwa urahisi.”

Ndugu Demeester anasema: “Ingawa ugonjwa wa virusi vya corona umetutenganisha katika njia nyingi, imependeza kuona jinsi ambavyo kutaniko letu limekuwa na uhusiano wa karibu zaidi wakati wa kipindi hiki cha corona. Ukumbusho wa mwaka huu umebadili maisha yetu!”

Kutaniko la Iqaluit linatazamia kwa hamu kujenga Jumba la Ufalme hivi karibuni, hali zitakaporuhusu. Kwa sasa, tunajua kwamba Yehova atabariki jitihada zao za kuhubiri habari njema katika maeneo ya kaskazini zaidi ya Kanada—mojawapo ya sehemu za mbali zaidi za dunia!—Matendo 1:8.