Hamia kwenye habari

Dada Galina Abrosimova

MEI 10, 2022
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI | Galina Abrosimova Ashinda Woga Wake

HABARI ZA KARIBUNI | Galina Abrosimova Ashinda Woga Wake

Agosti 11, 2022, Mahakama ya Eneo la Nizhny Novgorod ilikataa ombi la rufaa la Dada Galina Abrosimova. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Mei 6, 2022, Mahakama ya Wilaya ya Sovietskiy iliyo Nizhny Novgorod ilimhukumu Galina kifungo cha nje cha miaka sita.

Mfuatano wa Matukio

  1. Juni 4, 2019

    Wapelelezi walifungua kesi dhidi ya Mashahidi wa Yehova kadhaa katika Eneo la Nizhny Novgorod. Walishtakiwa kwa sababu ya kufanya mikutano, kukusanya michango, na kuwatia moyo wengine washirikiane na shirika la kidini lililopigwa marufuku

  2. Julai 17,2019

    Nyumba za familia 35 za Mashahidi wa Yehova zilivamiwa na kupekuliwa. Galina alikamatwa na kuwekwa kizuizini kwa siku mbili

  3. Oktoba 19, 2021

    Kesi ya uhalifu dhidi ya Galina ilianza

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kuwapa ujasiri ndugu na dada zetu nchini Urusi ili ‘wasimame mbele ya magavana na wafalme ili kuwa ushahidi kwao.’​—Marko 13:9.