Hamia kwenye habari

Ndugu Aleksandr Nikolayev akipokewa na mke wake, Yevgeniya, watoto wao watano, na mama ya Yevgeniya, baada ya kuachiliwa kutoka gerezani

SEPTEMBA 21, 2023
URUSI

Ndugu Aleksandr Nikolayev Ameachiliwa Kutoka Gerezani Nchini Urusi

Ndugu Aleksandr Nikolayev Ameachiliwa Kutoka Gerezani Nchini Urusi

Septemba 19, 2023, Ndugu Aleksandr Nikolayev aliachiliwa kutoka gerezani nchini Urusi baada ya kufungwa kwa karibu miaka miwili. Baada ya kuachiliwa, Aleksandr alipokewa na waabudu wenzake na kuunganishwa tena na mke wake, Yevgeniya, na watoto wao watano.

Mapema katika mwaka wa 2021, nyumba ya familia ya Nikolayev ilivamiwa na maofisa wa FSB na polisi wa kutuliza ghasia. Aleksandr alishtakiwa na kuhukumiwa kwamba alikuwa na “kosa” la kuzungumza kuhusu Biblia pamoja na familia na marafiki wake.

Kabla ya kukamatwa, Aleksandr alisema hivi kuhusu kile kinachomsaidia kudumisha ushikamanifu wake: “Nimetambua kwamba kuogopa wanadamu na kuogopa kitakachotokea kunaweza kulemaza uwezo wangu wa kufikiri waziwazi. Kwa hiyo, ninajaribu woga kama huo usinisumbue. Ninasali kwamba Yehova anipe uwezo wa kumtegemea kikamili zaidi, naye ameniimarisha.”

Tunashangilia kwamba Aleksandr sasa amewekwa huru na anaweza kufurahia kuwa na familia yake. Bila shaka Yehova “anawafurahia” watumishi wake washikamanifu wanapoonyesha imani na ujasiri licha ya ukosefu wa haki wanaokabili.​—Zaburi 149:4.