Hamia kwenye habari

MEI 31, 2024
BENIN

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa Katika Kifon

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa Katika Kifon

Mei 26, 2024, Ndugu Abdiel Worou, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Afrika Magharibi, alitangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kifon wakati wa programu ya pekee iliyofanyika kwenye Jumba la Kusanyiko la Abomey, nchini Benin. Ndugu na dada 920 walihudhuria programu hiyo uso kwa uso. Kwa kuongezea ndugu na dada 6,188 waliunganishwa kwenye programu hiyo kupitia video mtandaoni. Nakala zilizochapishwa za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ziligawanywa kwa wote waliohudhuria programu hiyo. Wakati huohuo pia toleo la rekodi za sauti na toleo la kielektroni lilipatikana kwa ajili ya kupakuliwa.

Watu milioni mbili hivi wanaozungumza Kifon wanaishi nchini Benin, kutia ndani zaidi ya ndugu na dada 4,000 wanaotumikia katika makutaniko na vikundi 84 vya Kifon. Baada ya kutolewa kwa Biblia—Habari Njema Kulingana na Mathayo mwaka wa 2022, vitabu vingine vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo viliendelea kutolewa hatua kwa hatua katika mfumo wa kielektroni.

Sisi pamoja na ndugu na dada zetu wanaozungumza Kifon, tunamshukuru sana Yehova kwa kufanya Neno lake la kweli lipatikane kwa wengi wanaotamani kufuata ushauri wake wenye hekima leo.​—Yohana 17:17.