Ona video zinazopatikana

Namna Tulifikia Kupata Biblia

Namna Tulifikia Kupata Biblia

Namna Tulifikia Kupata Biblia

Inashangaza sana kuona namna Biblia imetufikia leo bila kuharibiwa. Kazi ya kuandika Biblia ilimalizika kumepita zaidi ya miaka 1900. Biblia iliandikwa ku vitu vyenye vinaweza kuharibika, sawa vile ngozi ya wanyama ao makaratasi yenye kutengenezwa kwa kutumia mumea wenye kuitwa papyrus. Pia, maandishi ya kwanza-kwanza ya Biblia iliandikwa mu luga zenye watu kidogo tu njo wanajua leo. Tena, viongozi wa dini, watawala, na watu wengine wenye mamlaka walifanya yao yote juu ya kujaribu kuharibu Biblia.

Namna gani Biblia iliokoka ile miaka yote na kufikia kuwa kitabu yenye watu wanasoma zaidi? Tuzungumuzie tu mambo mbili.

Kufanya Kopi za Mingi Kulilinda Maandishi ya Biblia

Waisraeli walilinda kwa uangalifu vitabu vya kukunjwa vya maandishi ya kwanza-kwanza kabisa ya Biblia. Kwa mufano, Mungu aliambia wafalme wa Israeli wafanye ‘kopi ya Sheria . . ., kutoka katika kopi yenye makuhani Walawi waliweka.’​—Kumbukumbu la Torati 17:18.

Waisraeli wengi walipenda kusoma Maandiko, na walitambua kama ni Neno ya Mungu. Kwa hiyo, waandishi wenye uzoefu sana njo walikuwa wanafanya kopi za maandishi ya Biblia; walikuwa wanafanya vile kwa uangalifu sana. Ezra, mwanaume mumoja mwenye kumuogopa Mungu, anatajwa kuwa “mwandishi mwenye ufundi wa Sheria ya Musa, yenye Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa.” (Ezra 7:6, maelezo ya chini) Wamasora, watu wenye walifanya kopi za Maandiko ya Kiebrania, ao “Agano ya Kale,” kati ya karne ya sita na kumi walikuwa hata wanahesabu herufi za maandishi ili kuepuka kuingiza makosa. Kufanya kopi kwa uangalifu vile kulisaidia mu maandishi ya Biblia musiingie makosa na kulilinda Biblia hata kama maadui walijikaza sana juu ya kuiharibu.

Kwa mufano, mu mwaka wa 168 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Antioko wa Ine, mutawala wa Siria, alijaribu kuharibu kopi zote za Maandiko ya Kiebrania zenye zilipatikana mu inchi yote ya Palestina. Kitabu kimoja cha historia ya Wayahudi kinasema hivi: “Walipasua na kulunguza kila kitabu cha kukunjwa cha sheria chenye walipata.” Kitabu moja (The Jewish Encyclopedia) inasema hivi: “Maofisa wenye walipewa ile kazi, walifanya vile kwa bidii sana . . . Mutu mwenye alikuwa na kitabu kitakatifu . . . alihukumiwa kifo.” Hata vile, Maandiko iliendelea kupatikana katikati ya Wayahudi wenye walikuwa wanaishi Palestina na wenye walikuwa wanaishi mu maeneo ingine.

Wakati kidogo kisha waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki, ao “Agano Jipya,” kumaliza kazi yao, kopi za barua, habari za unabii, na habari zenye kuzungumuzia historia zenye waliandika kwa kuongozwa na roho ya Mungu, zilienea sana. Kwa mufano, Yohana aliandika Injili yake katika muji wa Efeso, ao karibu na Efeso. Hata vile, sehemu ya kopi ya Injili yake ilivumbuliwa Misri, mamia ya kilometre mbali na kwenye aliiandikiaka. Watu wenye elimu wanasema kama wakati ile kopi ilifanywa kulikuwa hakuyapita miaka 50 tangu Yohana aandike Injili yake. Ile inaonyesha kama Wakristo wa maeneo ya mbali walikuwa na kopi za maandishi yenye ilikuwa haijakawia tangu iandikwe kwa kuongozwa na roho.

Kuenea sana kwa Neno ya Mungu kulisaidia pia isipotee miaka mingi kisha Kristo. Kwa mufano, watu wanasema kama tarehe 23 Mwezi wa 2, mwaka wa 303, kisha kuzaliwa kwa Yesu, Mutawala Muroma Dioclétien alisimama na kuangalia namna maaskari wake walivunja milango ya kanisa fulani na kuunguza kopi za Maandiko. Dioclétien aliwaza kama atamaliza Ukristo kwa kuharibu maandishi matakatifu ya Wakristo. Siku yenye ilifuata, aliamuru kama mu Utawala wote wa Roma, kopi zote za Biblia zichomwe mbele ya watu. Hata vile, kopi fulani ziliokoka na kopi zingine za mupya zilifanywa. Kwa kweli, sehemu kubwa za kopi mbili za Biblia katika Kigiriki, zenye inaonekana zilifanywa wakati kidogo kisha Dioclétien kuamuru Biblia zote ziharibiwe, zingali mupaka leo. Kopi moja iko Roma, na ingine iko mu Maktaba ya Uingereza, katika muji wa Londres.

Hata kama hakuna maandishi ya kwanza kabisa ya Biblia yenye imepatikana, maelfu ya kopi za Biblia nzima ao sehemu, zenye ziliandikwa kwa mukono zimeokoka na kufikia mupaka leo. Kopi fulani ni za zamani sana. Ujumbe wenye ulikuwa mu maandishi ya kwanza kabisa ulibadilishwa wakati kopi zilikuwa zinafanywa? William Henry Green, mutu mwenye elimu, alisema hivi kuhusu Maandiko ya Kiebrania: “Tunaweza kusema kwa uhakika kama hakuna maandishi ingine ya zamani yenye imetufikia bila makosa sawa vile Biblia.” Frederic Kenyon, mutu mwenye elimu ya maandishi ya Biblia, aliandika kama kopi za zamani zaidi zenye zingali mupaka leo zilifanywa miaka kidogo tu kisha waandikaji wa Biblia kuandika vitabu vya Biblia. Njo maana tunaweza kuwa hakika kabisa kama Biblia yenye tuko nayo leo haina makosa. Hatuwezi kuwa hakika vile kuhusu kitabu ingine ya zamani.”

Kutafsiri Biblia

Sababu ingine kubwa yenye inafanya Biblia ikuwe kitabu yenye watu wanasoma zaidi ni hii: Inapatikana mu luga za mingi. Ile inaonyesha kama Mungu anapenda watu wa mataifa na luga zote wafikie kumujua na kumuabudu “kwa roho na kweli.”​—Yohana 4:23, 24; Mika 4:2.

Biblia ya Septante njo tafsiri ya kwanza yenye inajulikana ya Maandiko ya Kiebrania yenye ilitafsiriwa mu Kigiriki. Ilitafsiriwa kwa ajili ya Wayahudi wenye kuzungumuza Kigiriki, wenye walikuwa wanaishi inje ya Palestina. Na kazi ya kuitafsiri ilimalizika miaka mia mbili hivi mbele Yesu akuje ku dunia. Karne fulani kisha Biblia yote kumalizika, ilitafsiriwa mu luga za mingi. Wafalme na mapadri njo walipaswa kufanya yao yote ili kusaidia watu wapate Biblia, lakini kisha wakati fulani, walifanya yao yote ili kuzuia Biblia itafsiriwe mu luga zenye watu wengi walikuwa wanazungumuza. Walifanya vile juu hawakupenda watu wajue kweli juu ya Mungu.

Wanaume fulani wenye uhodari hawakutii wale wafalme na viongozi wa dini. Walitia maisha yao mu hatari juu ya kutafsiri mu luga zenye watu wengi walikuwa wanazungumuza. Kwa mufano mu 1530, mwanaume fulani Mwingereza mwenye kuitwa William Tyndale, mwenye alisomea ku masomo ya Oxford, alitafsiri vitabu tano vya kwanza vya Maandiko ya Kiebrania. Hata kama alipingwa sana, yeye njo alikuwa wa kwanza kutafsiri Biblia mu Kiingereza, moja kwa moja kutoka katika Kiebrania. Tyndale alikuwa pia mutu wa kwanza kutumia jina Yehova mu Biblia ya Kiingereza. Pia, katika Uhispania, mutu mwenye elimu ya Biblia mwenye kuitwa Casiodoro de Reina alitia maisha yake mu hatari wakati alikuwa anatafsiri Biblia mu Kihispania, kwa sababu watu fulani wa Kanisa Katoliki walikuwa wanatafuta kumuua. Alisafiri mu inchi mbalimbali juu amalize tafsiri yake; alienda Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Hollande, na Uswisi. *

Leo, Biblia inaendelea kutafsiriwa mu luga mingi zaidi, na Biblia za mingi sana ziko zinatolewa. Kuona namna Biblia iliokoka na kufikia kuwa kitabu yenye watu wanasoma sana kunaonyesha kama maneno yenye mutume Petro aliandika kwa kuongozwa na roho ni ya kweli. Aliandika hivi: “Majani yanakauka, na ua linaanguka, lakini neno la Yehova linadumu milele.”​—1 Petro 1:24, 25.

[Maelezo ya chini]

^ fu. 14 Tafsiri ya Reina ilitolewa mu mwaka wa 1569 na ilirekebishwa na Cipriano de Valera mu mwaka wa 1602.

[Kisanduku/​Picha]

NISOME TAFSIRI GANI?

Luga za mingi ziko na tafsiri za mingi za Biblia. Tafsiri fulani zinatumia maneno ya nguvu, yenye watu hawatumie tena leo. Watafsiri wengine wanatafsiri tu namna wanapenda, juu tu watu wafurahie kusoma, bila kuangalia kama mawazo yenye wanatafsiri inapatana kabisa na maandishi ya kwanza-kwanza. Na tafsiri zingine ni za neno kwa neno.

Tafsiri ya Kiingereza ya Biblia​Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova, ilitafsiriwa moja kwa moja kutoka katika luga zenye zilitumiwa juu ya kuandika Biblia. Wenye walifanya ile tafsiri hawakupenda majina yao ijulikane. Ile tafsiri imetumiwa juu ya kutafsiri Biblia mu luga zingine karibu 60. Hata vile, wale wenye walitafsiri Biblia mu zile luga zingine, walikuwa wanalinganisha sana tafsiri yao na maandishi ya luga zenye zilitumiwa juu ya kuandika Biblia. Wenye walifanya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya walijikaza kutafsiri neno kwa neno kama tu kufanya vile hakufiche maana. Wale watafsiri wanajikaza sana kufanya Biblia yenye watu wanaweza kuelewa wakati wanaisoma leo, sawa vile watu walikuwa wanaelewa wakati waliisoma mu luga za atu kwanza-kwanza.

Watu fulani wenye elimu ya luga wamechunguza tafsiri fulani za sasa, na pia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Walifanya vile juu wapate mawazo yenye haikutafsiriwa vile inafaa, na yenye inaegemea mafundisho ya dini fulani. Mumoja kati yao ni Jason David BeDuhn, mwalimu wa mambo ya dini ku Masomo ya Juu ya Arizona Kaskazini, katika Inchi ya Amerika. Mu 2003, alichapisha ripoti ya uchunguzi, yenye kurasa 200 kuhusu “Biblia [9] zenye zinasomwa sana na watu wenye kuzungumuza Kiingereza.” * Ripoti yake ilizungumuzia maandiko yenye watu wanazoea kubishana juu ya namna inapaswa kutafsiriwa, kwa sababu ni mu maandiko ya vile njo “ni mwepesi mutafsiri aegemee mawazo ya dini fulani.” Mu kila andiko, alilinganisha maandishi ya Kigiriki na kila tafsiri ya Kiingereza, na kutafuta sehemu kwenye walibadilisha maana kwa kuegemea mawazo ya dini fulani. Alivumbua nini?

BeDuhn anasema kama watu wa kawaida na watu wengi wenye elimu ya Biblia wanawaza kama kitu yenye inafanya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ikuwe tofauti na tafsiri zingine, ni juu wenye waliifanya waliegemea mawazo ya dini yao. Hata vile, anasema hivi: “Mambo mingi iko tofauti mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya juu ile tafsiri iko sahihi sana, ni ya neno kwa neno, na imetafsiriwa kwa uangalifu sana.” Hata kama BeDuhn hakubaliane na namna maandiko fulani imetafsiriwa mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, anasema kama ile njo tafsiri “yenye kuwa sahihi zaidi kati ya tafsiri zenye alilinganisha.” Anaiita kuwa tafsiri ya “muzuri sana.”

Benjamin Kedar, Mwebrania wa Israeli, mwenye elimu alisema pia vile kuhusu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Mu 1989, alisema hivi: “Ile tafsiri inaonyesha kama wenye waliifanya walijikaza sana kuelewa maandishi muzuri zaidi kadiri inawezekana. . . . Siyaonaka mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya nia yoyote ya kutafuta kusemesha andiko mambo yenye haiseme, juu tu ya kuunga mukono mawazo ya dini fulani.”

Ujiulize hivi: ‘Wakati ninasoma Biblia, nia yangu ni nini? Napenda tu habari yenye kuwa mwepesi kusoma, bila kuangalia kama iko na makosa ao hapana? Ao napenda kusoma habari yenye inapatana na maandishi ya kwanza-kwanza kwa kadiri inawezekana?’ (2 Petro 1:20, 21) Nia yenye uko nayo njo itakusaidia uchagule tafsiri yenye utasoma.

[Maelezo ya chini]

^ fu. 22 Zaidi ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, alichunguza pia The Amplified New Testament, The Living Bible, The New American Bible With Revised New Testament, New American Standard Bible, The Holy Bible​​New International Version, The New Revised Standard Version, The Bible in Today’s English Version, na King James Version.

[Picha]

“Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya” inapatikana mu luga za mingi

[Picha]

Maandishi ya Wamasora

[Picha]

Kipande cha karatasi chenye kuwa na maandishi ya Luka 12:7, “. . . Musiogope; ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.”

[Maneno ili kueleza kwenye picha zilitokea]

Ukurasa wa mbele: National Library of Russia, St. Petersburg; wa pili na wa tatu: Bibelmuseum, Münster; nyuma: © The Trustees of the Chester Beatty Library, Dublin