Ona video zinazopatikana

Acha pombe fasi yake

Acha pombe fasi yake

Acha pombe fasi yake

TONY, mwenye alizungumuziwa mu habari ya kwanza, angekuwa na maisha ya muzuri kama angepiganishaka tatizo yake ya kunywa sana. Juu alikuwa nakunywa sana na hakukuwa alama za kuonyesha kama amelewa, Tony aliwaza kama kunywa sana haikukuwa tatizo kwake. Juu ya nini alikuwa najidanganya?

Hakukuwa tena anafikiri muzuri juu alikuwa anakunywa sana. Ikuwe Tony alitambua ao hapana, ubongo wenye unaongoza mwili wake, akili yake, na hisia zake, haukukuwa unatumika muzuri wakati alikuwa amelewa. Kadiri aliendelea kunywa sana, ni vile alishindwa kutambua kama hali yake ilikuwa mubaya.

Sababu ingine yenye ilifanya Tony asitambue shida yake ni juu hakukuwa napenda kuacha kunywa. Ku mwanzo Allen, mwenye kuzungumuziwa mu habari yenye kutangulia, hakukubali kuwa alikuwa na tatizo ya kunywa sana. Anasema hivi: “Nilikuwa nafichika tabia yangu ya kunywa sana. Nilikuwa natafuta visababu vya kunywa sana na kujaribu kusadikisha wengine kama sikunywake sana. Nilikuwa na kusudi moya tu: Kuendelea kunywa.” Hata kama wengine waliona kuwa Tony na Allen walikuwa na tatizo ya kunywa sana, wao walikuwa wanajiambia kama hawana shida yoyote. Wote wawili walipaswa kufanya jambo fulani juu ya kupiganisha tabia yao ya kunywa sana. Walipaswa kufanya nini?

Ukuwe na Nia ya Kuacha!

Watu wengi waliacha tabia ya kunywa sana juu walitii hii maneno ya Yesu: “Kama jicho lako la kuume linafanya ujikwae, ulingoe na ulitupe mbali na wewe. Kwa maana ni muzuri zaidi upoteze kimoja cha viungo vyako kuliko mwili wako wote utupwe katika Gehena.”​—Matayo 5:29.

Yesu hakumaanisha kama tunapaswa kujiumiza, lakini alitumia ile maneno ya mufano juu ya kuonyesha kama tunapaswa kujikaza sana juu ya kuachana na kitu yoyote yenye inaweza kuharibu urafiki wetu na Mungu. Haikuwake mwepesi kufanya mabadiliko, lakini kufanya vile kunaweza kutusaidia tuepuke mawazo na hali zenye zinaweza kutufanya tukuwe watumwa wa pombe. * Kwa hiyo, kama wengine wanakuambia kuwa ulishaanza kunywa sana ujikaze kupunguza, na kama unashindwa kabisa kupunguza, uachane kabisa na pombe. Na hata kama inaweza kuwa nguvu sana kufanya vile, inaweza kuokoa maisha yako.

Hata kama hauko mutumwa wa pombe, unakuwaka na tabia ya kunywa sana? Kama ni vile, unaweza kufanya nini juu uache pombe fasi yake?

Nini Njo Itakusaidia?

1. Ukuwe na imani kama Yehova atakusaidia kama unasali kwake kwa ukawaida na kwa moyo wote. Biblia inashauria hivi watu wote wenye wanapenda kumufurahisha Yehova Mungu: “Katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:6, 7) Juu upate ile amani ya akili, unaweza kusali juu ya mambo gani?

Uitike kama uko na tatizo ya kunywa sana na kama weye njo unaweza kufanya jambo fulani juu ya kuimaliza. Uambie Mungu mambo yenye ungependa kufanya juu ya kushinda ile tatizo na atakusaidia upate nguvu ya kushinda ile tatizo na uepuke matatizo ingine ya nguvu zaidi. Biblia inasema hivi: “Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa, lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.” (Mezali 28:13) Yesu alisema pia kama tunaweza kusali hivi: “Usituingize katika jaribu, lakini utuokoe na ule muovu.” (Matayo 6:13; maelezo ya chini) Lakini, kisha kusali unapaswa kufanya nini? Na unaweza kupata wapi majibu ya sala zako?

2. Neno ya Mungu inaweza kukupatia nguvu. “Neno la Mungu liko na uzima na liko na nguvu . . . na linaweza kutambua mawazo na makusudio ya moyo.” (Waebrania 4:12) Kusoma na kufikiri sana juu ya maandiko ya Biblia kila siku, kumesaidia watu wengi wenye walikuwa walevi zamani. Muandikaji fulani wa zaburi mwenye kumuogopa Mungu aliandika hivi: “Mwenye furaha ni mutu mwenye hatembee kulingana na shauri la waovu. . . . Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova, na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini muchana na usiku. . . . kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.”​—Zaburi 1:1-3.

Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kulisaidia Allen aache kunywa sana. Anasema hivi: “Niko hakika kuwa kama Biblia na kanuni za Biblia hazingenisaidiaka niache kunywa, kama nilishakakufa.”

3. Ukomalishe sifa ya kujizuia. Biblia inasema kama mu kutaniko ya Kikristo ya kwanza-kwanza, watu wenye walikuwaka walevi zamani walisafishwa “kwa roho ya Mungu wetu.” (1 Wakorinto 6:9-​11) Roho ya Yehova iliwasaidia wakomalishe sifa ya kujizuia, na ile sifa njo iliwasaidia waache kunywa sana. Biblia inasema hivi: “Musilewe divai, yenye iko na upotovu ndani yake, lakini muendelee kujazwa roho.” (Waefeso 5:18; Wagalatia 5:21-​23) Yesu Kristo aliahidi hivi: “Baba yenu wa mbinguni atawapatia hata zaidi roho yake takatifu wale wenye kumuomba.” Njo maana alisema hivi: “Muendelee kuomba, na mutapewa.”​—Luka 11:9, 13.

Wale wenye wanapenda kumufurahisha Yehova wanapaswa kukomalisha sifa ya kujizuia kwa kusoma na kujifunza Biblia na kusali kwa ukawaida kwa moyo wote. Kuliko kuvunjika moyo, ukumbuke hii maneno yenye kuwa mu Neno ya Mungu: “Ule mwenye anapanda kwa roho, atavuna uzima wa milele kutokana na roho. Basi tusiache kufanya mema, kwa maana kwa wakati wenye kufaa tutavuna kama hatuchoke kabisa.”​—Wagalatia 6:8, 9.

4. Uchague marafiki wazuri. “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.” (Mezali 13:20) Ambia marafiki wako kama unapenda kabisa kupiganisha tatizo yako ya kunywa pombe. Neno ya Mungu inaonya kama wakati utaacha “kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, [na] mashindano ya kunywa,” wale wenye walikuwaka marafiki wako zamani ‘watashangaa’ na ‘kukutukana.’ (1 Petro 4:3, 4) Ukuwe tayari kuachana na marafiki wenye hawaheshimie uamuzi wako wa kuacha kunywa sana.

5. Uamue kiasi ya pombe yenye utakuwa nakunywa. “Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo, lakini mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.” (Waroma 12:2) Juu ya kuamua kiasi ya pombe yenye unaweza kunywa, fuata kanuni za Yehova, hapana mawazo ya marafiki ao ya “ulimwengu.” Kama unafanya vile utakuwa na maisha ya muzuri yenye inamufurahisha Mungu. Sasa, nini njo itakusaidia ujue ni kiasi gani njo unapaswa kunywa?

Kama kisha kunywa haufikiri tena muzuri, ujue kama pombe yenye umekunywa ni ya mingi. Kwa hiyo, kama unaamua kunywa ni jambo ya hekima ujiwekee mipaka yenye iko wazi; isikuwe yulu sana mupaka unakaribia kulewa. Wakati unachunguza tabia yako ya kunywa, usijidanganye kuhusu hali yako. Ujiwekee mipaka yenye kuwa wazi, na yenye kuwa na kiasi kabisa, yenye haitafanya uangukie mu mutego wa kunywa sana ao kulewa.

6. Ujifunze kukatala. “Muache tu neno lenu ndiyo limaanishe ndiyo, na hapana yenu imaanishe hapana.” (Matayo 5:37) Kama mutu anakupatia pombe, ujifunze kukatala kwa adabu. Biblia inasema hivi: “Maneno yenu yakuwe yenye kupendeza sikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mujue namna munapaswa kumujibu kila mutu.”​—Wakolosai 4:6.

7. Tafuta musaada. Omba musaada kwa marafiki wenye wanaweza kukusaidia upiganishe tatizo yako ya kunywa na wenye wanaweza kukusaidia uendelee kuwa rafiki ya Mungu. Biblia inasema hivi: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja kwa sababu wako na zawabu ya muzuri kwa ajili ya kazi yao ya nguvu. Kwa maana kama mumoja wao anaanguka, ule mwingine anaweza kusimamisha mwenzake.” (Muhubiri 4:9, 10; Yakobo 5:14, 16) Shirika fulani ya Amerika yenye inaangalia mambo ya ulevi inatoa pia hii shauri: “Wakati fulani inaweza kuwa nguvu kupunguza kiasi ya pombe yenye unakunywaka. Omba watu wa familia na marafiki wakusaidie ufikie muradi wako.”

8. Usichoke. “Mukuwe watendaji wa neno, na hapana wasikiaji tu, mukijidanganya wenyewe kwa mawazo ya uongo. Lakini ule mwenye anaangalia katika sheria kamilifu ya uhuru na anaendelea kuwa katika hiyo, amekuwa, hapana musikiaji musahaulifu, lakini mutendaji wa kazi; na atafurahia kile chenye anafanya.”​—Yakobo 1:22, 25.

Kuacha Kuwa Mutumwa wa Pombe

Haiko kila mutu mwenye anakunywaka sana njo anakuwaka mutumwa wa pombe. Lakini watu fulani wanakunywaka sana ao kunywa kila wakati, mupaka wanafikia kuwa watumwa wa pombe. Juu mwili wao na akili yao imezoea sana pombe, hawawezi kutoka mu ile hali kwa kujizuia tu ao kwa kupewa tu mashauri. Allen anasema hivi: “Wakati nilikuwa najikaza kuacha pombe, nilikuwa nasikia maumivu ya mwili ya nguvu sana. Ile ilifanya nielewe kama zaidi ya mashauri ya Biblia, nilikuwa pia na lazima ya kuonana na munganga.”

Watu wengi wenye wako na tabia ya kunywa sana wako na lazima ya kuonana na munganga juu waweze kufuata shauri ya Biblia ya kuacha tabia ya kunywa sana na juu wasiirudilie tena. * Wengine wako na lazima ya kupangishwa ku hopitale juu wanganga wawapatie dawa za kupiganisha maumivu ya nguvu yenye wanasikiaka kisha kuacha kunywa pombe, ao juu wawapatie dawa za kuwasaidia kupunguza hamu ya pombe, na kuwasaidia wasirudilie tena pombe. Mwana wa Mungu mwenye kuwa na nguvu ya kufanya miujiza alisema hivi: “Watu wenye nguvu hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake.”​—Marko 2:17.

Faida ya Kufuata Mashauri ya Mungu

Mungu njo anatupatia mashauri ya muzuri yenye kuwa mu Biblia kuhusu pombe, juu anapenda tufurahie maisha leo na milele. Miaka 24 kisha kuachana na pombe, Allen anasema hivi: “Nilifurahi sana kujua kama ningeweza kubadilika na kama Yehova alipenda kunisaidia ninyooshe maisha yangu. . .” Allen anasimama kidogo na kuzuia machozi yake wakati anakumbuka mambo ya zamani. Kisha anaongezea hivi: “Kujua kama Yehova ananielewa, ananihangaikia, na iko tayari kunipatia musaada wenye niko nao lazima, kumenigusa sana.”

Kama uko na tatizo ya kunywa sana, ao kama ulishakuwa mutumwa wa pombe usivunjike moyo haraka-haraka ao kuwaza kama hakuna tumaini. Allen na wengine walikuwa pia na ile tatizo, lakini waliweza kupunguza kiasi ya pombe yenye walikuwa nakunywa ao waliachana na pombe kabisa. Wanafurahia uamuzi wenye walikamata, na weye utafurahi kama unafanya vile.

Ikiwa unaamua kunywa pombe kwa kiasi ao unaamua kabisa kuacha kunywa pombe, ufuate hii shauri yenye Mungu anatupatia juu anatupenda: “Kama tu ungesikiliza amri zangu! Basi amani yako ingekuwa kama vile muto na haki yako kama mawimbi ya bahari.”​—Isaya 48:18.

[Maelezo ya chini]

^ Ona kisanduku “ Pombe Njo Iko Naongoza Maisha Yako?” ku ukurasa wa 8.

^ Kuko hopitale za mingi, mipango ya mingi, na fasi za mingi za kusaidia watu waachane na tatizo ya kunywa sana. Munara wa Mulinzi hautie watu moyo wafuate matunzo fulani. Kila mutu anapaswa kuchunguza matunzo mbalimbali na kukamata uamuzi wenye haupingane na kanuni za Biblia.

[Kisanduku/​Picha]

 Pombe Ilishakutawala?

Ujiulize hivi:

• Niko nakunywa sana kuliko zamani?

• Niko nakunywa mara mingi sana kuliko zamani?

• Nilishaanza kunywa pombe za makali sana?

• Ninakunywaka juu ya kupunguza mahangaiko ao kusahau magumu?

• Mutu wa familia ao rafiki alishaniambia kama niko na tatizo ya kunywa sana?

• Nimepata magumu ku nyumba, ku kazi ao mu safari juu ya tabia yangu ya kunywa?

• Siwezake kumaliza juma moya na sikunywe pombe?

• Ninasikiaka mubaya wakati wengine hawakunywe pombe?

• Ninafichikaka wengine kiasi ya pombe yenye nakunywaka?

Kama unajibia ndiyo ku ulizo moya ao zaidi kati ya ile maulizo, ni muzuri ufikirie mambo yenye unaweza kufanya juu upunguze ao uache kunywa pombe.

[Kisanduku/​Picha]

Kamata Maamuzi ya Muzuri Kuhusu Pombe

Mbele ya kunywa ujiulize hivi:

Ni jambo ya hekima nikunywe ao nisikunywe?

Shauri: Mutu mwenye hawezi kujizuia hapaswe kunywa.

Napaswa kunywa kiasi gani ya pombe?

Shauri: Uamue kiasi ya pombe yenye utakunywa mbele pombe ivuruge uwezo wako wa kufikiri.

Nitakunywa wakati gani?

Shauri: Usikunywe mbele ya kutembeza gari ao chombo ingine ya kusafiri, wakati uko nafanya kazi yenye inaomba ukuwe muangalifu, wakati uko nafanya mambo ya dini, wakati uko na mimba, ao wakati uko nakunywa dawa fulani.

Nikunywe na niko wapi?

Shauri: Ukunywe na uko fasi ya muzuri; usijifichike wakati uko nakunywa, na usikunywe mbele ya watu wenye wanakwazikaka wakati wanaona mutu iko anakunywa.

Nikunywe na nani?

Shauri: Ukunywe na marafiki wazuri ao watu wa familia; usikunywe na watu wenye wako na tatizo ya kunywa sana.

[Kisanduku/​Picha]

Neno ya Mungu Inasaidia Mutu Mwenye Alikuwa Mulevi Sana

Supot, wa Tailandi, alikuwaka nakunywa pombe sana. Ku mwanzo, alikuwaka tu anakunywa mangaribi. Lakini pole kwa pole akaanza kunywa pia asubui na midi. Mara mingi alikuwa nakunywa juu tu alewe. Kisha akaanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Wakati alijifunza kama Yehova Mungu anachukia ulevi, akaacha kunywa. Lakini kisha wakati fulani alirudilia tabia yake ya zamani ya kunywa sana. Familia yake ilihuzunika sana.

Lakini, Supot alikuwa angali anamupenda Yehova na alipenda kumuabudu mu njia yenye anakubali. Marafiki wa Supot waliendelea kumusaidia na walitia moyo watu wa familia yake wapitishe wakati pamoya naye na wasiache kumusaidia. Ile wakati, maneno yenye kuwa wazi ya 1 Wakorinto 6:10 yenye kusema kama ‘walevi hawatariti ufalme wa Mungu,’ ilimusaidia Supot aone kama ulevi ni kosa kubwa sana. Alielewa kama alipaswa kufanya yake yote juu aachane na ulevi.

Mara hii, Supot aliamua kuachana kabisa na pombe. Ku mwisho, kwa musaada wa nguvu ya roho takatifu ya Mungu, mashauri ya Neno ya Mungu, na kwa musaada wa watu wa familia yake na ya ndugu na dada, Suport alipata nguvu ya kushinda hamu yake ya kunywa pombe. Familia yake ilifurahi wakati alijitoa kwa Yehova na kubatizwa. Sasa Supot iko na urafiki muzuri na Mungu sawa vile alikuwa anapenda kuanzia zamani na iko natumia wakati yake juu ya kusaidia wengine pia wamujue.