MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 8, 2013

Gazeti hili linazungumuzia namna tunaweza kubaki watakatifu na kuendelea kufanya kazi ya Mungu, namna ya kuepuka kumulaumu Mungu kwa sababu ya matatizo yetu, namna ya kupambana na kuvunjika moyo.

Tumetakaswa

Chunguza mambo mane yanayoweza kutusaidia ili tubaki watakatifu na ili tuendelee kufanya kazi ya Mungu.

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Je, ni jambo lenye kufaa kwa wazazi Wakristo kukaa pamoja na mutoto wao aliyetengwa kwenye mikutano?

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Yehova ‘Ananibebea Muzigo Wangu Kila Siku’

Ijapokuwa matatizo makubwa ya afya, ni nini imemusaidia Maretha du Raan kufurahia kazi ya upainia huko Afrika Kusini kwa zaidi ya miaka 20?

Usimukasirikie Yehova Hata Kidogo”

Watu fulani wamemuwekea Mungu kinyongo katika mioyo yao. Wanamulaumu kwa sababu ya matatizo yao. Namna gani tunaweza kuepuka mutego huo?

Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Tangu Utoto Muchanga

Wazazi wanapaswa kuanza kuwazoeza watoto wao tangu wakati gani? Mazoezi hayo yanapaswa kutia ndani nini?

Tufikiriane na Kutiana Moyo

Namna gani tunaweza kusaidiana ili kuendelea kumutumikia Mungu kwa uaminifu hata wakati tunapambana na matatizo?

Tunapaswa Kuwa Watu wa Namna Gani?

Shetani hataki tukubaliwe na Mungu. Tunaweza kufanya nini ili tulinde urafiki wetu pamoja na Yehova?

Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto—Je, Wewe Pia Unayaona?

Elisha alisitawisha imani yenye nguvu na alimutumainia Yehova kabisa. Mufano wake unaweza kutufundisha nini?

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Mufalme Alifurahi Sana!

Jifunze namna mufalme mumoja huko Swaziland alivyofurahia kujifunza mafundisho ya kweli ya Biblia.